Riwaya: Nitakupata tu

Hahahaaa kuna lugha niliisikia kwa waswahili wakisema kama ushuzi basi ushapata mjambaji yaani rais ataomba Poo sasa Teddy Ndiyo kabisa kifo chake kimefika maana kama usingizi masimba kashampata Veronica
 
Aah Ibra ee kuanzia ya kwanza naweza kuipata?
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 089

Hakuwa na Haraka ya kuinuka kwa kuwa alijua kuna mtu yupo sehemu akimtizama. Hata wale watu wawili ambao walikuwa wamesimama umbali mfupi kutoka kilipokijiwe cha kahawa bado hawakuondoka. Walionyesha bado walikuwa na maongezi marefu. Hata Mtu yule naye akakakaa na kuwatizama. Haukupita muda mmoja kati ya watu waliokuwa wakifanya mazungumzo akaaga na kuondoka akiivuka barabara kuelekea maeneo ya Posta mpya. Yule mmoja naye Alikuwa amerudi nyuma akiongoza kama alikuwa akielekea chuo cha Elimu ya Biashara. Mtu huyu alikuwa akiwatizama huku akicheka kimoyomoyo. Aliitambua kasumba ya Wana usalama wengi. Aliitambua staili yao na pia aliitambua aina yao ya maigizo. Kilichokuwa kikifanywa na watu wawili waliokuwa wakizungumza ndicho kitu kilichotoa mwanya kwa Wana usalama wengine kuondoka na mtoto wa Rais. Baada ya kuhakikisha hakuna mtu mwingine wa kumtilia mashaka. Alilipa pesa ya kahawa kisha akainuka na kuiendea Gari yake aliyekuwa ameipaki pembezoni kidogo mwa barabara. Akaingia ndani ya gari, safari ya kuelekea alikopaswa ikaanza. Wakati gari ikiendelea kutembea taratibu, bastard akafungua sehemu fulani ndani ya gari na kutoa kitu mfano wa Saa. Baada ya kukitoa kitu Hicho akaingiza maneno kadhaa. Katika sekunde ile ile kitu kile kikawaka. Akasubiri Kidogo Kisha Akaingiza namba za Gari Iliyoondoka na Mtoto wa Rais. Akaendelea kusubiri huku Gari ikiendelea kutembea. Dakika Tano mbele Kitu kile mfano wa Saa Kikaonyesha Neno Oysterbay block no 451. Bastard akatabasamu na wakati huo huo akakizima kitu kile mfano wa saa. Kwa mara nyingine alikuwa ameingia kwenye mission ya Hatari. Mission ambayo Ina mkutanisha mara nyingine na Wana usalama. Wana usalama wa Tanzania. Kichwa chake hakikusahau mission ya kwanza ambayo ilimlazimu Kusafiri mpaka Nchini Canada. Alikuwa sambamba na MOA, JENIPHER Sambamba Na Neema. Ilikuwa mission ngumu sana kupambana na mashirika makubwa ya Kijasusi Duniani. Ni mkasa ambao ukiwapa Sifa kubwa, Sifa ambayo ilishawishi mpaka mataifa makubwa ya kijasusi kuamba kufanya kazi na watu hao. Mkasa ambao Uligundua Siri kubwa Iliyojificha Nyuma ya Mauaji ya Mke Wa Rais. Leo hii alikuwa amekutana tena na Masimba. Lakini safari hii sio masimba pekee yake, bali alikutana na Veronica. Vero Mwanamke Kutoka Nchini Italy. Veronica Ambaye alikuwa ni mwanachama Mwandamizi wa Kundi la Mafia. Gari akazidi kushika kasi, alihitaji kwenda kumchukua Mtoto wa Rais kwa sababu ya kymshinikiza Baba yake Aitoe ile betri. Alijua ilikuwa kazi ngumu, lakini ilikuwa Lazima Aifanye. Ilikuwa lazima atengeneze hilo. Akalivuka daraja la Salenda. Mbele kidogo akaingia kulia kam anaelekea Masaki. Kufika Mbele kidogo akaingia kushoto na kuingia katika Eneo hilo. Akaongoza mpaka sehemu maalum ya kuegeshea magari. Baada ya kuegesha gari, akashuka akaifunga milango vizuri kisha kusogea mpaka alipomlizi wa Sehemu hiyo. Baada ya kumfikia mlinzi alichomoa noti ya Elfu kumi akamkabidhi mkononi akimuacha mlinzi yule akifurahi. Baada ya kumalizana na Mlinzi, Bastard akatembea kwa kawaida kuliacha eneo hilo. Akatokea kwenye Chochoro moja Ambayo ilimuongoza kuelekea lilipo jengo ambalo aliishi mtoto wa Rais. Hakuogopa chochote kile.

Alikuwa tayari kwa kila ambacho kiko mbele yake. Akaupita uchochoro ule pasipo kutokea rabsha yoyote. Mbele kidogo akauvuka Uzio wa Kiwanda fulani. Baada ya kuuvuka Uzio Huo akajikuta akitizamana na jengo ambalo alikuwa akiishi mtoto wa Rais. Akatulia kwanza akilitizama Jengo lile Kwa Umakini Mkubwa. Macho yake yalikuwa yakitizama na kuhesabu askari ambao walikuwa hapo. Askari wa nne wenye Bunduki walikuwa Geti la mbele sambamba na wana usalama wengine watatu. Upande wa nyuma wa Jengo hili pia walisimama Askari watatu na wengine ambao walivaa kiraia. Akaamua kuhama Eneo hilo na kuizunguka lile Jengo. Muda wote alikuwa akiwatizama walinzi ambao walikuwa mbele yake. Hawa walikuwa wawili tu, huku mmoja akionyesha kuwa Amelala. Akaona hapa ndipo sehemu sahihi ya kuingia ndani Alitaka kuingilia hapo katika namna yoyote ile. Alitambua sehemu ile ndiyo ingeweza kumfanya aingie ndani bila wasiwasi. Akahama Upande ule na kukivuka kibarabara fulani. Baada ya kuvuka hapo. Sasa alikuwa amewakaribia Walinzi hawa wawili. Akatembea Akinyata taratibu, alikuwa akitembea mfano wa chui. Kwa mwendo wa silika akachupa na kutua katikati ya walinzi hawa. Kilikuwa kitendo cha sekunde tu kutendeka. Mlinzi mmoja alikuwa chini akiwa ameshika koromeo. Wakati mlinzi huyu wa pili akikurupuka kutoka usingizini. Akakutana na Ngumi moja ya Shingo iliyompeleka Chini. Wakati mlinzi huyu akihangaika kuinuka, bastard akamuwahi pale chini na kumnyonga Shingo. Baada ya Kummaliza Huyu akageuka kumuendea huyu mwingine. Lakini akakuta Tayari Alikuwa Amekufa. Hapo akaongoza kuelekea kwenye Nyumba hii. Haukupita Muda alikuwa ameshauparamia ukuta na kuingia Ndani. Kitendo cha kutua tu, akaichomoa Bastola Yake. Akaanza kutambaa taratibu kuelekea ndani kabisa ya nyumba. Alitembea akifuata vivuli vya miti. Kufika mbele kidogo akasimama kwenye shina la mti baada ya kusikia sauti za watu kwa mbali. Akatega sikio zaidi na zaidi. Akagundua sauti zilikuwa zikitokea ndani kidogo ya Jengo lile. Akatulia hapo zaidi na zaidi. Punde mlango ukafunguliwa kisha uso wa binti mrembo ukaonekana kuchomoza katika tabasamu tamu. Hakuwa binti pekee bali alikuwa na Mtoto wa Rais. Kila moja alikuaa amevaa pajama wakionyesha kuutafuta ubaridi. Ubaridi ambao hakuujua ni wa nini mpaka pale binti yule aliyekuwa na mtoto wa Rais alipolitoa vazi lile pekee Mwilini. Pale alipobakia kama alivyozaliwa. Alipokewa na Chuchu safi na za kuvutia kama za Mtoto Swahiba. Chuchu ambazo zilifaa kwa kunyonya kulamba na hata kumalizia kwa Shida nyingine. Alikuwa mweupe chuchu zikisimama mithili ya michongoma. Huyu alikuwa ni zaidi ya Shunie na Hata Heaven Sent. Huyu alikuwa Akivutia na kutia hamasa mfano wa Black woman Wa Jf. Alivutia na kutia hamu. Uwanja wake wakuchezea ulikuwa na Majani Madogomadogo ambayo yaliupendezesha na kuufanya upendeze. Ni umbo lililoutatanisha Ubongo wa Mwanaharamu. Umbo ambalo lilisababisha mtafaruku kichwani kwa binadamu huyu aliyelaaniwa. Akatamani aitumie bastola kumuondoa mtoto wa Rais ili akichukue kiumbe hiki. Kiumbe ambacho hakikufanana na Nuru na Hata Mwadi. Huyu alifanana kabisa na Tete. Tete ambaye alikuwa akimilikiwa na Jasusi liitwalo muteba. ( R.I.P Elvis Musiba) akatamani kuitupa bastola yake ilikuwavamia watu hawa aondoke na Binti Huyu. Hata pale binti alipojilaza kwenye kitanda maalum pale nje kisha kuiachanisha miguu yake huku na Huko bado Mwanaharamu alilitizama tukio hili. Hata pale mtoto wa Rais aliposogea na kukaaa karibu ya malaika yule. Bado Mwanaharamu akatulia kanakwamba hakuwa anakiangalia kitendo hiki. Macho yake yakajakubadilika baada ya mkono wa Binti Yule usio na Adabu ulipoingia ndani ya Vazi la Mtoto wa Rais. Mkono ambao ulitulia kwa muda ukitafuta kitu ambacho ulipoteza. Mkono huo ndio uliomkumbusha kuwa alikuwa hapo kwa mission maalum. Yupo hapo kwa Ajili ya kumchukua Huyu mtu. Dakika hii alikuwa ameinuka akielekea pale walipokuwa watu hawa wakifanya ufirauni. Binti mdomo wake ulikuwa ukipanda na kushuka maeneo fulani, wakati mtoto wa Rais alikuwa amesinzia akisikilizia kitu ambacho hakikujulikana. Kutokana na kilichokuwa kikitendeka pale, watu hawa hawakumuona Mwanaharamu alipokuwa Akisogea hapo. Mwanaharamu akatembea na muda mfupi alikuwa Amesimama hatua mbili kutoka Walipo watu hawa. Mdomo wa bastola kumgusa mwanamke huyu ndicho kilichowashtua wote. Mwanamke kuinua Macho yake na kukutana na Mdomo Wa Bastola, akajikuta akipiga yowee. Ni yowee lililoifanya Bastola Ya mwanaharamu Ikohoe. Risasi zikiingia kifuani Kwa Binti Huyu na kumtupa umbali wa hatua kumi na tano. Risasi Nyingine Zikikifumua kichwa Cha Mtoto wa Rais. Hapakuwa na Jinsi zaidi ya alichokifanya. Mipango yake Ilikuwa imevurugwa na Mwanadada huyu. Hakutaka kuupoteza muda. Akataka kuondoka na kutoweka eneo hili. Lakini hakuwahi kufanya hivyo. Akashuhudia wana usalama katika namna iliyovutia. Kuvutia kwa mapambano. Muda huo huo akasikia Risasi zikivurumishwa kuelekea kwake. Hakuchelewa wala kusubiri chochote kitokee. Alikuwa amechupa tayari na wakati huo huo akiachia risasi mfululizo kuelekea walipo walinzi. Risasi Zilivurumishwa bila kukoma. Walinzi hawa hawakutaka kumpa nafasi Mwanaharamu. Mwanaharamu akatambua hapo ilikuwa ni Lazima Aondoke hapo kabla ya wana usalama wengine kufika. Akainyanyua Bastola yake na kuilenga taa. Muda mfupi baadae Sehemu yote ilikuwa Giza. Hapo ndipo alipoinuka taratibu na kutambaa mpaka usawa wa ukuta. Akajivuta Taratibu na kufanikiwa kuanguka upande wa pili. Baada ya kutua salama, akatembea taratibu na giza mpaka fukwe za coco. Kutoka hapo akajichanganya na watu ambao walikuwepo hapo. Kabla ya kurudi kwenye maegesho ya Magari na kuichukua gari yake, nakuondoka taratibu katika eneo hilo. Wakati akijua ameshamaliza kile alichokitenda. Akawaona watu watano Wenye Silaha wakiwa mbele yake. Baada ya kuwafikia mmoja akampa Ishara ya kumtaka asimamishe gari. Mwanaharamu Akatiii!! Akaisimamisha Gari na kuizima kabisa. Akatulia tuli kuwasubiri watu hawa ambao sasa walikuwa wakimsogelea.
 
Mmh mdogo wangu ibra ndio umeshampenda shunie nini? Maana sio kwa kumpaisha huko
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…