Marilyn Monroe
Member
- Apr 2, 2020
- 80
- 166
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA KUMI NA SITA
Alitupa tena macho upande wa pili wa ile barabara, na kuna gari jingine likawa linapita hivyo hakumuona yule jamaa mwenye tai mpaka lilipopita, ambapo alimuona yule jamaa akiinuka kutoka pale alipokuwa amechutama. Mara moja yule mtu mrefu mwenye koti refu aligundua kitu kisicho cha kawaida. Mkono wa kulia wa yule mtu mwenye tai ulikuwa unatokea nyuma ya bati linalofunika tairi la mbele la gari lile!
Ala!
Yule mtu mwenye tai alisimama kwa sekunde chache zaidi kama mtu anayetaka kuvuka barabara. Kisha taratibu alitumbukiza mikono yake kwenye mifuko ya suruali yake ya buluu, akageuka nyuma taratibu kuangalia upande ambao Jaka na Clara wangetokea, halafu aligeuka tena taratibu na kutazama kule ambapo ilipoegeshwa ile Raum nyeupe.
Hapo yule mtu mrefu mwenye koti refu alijua kuwa yule jamaa alikuwa ni mtaalamu kwenye fani yake kwani alikuwa akigeuka kwa namna ambayo kwa mtu mwingine yeyote angeonekana kuwa ni mtu wa kawaida aliyekuwa akimsubiri rafiki au jamaa aliyechelewa miadi. Katika kugeuka kwake, alikuwa akizungusha mwili wake kutokea kiunoni kuja juu, na wakati akifanya hivyo alikuwa akitupa tupa miguu yake mbele, mara moja au mbili akijaribu kupiga teke vijiwe vidogo vilivyokuwa pale barabarani. Hii ilileta picha kuwa alikuwa akimsubiri mtu, na subira yake ilikuwa inaelekea ukingoni.
Haya yote yaliendelea kutazamwa kwa utulivu wa hali ya juu na yule bwana mwenye kofia pana, kwani naye, kama yule mtu mwenye tai ng'ambo ya pili ya barabara, alikuwa ni mtaalamu kwenye fani yake. Mara ile yule mtu mwenye tai aliinua mkono wake wa kulia na kuangalia saa. Mtu mwenye pama alitabasamu, kwani alielewa ni nini kitafuata baada ya kitendo kile. Yule bwana mwenye tai alishusha mkono wake na kuanza kuvuka barabara taratibu kuelekea kule ilipokuwa imeegeshwa ile Raum.
Jamaa mwenye kofia pana alijua kuwa hakuwa peke yake aliyekuwa akimvizia Jaka siku ile. Yeye
binafsi alijua ni kwa nini alikuwa anamfuatilia Jaka siku ile. Tatizo ni wale jamaa wengine. Wanahusiana vipi na Jaka? Kwa nini hawakutokea siku zote wakaamua kutokea leo? Na jambo alilofanya yule bwana mwenye tai pale kwenye gari la akina Jaka....
Maswali haya yalipita kichwani mwake huku akijaribu kuoanisha matendo ya yule mtu mwenye tai na uwepo wa akina Jaka kwenye eneo lile. Jibu la jumla alilolipata ni kwamba jambo baya sana lilikuwa linaandaliwa...limeandaliwa pale.
Alibaki pale pale alipokuwa amesimama. Jamaa aliingia ndani ya ile Raum na kutulia kando ya dereva. Kinyume na matarajio ya yule bwana mwenye pama, ile Raum iliendelea kubai pale pale, haikuondoka, Aliitazama ile gari na kujikuta akizikariri namba za usajili za gari lile.
Ni jambo gani limefanyika pale?
Kwa nini?
Hakupata jibu. Dakika zilisogea. Nusu saa ilipita. Dakika aribaini na tano. Hakuna badiliko. Ile Raum bado ilikuwa imeegeshwa pale pale na wale watu wawili wakiwa ndani yake.
Sasa wanasubiri nini? Yule mtu alipitisha mkoni chini ya ile Vitara...kwa nini...?
Wakati akiendelea kujiuliza maswali hayo, alizidi kuchanganyikiwa pale alipowaona Jaka na Clara wakitoka nje ya eneo lile la Nyerere Square kuelekea kwenye gari lao huku wakiongea na kucheka kwa furaha, Clara akiwa amebeba kifurushi kidogo bila shaka cha vipochopocho walivyonunua eneo lile.. Aligeukia tena kule kwenye ile Raum. Dereva wa ile gari alikuwa ametoa kichwa nje ya dirisha akiangalia kule ambapo akina Jaka walikuwako. Na hata pale alipokuwa akimtazama, alimuona yule dereva wa Raum akiinamisha uso kutazama saa yake na kuuinua tena uso kuwatazama akina Jaka.
Ina maana gani?
Kama kuna jambo lolote lililoandaliwa pale, basi sasa ndio ulikuwa wakati wa jambo hilo kutokea. Akili ilimwenda mbio...
Kule upande wa pili wa barabara Jaka alikuwa anazunguka mbele ya ile Vitara ili aende upande wa dereva ambao ulikuwa upande wa barabarani. Clara alikuwa amesimama upande wa mlango wa abiria wa gari lile....
Ni nini kitatokea pale?
Na mara alikumbuka.
Ilimjia kichwani mwake kwamba katika nukta moja ya sekunde baina ya kupita gari la kwanza na la pili aliweza kumuona yule mtu mwenye tai akiwa ameinama pale chini, na katika nukta ile macho yake yalikuwa yanautafuta mkono wa kulia wa yule mtu, kwai ilimjia kama anayefunga kamba kw amkono mmoja tu...mkono wa kushoto. Katika nukta moja ile, alihisi aliuona ule mkono wa kulia wa yule mtu ukiwa umeshika tairi la mbele la lile gari...au ulikuwa umefichwa na bati la gari lile linalofunika tairi...?
Aligeuka tena kushoto kwake.
Ile Raum ilikuwa inaondoka taratibu kutoka eneo lile; na sasa alimuona yule mtu mwenye tai, akiwa ndani ya gari akigeuka kutazama pale lilipokuwa gari la akina Jaka. Naye upesi aligeuka tena kutazama kule walipokuwa akina Jaka.
Jaka alikuwa ameegemeza sehemu ya mbele ya mwili wake kwenye boneti la gari lile akipokea funguo za gari kutoka kwa Clara aliyekuwa upande wa pili wa gari lile.
Akili ilizidi kumzunguka jamaa mwenye pama.
Ilikuwa haileti maana....kwa nini yule mtu, ambaye kwa hakika alikuwa akiwasubiri akina Jaka, aamue kuondoka baada ya watu aliokuwa akiwasubiri kutokea...bila ya kuongea nao chochote? Au...?
Hakufikiri zaidi.
Alikurupuka na kutoka kasi kukimbilia kule walipokuwa akina Jaka huku akimwita Jaka kwa kelele na akimpungia mikono ili amuone.
"Jaka...! Jakaaaaaaa! Toka hapoooo....tokeniiiih! Kimbienii....ondokaaaaa...uppeeeesssss!" Yule mtu alikuwa akipiga kelele huku akivuka barabara kuelekea kule walipokuwa akina Jaka.
Jaka aligeuka kwa mshituko aliposikia jina lake likiitwa kwa kelele hadharani. Na hata pale alipogeuka alimuona yule mtu mwenye koti refu akiingia barabarani huku akimkimblia bila kujali magari. Gari moja lilifunga breki kali na kuserereka huku tairi zake zikitoa sauti kali ya msuguano na lami huku honi kali ikirindima. Lile gari lilikuwa linaelekea kumgonga lakini yule mtu aliweka mkono wake wa kulia kwenye boneti la lile gari na kujisereresha juu ya boneti lile na kudondokea upande wa pili wa gari ile. Watu walioshuhudia tukio lile walipiga kelele za woga na mshituko juu ya kitendo kile hali wengine wakibaki midomo wazi na kujishika vichwa. Jamaa hakujali. Aliendelea kuwakimbilia akina Jaka huku akiwapigia kelele kama mwehu.
"Ondoka wewweeeh....! Kimbia...! You are going to die gaddemmiiiitt! Toka...! Hilo gariiii!"
Mara moja alimtambua John Doe. Alimuona alivyokuwa akiwaendea mbio huku akipunga mikono hewani na akipiga mayowe kama mwehu, na alishuhudia kwa mshituko jinsi alivyoruka juu ya boneti la gari lililokuwa kwenye mwendo wa kasi. Alipoona bado John Doe anazidi kuwakimbilia namna ile baada ya kukoswa kugongwa na gari, alijua ni lazima afanye kitu. Alisikia maneno yaliyokuwa yakitoka kinywani mwa yule mtu na aliiona hofu iliyojianika usoni kwa yule jamaa wakati akiwakimbilia namna ile. Jamaa alikuwa hafanyi utani.
Kutokea kule alipokuwa Jaka aligeuka na kuudaka mkono wa Clara na kumvuta pembeni huku na yeye akijisukuma kutoka ubavuni mwa lile gari kuelekea mbele ya lile gari. Clara alipiga kelele za hamaniko bila ya kuelewa kilikuwa kinatokea. Jaka alimkamata kiuno na kujitahidi kumvutia pembeni, mbali na lile gari lao. Walipepesuka vibaya huku raia waliokuwa eneo lile nao wakipiga kelele za kutoelewa.
Sasa John Doe alikuwa karibu sana na walipokuwa wakipepesukia. Jaka alijigeuza mzima mzima na kumkabili yule jamaa mwenye ngumi nzito huku akiwa amemkinga Clara kwa mgongo wake. Alikuwa akijitahidi kuongeza umbali baina yao na John Doe kwa kurudi nyuma huku akimsukuma Clara kwa nyuma. Watu wengi waliokuwa katika eneo lile walitawanyika mbio kila mmoja kwa upande wake bila ya kujua ni nini hasa walichokuwa wanakikimbia.
"Hilo gari hilo weweee...! Gariii! Kaa mbali naloo...ebbo! TOKA HAPOOO! Kimbieniii, Pummm-bbaaavvvv!" John Doe aliendelea kubwata huku akiwakimbilia. Jaka aliduwaa kidogo, na hapo John Doe alienda hewani mzima mzima akiwa ametanguliza mikono yake na kumkumba Jaka kwa kishindo, bega lake la kushoto likijikita tumboni kwa Jaka na wakati huo huo mkono wake wa kushoto uking'ang'ania kiunoni Clara aliyekuwa nyuma ya Jaka. Kwa wahka Jaka alirusha ngumi kwa mkono wake wa kushoto akiamini kuwa jamaa alikuwa anashambulia, lakini yule jamaa jabari aliipangua ngumi ile na hapo hapo akamdaka mkono ule kwa mkono wake wa kulia na wote watatu wakawa wanaelekea kupiga mweleka mzito.
Jaka hakuwa na la kufanya zaidi ya kung'ang'ania koti la yule mtu kwa mgongoni kwa mkono wake wa kulia. Nyuma yake, Clara akajigonga kisigino kwenye ukingo wa barabara na kupoteza kabisa mwelekeo. Alibaki akimng'ang'ania Jaka mgongoni huku akipiga kelele zisizoeleweka.
Msukumo wa yule mtu alivyowaparamia, na kujikwaa kwa Clara, viliwafanya wote watatu waruke hewani na kujibwaga bila mpangilio juu ya meza za wachuuzi wachache waliokuwa kando ya barabara ile. Mayowe yalizagaa wakati wao wakijipigiza chini kwenye vumbi wakisambaratisha meza na bidhaa zilizokuwa juu yake huku wale wachuuzi wakipiga mayowe na kukimbia hovyo. Jaka alikuwa akijaribu kujiinua kutoka pale chini akiwa amemlalia Clara kwa mgongo wake huku yule jamaa akiwa amemlalia kwa tumbo lake juu yake. Lakini kila alivyojaribu kujiinua ndivyo yule jamaa alivyozidi kumkandamiza chini kwa nguvu na ndivyo walivyozidi kumwelemea Clara aliyekuwa chini kabisa akipiga kelele vibaya sana.
Na mara hiyo hiyo mlipuko mkubwa sana ulisikika.
Jaka akiwa amekandamizwa chini na yule mtu aliweza kushuhudia kwa mshituko na kutoamini kukubwa kabisa jinsi gari lao likipasuka kuanzia sehemu ya mbele sanjari na mlipuko ule. Moto mkubwa uliruka hewani na aliliona lile gari likinyanyuliwa zima zima kutoka pale lilipokuwa limeegeshwa na kutupwa hewani huku likisambaratika vipande vipande. Vipande vya vioo vilirushwa huku na huko na kurudi ardhini kama matone ya mvua, vikijeruhi watu waliokuwa wamezagaa eneo lile. Tairi moja lilichomoka na kutupwa angani huku likiwaka moto na kufuka moshi.
Yote haya Jaka aliyaona ndani ya sekunde moja tu.
Macho yalimtoka pima na kinywa kilimchanua pasi sauti kutoka.
Mayowe, vilio na heka heka vilitawala eneo la Nyerere Square asubuhi ile. Watu walikibia huku na kule wakijaribu kuokoa maisha yao bila ya kujua ni wapi hasa palikuwa salama. Katika kelele zao hizo, Jaka alimsikia Clara akipiga mayowe ya woga na maumivu kutokea nyuma yake.
Clara likuwa amelalia mgongo pale chini. Juu alikuwa amelaliwa na mgongo wa Jaka. Juu ya Jaka John Doe alikuwa amelalia tumbo uso wake akiwa ameuficha upande wa kulia wa shingo ya Jaka huku akijikinga kichwa chake kwa mkono wake wa kushoto. Uso wa Jaka ulitokeza juu ya bega la kushoto la yule mtu ukitazama angani.
Na mara nyingine tena kilisikika kishindo kingine kilichotokana na mabaki ya lile gari kujibwaga tena ardhini katikati ya barabara na kulalia ubavu huku likiendelea kuteketea kwa moto. Watu walianza kulikimbilia na kulizunguka, hali wengine wakiwazunguka akina Jaka waliojirundika pale chini.
John Doe alijiinua kutoka pale chini, na haraka Jaka aliyechanganyikiwa naye akakurupuka kutoka pale chini. Alipepesuka na kuanguka tena chini. John Doe alimsaidia Clara kuinuka kutoka pale chini na kumshikilia asianguke kama Jaka. Uso wake ulionekana kutulia na kutokuwa na woga hata kidogo. Hatimaye Jaka aliinuka na kujivuta mpaka pale alipokuwa amesimama Clara huku macho yakiwa yamemtoka pima.
"Oh! Jaka...Jaka...tungekufa leo dear!" Clara alibwabwaja huku akilia. Jaka alimkumbatia kwa nguvu huku akimpigapiga mgongoni.
"Ni kweli. Lakini bado tunapumua...hatujafa...." Jaka alimliwaza huku macho yake yakiangaza huku na kule akimtafuta yule mtu mwenye koti refu ambaye alionekana kuyeyuka kama upepo mara Jaka alipomfikia Clara pale walipokuwa wamesimama. Kwa hakika yule mtu alikuwa amewaokoa kutokana na kifo kibaya sana, na sasa jumla ya maswali yaliyopita kichwani mwake ilikuwa haisemeki. Swali moja lilibaki kuwa kubwa kuliko yote.
Kwa nini?
"Imekuwaje...? Nini kimetokea...?" Alijikuta akibwabwaja peke yake huku akiendelea kutembeza macho kila kona bila ya mafanikio, kundi la mashuhuda liliowazunguka ulilifanya zoezi la kumuona yule mkombozi wao asiyetarajiwa kuwa gumu sana.
"Mlitegewa bomu....na wewe ndiye uliyekusudiwa." Sauti ilimjibu kwa upole kutokea nyuma yake. Aligutuka huku akigeukia kule sauti ilipotokea, na kumuona yule mtu mwenye koti refu. Alikuwa amesimama huku macho yake akiwa ameyaelekeza kule lilipokuwa linateketea lile gari.Yaani jamaa alikuwa amemjibu bila ya kumtazama na hakutaka kumtazama.
"Lakini wewe...? Kwa nini umeni...umetu....mbona... Ah! We' nani kwani...?" Jaka alibwabwaja huku akimkodolea macho yule mtu na akishindwa kabisa kuzipangilia sentesi zake. Mara ving'ora vya magari ya polisi vilisikika, na muda mfupi baadaye magari matatu ya polisi yalifika eneo lile kwa makeke. Askari wa jeshi la polisi waliruka kutoka kwenye magari yale na kuzidi kuwatia hofu wananchi waliojazana eneo lile.
ITAENDELEA
Alitupa tena macho upande wa pili wa ile barabara, na kuna gari jingine likawa linapita hivyo hakumuona yule jamaa mwenye tai mpaka lilipopita, ambapo alimuona yule jamaa akiinuka kutoka pale alipokuwa amechutama. Mara moja yule mtu mrefu mwenye koti refu aligundua kitu kisicho cha kawaida. Mkono wa kulia wa yule mtu mwenye tai ulikuwa unatokea nyuma ya bati linalofunika tairi la mbele la gari lile!
Ala!
Yule mtu mwenye tai alisimama kwa sekunde chache zaidi kama mtu anayetaka kuvuka barabara. Kisha taratibu alitumbukiza mikono yake kwenye mifuko ya suruali yake ya buluu, akageuka nyuma taratibu kuangalia upande ambao Jaka na Clara wangetokea, halafu aligeuka tena taratibu na kutazama kule ambapo ilipoegeshwa ile Raum nyeupe.
Hapo yule mtu mrefu mwenye koti refu alijua kuwa yule jamaa alikuwa ni mtaalamu kwenye fani yake kwani alikuwa akigeuka kwa namna ambayo kwa mtu mwingine yeyote angeonekana kuwa ni mtu wa kawaida aliyekuwa akimsubiri rafiki au jamaa aliyechelewa miadi. Katika kugeuka kwake, alikuwa akizungusha mwili wake kutokea kiunoni kuja juu, na wakati akifanya hivyo alikuwa akitupa tupa miguu yake mbele, mara moja au mbili akijaribu kupiga teke vijiwe vidogo vilivyokuwa pale barabarani. Hii ilileta picha kuwa alikuwa akimsubiri mtu, na subira yake ilikuwa inaelekea ukingoni.
Haya yote yaliendelea kutazamwa kwa utulivu wa hali ya juu na yule bwana mwenye kofia pana, kwani naye, kama yule mtu mwenye tai ng'ambo ya pili ya barabara, alikuwa ni mtaalamu kwenye fani yake. Mara ile yule mtu mwenye tai aliinua mkono wake wa kulia na kuangalia saa. Mtu mwenye pama alitabasamu, kwani alielewa ni nini kitafuata baada ya kitendo kile. Yule bwana mwenye tai alishusha mkono wake na kuanza kuvuka barabara taratibu kuelekea kule ilipokuwa imeegeshwa ile Raum.
Jamaa mwenye kofia pana alijua kuwa hakuwa peke yake aliyekuwa akimvizia Jaka siku ile. Yeye
binafsi alijua ni kwa nini alikuwa anamfuatilia Jaka siku ile. Tatizo ni wale jamaa wengine. Wanahusiana vipi na Jaka? Kwa nini hawakutokea siku zote wakaamua kutokea leo? Na jambo alilofanya yule bwana mwenye tai pale kwenye gari la akina Jaka....
Maswali haya yalipita kichwani mwake huku akijaribu kuoanisha matendo ya yule mtu mwenye tai na uwepo wa akina Jaka kwenye eneo lile. Jibu la jumla alilolipata ni kwamba jambo baya sana lilikuwa linaandaliwa...limeandaliwa pale.
Alibaki pale pale alipokuwa amesimama. Jamaa aliingia ndani ya ile Raum na kutulia kando ya dereva. Kinyume na matarajio ya yule bwana mwenye pama, ile Raum iliendelea kubai pale pale, haikuondoka, Aliitazama ile gari na kujikuta akizikariri namba za usajili za gari lile.
Ni jambo gani limefanyika pale?
Kwa nini?
Hakupata jibu. Dakika zilisogea. Nusu saa ilipita. Dakika aribaini na tano. Hakuna badiliko. Ile Raum bado ilikuwa imeegeshwa pale pale na wale watu wawili wakiwa ndani yake.
Sasa wanasubiri nini? Yule mtu alipitisha mkoni chini ya ile Vitara...kwa nini...?
Wakati akiendelea kujiuliza maswali hayo, alizidi kuchanganyikiwa pale alipowaona Jaka na Clara wakitoka nje ya eneo lile la Nyerere Square kuelekea kwenye gari lao huku wakiongea na kucheka kwa furaha, Clara akiwa amebeba kifurushi kidogo bila shaka cha vipochopocho walivyonunua eneo lile.. Aligeukia tena kule kwenye ile Raum. Dereva wa ile gari alikuwa ametoa kichwa nje ya dirisha akiangalia kule ambapo akina Jaka walikuwako. Na hata pale alipokuwa akimtazama, alimuona yule dereva wa Raum akiinamisha uso kutazama saa yake na kuuinua tena uso kuwatazama akina Jaka.
Ina maana gani?
Kama kuna jambo lolote lililoandaliwa pale, basi sasa ndio ulikuwa wakati wa jambo hilo kutokea. Akili ilimwenda mbio...
Kule upande wa pili wa barabara Jaka alikuwa anazunguka mbele ya ile Vitara ili aende upande wa dereva ambao ulikuwa upande wa barabarani. Clara alikuwa amesimama upande wa mlango wa abiria wa gari lile....
Ni nini kitatokea pale?
Na mara alikumbuka.
Ilimjia kichwani mwake kwamba katika nukta moja ya sekunde baina ya kupita gari la kwanza na la pili aliweza kumuona yule mtu mwenye tai akiwa ameinama pale chini, na katika nukta ile macho yake yalikuwa yanautafuta mkono wa kulia wa yule mtu, kwai ilimjia kama anayefunga kamba kw amkono mmoja tu...mkono wa kushoto. Katika nukta moja ile, alihisi aliuona ule mkono wa kulia wa yule mtu ukiwa umeshika tairi la mbele la lile gari...au ulikuwa umefichwa na bati la gari lile linalofunika tairi...?
Aligeuka tena kushoto kwake.
Ile Raum ilikuwa inaondoka taratibu kutoka eneo lile; na sasa alimuona yule mtu mwenye tai, akiwa ndani ya gari akigeuka kutazama pale lilipokuwa gari la akina Jaka. Naye upesi aligeuka tena kutazama kule walipokuwa akina Jaka.
Jaka alikuwa ameegemeza sehemu ya mbele ya mwili wake kwenye boneti la gari lile akipokea funguo za gari kutoka kwa Clara aliyekuwa upande wa pili wa gari lile.
Akili ilizidi kumzunguka jamaa mwenye pama.
Ilikuwa haileti maana....kwa nini yule mtu, ambaye kwa hakika alikuwa akiwasubiri akina Jaka, aamue kuondoka baada ya watu aliokuwa akiwasubiri kutokea...bila ya kuongea nao chochote? Au...?
Hakufikiri zaidi.
Alikurupuka na kutoka kasi kukimbilia kule walipokuwa akina Jaka huku akimwita Jaka kwa kelele na akimpungia mikono ili amuone.
"Jaka...! Jakaaaaaaa! Toka hapoooo....tokeniiiih! Kimbienii....ondokaaaaa...uppeeeesssss!" Yule mtu alikuwa akipiga kelele huku akivuka barabara kuelekea kule walipokuwa akina Jaka.
Jaka aligeuka kwa mshituko aliposikia jina lake likiitwa kwa kelele hadharani. Na hata pale alipogeuka alimuona yule mtu mwenye koti refu akiingia barabarani huku akimkimblia bila kujali magari. Gari moja lilifunga breki kali na kuserereka huku tairi zake zikitoa sauti kali ya msuguano na lami huku honi kali ikirindima. Lile gari lilikuwa linaelekea kumgonga lakini yule mtu aliweka mkono wake wa kulia kwenye boneti la lile gari na kujisereresha juu ya boneti lile na kudondokea upande wa pili wa gari ile. Watu walioshuhudia tukio lile walipiga kelele za woga na mshituko juu ya kitendo kile hali wengine wakibaki midomo wazi na kujishika vichwa. Jamaa hakujali. Aliendelea kuwakimbilia akina Jaka huku akiwapigia kelele kama mwehu.
"Ondoka wewweeeh....! Kimbia...! You are going to die gaddemmiiiitt! Toka...! Hilo gariiii!"
Mara moja alimtambua John Doe. Alimuona alivyokuwa akiwaendea mbio huku akipunga mikono hewani na akipiga mayowe kama mwehu, na alishuhudia kwa mshituko jinsi alivyoruka juu ya boneti la gari lililokuwa kwenye mwendo wa kasi. Alipoona bado John Doe anazidi kuwakimbilia namna ile baada ya kukoswa kugongwa na gari, alijua ni lazima afanye kitu. Alisikia maneno yaliyokuwa yakitoka kinywani mwa yule mtu na aliiona hofu iliyojianika usoni kwa yule jamaa wakati akiwakimbilia namna ile. Jamaa alikuwa hafanyi utani.
Kutokea kule alipokuwa Jaka aligeuka na kuudaka mkono wa Clara na kumvuta pembeni huku na yeye akijisukuma kutoka ubavuni mwa lile gari kuelekea mbele ya lile gari. Clara alipiga kelele za hamaniko bila ya kuelewa kilikuwa kinatokea. Jaka alimkamata kiuno na kujitahidi kumvutia pembeni, mbali na lile gari lao. Walipepesuka vibaya huku raia waliokuwa eneo lile nao wakipiga kelele za kutoelewa.
Sasa John Doe alikuwa karibu sana na walipokuwa wakipepesukia. Jaka alijigeuza mzima mzima na kumkabili yule jamaa mwenye ngumi nzito huku akiwa amemkinga Clara kwa mgongo wake. Alikuwa akijitahidi kuongeza umbali baina yao na John Doe kwa kurudi nyuma huku akimsukuma Clara kwa nyuma. Watu wengi waliokuwa katika eneo lile walitawanyika mbio kila mmoja kwa upande wake bila ya kujua ni nini hasa walichokuwa wanakikimbia.
"Hilo gari hilo weweee...! Gariii! Kaa mbali naloo...ebbo! TOKA HAPOOO! Kimbieniii, Pummm-bbaaavvvv!" John Doe aliendelea kubwata huku akiwakimbilia. Jaka aliduwaa kidogo, na hapo John Doe alienda hewani mzima mzima akiwa ametanguliza mikono yake na kumkumba Jaka kwa kishindo, bega lake la kushoto likijikita tumboni kwa Jaka na wakati huo huo mkono wake wa kushoto uking'ang'ania kiunoni Clara aliyekuwa nyuma ya Jaka. Kwa wahka Jaka alirusha ngumi kwa mkono wake wa kushoto akiamini kuwa jamaa alikuwa anashambulia, lakini yule jamaa jabari aliipangua ngumi ile na hapo hapo akamdaka mkono ule kwa mkono wake wa kulia na wote watatu wakawa wanaelekea kupiga mweleka mzito.
Jaka hakuwa na la kufanya zaidi ya kung'ang'ania koti la yule mtu kwa mgongoni kwa mkono wake wa kulia. Nyuma yake, Clara akajigonga kisigino kwenye ukingo wa barabara na kupoteza kabisa mwelekeo. Alibaki akimng'ang'ania Jaka mgongoni huku akipiga kelele zisizoeleweka.
Msukumo wa yule mtu alivyowaparamia, na kujikwaa kwa Clara, viliwafanya wote watatu waruke hewani na kujibwaga bila mpangilio juu ya meza za wachuuzi wachache waliokuwa kando ya barabara ile. Mayowe yalizagaa wakati wao wakijipigiza chini kwenye vumbi wakisambaratisha meza na bidhaa zilizokuwa juu yake huku wale wachuuzi wakipiga mayowe na kukimbia hovyo. Jaka alikuwa akijaribu kujiinua kutoka pale chini akiwa amemlalia Clara kwa mgongo wake huku yule jamaa akiwa amemlalia kwa tumbo lake juu yake. Lakini kila alivyojaribu kujiinua ndivyo yule jamaa alivyozidi kumkandamiza chini kwa nguvu na ndivyo walivyozidi kumwelemea Clara aliyekuwa chini kabisa akipiga kelele vibaya sana.
Na mara hiyo hiyo mlipuko mkubwa sana ulisikika.
Jaka akiwa amekandamizwa chini na yule mtu aliweza kushuhudia kwa mshituko na kutoamini kukubwa kabisa jinsi gari lao likipasuka kuanzia sehemu ya mbele sanjari na mlipuko ule. Moto mkubwa uliruka hewani na aliliona lile gari likinyanyuliwa zima zima kutoka pale lilipokuwa limeegeshwa na kutupwa hewani huku likisambaratika vipande vipande. Vipande vya vioo vilirushwa huku na huko na kurudi ardhini kama matone ya mvua, vikijeruhi watu waliokuwa wamezagaa eneo lile. Tairi moja lilichomoka na kutupwa angani huku likiwaka moto na kufuka moshi.
Yote haya Jaka aliyaona ndani ya sekunde moja tu.
Macho yalimtoka pima na kinywa kilimchanua pasi sauti kutoka.
Mayowe, vilio na heka heka vilitawala eneo la Nyerere Square asubuhi ile. Watu walikibia huku na kule wakijaribu kuokoa maisha yao bila ya kujua ni wapi hasa palikuwa salama. Katika kelele zao hizo, Jaka alimsikia Clara akipiga mayowe ya woga na maumivu kutokea nyuma yake.
Clara likuwa amelalia mgongo pale chini. Juu alikuwa amelaliwa na mgongo wa Jaka. Juu ya Jaka John Doe alikuwa amelalia tumbo uso wake akiwa ameuficha upande wa kulia wa shingo ya Jaka huku akijikinga kichwa chake kwa mkono wake wa kushoto. Uso wa Jaka ulitokeza juu ya bega la kushoto la yule mtu ukitazama angani.
Na mara nyingine tena kilisikika kishindo kingine kilichotokana na mabaki ya lile gari kujibwaga tena ardhini katikati ya barabara na kulalia ubavu huku likiendelea kuteketea kwa moto. Watu walianza kulikimbilia na kulizunguka, hali wengine wakiwazunguka akina Jaka waliojirundika pale chini.
John Doe alijiinua kutoka pale chini, na haraka Jaka aliyechanganyikiwa naye akakurupuka kutoka pale chini. Alipepesuka na kuanguka tena chini. John Doe alimsaidia Clara kuinuka kutoka pale chini na kumshikilia asianguke kama Jaka. Uso wake ulionekana kutulia na kutokuwa na woga hata kidogo. Hatimaye Jaka aliinuka na kujivuta mpaka pale alipokuwa amesimama Clara huku macho yakiwa yamemtoka pima.
"Oh! Jaka...Jaka...tungekufa leo dear!" Clara alibwabwaja huku akilia. Jaka alimkumbatia kwa nguvu huku akimpigapiga mgongoni.
"Ni kweli. Lakini bado tunapumua...hatujafa...." Jaka alimliwaza huku macho yake yakiangaza huku na kule akimtafuta yule mtu mwenye koti refu ambaye alionekana kuyeyuka kama upepo mara Jaka alipomfikia Clara pale walipokuwa wamesimama. Kwa hakika yule mtu alikuwa amewaokoa kutokana na kifo kibaya sana, na sasa jumla ya maswali yaliyopita kichwani mwake ilikuwa haisemeki. Swali moja lilibaki kuwa kubwa kuliko yote.
Kwa nini?
"Imekuwaje...? Nini kimetokea...?" Alijikuta akibwabwaja peke yake huku akiendelea kutembeza macho kila kona bila ya mafanikio, kundi la mashuhuda liliowazunguka ulilifanya zoezi la kumuona yule mkombozi wao asiyetarajiwa kuwa gumu sana.
"Mlitegewa bomu....na wewe ndiye uliyekusudiwa." Sauti ilimjibu kwa upole kutokea nyuma yake. Aligutuka huku akigeukia kule sauti ilipotokea, na kumuona yule mtu mwenye koti refu. Alikuwa amesimama huku macho yake akiwa ameyaelekeza kule lilipokuwa linateketea lile gari.Yaani jamaa alikuwa amemjibu bila ya kumtazama na hakutaka kumtazama.
"Lakini wewe...? Kwa nini umeni...umetu....mbona... Ah! We' nani kwani...?" Jaka alibwabwaja huku akimkodolea macho yule mtu na akishindwa kabisa kuzipangilia sentesi zake. Mara ving'ora vya magari ya polisi vilisikika, na muda mfupi baadaye magari matatu ya polisi yalifika eneo lile kwa makeke. Askari wa jeshi la polisi waliruka kutoka kwenye magari yale na kuzidi kuwatia hofu wananchi waliojazana eneo lile.
ITAENDELEA