Riwaya : Mbwa wa Geti
Na Bahati Mwamba
hapohapo na hapo akili yake ikamrudisha saa chache nyuma kabla hajakutana na adha ile.
Ilikuwa hivi
Alishushwa chini kama kiroba,ni baada ya kuwekwa kichwa chini,miguu juu kwa zaidi ya siku mbili,huku macho yake yakiwa yapo gizani kwa sababu ya kufungwa na kitambaa usoni.
Licha ya kushushwa,chini lakini katu hawakumfungua mikono iliokuwa imefungwa nyuma kwa kutumia kamba ngumu.
Akiwa hivyo akasikia sauti za watu zikiongea na punde akanyanyuliwa na kukalizwa chini kama mtoto mdogo,huku macho yake yakiingiwa nuru baada ya kutolewa kitambaa.
Macho yake yalipata kuona watu Kama sita hivi wakiwa wamesimama wima mbele yake na bunduki zao mikononi,hawakuonekana kuwa kama watu wa kimasihara,mikono yao ilijazia nyama,na vifua vyao vilikuwa vimetuna mithilia ya wacheza mieleka nchini marekani.
Aliwatizama tena watu wale mbele yake,lakini macho yake hayakupeleka idadi ile kama ilivyo,bali ikaongeza idadi nyingine ya watu zaidi ya watano wakiwa wamefungwa kwenye viti huku wakionekana dhahiri wakiwa zoofu kwa mateso ama njaa waliokuwa nayo watu wale.
Macho yake yakatamani kuona zaidi pale ndani,akageuza shingo yake kushoto na kisha kulia na hapo akakutana na idadi nyingine ya watu wakiwa wamefungwa kwa kuninginizwa kichwa chini miguu juu,huku wakiwa wanapepea to kwenye kamba zile zilizokuwa zimefungwa juu kwenye dali na pale walipokuwa palionesha kuwa kama ni godauni flani kutokana na ukubwa wa jengo lile.
Akashusha pumzi nyingi na kuzivuta, hapo pua zake zikakutana na harufu ya uozo wa kitu na akili ikamwambia uozo huo upo hapo hapo ndani,akatambaza tena macho yake.
Kutoka pale alipokaa akaona kwa mbele yake kuna mzoga,mzoga wa mtu aliekufa na funza walikuwa wanamtambaa mwilini mwake.
Akatamani kutapika,ila tumbo likamsaliti likaunguruma kwa njaa,na koo lilikuwa limekauka na lilihitaji maji,akameza mate,kisha akawatazama wale watu waliokuwa wamesimama mbele yake,ambao walikuwa na afya nzuri kuliko watu waliokuwa mle kama mateka,watu wale hawakuonekana kujali na ndo kwanza walitoa kicheko,kicheko cha kejeli,kejeli ya wazi kabisa ikautesa moyo wake,akatamani afunguliwe zile kamba na awaoneshe shuguli lakini nafasi hiyo haikutokea kabisa.
*****
Lango la godauni ile likafunguliwa na akiwa sasa amekalishwa kwenye kiti na kufungwa kama wale watu wengine aliowaona,akapata kushuhudia mtu mmoja akiingia na nyuma akiwa amezungukwa na walinzi kama saba hivi.
Mtu yule alimfahamu,alimfahamu kwa sababu alikuwa ni kijana mwenzie na alikuwa ni kijana mwenye pesa chafu mjini Dodoma.
Alimfahamu kwa kuwa alikuwa ni mume mwenzie,alimfahamu kwa kuwa alikuwa amefanikiwa kumpokonya mwanamke wake na alifanikiwa kuisambaratisha familia yake.
Uchungu ulimkaa kooni,akatamani kumvamia na kumsushia makonde,lakini hakuweza alikuwa na njaa na pia alikuwa amefungwa sawia kwenye kiti kwa kamba imara na wagungaji walijua kazi yao.
Alimuona kijana yule akizidi kumkaribia huku usoni akiwa ameweka tababasamu la dhihaka,tabasamu bandia,tabasamu la kidhalimu.
“Zedi Wimba,huna jipya komando wa zamani,huna jipya ndugu yangu ,na jilaumu kwa kiherehere chako,unataka mke mzuri wakati pesa huna,eeh hebu kuwa makini siku nyingine,kuna namba za kurukia ila si hii niliovaa mimi.
Zedi Wimba alimtizama kijana huyu aliekuwa akiongea kwa tambo ,huku akiwa kasimama mbele yake mikono mfukoni,alimtizama bila japo kupata sauti ya kuunguruma mbele yake,uchungu ulikitawala kinywa chake na akabaki kumtizama tu bwana yule mwenye tambo za ajabu.
“Zedi nitakunyanyasa wewe na familia yako,nitakunyanyasa Kama ulivyomnyanyasa baba yangu hadi ukampa umauti,Zedi hustahili kuishi ila kabla sijakuua lazima uyaone mateso ya damu yako,kisha ujue vile inauma…”
Zedi akimtizama tena kijana yule,alikuwa anaongea kwa kujiamini,lakini kicho fanya amtizame tena ni vile kusikia akimlaumu kwa mauji ya baba yake,na hapo swali likamjia kichwani mwake
Ina maana si mapenzi tena,kumbe ni kisasi,sasa mbona amezunguka sana,na baba yake ni yupi
Aliona hawezi kujiuliza wakati wa kumjibu yupo mbele yake,akaamua kumuuliza
Baba yako ni nani,na kwanini usiniue mimi tu ukaamua kuitesa na familia yangu?
Kijana yule akacheka kicheko cha dharau kisha akamwinamia kama anabembeleza mtoto akasema
“Baba yangu ni Ibra Mbaya,yule uliemuua miaka sita nyuma,na ukadhani yameisha ulijidanganya Zedi.
Naitwa Kabah Mbaya,ni mtoto wa pekee wa hayati Ibra Mbaya…”
Baada ya maelezo hayo mafupi Zedi akabaki mdomo wazi,alimjua Ibra,alimjua kwa unyama wake ila hakujua kama Ibra aliacha damu kama yake,damu ya maovu.
Zedi akatulia tuli juu ya kiti na aliona hatari ilio mbele yake kwa kuingia mikononi mwa mtu kama yule.
Hakujua kama yote yanamkuta kwa sababu ya kisasi yeye alijua ni Vita,vita ya mapenzi kumbe ilikuwa ni Vita alioingia bila tahadhari na matokeo yake yupo mikono isio salama.
Sesa!! Hilo jina likamwijia kichwani,akakurupukakama anaetaka kukata kamba lakini akatulizwa kwa ngumi safi iliojaa katikati ya kifua chake na kisha ikamwacha akiugulia maumivu.
Sesa lilikuwa jina la mtoto wake wa kiume,mtoto wa pekee kwake mke wake.
Zedi machozi yalianza kushuka kwenye mashavu yake,hakujua hali ya mwanae,hakujua yupo na nani wakati huo.
Kabah akimtizama kwa dharau kisha akatema mate sakafuni na kwa ishara akaashiria mlinzi wake mmoja ampe bakora aliokuwa ameweka kiunoni,baada ya kupewa akaanza kumchapa Zedi kama mtoto,alimchapa bila kujali anamchapa eneo gani.
Zedi alilia kwa uchungu kwa bakora zile kutoka kwa Kabah,lakini Kabah hakuonesha kujali kitu.
Kabah aliporidhika na kipigo kile,akavua shati na kuwapa vibaraka wake,kisha akaanza kurusha makonde mazito kwenye mwili wa Zedi,Zedi aligeuzwa punching bag na Kabah.
Baada ya dakika kumi za kutoa kipigo kabah alikuwa ameloa jasho mwili mzima huku Zedi akiwa anavuja damu usoni na midomo yake ilikuwa imechanika,alinyanyua uso kumtazama Kabah akaona Kabah anatabasamu,tabasamu la ushindi.
Mwiteni dokta
Kabah aliamrisha huku Zedi akiwa hajui dokta anaeitwa ni wa nini,lakini hakuwa na nguvu za kufanya lolote akaamua kusubiri kitakachojiri,huku macho yake yakiwa bado yanawatazama wale watu waliokuwa wamefungwa kama yeye wakiwa hawajiwezi.
Like,coment twende sawa