RIWAYA: Mifupa 206

Haka kajamaa kayeyushaji tu, kashawaona ninyi ni makolo wake, mkalambe miguu kenyewe ndo kanajisikia furaha. Funga thread yako hii hadith kawasimulie wanao kitandani
 
Haka kajamaa kayeyushaji tu, kashawaona ninyi ni makolo wake, mkalambe miguu kenyewe ndo kanajisikia furaha. Funga thread yako hii hadith kawasimulie wanao kitandani
Mkuu bora kuvumilia kuliko koikosa hii stor
 
Hey you GAY no body brought you here you. Don't try to use me as your ladder for fame. Hapa hatununui matak... kwa hali ya kawaida nahisi unataka kutoa namba yako ushughurikiwe lakini naamini wasomaji wote aren't for that business you're trying to promote. Save your ass pliz
Mkuu the banker huu muda ungetupia stories badala ya kuzozana na watu ingependeza sana.Nilipoona new alert nikaja speed nikijua umetupia!
 
baadhi yakiwa ni maduka ya kampuni kubwa na maarufu za jijini Dar es Salaam na
mengine maduka ya watu binafsi. Maduka yale ya kisasa yalikuwa yamezungukwa
na kuta kubwa za vioo visafi vinavyomwezesha mtu yeyote kuweza kuona bidhaa
zilizokuwa ndani ya maduka yale.
Ile korido ya mbele ilikuwa ikielekea katika Supermarket kubwa ya kisasa iliyokuwa
na bidhaa nyingi za matumizi ya kawaida ya binadamu yenye wahudumu waliovaa sare
maalum za kuwatambulisha na vitambulisho vyao vikiwa vimening’inizwa kwa kamba
maalum shingoni. Ile korido ya upande wa kulia ilikuwa ikitazamana na maduka
mengi ya bidhaa tofauti zikiwemo ofisi za kampuni za mawasiliano ya mitandao ya
simu. Koplo Tsega akajikuta akiyakumbuka vyema maelezo ya Aden Mawala yule
meneja wa benki ya Zanzibar Marine kuwa duka la Zanzibar Stone City Bazaar
lilikuwa likitazamana na duka la vinyago la Afrikan art craft mle ndani. Hivyo Koplo
Tsega akashika uelekeo wa upande wa kulia akiifuata ile korido iliyokuwa ikitazamana
na maduka mbalimbali.
Kulikuwa na watu wengi katika korido ile huku kila mmoja akionekana kuzama
katika hamsini zake. Koplo Tsega wakati akitembea akawa akiyatembeza macho
yake taratibu kuzichunguza sura za watu aliokuwa akipishana nao kwenye korido ile.
Hakumuona mtu yeyote wa kumtilia mashaka ingawa baadhi ya watu hawakujizuia
kumtazama huku dhahiri wakionekana kuvutiwa na mtindo wa uvaaji wake kama siyo
weusi wake wa asili.
Ilikuwa ni wakati Koplo Tsega alipokuwa mbioni kufika mwisho wa korido ile
pale alipoliona duka kubwa la vinyago lenye maandishi makubwa ya African art craft
upande wa kushoto. Ndani ya duka lile kulikuwa kijana mmoja aliyekuwa akiwaelekeza
jambo wazungu wawili,mwanamke na mwanaume waliokuwa wakikitazama kinyago
kimoja kikubwa cha kimakonde cha mti wa mpingo cha mwanamke wa kiafrika
aliyebeba mtoto wake mgongoni kwa mbeleko. Kinyago kizuri kilichochongwa kwa
umakini wa hali ya juu.
Koplo Tsega alipolifikia lile duka la vinyago akasimama mbele yake na
kuyatembeza macho yake taratibu upande wa kulia. Maelezo ya yule meneja wa
benki ya Zanzibar Marine yalikuwa sahihi kwani duka la Zanzibar Stone City Bazaar
lilikuwa likitazamana na duka lile la African art craft kwa upande wa kulia. Kwa dakika
kadhaa Koplo Tsega akasimama akilitazama duka lile kwa utulivu kama mtu ambaye
hayaamini vizuri macho yake.
Duka la Zanzibar Stone City Bazaar lilikuwa ni miongoni mwa maduka
yaliyokuwa na pilikapilika nyingi za wateja baadhi wakiingia mle ndani na kutazama
bidhaa zilizokuwa mle ndani huku wengine wakifanya manunuzi ya bidhaa. Lilikuwa
ni duka kubwa lenye maduka mengi madogo madogo ndani yake ya bidhaa kama
nguo,simu,vyakula,vyombo vya nyumbani,vifaa vya umeme,vitabu,vifaa vya
maofisini,viatu,mikoba na vifaa vingine muhimu vya mahitaji ya binadamu. Hata hivyo
wateja wengi waliokuwa ndani ya maduka yale walikuwa wanawake ambao wengi
wao walionekana kuvutiwa zaidi na bidhaa kama nguo,viatu,mikoba na vyombo vya
nyumbani.
Fikra za mtu aliyekuwa akifahamika kwa jina la White Sugar zikiwa zimeanza
kujengeka upya kichwani mwake Koplo Tsega akaanza taratibu kuzitupa hatua
zake akielekea kwenye lile duka la Zanzibar Stone City Bazaar huku akigeuka na
kuyatembeza macho yake huku na kule katika namna ya kuhakikisha kuwa hakuna
mtu yeyote aliyekuwa akizifuatilia nyendo zake. Wakati Koplo Tsega akiufikia mlango
wa duka lile pale mlangoni akapishana na mwanaume mmoja mrefu na mweusi akiwa
katika mavazi yake ndhifu ya suti ya kijivu ya Marks & Spenser,shati la rangi nyeusi na
tai ya rangi ya zambarau.
Mtu yule alikuwa amenyoa upara na macho yake alikuwa ameyafunika kwa miwani
kubwa nyeusi yenye kumwezesha kuiona dunia pasipo usumbufu wowote. Mkononi
alikuwa amevaa saa ya gharama sana ya dhahabu aina ya Maurice Lacroix huku akiwa
amebeba briefcase nyeusi inayotumia mfumo wa codenumber maalum katika kuifungua.
Miguuni alikuwa amevaa viatu vyeusi nadhifu vya ngozi huku marashi yake ya gharama
yenye harufu nzuri ya tafsiri ya ukwasi yakiongeza ziada nyingine katika utanashati
wake.
Akionekana ni mwenye haraka mara tu mtu yule alipopishana na Koplo Tsega pale
mlangoni akaanza kutembea kwa kuharakisha akishika uelekeo wa upande wa kushoto
wa ile korido pana mbele ya lile duka huku mara kwa mara akiunyanyua mkono
na kuitazama ile saa yake ya mkononi kama mtu aliyekuwa nyuma ya muda katika
tukio fulani. Kwa sekunde kadhaa Koplo Tsega akajikuta amesimama pale mlangoni
na kumtazama yule mtu namna alivyokuwa akitokomea kwenye ile korido kama
kimbunga kisha akageuka na kuingia mle ndani ya lile duka huku akiyapuuza macho
ya watu waliokuwa wakimtazama eneo lile kana kwamba alikuwa amebabaishwa na
kutekwa na muonekano wa yule mwanaume aliyetoka kwenye lile duka.
Jina la White Sugar likiwa limerudi tena kwenye fikra zake mara tu alipoingia
ndani ya lile duka Koplo Tsega akajisogeza upande wa kulia sehemu kulipokuwa na
duka la simu za mkononi za kisasa zilizopangwa ndani ya rafu nzuri ya vioo. Kijana
mmoja wa kiume aliyekuwa akihusika na biashara ile haraka akasimama kutoka
kwenye kiti alichoketi nyuma ya ile rafu ya vioo na kusogea karibu na Koplo Tsega
kama afanyavyo kwa wateja wengine waliokuwa wakiingia mle ndani na kuonekana
kuvutiwa na bidhaa zake.
“Mambo vipi dada?’’ yule kijana akamsalimia Koplo Tsega kwa makeke
“Poa” Koplo Tsega akaitikia huku usoni akiumba tabasamu la kirafiki
“Karibu sana”
“Ahsante” Koplo Tsega akaitikia huku akigeuka na kuyatembeza macho yake
kuzichunguza sura za watu waliokuwa mle ndani kabla ya kuyarudisha tena mbele
yake na kuanza kuzitazama simu zilizokuwa ndani ya ile rafu ya vioo ingawa dhahiri
mawazo yake hayakuwa katika zile simu. Yule kijana muuzaji wa lile duka kuona vile
akasogea karibu akijitahidi kuyapatiliza kwa ukaribu macho ya Koplo Tsega. Koplo
Tsega alipoyainua macho yake kumtazama yule kijana akavunja ukimya akiuliza swali
la hila.
“Hili ndiyo duka la Zanzibar Stone City Bazaar?”
“Maduka ya humu ndani yote ni ya Zanzibar Stone City Bazaar” yule kijana
akafafanua huku akishindwa kuelewa hoja muhimu katika swali lile.
“Ninashida na meneja wa hili duka,unaweza kunisaidia nikaonana naye?’’Koplo
Tsega akamuuliza yule kijana kwa utulivu huku akimtongoza kwa tabasamu lake
maridhawa.
“Shida gani?’’ yule kijana akauliza huku akimtazama Koplo Tsega kwa udadisi
“Shida binafsi inayohusu biashara” Koplo Tsega akadanganya huku akimtazama
yule kijana kwa makini.
“Umepishana naye sasa hivi pale mlangoni wakati ulipokuwa ukiingia humu
ndani” jibu la yule kijana likapelekea mshtuko mkubwa kwa Koplo Tsega,moyo wake
ukalipuka kabla ya baridi nyepesi kuanza kusafiri mgongoni mwake huku kijasho
chembamba kikichomoza taratibu katika sehemu mbalimbali za mwili wake na
hatimaye utulivu kupotea kabisa moyoni mwake ingawa alijitahidi kuumeza mshtuko
ule kwa kila hali.
Kwa sekunde kadhaa akili ya Koplo Tsega ilishindwa kabisa kuamini kuwa yule
mwanaume aliyepishananaye muda mfupi pale mlangoni wakati akiingia kwenye lile
duka ndiye angekuwa White Sugar,mtu aliyekuwa akimtafuta. Koplo Tsega akajikuta
akishawishika kuwa muda uleule atoke kwenye lile duka na kuanza kutimua mbio
akashika ule uelekeo wa yule mtu kule alikotokomea. Hata hivyo baada ya kufikiri kwa
kina Koplo Tsega akajikuta akiuweka kando mpango ule pale alipohisi kuwa kwa ule
muda uliopita yule mtu angeweza kuwa tayari amekwishafika mbali sana na eneo lile
kwa vile alivyoonekana kuwa na haraka ya kupita kiasi istoshe hakufahamu mtu yule
alikuwa akielekea wapi.
“Oh! masikini mimi nimekuwa mzembe kwa kuchelewa” Koplo Tsega akalaani
kitendo kile huku akishindwa kuamini.
“Kwani hamfahamiani?” yule kijana akauliza
“Hatufahamiani ila kuna mtu anayefahamiana naye ndiye aliyenielekeza kwake”
Koplo Tsega akadanganya wa hila
“Pole sana basi uache business card yako ili siku atakaporudi nimpe akutafute”
yule kijana akatoa wazo huku akimtazama Koplo Tsega katika mtazamo wa kimapenzi
hata hivyo Koplo Tsega akampuuza.
“Bahati mbaya sana leo nimesahau kutembea na business card yangu. Kwani
hatorudi tena leo?” Koplo Tsega akamuuliza yule kijana
“Hapana hatorudi tena na imekuwa ni bahati sana kumuona kirahisi namna
ile kwani mara nyingi sana huwa yupo safarini nje ya nchi” yule kijana akaendelea
kutanabaisha na Koplo Tsega alipomtazama akagundua kuwa maelezo yake yalikuwa
yamekomea pale katika kumfahamu White Sugar na ile ndiyo ilikuwa salama yake.
“Ameelekea wapi?” Koplo Tsega akauliza kwa utulivu huku akimtazama yule
kijana kwa makini.
“Anawahi boti ya kuelekea kisiwani Zanzibar”
“Kwani anaishi Zanzibar?”
“Ndiyo maskani yake yalipo’’ yule kijana akafafanua huku akionekana kuwa na
hakika na maelezo yake na hapo kitambo kifupi cha ukimya kikafuata huku Koplo
Tsega akizidi kujilaani kwa namna alivyopishana na bahati ile pasipo kujua. Mwishowe
akavunja ukimya kuuliza
“Unaweza kunisaidia namba zake za simu?’’
“Namba zake za simu nilizonazo ukimpigia huwa hapatikani” yule kijana
akaendelea kufafanua na kupitia maelezo yake Koplo Tsega akatambua kuwa
asingeweza kupata ziada nyingine kutoka kwake hivyo haraka akaunyanyua mkono
na kuitazama saa yake ya mkononi na alipomaliza na kuyahamishia macho yake kwa
yule kijana akaumba tabasamu jepesi lisilo na maana yoyote usoni mwake kabla ya
kuvunja ukimya
“Nashukuru sana wacha niende nitakuja siku nyingine”
“Pole sana dada yangu kama vipi niachie namba yako ya simu ili siku yoyote
atakaporudi nikufahamishe” yule kijana akasisitiza akijaribu bahati yake na Koplo
Tsega alipomtazama akayaona macho yake yalivyojawa na uchu wa ngono hali
iliyompelekea atabasamu kidogo na kuanza kumtajia namba ya simu ya kufikirika
kichwani isiyopatikana. Yule kijana akawahi kuinakili haraka ile namba kwenye simu
yake na wakati alipomaliza kubofya tarakimu ya mwisho na kuinua macho yake
kumtazama Koplo Tsega mbele yake,Koplo Tsega tayari alikuwa amekwisha toka nje
ya lile duka na kutokomea.
 
TAARIFA ZA KUUAWA KWA MENEJA wa benki ya Zanzibar Marine tawi la
jijini Dar es Salaam lilipo eneo la Morocco zilikuwa zimesambaa haraka kama ubuyu
na kuvifikia vyombo vya usalama. Ndani ya dakika chache baada ya mwili wa meneja
wa ile benki kugundulika ofisini kwake taarifa kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa
benki ile haraka zilikuwa zimekifikia kituo cha polisi cha Oysterbay kilichokuwa na
dhamana ya kusimamia usalama wa eneo lile. Mkuu wa kituo kile cha polisi alipofika
eneo la tukio na kutathmini mazingira ya tukio zima akaamua kuomba nguvu ya
wataalam wa kuchukua vipimo na alama za mwalifu kutoka makao makuu ya jeshi
la polisi. Taarifa zilipoyafikia makao makuu ya jeshi la polisi juu ya ombi la wataalam
wake kutokana na unyeti wa tukio lenyewe,taarifa hizo zikawa zimevuja na kuwafikia
vijana wa Sulle Kiganja waliokuwa wamepandikizwa kila kona katika kuhakikisha
kuwa mhusika wa mauaji ya wanausalama yaliyokuwa yakiendelea jijini Dar es Salaam
anakamatwa.
Hivyo Sulle Kiganja na vijana wake wa kazi wakawa ndiyo watu wa kwanza kufika
katika eneo la tukio ndani ya ofisi ile ya meneja wa benki ya Zanzibar Marine yale
mauaji yalipotokea.
Kamera za usalama za CCTV zilizokuwa zimefungwa katika kila pembe ya lile
jengo la benki ya Zanzibar Marine ikiwemo kamera iliyokuwa ndani ya ofisi ya meneja
wa ile benki aliyouwawa zilikuwa zimehifadhi kumbukumbu ya matukio yote muhimu
ya mtu aliyesemekana kuhusika na kifo cha meneja wa benki ile. Sulle Kiganja na vijana
wake wa kazi baada ya kumaliza kupitia picha zote zilizonaswa na kamera za usalama
za jengo lile chini ya mkuu wa idara ya teknolojia ya mawasiliano (IT) akajiridhisha
na kuhitimisha kuwa muuaji alikuwa ni mwanamke mwenye umri kati ya miaka
ishirini na sita hadi thelathini ingawa sura yake haikuweza kuonekana vizuri kutokana
na miwani ya jua aliyoivaa na kofia ya Sombrero aliyojifunika kichwani. Msichana
mwembamba mwenye umbo kakamavu akiwa amevaa pullneck nyeusi,shati gumu
la jeans,suruali ya jeans iliyolichora vyema umbo lake,viatu vya rangi ya udongo aina
ya Travolta miguuni huku akiwa amebeba begi jeusi,jembamba na refu mgongoni
lisiloeleweka kuwa na kitu gani ndani yake.
Hata hivyo kulikuwa na mambo mawili matatu yaliyokuwa yamemchagiza Sulle
Kiganja wakati alipokuwa akizipitia zile picha za matukio ya muuaji zilizonaswa
na kamera za usalama za ile benki. Kwanza kabla ya kuanza kupitia picha zile za
matukio moja kwa moja alikuwa ameamini kuwa kwa vyovyote muuaji angekuwa ni
mwanaume tena kwa hakika angekuwa ni Chaz Siga mwanaume aliyewatoroka siku
ile chini ya lile jengo la ghorofa lililopo kule maeneo ya posta kwani uchunguzi wa
awali wa matukio yote ya mauaji yaliyokuwa yakiendelea kufanyika jijini Dar es Salaam
yalikuwa na viashiria vilivyokuwa vikimhusisha yeye kwa namna moja au nyingine.
Lakini kitendo cha kuziona picha zile za muuaji zilikuwa ni za msichana kilikuwa
kimeutibua vibaya ubongo wake na kutengeneza ukinzani mkubwa katika mwenendo
wa mikakati yake ya kumnasa muuaji.
Vilvile picha za matukio ya mauaji yale zilizonaswa na kamera za usalama za ile benki
zilikuwa zimeonesha kuwa kulikuwa na namna ya maongezi ya kawaida yaliyofuatiwa
na majibishano makali kati ya yule mwanamke aliyeingia ndani ya ile ofisi ya meneja
wa benki na yule meneja wa ile benki kabla ya mauaji yale kufanyika. Mabishano yale
kati ya yule muuaji na meneja wa ile benki baadaye yakawa yamepelekea yule dada
muuaji kutoa karatasi fulani kutoka kwenye bahasha iliyokuwa kwenye mfuko mmoja
wa suruali yake ya jeans na kuisogeza pale mezani katika namna ya kumtaka yule
meneja wa benki asome kile kilichokuwa kimeandikwa kwenye karatasi ile. Ingawa
kamera zilionesha kuwa mara baada ya meneja wa ile benki kumaliza kusoma kile
kilichokuwa kimeandikwa kwenye karatasi ile alionekana kukataa kukubaliana nacho
lakini tukio lile lilikuwa limeibua maswali mapya kichwani kwa Sulle Kiganja kuwa
muuaji hakuwa mwendawazimu kama walivyokuwa wauaji wengine wasio na sababu
katika kutekeleza unyama wao bali alionekana kuwa na hoja fulani ya kusimamia
ambayo bila shaka ilikuwa imejificha kwenye karatasi ile.
Zile picha za matukio bado ziliendelea kuonesha kuwa mara baada ya yule meneja
wa benki kuonekana kutokukubaliana na kile kilichokuwa kimeandikwa kwenye
ile karatasi iliyotolewa mfukoni kutoka kwenye bahasha. Yule dada muuaji alikuwa
ameichukua ile karatasi na kuitia kwenye bahasha kabla ya kuirudisha mfukoni kisha
kukafutiwa na kitambo kingine cha maongezi ya majibishano makali kabla ya yule
dada muuaji kutoa tena bahasha nyingine kutoka katika mfuko mwingine wa suruali
yake ambapo alipoifungua alitoa vipande vya karatasi vinavyolingana na kuvisogeza
karibu na meneja wa ile benki juu ya ile meza ya ofisini iliyokuwa mle ndani. Kufikia
pale Sulle Kiganja akawa amemuomba mkuu wa idara ya teknolojia ya mawasiliano
wa ile benki ambaye ndiye aliyekuwa na dhamana ya kusimamia ufanyaji wa kazi wa
zile kamera za usalama za ile benki aivute kwa karibu taswira ya vile vipande vya
karatasi vilivyokuwa vimewekwa pale mezani na yule muuaji na hatimaye kuikuza
taswira yake. Picha ya karibu iliyoonekana ikathibitisha kuwa vipande vile vya karatasi
vilivyowekwa pale mezani na yule muuaji zilikuwa ni hundi na hundi zile zilikuwa ni
za ile benki ya Zanzibar Marine. Sulle Kiganja akazidi kuingiwa na mashaka kuwa
kulikuwa na jambo la hatari zaidi lililokuwa limefichika hadi kupelekea mauaji ya
meneja wa ile benki.
Halafu taratibu Sulle Kiganja alipokuwa akiendelea kuzipitia zile picha hoja
nyingine zikawa zikiendelea kuibuka kichwani mwake. Kamera ziliendelea kuonesha
kuwa mara baada ya yule meneja wa ile benki kumaliza kuzipitia zile hundi zilizowekwa
pale mezani na yule muuaji bado meneja wa ile benki alionekana kukataa kukubaliana
na hoja ya muuaji kiasi cha kumpelekea yule muuaji kuzichukua zile hundi na
kuzirudishia kwenye bahasha yake na hatimaye kuzitia mfukoni. Yule muuaji wakati
akishughulika na kuitia ile bahasha mfukoni kamera zikaendelea kuonesha kuwa yule
meneja wa benki alikuwa akiupeleka mkono wake taratibu kwa hila kuufungua mtoto
wa meza yake ya ofisini kabla ya hila yake kushtukiwa na kusukumiwa ile meza ya
ofisini iliyombana vyema huku akiwa ameketi kwenye kile kiti chake cha ofisini.
Kitendo cha Sulle Kiganja kumuona muuaji akisimama ghafla na kuichomoa bastola
yake mafichoni akimwendea yule meneja wa benki pale kwenye kile kiti alipobanwa
na ile meza ya ofisini kikawa kimempelekea awe makini na kuzidi kusogea karibu
kulitazama tukio lile. Muuaji alikuwa ameishtukia mapema dhamira ya yule meneja
wa benki wakati alipokuwa akiuvuta ule mtoto wa meza kwa hila kwani yule muuaji
alipofika pale kwenye meza na kupenyeza haraka mkono kwenye ile droo na mkono
ule ulipotoka ulikuwa na bastola ambapo yule muuaji haraka akachomoa magazini ya
ile bastola aliyoitoa kwenye mtoto wa ile meza na kuitupa mle ndani sakafuni. Tukio
lile likamaanisha kuwa yule meneja wa benki alikuwa akitaka kuichukua ile bastola kwa
hila ili aweze kujihami dhidi ya yule muuaji. Hoja nyingine ikaibuka kichwani kwa Sulle
Kiganja akijiuliza kama meneja wa ile benki alikuwa akimiliki ile bastola kwa kufuata
misingi ya sheria au lah!.
Matukio mengine yaliyofuata kupitia zile kamera za usalama za ile benki
zilimuonesha yule muuaji namna alivyokata waya wa simu ya mezani ya mle ndani
ofisini kabla ya kuutumia waya ule kumkaba shingoni yule meneja wa benki huku
akimshinikiza kufanya jambo fulani kwenye ile kompyuta yake ya mezani. Kamera
bado ziliendelea kuonesha kuwa bado yule meneja wa benki hatimaye aliamua kukubali
na kutekeleza kile alichoshinikizwa kukifanya kabla ya kuonekana akishughulika
na kompyuta yake na baadaye kuonekana akiprint taarifa fulani. Kufikia pale Sulle
Kiganja akamuomba tena yule mtaalam wa teknolojia ya mawasiliano wa ile benki
kuvuta karibu ile picha ya ile karatasi iliyotoka kwenye ile printer ya mle ndani na
kuyakuza maandishi yake. Taswira ile ilipopatikana vizuri afisa mwingine wa ile benki
aliyekuwa nyuma yao akahitimisha kuwa taarifa ile iliyotolewa na printer ilikuwa ni
taarifa iliyofahamika kitaalam kama Bank cash flow ya ile benki ya Zanzibar Marine
na taarifa nyingine iliyofuatia kutolewa na ile printer ilikuwa ni Bank statement na
taswira yake iliposogezwa karibu jina la Zanzibar Stone City Bazaar likasomeka kwa
ufasaha kiasi cha kumpelekea Sulle Kiganja kuupindisha mdomo wake kwa dharau.
Kisha akamgeukia yule afisa wa benki aliyekuwa muda wote amesimama nyuma yao
akiufuatilia ule mchakato kwa makini ndani ya kile chumba kidogo cha mtaalam wa
teknolojia ya mawasiliano wa ile benki,kijana mdogo na mtundu wa kompyuta.
“Cash flow statement na Bank statement zina maana gani kwako?”
“Cash flow statement ni taarifa ya benki inayoonesha kiasi cha pesa kilichoingia
na kutoka kwenye benki kwa muda wa mwezi mmoja wakati Bank statement ni ripoti
inayotolewa na benki katika tarehe maalum kila mwezi ambayo ndani yake huorodhesha
matukio yote ya kuweka na kutoa pesa kwenye akaunti yaliyofanyika,hundi zilizolipwa
kama zitakuwepo,riba iliyotozwa na makato ya huduma za benki au faini zilizotozwa
kwenye akaunti husika” yule afisa wa benki akafafanua kwa ufasaha.
“Kupitia hiyo Cash flow statement na hiyo Bank statement ambazo meneja wa
benki yenu alionekana kushinikizwa kuziprint unadhani muuaji alitaka kufahamu
nini?” Sulle Kiganja akamuuliza tena yule afisa wa benki kwa utulivu huku akiendelea
kuzitazama zile picha za matukio kwa makini kwenye zile kamera.
“Sina hakika ingawa nahisi kuwa huwenda alikuwa akitaka kufahamu pesa fulani
iliyokuwa imeingia kwenye hii benki na kutoka pamoja na jina la mhusika wa akaunti
iliyotumika kufanya muamala huo” Sulle Kiganja akageuka na kumtazama kwa makini
yule afisa wa benki kama mtu afikiriaye jambo fulani kisha akawa ni kama aliyeona
kuwa hapakuwa na swali jingine la ziada la kumuuliza tena yule mtu kwa wakati ule.
“Okay! nashukuru sana kwa ushirikiano wenu” hatimaye Sulle kiganja
akawashukuru yule afisa wa benki na yule mtaalam wa teknolojia ya mawasiliano wa
ile benki kisha akasogeza kiti nyuma na kusimama.
“Ningependa kumuona huyo mfanyakazi wenu wa idara ya huduma kwa wateja
anayesemekana kuwa ndiye aliyemkaribisha huyu mtuhumiwa wa mauaji pamoja
na huyo mwanaume aliyemuona muuaji wakati alipokuwa akitoka kwenye ofisi ya
meneja wa benki” Sulle Kiganja akasisitiza akiyakumbuka maelezo ya awali aliyokuwa
amepewa na yule afisa wa benki wakati alipofika. Kisha akaanza kuondoka taratibu
kwenye ile ofisi ya idara ya teknolojia na mawasiliano huku akiwa ameongozana na
vijana wake kuelekea kwenye ile ofisi ya meneja wa ile benki yale mauaji yalipotoke.
Muda mfupi uliyofuata Sulle Kiganja na vijana wake walikuwa ndani ya ile ofisi ya
meneja wa benki. Alipofika mle ndani akawakuta vijana wake wakiendelea kuchukua
vipimo maalum vya kiuchunguzi mle ndani na kutoka katika ule mwili wa yule meneja
wa benki ukiwa bado haujaondolewa pale kwenye kile kiti chake cha ofisini huku
kifuani akiwa amelowa damu nyingi iliyokuwa ikiendelea kuvuja taratibu kutoka
kwenye yale majeraha ya risasi kifuani mwake.
Dakika chache baada ya Sulle Kiganja kuingia mle ndani ya ile ofisi ya yule meneja
wa ile benki yule dada mlimbwende mfanyakazi wa ile idara ya huduma kwa mteja
na yule mwanaume aliyepishana na Koplo Tsega mlangoni wakati ule alipokuwa
akitoka kwenye ile ofisi ya meneja wa benki nao wakaingia mle ndani. Sulle Kiganja
alipogeuka na kuwatazama wale watu sura yake ikatengeneza tabasamu jepesi kabla
ya kuwapa mkono na kusalimiana nao na baada ya pale mahojiano mafupi yakafuatia
huku akianza na yule dada mlimbwende mfanyakazi wa idara ya huduma kwa wateja
wa ile benki.
“Naitwa Sulle Kiganja mimi ni afisa usalama ningependa kusikia maelezo
machache muhimu kutoka kwako kufuatia hili tukio la mauaji ya meneja wa benki
yenu wewe ukiwa kama mtu aliyepata nafasi ya kumuona muuaji kwa ukaribu zaidi na
kuzungumza naye machache” Sulle Kiganja akafafanua.
“Naitwa Bi.Husna Mansour,afisa wa idara ya huduma kwa wateja wa benki hii”
yule dada mlimbwende akajitambulisha huku machozi yakimlengalenga.
“Ulionana na mwanamke aliyeingia humu ndani kabla ya mauaji haya kutokea?”
Sulle Kiganja akauliza huku akimtazama Bi.Husna Mansour kwa utulivu.
“Ndiyo”
“Ilikuwa saa ngapi”
“Kati ya saa saba na nusu mchana hadi saa nane” Bi.Husna Monsour akaongea
kwa utulivu huku akijifuta machozi kwa kitambaa chake mkononi.
“Umewahi kumuona popote hapo kabla?”
“Hapana” Sulle Kiganja akamtazama Bi.Husna kwa utulivu kabla ya kuendelea.
“Huyo mwanamke alikwambia shida iliyomleta hapa kukutana na meneja wenu
wa benki?”
“Ndiyo”
“Shida gani?”
“Aliniambia kuwa alikuwa amefika hapa katika kutaka kujua utaratibu ambao
ungewezesha mishahara ya wafanyakazi wa kampuni yake iwe inapitia kwenye benki
yetu”
“Alikutajia jina la hiyo kampuni au kukuonesha kitambulisho chake?” swali la
Sulle Kiganja likampelekea Bi.Husna Mansour asite kwani tayari alishagundua kosa
alilolifanya la kutokuhoji jina la yule dada muuaji kama siyo kuchukua maelezo yake.
“Hapana” hatimaye akaongea kwa sauti iliyopwaya.
“Ni kawaida yenu kufanya hivyo?” Sulle Kiganja akauliza tena
“Hapana nadhani nilifanya makosa kwa vile mtu mwenyewe alionekana kuwa na
haraka” maelezo ya Bi.Husna Mansour yakapelekea tena kitambo kifupi cha ukimya
kufuata. Sule Kiganja alipozidi kufikiria akagundua kuwa ile sababu ya kutaka kuonana
na meneja wa ile benki iliyotolewa na muuaji ilikuwa ni ya uongo wa kutengeneza
katika namna ya kuhakikisha kuwa muuaji anatimiza lengo lake.
“Wakati mwingine jitahidi kuwa makini zaidi dada dunia ya sasa imeharibika” Sulle
Kiganja akasisitiza na kisha kufuatiwa na kitambo kingine cha ukimya huku akifikiria
jambo fulani.
“Rekodi tuliyoipata kupitia kamera zenu inaonesha kuwa muuaji alikaa ofisini kwa
meneja wa benki yenu kwa muda usiopungua nusu saa. Hili ni jambo la kawaida
kutokea?”
“Hakuna muda rasmi wa mteja kuonana na meneja au mtu yeyote wa humu ndani
kwani hiyo hutegemeana na shida yenyewe na hali itakavyokuwa. Mfano kama meneja
hana kazi nyingi anaweza kutumia muda mwingi zaidi kuonana na wateja au mtu
yeyote yule mwingine” Bi.Husna Mansour akafafanua.
“Ukimuona muuaji unaweza ukamuelezeaje kwa muonekano wake?”
“Ni dada mrembo,mweusi,mwembamba kiasi na mrefu mwenye umbo zuri la
kike lakini kakamavu. Sura yake ni nyembamba kiasi ingawa sikuweza kumuona vizuri
kutokana na kofia aliyoivaa kichwani na miwani myeusi pana ya jua machoni mwake”
“Wakati alipokuwa akitoka humu ofisini kwa meneja wa benki yenu ulimuona?”
“Ndiyo”
“Ukiwa wapi?” Sulle kiganja akauliza kwa makini huku akimtazama Bi.Husna
Mansour machoni
“Pale kwenye sehemu yangu ya kazi”
“Alikuaga?”
“Nilimuuliza kama alihudumiwa shida yake akaniambia kuwa alishapewa
utaratibu wa kufanya hivyo angerudi hapa mapema sana baada ya kukamilisha vigezo
vinavyohitajika”
Sulle Kiganja akamtazama tena Bi.Husna Mansour kwa utulivu huku akiyatafakari
maelezo yake kabla ya kuvunja ukimya.
“Okay! nashukuru sana kwa maelezo yako nadhani sina kingine cha kuuliza
kwa sasa hata hivyo ningekuomba unipe ushirikiano wa kutosha kama nitakuhitaji
tena” Sulle Kiganja akamshukuru Bi.Husna Mansour na kumuacha akaendelee na
majukumu yake kisha akageuka na kumtazama yule mwanaume aliyesimama kando
yake kabla ya kumuuliza.
“Unaitwa nani?”
“Paul Soko” yule mwanaume akajitambulisha huku akionekana kuzama katika
kuangalia wale makachero wengine walivyokuwa wakichukua vipimo vya kitaalum
kutoka kwenye ule mwili wa yule meneja wa benki kwenye kiti chake cha ofisini mle
ndani.
“Nadhani umeyasikia vizuri maelezo ya yule dada mfanyakazi wa hii benki
aliyeondoka hapa sasa hivi!”
“Ndiyo” yule mtu akaitikia huku akitikisa kichwa.
“Maelezo yake yanaendana na huyo mwanamke uliyepishana naye wakati akitoka
kwenye hii ofisi ya meneja?” Sulle Kiganja akauliza kwa utulivu huku akimtazama kwa
makini yule mtu.
“Yupo sahihi kabisa”
“Wewe ni mfanyakazi wa hii benki?”
“Hapana! mimi ni mteja tu na nilikuwa na shida yangu binafsi ya kuonana na
meneja”
“Wakati ulipopishana na huyo mwanamke muuaji mlizungumza kitu chochote?”
“Aliniambia kuwa meneja alikuwa akizungumza na mtu mwingine humu ofisini
hivyo nisubiri kwanza”
“Ulifanya hivyo?”
“Ndiyo,sikuingia badala yake nikaendelea kusubiri pale mlangoni kwa vile namimi
nilikuwa na haraka” yule mtu akaongea huku akisikitika.
“Baadaye ikawaje?” Sulle Kiganja akauliza huku akiuvuta mkono wa shati na
kuitazama saa yake ya mkononi.
“Niliendelea kusubiri pale mlangoni kwa muda mrefu baadaye nikahisi kukata
tamaa baada ya kuona kuwa muda ulikuwa ukienda bila huyo mtu anayesemekana
kuongea na meneja kutoka. Lakini vilevile nilipokumbuka kuwa yule dada aliyeondoka
hapa alikuwa amenieleza kuwa kabla yangu kulikuwa na mtu mmoja tu aliyenitangulia
kuingia humu ofisini kwa meneja ambaye ndiye yule dada niliyepishana naye mlangoni
sikuona sababu ya kuendelea kusubiri zaidi hivyo nikausogelea mlango na kuufungua
nikiingia humu ndani pasipo kugonga hodi ndiyo nikakuta haya mauaji” yule mtu
akaweka kituo.
“Kwa hiyo wewe ndiye mtu wa kwanza humu ndani kuyashuhudia haya mauaji?”
Sulle Kiganja akamuuliza yule mtu huku akimtazama usoni.
“Ndiyo na mimi ndiye niliyewajulisha wafanyakazi wa humu ndani juu ya haya
mauaji”
“Umewahi kumuona huyo dada kabla ya hapo?”
“Sura yake ni ngeni kabisa machoni mwangu na sijawahi kumuona” yule mtu
akaongea huku akitikisa kichwa kuonesha kukataa na hapo Sulle Kiganja akamtazama
kwa makini kabla ya kumuuliza.
“Una lolote jingine la ziada la kuniambia juu ya hili tukio la mauaji lililotokea”
“Hapana”
“Okay! vizuri na mimi nadhani sina swali jingine la kukuuliza kwa sasa nipe
namba yako ya simu ili kama nitahitaji maelezo mengine ya ziada kutoka kwako
uweze kunisaidia” Sulle Kiganja akahitimisha mahojiano huku akitoa kitabu kidogo
na kalamu kutoka mfukoni na kuanza kuiandika namba ya simu aliyoanza kutajiwa na
yule mtu na alipomaliza akafunika kile kitabu na kukitia mfukoni.
“Nashukuru sana kwa ushirikiano wako nadhani unaweza kuondoka na kuendelea
na shughuli zako” Sulle Kiganja akaongea huku akimpa mkono wa shukurani yule
mtu.
“Nashukuru na wewe kazi njema kwako”
“Na wewe pia”
Mara baada ya kuagana Sulle Kiganja akaendelea kusimama akimtazama yule
mtu hadi pale alipofungua mlango wa ile ofisi na kutokomea ndipo akayarudisha
macho yake mle ndani na kuwatazama vijana wake wa kazi namna walivyokuwa
wakishughulika na majukumu yao. Wakati Sulle Kiganja akiendelea kuwasimamia
vijana wake kuchukua taarifa mbalimbali za kiuchunguzi kuhusiana na lile tukio la
mauaji ya meneja wa ile benki,vijana wake wengine wawili wa kazi Roby na Kaombwe
wao walikuwa nje ya lile jengo la benki Zanzibar Marine ng’ambo ya barabara
wakivuna taarifa zote muhimu kuhusiana na mshukiwa wa mauaji yale na waliporudi
mle ndani walikuwa na jambo la kuzungumza.
“Mmepata taarifa zozote mpya?” Sulle Kiganja akageuka na kuwauliza vijana wale
baada ya kuingia mle ndani na kumkaribia pale aliposimama.
“Mahojiano tuliyofanya na wahudumu wawili wa mgahawa wa Seafoods ng’ambo
ya barabara yanashabihiana na yule dada tuliyemuona kupitia kamera za usalama za
hili jengo” Roby akafafanua huku akimtazama Sulle Kiganja kwa utulivu.
“Wanasema walimuona dada huyo wakati alipokuwa akiegesha gari lake kwenye
sehemu ya maegesho ya mgahawa ule na kushuka akivuka barabara kuja kwenye hii
benki na namna ya uvaaji wake ni vilevile kama tulivyoona kwenye kamera za humu
ndani” Kaombwe akazidi kufafanua vizuri na Sulle Kiganja akawatazama vijana wake
na kutabasamu.
“Alikuwa akiendesha gari gani?”
“Toyota corolla nyeupe yenye mstari wa njano ubavuni na kibandiko cha teksi juu
yake” Roby akaongea huku akijaribu kukumbuka.
“Namba za gari?” Sulle Kiganja akauliza. Kaombwe akachukua kitabu kidogo
kutoka mfukoni mwake na kupekua haraka hadi kurasa fulani na kuweka kituo kisha
akaanza kuzitaja namba za gari alizoambiwa na mhudumu mmoja wa ule mgahawa
wa Seafoods ulioko ng’ambo ya barabara nje ya lile jengo la benki. Sulle Kiganja
aliposogea karibu na kuzitazama zile namba haraka akazigundua kuwa zilifanana na
zile alizopewa na Fulgency Kassy,Pweza na Kombe ikisemekana kuwa gari lenye
namba zile ndiyo lililoonekana likitoweka kwa kasi muda mfupi baada ya mauaji ya
P.J. Toddo kwenye sehemu ya maegesho ya magari ya jengo la Rupture & Capture
lililokuwa likitazamana na jengo la Vampire Casino siku ile.
Sulle Kiganja kuona vile haraka akawaita Fulgency Kassy,Pweza na Kombe
waliokuwa bado wakiendelea na uchunguzi dhidi ya yale mauaji ya meneja wa benki
mle ndani kisha haraka akawataka waingie mitaani na kuanza kulitafuta lile gari
lililokuwa likitumiwa na muuaji huku akiwataka waanzie uchunguzi wao Mlimani City
Shopping Mall kwenye duka kubwa la Zanzibar Stone City Bazaar.
Muda mfupi baada ya Fulgency Kassy,Pweza na Kombe kuondoka eneo lile zoezi
la kuchukua vipimo vya uchunguzi dhidi ya yale mauaji ya meneja wa benki likawa
limekamilika. Ule mwili ukaondolewa na kupelekwa hospitali ya taifa ya Muhimbili
kuhifadhiwa hata hivyo Sulle Kiganja kabla ya kuondoka akautahadharisha ule
uongozi wa ile benki kutokutoa taarifa zile kwa waandishi wa habari wala mtu yeyotemwingine kwa kigezo kuwa uchunguzi bado ulikuwa ukiendelea.
 
AKIWA KWENYE FOLENI YA MAGARI umbali mfupi kabla ya kuyafikia
makutano ya barabara eneo la Magomeni, Koplo Tsega kupitia vioo vya ubavuni vya
gari lake akajikuta akishtushwa haraka na gari aina ya Landcruiser jeupe lililokuwa
likijitahidi kupenya na kuyapita magari yaliyokuwa kwenye foleni ile nyuma yake
kumkaribia. Aliposogea karibu na kioo cha ubavu wa gari lake na kutazama vizuri
nyuma yake haraka machale yakamcheza baada ya kuliona gari lile Landcruiser jeupe
lenye vioo vyeusi tinted namna lilivyokuwa likipenya na kuyapita magari mengine
kumkaribia. Moyo ukamlipuka kwa hofu,nywele zikamcheza na jacho jembamba
likaanza kumtoka. Haraka akaingiza gia kisha akaitoa gari yake kwenye mwambata
wa foleni na kuingia kwa kazi upande wa kushoto kwenye barabara ya watembea kwa
miguu na kumkosakosa muuza machungwa kabla ya kuligonga toroli lake na kulitupia
mtaroni huku akiipuuza taharuki ya watu eneo lile.
Yule dereva wa ile Landcruiser kuona vile naye akaingia upande wa kushoto
akiifuata ile barabara ya watembea kwa miguu akilifukuza lile gari ya Koplo Tsega.
Koplo Tsega akaendelea kuendesha gari kwa kasi akiwakwepa watembea kwa
miguu kwenye barabara ile na haukupita muda mrefu mara mvua ya risasi ikaanza
kumiminika kutoka kwenye ile Landcruiser. Koplo Tsega akaingiwa na hofu na
kuanza kuliyumbisha lile gari lake huku na kule akiyakwepa mashambulizi yale.
Mashambulizi ya risasi kutoka kwenye ile Landcruiser hatimaye yakaanza kuleta
maafa. Kioo cha nyuma cha lile gari la Koplo Tsega kikachanguka na kusambaratika
vibaya,taa za nyuma nazo zikapasuka na muda uleule sauti kali ya mpasuko wa
magurudumu ikasikika. Gurudumu moja la nyuma na jingine la mbele yakapata
dhoruba na kusababisha lile gari kuanza kuyumba ovyo. Hata hivyo Koplo Tsega
alijitahidi kuudhibiti usukani wa lile gari kwa jitihada zake zote ingawa lile gari
Landcruiser nyuma yake halikumpa nafasi ya kujitetea na baada ya muda likawa tayari
limemfikia na kuanza kumgonga kwa nyuma.
Wakati ule mtafaruku ukiendelea hatimaye wakajikuta tayari wameyafikia yale
makutano ya barabara ya eneo la Magomeni. Ghafla Koplo Tsega alipotazama upande
wa kulia wa ile barabara akaliona lori kubwa la mafuta kwa kasi likitokea maeneo ya
Kigogo na kukatisha lile eneo la makutano ya barabara kuelekea eneo la Kinondoni.
Yule dereva wa lile lori hakuonekana kufanya jitihada zozote za kupunguza mwendo
kwa vile ilikuwa zamu ya foleni ya barabara ile kuruhusiwa. Kuona vile Koplo Tsega
akakanyaga mafuta na kuongeza mwendo akiwahi kuyavuka makutano yale kabla
ya lile lori halijamfikia akiifuata barabara ya Morogoro kuelekea Jangwani. Hata
hivyo mahesabu yake yaligonga mwamba kwani wakati akikaribia kulivuka lile eneo
la makutano ya barabara lile lori la mafuta tayari lilikuwa limekwishafika katikati ya
makutano ya zile barabara. Kuona vile Koplo Tsega haraka akakanyaga breki lakini
kutokana na ule mwendo kasi lile gari likaserereka na kusota huku magurudumu yake
yakiumana vibaya na lami kulifuata lile tenki la mafuta la lile lori na kusababisha harufu
kali ya mnuko wa magurudumu yale.
Hofu ikiwa imeanza kumuingia juu ya kutokea kwa ajali mbaya ya kukatisha
maisha yake Koplo Tsega haraka akafyatua kabari ya mlango na kujirusha kwa kasi
akipotelea chini ya uvungu wa lile lori huku macho yake yakiwa makini kuyakwepa
magurudumu makubwa ya lile lori. Abiria waliokuwa ndani ya daladala maeneo yale
wakapiga mayowe ya hofu baada ya kuliona tukio lile la kutisha wakati yule dereva wa
lile gari Landcruiser naye akiminya breki kwa nyuma. Lilikuwa tukio la kushangaza
sana na kuogopesha.
Wakati Koplo Tsega akitokezea upande wa pili wa uvungu wa lile lori muda uleule
sauti kubwa ya mlipuko ikasikika kabla ya moto mkubwa kuzuka eneo lile na moshi
mkubwa mweusi kutanda angani. Dereva wa lile lori la mafuta alikua amejitahidi
kulikwepa lile gari la Koplo Tsega kwa kukanyaga breki ya ghafla huku lile gari la
Koplo Tsega likiwa tayari limeshaingia kwenye uvungu wa lile lori. Tenki la mafuta la
lile lori lilikuwa limeyumba na kupoteza uelekeo hali iliyopelekea lile lori kupinduka
yale mafuta kumwagika na hatimaye kulipuka. Watu waliokuwa eneo lile ndani ya
magari wakashuka na kuanza kutimua mbio kila mtu akishika uelekeo wake huku
wakipiga mayowe na vilio vya hofu wakiukimbia ule moto.
Koplo Tsega hakutaka kusubiri huku akiwaza kuwa ile ndiyo ingekuwa nafasi yake
ya pekee ya kuwatoroka wale watu waliokuwa kwenye lile gari Landcruiser lililokuwa
nyuma yake. Hivyo haraka akasimama na kuanza kutimua mbio akikatisha katikati ya
barabara ya mabasi yaendayo mwendo kasi kuelekea posta.
Fulgency Kassy,Pweza na Kombe baada ya kupata maelezo ya kutosha kutoka
kwa yule kijana mfanyakazi wa duka la Zanzibar Stone City Bazaar kuwa yule dada
aliyehusika na mauaji ya meneja wa benki alikuwa amefika pale na kumuulizia meneja
wa duka lile wakawa wameingiwa na hisia kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa kuwa
mara baada ya Koplo Tsega kumkosa meneja wa lile duka kwa vyovyote asingejipa
subira badala yake angefunga safari na kuelekea kisiwani Zanzibar kumfuata yule
meneja na tukio lile lingemaanisha kifo cha mtu mwingine muhimu katika mtandao
wao. Hivyo haraka wakaondoa gari kwenye maegesho ya magari ya Mlimani City
Shopping Mall na kuivuka barabara ya Sam Nujoma wakitokomea vichochoroni.
Muda mfupi baadaye wakawa wametokezea barabara ya Shekilango ambapo mbele
yake waliingia upande wa kushoto na kuifuata barabara ya Morogoro wakielekea eneo
la forodhani bandarini kumuwahi Koplo Tsega kabla hajapanda boti na kuelekea
kisiwani Zanzibar.
Koplo Tsega aliendelea kutimua mbio akikatisha katikati ya uwazi uliofanywa
baina ya barabara ya kwenda na ile ya kurudi katikati ya barabara ya mabasi yaendayo
mwendo kasi huku watu wakiendelea kumshangaa hata hivyo hakusimama.
Kumbukumbu ya kifo na mazishi yake katika makaburi ya Mwananyamala jiji Dar
es Salaam ilikuwa ni historia inayomuwinda ambayo aliapa kuipigania hadi pale
ambapo ushindi ungepatikana. Hakutaka kamwe Fulgency Kassy,Pweza na Kombe
wafahamu kuwa bado alikuwa hai na siyo yule waliyemzika kule kwenye makaburi
ya Mwananyamala kwani endapo wangegundua wangeweza kuzipeleka taarifa zake
kwenye makao makuu ya jeshi la wananchi na hivyo kujikuta matatani zaidi kwa
kufanya udanganyifu lakini vilevile kwa kuhusika na vifo vya maafisa kadhaa wa
usalama ambao alikuwa akiendelea kuwaua jijini Dar es Salaam kama mkakati wake
wa kulipiza kisasi kwa wale wote waliopanga njama na kuhusika na mpango mchafu
wa vifo vyao nchini D.R Congo. Fulgency Kassy, Pweza na Kombe hawakuwa
wamehadaika kirahisi kuwa yule mtu waliyekuwa wakimfukuza alikuwa amekufa
kwenye lile gari Toyota corolla nyeupe baada ya lile gari kuingia chini ya uvungu wa
lile lori la mafuta na ajali kubwa kutokea na hivyo kusababisha mlipuko mkubwa wa
mafuta ya petroli kwenye makutano yale ya barabara zile. Hivyo haraka wakashuka
kwenye ile Landcruiser nyeupe na bastola zao mikononi wakianza kutimua mbio
kulizunguka lile lori na kutokea upande wa pili huku wakiamini kuwa yule mwanamke
waliyekuwa wakimfukuza angeweza kuutumia mwanya ule kuwatoroka.
Akiwa bado anatimua mbio Koplo Tsega akageuka tena na kutazama nyuma na
hapo akaliona wingu zito la moshi wa mafuta ya lile lori ukisambaa hewani kwenye
yale makutano ya zile barabara eneo la Magomeni kabla ya kuwaona wanaume watatu
waliovaa suti nadhifu nyeusi na bastola zao mikononi wakitimua mbio kumfukuza
nyuma yake. Hisia zikamueleza kuwa watu wale wangekuwa ni Fulgency Kassy,Pweza
na Kombe na kwa vile alifahamu kuwa nafasi yeyote ambayo wangeipata wasingeacha
kuitumia kumshindilia risasi haraka akaamua kuvuka ile barabara na kuhamia upande
wa kushoto kisha akavizia daladala moja lililokuwa mbioni kumpita akakimbia
na kudandia mlangoni. Utingo wa daladala lile alitaka kumzuia Koplo Tsega kwa
vile watu walishaanza kuingiwa na mashaka naye tangu walipomuona madirishani
akikimbia lakini Koplo Tsega aliwahi kuichomoa bastola yake na kuikamata mkononi
tukio lililompelekea yule utingowa lile daladala ampishe kwa woga na kumruhusu
aingie mle ndani.
Mara tu Koplo Tsega alipoingia mle ndani haraka akawatahadharisha abiria wote
waliokuwa mle ndani ya lile daladala kuwa wasithubutu kumtaja kuwa alikuwa mle
ndani huku akitoa vitisho kuwa mtu yeyote ambaye angemtaja angekiona cha mtema
kuni. Abiria wote ndani ya lile daladala wakawa wamenyamaza kimya na kumtazama
kwa mashaka kama simba aliyeko usingizini. Koplo Tsega akajichomeka katikati ya
abiria wengine waliosimama katikati ya daladala lile na kushika bomba la kuning’inizia
mikono chini ya paa la daladala lile huku akigeuka na kutazama kule nyuma alipotoka
kupitia kioo cha nyuma cha lile daladala.
Lile daladala likiwa linaendelea na safari yake taratibu haukupita muda mrefu mara
Koplo Tsega akawaona Fulgency Kassy,Pweza na Kombe wakikimbia kandokando
ya ile barabara na bastola zao mikononi huku wakichunguza kwa makini sura za
watu waliokuwa ndani ya magari yote yaliyokuwa yakiendelea na safari taratibu katika
barabara ile. Koplo Tsega alipowaona Fulgency Kassy,Pweza na Kombe wakilikaribia
lile daladala akazidi kujichomeka katikati ya kundi la abiria wale huku akiwatazama
wale watu kwa makini. Jamaa walikuwa wakihema ovyo na kutokwa na jasho jingi
huku sura zao zimefura kwa hasira kama mjeruhi wa mbogo.
Fulgency Kassy,Pweza na Kombe walipolifikia lile daladala alilokuwamo Koplo
Tsega wakasogea na kuanza kuchungulia dirishani huku lile daladala likiendelea na
safari yake taratibu kutokana na foleni kubwa iliyokuwa eneo lile. Hata hivyo kwa
kukosa umakini wakawa hawajamuona Koplo Tsega ndani ya lile daladala hivyo baada
ya kuchoka kuchungulia madirishani wakaamua kuliacha lile daladala na kukimbia
mbele zaidi kuyakagua magari mengine. Kuona vile Koplo Tsega akashusha pumzi
taratibu na kuirudisha bastola yake mafichoni.
Ile foleni ya magari ilikuwa imeanza kupungua baada ya magari ya barabara
ile kuruhusiwa kule mbele hivyo lile daladala likawa limeanza kukoleza mwendo
likimalizia kukatisha eneo lile la jangwani na wakati likiendelea na safari mbele kidogo
Koplo Tsega akawaona Fulgency Kassy,Pweza na Kombe wakiwa wamesimama kwa
uchovu,wakihema ovyo huku mikono yao viunoni wakionekana kukata tamaa na
kuanza kushauriana jambo kabla ya kugeuka na kutazama kule nyuma walipotoka.
Wakati lile daladala lililokuwa na Koplo Tsega likiwapita Koplo Tsega akageuka na
kuwatazama kwa makini huku akijitahidi kuimeza hasira yake moyoni hadi lile daladala
lilipotokomea mbali nao na ile ikawa nafuu kubwa kwa Koplo Tsega.
Lile daladala kwa kuwa lilikuwa likielekea maeneo ya Kariakoo hivyo lilipofika tu
maeneo ya Fire Koplo Tsega akasogea mlangoni na kuruka chini akiliacha lile daladala
likiendelea na safari yake kisha akavuka barabara na kuita bodaboda moja iliyokuwa
eneo lile. Ile bodaboda ilipokuja Koplo Tsega akapanda na kumtaka dereva wa
bodaboda ile ampeleke forodhani bandarini kwenye ofisi za boti za kuelekea kisiwani
Zanzibar.
 
SAA KUMI NA MOJA JIONI BOTI aliyoipanda Koplo Tsega ilikuwa ikitoa
nanga bandari ya Dar es Salaam na kuanza safari ya kuelekea kisiwani Zanzibar baada
ya kuchelewa kidogo na kuikosa boti iliyotangulia ambayo aliamini kuwa ndani yake
alikuwepo White Sugar. Mtu aliyekuwa akimtafuta kwa udi na uvumba. Wakati wote
kabla ya safari kuanza Koplo Tsega alikuwa na wasiwasi mwingi wa kutarajia kuwaona
Fulgency Kassy,Pweza na Kombe wakifika eneo lile lakini kitendo cha kutowaona
kikawa kimemtia faraja na kurudisha matumaini makubwa moyoni mwake.
Jua lilikuwa limeanza kuzama na hivyo ukungu mwepesi wa giza kuanza kutanda
angani. Koplo Tsega akiwa sehemu ya juu kabisa ya ile boti akaendelea kutazama
nyuma namna boti ile ilivyokuwa ikikata mawimbi taratibu kuiacha bandari salama
huku taswira ya majengo mengi marefu ya ghorofa yaliyojazana eneo la posta yakianza
taratibu kutoweka machoni mwake kadiri boti ile ilivyokuwa ikikata mawimbi na
kutokomea mbali na eneo lile.
Wakati Fulgency Kassy,Pweza na Kombe wakifika bandarini Koplo Tsega tayari
alikuwa yuko mbali na bandari ile kwa muda wa nusu saa huku wasijue la kufanya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom