RIWAYA: Kikosi cha Pili

RIWAYA: Kikosi cha Pili

Sehemu ya 8*

Ilikuwa ni siku ya tatu tangu waanze mazoezi na vijana wake Kimbu,
Kama ungeliwatizama ungehisi ni zaidi ya miezi wamekuwa wakijifunza msituni mle,vijana walikuwa na ari ya kupokea mafunzo kutoka kwa makomando wa kitanzania waliokubuhu katika fani hiyo,

Vijana yapata thelathini walikuwa wako makini kuipanda milima na kushuka huku wakifanya kila alichokifanya koplo Makame,walibeba vitu vizito na kupanda navyo milimani,kisha walishuka navyo,ilipendeza kuwatizama,

Walipokwisha maliza mazoezi ya ukakamavu wakapokelewa na koplo Ziga aliewapa mazoezi ya kukabiliana na adui bila silaha,.

Ilikuwa ni heka heka ndani ya misitu ya Goma,hakuna kulala ni kupumzika masaa machache na kuendelea na mazoezi,.

Wakati Koplo Ziga na Koplo Makame wakiwafunza weledi waasi wa kikosi cha La People Front upande wa pili koplo Mwita au 01 kama alivyotambulika alikuwa katikati ya mateso makali hii ni baada ya kutibiwa majeraha ya risasi kisha akapata nafuu kidogo,
Vipigo viliendelea bila huruma,kwa muda alikuwa hoi damu zilimtapakaa kila mahali.

Haya yote yalikuwa yakitazamwa na Zeso muasi asiekuwa na huruma hata kidogo,lengo lake alitaka aambiwe ni nani aliwatuma kumkomboa Ibra Mbaya mshirika wa Loraa Nkunda,.

Kila alipoulizwa hakuwa na jibu la kuwapa,alikuwa ni kama bubu,ila kiukweli komando huyu mbali ya mafunzo ya kuhimili mateso ya kila aina kuwa nayo lakini hakuwa anajua hadi muda huo Ibra mbaya na K3 au luteni Zegera wako wapi na kwanini walimsaliti pia hakujua wenzie walipo,.
Hata angeliteswa vipi hakuwa na ukweli wowote zaidi ya kujua walitumwa na serikali ya Tanzania kumkomboa Ibra Mbaya.

Baada ya kuona mbinu zake hazizai matunda,Zeso aliamuru wasitishe mateso kwa koplo Mwita na arudishwe kwenye mahabusu yao ndani ya ngome ya waasi hao wa AGFT.

Kumfundisha muasi mbinu za mapigano za hali ya juu ni sawa na mtu anae beti,kuna kukosa na kupata na mtu anaebeti anauwezekano mkubwa wa kukosa kuliko kupata kwa hiyo wao wakati huo walikuwa wanabeti kwa waasi wale ambao kiuhalisia hawajui upande halisi waliopo ni upi,

Waliendelea kushauriana wakati wakipata chakula cha usiku pembeni kidogo ya kambi yao,alikuwa ni koplo Ziga aliefikisha wazo hilo kwa koplo Makame.
Koplo Makame nae akaunga mkono kisha wakashauriana kufanya jambo moja nalo ni kuwafundisha waasi wale hadi ngazi ya kuwa kama askari wa jeshi la wananchi na si kufikia kiwango cha ukomando.

Wakamaliza kula chakula wakamwita Kimbu mkuu wa LPF, wakamweleza wanahitaji kujua japo kidogo kuhusu kusalitiwa kwao na ilikuwaje waasi wale wa AGFT waliweza kukaa na Ibra Mbaya nae alijuaje watakuja kumwokoa ilihali wao walikuwa hawajui wanakuja kumwokoa nani.

Akawatazama kisha akawaambia yeye hana taarifa nzuri za kuwahusu isipokuwa taarifa zao atakuwa nazo mtu mmoja maarufu sana kwa jina la Papaa Deo Mukamba nae anaishi katikati ya Goma mjini karibu kabisa na kituo cha kuoshea magari ya wafaransa,Mtaa wa Haidu nyumba namba 24 kushoto mwa barabara ya Nyerere.

Baada ya taarifa hizo wakaahidi kumfikia huyo mtu wapatapo nafasi ila ni kwa kuwa hawakumjua Papaa Deo Mukamba ni nani.

***************
Alistuka dakika chache baada ya kupoteza fahamu,na ni baada ya kumwagiwa maji ya baridi,alijikuta kafungwa kwenye kiti na kamba ngumu ya katani,akapepesa macho pembeni yake kulikuwa na mtu mwingine nae alikuwa amefungwa kamba kama yeye tofauti yao ni kuwa yule mtu alionekana kupitia mateso makali ndani ya muda mfupi uliopita.

Alipokwisha kumtathimini yule mateka mwenzie akahamishia macho kwa mabwana wawili waliokuwa wamesimama mbele yake huku mmoja akiwa ameshika fimbo kama zile zitumikazo kwenye mchezo wa gofu,na mmoja alikua imara na bastola mkononi huku akimtizama Zedi kwa uchu wa kufanya lolote.

Yule alieshika fimbo alimsogelea Zedi kisha akamuuliza
" wewe ni nani na unafanya nini hapa"
Zedi akamtazama kisha akamjibu
"labda nikuulize wewe na kwanini umeniteka raia kama mimi"
Mtu yule aliekuwa amejazia vizuri kimazoezi kama wacheza rugby alimtizama kwa jicho la hasira na kumzaba kofi kali usoni lililompelekea Zedi kuziona nyota za anga zipo ardhini.

Wakati bwana yule akishika fimbo yake vizuri kwa ajili ya kumuadhibu Zedi simu yake ikaita,akaitoa mfukoni na kupokea kisha kusikiliza maongezi upande wa pili,.
Alipokwisha kusikiliza akageuka upande wa pili alipo mwenzie na kuteta nae jambo na kisha wakaanza kumwendea Zedi,Ila hawakumfikia lilitokea tukio ambalo hawakulitegemea na wakabaki vinywa wazi kila mmoja akishangaa.......

Ndimi kudo(Bahati Mwamba)

Kesho ninaeza kuianza hadithi nyingine hapa Jf naeza kuiunganisha au nikafungua thread nyingine kwa ajili ya hiyo.
 
[HASHTAG]#Moneytalk[/HASHTAG],kingongoi,billduke,maga junior,bright platnumz,wolf man,popular famous,kiker,i keep ma promise,Emmanuel nemes,donlucchese,shunie,Tumosa,sirbuff,Maxmizer,Nelson nely,Nassib nyika,kichwa kikubwa,#
 
Anzishaa thread nyingineee... Ilaa mkuu ongezaa vipandee hata vinnee kwa siku.....
 
asante mkuu ,hiyo nyengine ifungulie thread itapendeza
 
[HASHTAG]#Moneytalk[/HASHTAG],kingongoi,billduke,maga junior,bright platnumz,wolf man,popular famous,kiker,i keep ma promise,Emmanuel nemes,donlucchese,shunie,Tumosa,sirbuff,Maxmizer,Nelson nely,Nassib nyika,kichwa kikubwa,#
Bwn,kudo fanya kunitag pliz!
 
Mkuu naomba unitag kwenye hiyo nyingine utakayoianzisha!
 
Sehemu ya 9*


Kosa moja walilolifanya watekaji wale,nikumwacha Zedi na nguo zake,na mara nyingi alipenda kuvaa shati la mikono mirefu ambalo hutumia kuhifadhi visu vyake vidogo,ni wakati alipokuwa akimtizama yule mtu aliepokea simu nae akafanya hila kwenye mikono iliofungwa kisu kidogo kikateleza kutoka kwenye shati lile kikadondoka kwenye kiganja moja wapo,haikuwa ngumu kukata kamba ya katani na alipokwisha kumaliza ndipo wale mabwana wakawa wakimfuata kwa gadhabu nao wakashuhidia mateka wao akisimima wima kitendo bila kusubiri akatawanya miguu yake hewani na kuwapata watekaji wale,wakati wakidondoka kila mmoja kivyake,yeye akawahi kuikota bastola iliokuwa imedondoka upande mwingine na kitendo bila kusubiri akaachia risasi mbili zilizoenda kumtupa yule mtu alimpiga kofi kisha akamwelekezea yule aliekuwa ameishika hiyo bastola ilioko mikononi mwake nae akagwaya akabaki anamtizama mwanaume Zedi.

Zedi kwa mbwembwe akamsogelea yule mtu kisha akaishusha bastola na kuitupa pembeni akamwonyesha ishara yule mtu anahitaji mapambano ya mkono kwa mkono,yule bwana nae akaafiki akajipanga katika mtindo uliovutia akimaanisha na yeye si haba katika fani hiyo,akamtazama Zedi aliekuwa amesimama hatua kadhaa kutoka kwake,akamwendea kwa pupa akakutana na hewa kwa wepesi wa mbinyo wa jicho akageuka na kurusha teke lenye uzani wa kilo kumi ila lilipangulia kiustadi na Zedi,kisha bila kusubiri akauvuta ule mguu kumfuata alipo kisha yeye zedi akawa kama anapishana nao akarudi kumkumba yule bwana kwa kutumia kiwiko,yule bwana akajaribu kukika lile pigo likawa kosa akakutana na mapigo mengine ya haraka yaliompeleka chini,huku yakimwacha Zedi akiwa amesimama imara akimngojea asimame,kwa maumivu makali na kwa kujizoa zoa alisimama akajipanga ila hakumaliza kujipanga mateke matatu ya uzani wa kilogram kadhaa yakatua katika mwili wake akayumba na kuanguka chini kisha akajikuta akikabwa na mikono imara ya mwanaume anaekula dona au ugali wa mtama Zedi.

Zedi akamtandika makofi mawili kisha akamuuliza wako pale kwa nini,yule bwana hakujibu zaidi ya kutabasamu tabasamu la kukera machoni kwa Zedi.
Zedi hakutaka kupoteza akampa kipigo cha sema unalolijua, nae yule bwana akazungumza kiswahili cha Kiha,kwamba yeye hajui la kichwa wala miguu zaidi alitumwa tu kulinda yeyote atakae fika hapo ni halali yake,na aliempa hiyo tenda akamtaja kwa jina la Masunga,.

Zedi aliipoona yule bwana hana analolijua akaamua kumpeleka kwa mungu akajibu tuhuma zake za kufanya uhalifu,kisha akasimama na kumwendea mateka yule alikuwa bado kafungwa kwenye kiti huku akiwa anatizama yote yale,akamfuata na kumfungua kisha akamkokota na kwenda nae sehemu alioacha gari lake,akamsaidia kumwingiza ndani ya gari kisha akamuuliza
" Hujabakwa na wale vilaza?" yule binti aliekuwa ametekwa akatikisa kichwa kukataa na bila maelezo mengi Zedi akalitia moto gari likaanza kulikata pori la Chaya kuitafuta Manyoni.

Masunga alipagaishwa na taarifa za kuonekana mwanaume amefika kwenye eneo lile huku tayari akiwa na taarifa za kutekwa kwa mwanamke ambae alikuwa eneo lile mwanamke yule baada ya kufuatilia habari zake hawakukawia kujua ni kutoka katika idara ya usalama Ikulu,aliekwenda kwa jina la Sajini Mina,mwanamke mwenye weledi katika ushushu,kilichompagawisha zaidi ni baada ya kupokea taarifa kuwa vijana waliwekwa pale wamepoteza uhai huku si Sajini Mina au mwanaume yule alifahamika aliko,kibaya zaidi mwanaume yule kimwonekano ni sawa na yule alieoonekana Morogoro,
Hakukubali kulifumbia macho akatoa taarifa kwa kiongozi wake Ibra Mbaya,Ibra nae akafikisha taarifa anakokujua punde taarifa zakamrudia Masunga,yule mwanaume ni komando Zedi Wimba aliekataa jeshi na kuamua kuishi kitaa,kisha akapewa mikakati ya kumpata Zedi akaingia kazini kwa miguu yote.

******
Kufikishiwa taarifa ya kuwa Zedi yupo mtaani kutafuta ukweli kukampa mashaka Luteni Zegera,akaona hila zao hazitazaa matunda wala wayatarajiayo yanaeza yasifanikiwe hapo akaomba kukutana na wakuu wa mpango Tikisa,akiwemo mnadhimu mkuu wa jeshi,kikao kikakaliwa huku hoja ni vipi wataeza zimisha juhudi za Zedi Wimba,kibaya zaidi itakuwa Ikulu imeshanusa ubaya ndio maana alitumwa Sajini Mina,ila Zegera akatoa wazo na hilo wazo likatekelezwa kwa kuwa mmoja ya vinara wa mpango Tikisa alikuwepo pia,

Ilikuwa kama utani ila ndivyo ilikuwa usiku huo ambao Zedi na Mina wako njiani kurudi Dar,tayari Dar kulishasambaa taarifa ya kutajwa kwa mhusika wa mauji yale ya wanajeshi watatu,vyombo vyote vya ulinzi na usalama vikawa chonjo usiku huo na taarifa ikafika ya kuwa mlengwa yupo njiani kufika Dar,wakatumwa wanajeshi kikosi kazi kuweka kizuizi njiani si jeshi tu hata polisi nao walikuwa kwenye magari yao wakiweka ulinzi kwenye kila uchochoro wa kupita gari,usiku huo ukageuka kuwa usiku Tikisa mikoa mitatu morogoro,dodoma na Dar,huku madereva taxi wakipata adha ya kupekuliwa kila dakika.

*****.......



Ndimi Kudo (Bahati Mwamba)

Nb: leo jioni majira ya saa kumi Riwaya nyingine hapa kama hii haijakufurahisha ijayo itakusisimua,
Lengo langu la kuweka hapa hizi Riwaya ni kuwaomba wale wenye nia na kuunga mkono kazi za waandishi mchango wowote ule ili niweze kutoa nakala za Riwaya mbili ambazo tayari zimekwisha kufanyiwa mastering,pesa nilionayo haijakidhi matakwa ya mapablisher,
Napenda kuona kipaji changu kikiendelea ili niweze kutimiza malengo yangu,

Kwa yeyote atakaekuwa radhi kuniunga mkono atapata nakala zote mbili za hizo riwaya haijalishi atakuwa amechangia kiasi gani cha pesa,.
Yaeza kuwa si pesa tu hata vocha Mimi napokea ilimradi nisikwame kuweka humu riwaya kila siku,

Mwenye kuwa tayari kutoa chochote natumia namba hizi

0758573660,
0658564341
0624155629

Angalizo
Hakuna kulazimishana kwenye kuchangia utachangia kutoka kwenye makubaliano na moyo wako hata yule asiechangia awe huru kusoma hadithi hizi hazitakatishwa zitaenda hadi mwisho.
 
[HASHTAG]#Tumosa[/HASHTAG],dumejeuri,Ngolokolo,i keep Ma promise,madame s,maxmizer,[HASHTAG]#Nassib[/HASHTAG] nyika,Nelson nely,donlucchese,sirbuff,Emmanuel nemes,[HASHTAG]#kichwa[/HASHTAG] kikubwa,kongoi,kiker,wolf man,moneytalk,kigongoi,maga junior,billduke,bright platnumz,popular famous#
 
Noted mkuu! Daah kumbe jf kubwa hivi!! Mwee huku cjawah fika asee! Unaona bila hofu ya kuchunguliwa location Na wazee wa suti nyeusi
 
[HASHTAG]#Tumosa[/HASHTAG],dumejeuri,Ngolokolo,i keep Ma promise,madame s,maxmizer,[HASHTAG]#Nassib[/HASHTAG] nyika,Nelson nely,donlucchese,sirbuff,Emmanuel nemes,[HASHTAG]#kichwa[/HASHTAG] kikubwa,kongoi,kiker,wolf man,moneytalk,kigongoi,maga junior,billduke,bright platnumz,popular famous#
barikiwa kudo900
 
[HASHTAG]#Tumosa[/HASHTAG],dumejeuri,Ngolokolo,i keep Ma promise,madame s,maxmizer,[HASHTAG]#Nassib[/HASHTAG] nyika,Nelson nely,donlucchese,sirbuff,Emmanuel nemes,[HASHTAG]#kichwa[/HASHTAG] kikubwa,kongoi,kiker,wolf man,moneytalk,kigongoi,maga junior,billduke,bright platnumz,popular famous#
Kudo900 ukiweka mpya ucsahau kutusogezea link bac
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom