Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,821
- 6,122
- Thread starter
- #41
Sehemu ya 8*
Ilikuwa ni siku ya tatu tangu waanze mazoezi na vijana wake Kimbu,
Kama ungeliwatizama ungehisi ni zaidi ya miezi wamekuwa wakijifunza msituni mle,vijana walikuwa na ari ya kupokea mafunzo kutoka kwa makomando wa kitanzania waliokubuhu katika fani hiyo,
Vijana yapata thelathini walikuwa wako makini kuipanda milima na kushuka huku wakifanya kila alichokifanya koplo Makame,walibeba vitu vizito na kupanda navyo milimani,kisha walishuka navyo,ilipendeza kuwatizama,
Walipokwisha maliza mazoezi ya ukakamavu wakapokelewa na koplo Ziga aliewapa mazoezi ya kukabiliana na adui bila silaha,.
Ilikuwa ni heka heka ndani ya misitu ya Goma,hakuna kulala ni kupumzika masaa machache na kuendelea na mazoezi,.
Wakati Koplo Ziga na Koplo Makame wakiwafunza weledi waasi wa kikosi cha La People Front upande wa pili koplo Mwita au 01 kama alivyotambulika alikuwa katikati ya mateso makali hii ni baada ya kutibiwa majeraha ya risasi kisha akapata nafuu kidogo,
Vipigo viliendelea bila huruma,kwa muda alikuwa hoi damu zilimtapakaa kila mahali.
Haya yote yalikuwa yakitazamwa na Zeso muasi asiekuwa na huruma hata kidogo,lengo lake alitaka aambiwe ni nani aliwatuma kumkomboa Ibra Mbaya mshirika wa Loraa Nkunda,.
Kila alipoulizwa hakuwa na jibu la kuwapa,alikuwa ni kama bubu,ila kiukweli komando huyu mbali ya mafunzo ya kuhimili mateso ya kila aina kuwa nayo lakini hakuwa anajua hadi muda huo Ibra mbaya na K3 au luteni Zegera wako wapi na kwanini walimsaliti pia hakujua wenzie walipo,.
Hata angeliteswa vipi hakuwa na ukweli wowote zaidi ya kujua walitumwa na serikali ya Tanzania kumkomboa Ibra Mbaya.
Baada ya kuona mbinu zake hazizai matunda,Zeso aliamuru wasitishe mateso kwa koplo Mwita na arudishwe kwenye mahabusu yao ndani ya ngome ya waasi hao wa AGFT.
Kumfundisha muasi mbinu za mapigano za hali ya juu ni sawa na mtu anae beti,kuna kukosa na kupata na mtu anaebeti anauwezekano mkubwa wa kukosa kuliko kupata kwa hiyo wao wakati huo walikuwa wanabeti kwa waasi wale ambao kiuhalisia hawajui upande halisi waliopo ni upi,
Waliendelea kushauriana wakati wakipata chakula cha usiku pembeni kidogo ya kambi yao,alikuwa ni koplo Ziga aliefikisha wazo hilo kwa koplo Makame.
Koplo Makame nae akaunga mkono kisha wakashauriana kufanya jambo moja nalo ni kuwafundisha waasi wale hadi ngazi ya kuwa kama askari wa jeshi la wananchi na si kufikia kiwango cha ukomando.
Wakamaliza kula chakula wakamwita Kimbu mkuu wa LPF, wakamweleza wanahitaji kujua japo kidogo kuhusu kusalitiwa kwao na ilikuwaje waasi wale wa AGFT waliweza kukaa na Ibra Mbaya nae alijuaje watakuja kumwokoa ilihali wao walikuwa hawajui wanakuja kumwokoa nani.
Akawatazama kisha akawaambia yeye hana taarifa nzuri za kuwahusu isipokuwa taarifa zao atakuwa nazo mtu mmoja maarufu sana kwa jina la Papaa Deo Mukamba nae anaishi katikati ya Goma mjini karibu kabisa na kituo cha kuoshea magari ya wafaransa,Mtaa wa Haidu nyumba namba 24 kushoto mwa barabara ya Nyerere.
Baada ya taarifa hizo wakaahidi kumfikia huyo mtu wapatapo nafasi ila ni kwa kuwa hawakumjua Papaa Deo Mukamba ni nani.
***************
Alistuka dakika chache baada ya kupoteza fahamu,na ni baada ya kumwagiwa maji ya baridi,alijikuta kafungwa kwenye kiti na kamba ngumu ya katani,akapepesa macho pembeni yake kulikuwa na mtu mwingine nae alikuwa amefungwa kamba kama yeye tofauti yao ni kuwa yule mtu alionekana kupitia mateso makali ndani ya muda mfupi uliopita.
Alipokwisha kumtathimini yule mateka mwenzie akahamishia macho kwa mabwana wawili waliokuwa wamesimama mbele yake huku mmoja akiwa ameshika fimbo kama zile zitumikazo kwenye mchezo wa gofu,na mmoja alikua imara na bastola mkononi huku akimtizama Zedi kwa uchu wa kufanya lolote.
Yule alieshika fimbo alimsogelea Zedi kisha akamuuliza
" wewe ni nani na unafanya nini hapa"
Zedi akamtazama kisha akamjibu
"labda nikuulize wewe na kwanini umeniteka raia kama mimi"
Mtu yule aliekuwa amejazia vizuri kimazoezi kama wacheza rugby alimtizama kwa jicho la hasira na kumzaba kofi kali usoni lililompelekea Zedi kuziona nyota za anga zipo ardhini.
Wakati bwana yule akishika fimbo yake vizuri kwa ajili ya kumuadhibu Zedi simu yake ikaita,akaitoa mfukoni na kupokea kisha kusikiliza maongezi upande wa pili,.
Alipokwisha kusikiliza akageuka upande wa pili alipo mwenzie na kuteta nae jambo na kisha wakaanza kumwendea Zedi,Ila hawakumfikia lilitokea tukio ambalo hawakulitegemea na wakabaki vinywa wazi kila mmoja akishangaa.......
Ndimi kudo(Bahati Mwamba)
Kesho ninaeza kuianza hadithi nyingine hapa Jf naeza kuiunganisha au nikafungua thread nyingine kwa ajili ya hiyo.
Ilikuwa ni siku ya tatu tangu waanze mazoezi na vijana wake Kimbu,
Kama ungeliwatizama ungehisi ni zaidi ya miezi wamekuwa wakijifunza msituni mle,vijana walikuwa na ari ya kupokea mafunzo kutoka kwa makomando wa kitanzania waliokubuhu katika fani hiyo,
Vijana yapata thelathini walikuwa wako makini kuipanda milima na kushuka huku wakifanya kila alichokifanya koplo Makame,walibeba vitu vizito na kupanda navyo milimani,kisha walishuka navyo,ilipendeza kuwatizama,
Walipokwisha maliza mazoezi ya ukakamavu wakapokelewa na koplo Ziga aliewapa mazoezi ya kukabiliana na adui bila silaha,.
Ilikuwa ni heka heka ndani ya misitu ya Goma,hakuna kulala ni kupumzika masaa machache na kuendelea na mazoezi,.
Wakati Koplo Ziga na Koplo Makame wakiwafunza weledi waasi wa kikosi cha La People Front upande wa pili koplo Mwita au 01 kama alivyotambulika alikuwa katikati ya mateso makali hii ni baada ya kutibiwa majeraha ya risasi kisha akapata nafuu kidogo,
Vipigo viliendelea bila huruma,kwa muda alikuwa hoi damu zilimtapakaa kila mahali.
Haya yote yalikuwa yakitazamwa na Zeso muasi asiekuwa na huruma hata kidogo,lengo lake alitaka aambiwe ni nani aliwatuma kumkomboa Ibra Mbaya mshirika wa Loraa Nkunda,.
Kila alipoulizwa hakuwa na jibu la kuwapa,alikuwa ni kama bubu,ila kiukweli komando huyu mbali ya mafunzo ya kuhimili mateso ya kila aina kuwa nayo lakini hakuwa anajua hadi muda huo Ibra mbaya na K3 au luteni Zegera wako wapi na kwanini walimsaliti pia hakujua wenzie walipo,.
Hata angeliteswa vipi hakuwa na ukweli wowote zaidi ya kujua walitumwa na serikali ya Tanzania kumkomboa Ibra Mbaya.
Baada ya kuona mbinu zake hazizai matunda,Zeso aliamuru wasitishe mateso kwa koplo Mwita na arudishwe kwenye mahabusu yao ndani ya ngome ya waasi hao wa AGFT.
Kumfundisha muasi mbinu za mapigano za hali ya juu ni sawa na mtu anae beti,kuna kukosa na kupata na mtu anaebeti anauwezekano mkubwa wa kukosa kuliko kupata kwa hiyo wao wakati huo walikuwa wanabeti kwa waasi wale ambao kiuhalisia hawajui upande halisi waliopo ni upi,
Waliendelea kushauriana wakati wakipata chakula cha usiku pembeni kidogo ya kambi yao,alikuwa ni koplo Ziga aliefikisha wazo hilo kwa koplo Makame.
Koplo Makame nae akaunga mkono kisha wakashauriana kufanya jambo moja nalo ni kuwafundisha waasi wale hadi ngazi ya kuwa kama askari wa jeshi la wananchi na si kufikia kiwango cha ukomando.
Wakamaliza kula chakula wakamwita Kimbu mkuu wa LPF, wakamweleza wanahitaji kujua japo kidogo kuhusu kusalitiwa kwao na ilikuwaje waasi wale wa AGFT waliweza kukaa na Ibra Mbaya nae alijuaje watakuja kumwokoa ilihali wao walikuwa hawajui wanakuja kumwokoa nani.
Akawatazama kisha akawaambia yeye hana taarifa nzuri za kuwahusu isipokuwa taarifa zao atakuwa nazo mtu mmoja maarufu sana kwa jina la Papaa Deo Mukamba nae anaishi katikati ya Goma mjini karibu kabisa na kituo cha kuoshea magari ya wafaransa,Mtaa wa Haidu nyumba namba 24 kushoto mwa barabara ya Nyerere.
Baada ya taarifa hizo wakaahidi kumfikia huyo mtu wapatapo nafasi ila ni kwa kuwa hawakumjua Papaa Deo Mukamba ni nani.
***************
Alistuka dakika chache baada ya kupoteza fahamu,na ni baada ya kumwagiwa maji ya baridi,alijikuta kafungwa kwenye kiti na kamba ngumu ya katani,akapepesa macho pembeni yake kulikuwa na mtu mwingine nae alikuwa amefungwa kamba kama yeye tofauti yao ni kuwa yule mtu alionekana kupitia mateso makali ndani ya muda mfupi uliopita.
Alipokwisha kumtathimini yule mateka mwenzie akahamishia macho kwa mabwana wawili waliokuwa wamesimama mbele yake huku mmoja akiwa ameshika fimbo kama zile zitumikazo kwenye mchezo wa gofu,na mmoja alikua imara na bastola mkononi huku akimtizama Zedi kwa uchu wa kufanya lolote.
Yule alieshika fimbo alimsogelea Zedi kisha akamuuliza
" wewe ni nani na unafanya nini hapa"
Zedi akamtazama kisha akamjibu
"labda nikuulize wewe na kwanini umeniteka raia kama mimi"
Mtu yule aliekuwa amejazia vizuri kimazoezi kama wacheza rugby alimtizama kwa jicho la hasira na kumzaba kofi kali usoni lililompelekea Zedi kuziona nyota za anga zipo ardhini.
Wakati bwana yule akishika fimbo yake vizuri kwa ajili ya kumuadhibu Zedi simu yake ikaita,akaitoa mfukoni na kupokea kisha kusikiliza maongezi upande wa pili,.
Alipokwisha kusikiliza akageuka upande wa pili alipo mwenzie na kuteta nae jambo na kisha wakaanza kumwendea Zedi,Ila hawakumfikia lilitokea tukio ambalo hawakulitegemea na wakabaki vinywa wazi kila mmoja akishangaa.......
Ndimi kudo(Bahati Mwamba)
Kesho ninaeza kuianza hadithi nyingine hapa Jf naeza kuiunganisha au nikafungua thread nyingine kwa ajili ya hiyo.