bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,095
RIWAYA: JOTO LA MSHUMAA
MTUNZI: MUDHIHILI MNALI
SIMU: 0652667153
LINDI-RUANGWA
SEHEMU YA KWANZA 01
Anza nayo...............
Ndani ya kijiji kimoja kijulikanacho kwa jina la
BWAWANI. Kwenye familia moja ambayo ilikuwa
chini ya usimamizi wa bwana Mzee MAMBO SASA,
alikuwa anishi na familia yake mkewe pamoja na
mwanawe wa kike aliyejulikana kwa jina la SIKITU.
Katika maisha ya mzee huyo alijiwekea utaratibu
ambao ulihusiana na kumuweka mwanae katika
utaratiibu na desturi za adabu na heshima, pia
aliweza kumsomesha mwanae japokuwa ndani ya
kijiji cha Bwawani hakikuwa na muamko kabisa na
swala la usomeshaji wa watoto zao. Hivyo ilikuwa
ngumu sana katika maendeleo ya elimu ndani ya
kijiji hiko. Mzee Mambo sasa siku moja aliokaa na
mwanae na kumuambi mambo muhimu sana
ambayo hayakuenda mbali na maswala ya kumjenga
kielimu zaidi.
''Mwanangu mimi baba yako naomba nikueleze
jambo ambalo lina manufaa sana katika maisha
yako ya sasa pamoja na baadae, kwanza naomba
ushike sana masomo mkwani hata wengi wetu
wanasema kuwa elimu ni ufunguo wa maisha sawa
Sikitu''
Mzee Mambo sasa aliweza kumueleza mwanae
swala hilo huku sikitu akiwa makini sana katika
kumsikiliza baba yake. alionekana kumuelewa
vyema sana baba yake kutokana na umakini wake
wa kusikiliza.
''Baba nimekuelewa na nitafanya kama hivyo
unavyoniambia nifanye baba yangu''
baba yake hakuwa na neno zaidii ya kumsisitizia
kwa yale ambayo alishamueleza ayazingatie. lakini
Mzee huyo alionekana kuwa na shauku kubwa ya
kutaka kumueleza mengi sana mwanae juu ya
umuhimu wa hayo mambo kuyashika kwa makini.
''Nakuomba SIKITU uyashike sana haya mambo
usiwe kama wasichana wenzako hapa kijijini sitaki
hata kusikia ukifanya upuuzi kama wanaoufanya hao
wenzako, jitahidi ufikie hatua kama aliyofikia baba
yako mdogo ambae kwa sasa yuko mjini
nilimsomesha vyema mpaka kafikia pale na wewe
napenda ufikie kama alipo yeye, haya mimi
naelekea shambani nitakukuta baadae nikisharudi''
Mzee MAMBO SASA aliinuka na kuelekea ndani na
kuchukua baadhi ya vifaa kama jembe, panga na
dumu la maji. kwa kuwa ilikuwa majira ya asubuhi
yeye alikuwa kachelewa kidogo kutokana na mambo
ya nyumbani ambayo alikuwa akiyafanya hapo
nyumbani kwake. Alifanya haraka kuelekea
shambani huku akiwa anaimba nyimbo za hapa na
pale. Baada ya muda fulani aliweza kufika hadi
shambani na kumkuta Mmama sikitu akiwa
anaendelea kulima. Kumbe mama sikitu alitangulia
na kumuacha mumewe akiwa anaongea na mwanae
sikitu, Mzee huyo alimueleza mkewe kuhusu
mipango yake ya kutaka mwanae akae katika
maisha yenye mwenendo wa kusoma ili atofautiane
na wanawake wengine wa pale Bwawani. Baada ya
muda Mama sikitu aliweza kuondoka kwani alikuwa
tayari keshachoka hivyo akamuaga mumewe na
kumuacha mzee huyo akiendelea kupiga jembe.
Baada ya muda kupita naye aliweza kuchoka na
kuacha kuendelea kulima kisha akakusanya vifaa na
kuanza kuondoka. Akiwa njiani anakutana na Mzee
mwenzake alioyejulikana kwa jina la Mzee SIKUJUA.
Alisalimiana nae kisha wakaongozana pamoja katika
safari nzima ya kwenda majumbani kwao, Mzee
Sikujua alianzisha mazungumzo ambayo hata mzee
Mambo sasa aliweza kuchangia kwa ufasaha, lakini
kila muda ulipozidi mazungumzo hayo yali0onekana
kuwa chachu kwa Mzee Mambo Sasa.
''Bwana Sikujua unafahamu kuwa mwanangu kwa
kipindi hiki alichonacho nataka ajitahidi afike mbali
kupitia elimu yake mana bila kusoma hawezi
kuendelea kabisa kwa sasa'' Aliongea maneno hayo
kumueleza rafiki yake huyo
''Mh! Sawa lakini wewe hukusoma sasa mbona
maisha yako yako mazuri tu bwana Mambo Sasa,
alafu kwa biti wa kike haki ya nani nakuhakikishia
kuwa unamaliza fedha zako tu kumsomesha
mwanao wa kike hivyo cha kufanya acha
kumsomesha kabisa mwanao huyo na hizo fedha ni
boira upeleke kwenye mashamba na upate fedha
nyingi sana''
Maneno hayo yalimchoma kabisa bwana Mambo
sasa hivyo alimuangalia sana bwana Sikujua na
kumtoa umaana kabisa kwa mtu mzima kama huyo.
'' yani wewe nilikuona kama mtu mkubwa wa umri
na utakuwa na mawazo mazuri yenye maendeleo
lakini una ukubwa wa mwili na miaka lakini hakuna
kitu kabisa kichwani mwako unafikiria pumba tu
yani niache kumsomesha ,mwanangu kwa akili zako
finyu kweli '' Mambo sasa alionekana kukasirika
sana
'' kwa hiyo unanitukana mimi, sasa hii taarifa
itawafikia viongozi wa kijiji kuwa umenitusi kama
uanaona kuna ubaya wa haya niliyokuambia basi
tutaona nani mjanja na kama huyo mwanao utafikia
hatua ya kumsomesha mbali na akafika mjinga
wewe, yani wewe ni mdogo kabisa kwangu na
unanitukana mimi tutaona'' Mzee Sikujua nae
hakuwa mbali aliweza kujibu mashambulizi na hapo
pakawa hapaeleweki kabisa na mtafaruku ulitaka
kufika mbali ndipo alitokea bwana mwingine kijana
kwa umri ambae nae alikuwa anatokea shambani na
kuwakuta wakiw wanazozana hapo wazee hao
wawili. Aliamua kuwatawanya kwa busara sana
ambazo ziliweza kueleweka kwa Mzee Mambo sasa
na si kwa Sikujua.
'' Jamani wazee wangu mbona mnataka kufikia
mbali hivyo nyinyi ndio tunawategemea hapa kijijini
na ndio kioo ambacho mnatufunza sisi vijana na
kutukanya pale tunapokosea sasa mkionekana
mnazozana hapa njiani sisi mnatufunza nini ambao
tunawaona cha kufanya nendeni mkae chini na
mtatue msije kufika pabaya jamani''
Kijana huyo alimaliza na kuwaondoa kwani
walikaribiana na kutaka kuonyeshana umwamba.
lakini mzee sikujua hakutaka kuelewa chochote
kabisa zaidi ya kuendelea kuongea maneno
makubwa ambayo hayakuwa na sitara kwa Mee
mwenzake.
'' Yani nakuambia kuwa utanitambua siji kukusaidia
kwa chochote yani unanitukana mimi kuwa ni
mpumbavu nisiyejua kufikili na nina ukubwa wa umri
lakini sina akili sawa mimi naenda lakini
utanitambua''
Mzee Sikujua aliondoka na kumuacha kijana na
Mzee Mambo sasa wakiwa wanaongea. Walirudi na
kuachana pale kisha Mzee Mambo sasa akaenda
nyumbani. Ulipita muda sana mpaka jioni wakiwa
nyumbani hapo walikaa kama familia na Mzee
Mambo sasa akiwa na mawazo juu ya ugomvi ule
ambao ulijitokeza muda mchache uliopita. Hali hiyo
iliweza kuonekana kwa mkewe na sikitu ambae
alikuwa karibu sana na mama yake. kutokana na
hali ya maisha yao yalivyo yalikuwa ni ya duni sana
ndio maana mzee huyo alijikita zaidi kwenye kilimo
cha korosho na kupata fedjha ambazo zinatumika
kumsomeshea mwanae ambae yuko shule ya
msingi Bwawni darasa ;la saba akiwa anakaribia
kumaliza elimu yake.
'' Mume wangu mbona leo hauko sawa kabisa kama
siku zote kuna nini ambacho kinakusibu maana
tangu mchana nimekuacha shambani uko na furaha
yako lakini umerudi aaah umebadilika kabisa'' Mke
wa Mzee huyo alihoji baada ya kumuona mumewe
hayuko kwenye hali ya kawaida kama alivyoizoea.
'' Ni kweli mke wangu lakini si ya kuzungumza sasa
hivi tutaongea baadae au ngoja kwanza sikitu ebu
kaangalie kwanza kuku kama wametimia ndani
humo alafu uje uniambie''
sikitu alinyanyuka na kuelekea kwenye banda la
kuku ambalo aliambiwa na kuwaacha wazazi wake
wakiendelea kuongea
'' Mke wangu nimemtoa mtoto ili nikueleze kuwa
nimegombana na mzee Sikujua'' Aliongea
kimyakimya
'' Heeee kwa yapi tena mume wangu mpaka
ugombane nae jamani''
'' Eh wakati narudi nyumbani, njiani tulikutana na
sikujua sasa akili yake anataka nisimsomeshe sikitu
kwa kuepusha gharama kubwa aliyoifikilia mimi
nikamuambia msimamo wangu juu ya huyu mtoto
ndipo ugomvi ulipoanzia lakini akawa ananitishia
amani jambo ambalo maishani mwangu siliogopi''
wakati wanamalizia maongezi ndipo sikitu alirejea
na kumuambia kuwa wameshatimia. Walilala usiku
huo mpaka asubuhi lakini mzee Mambo sasa
hakutaka kwenda shambani kwani hakuwa sawa
kiakili kutokana na mambo mengi sana
yanayoendelea pale kwake. Wakati huo anagongewa
mlango akiombwa atoke nje alivyotoka anakutana
na mwenyekiti ambae mkononi alikuwa na barua na
akapatiwa aisome baada ya salamu na kukabidhiwa
karatasi hiyo akaaga na kuondoka zake. Mzee huyo
aliduwaa sana kisha akaingia ndani na kutaka
kuanza kuisoma...........
MTUNZI: MUDHIHILI MNALI
SIMU: 0652667153
LINDI-RUANGWA
SEHEMU YA KWANZA 01
Anza nayo...............
Ndani ya kijiji kimoja kijulikanacho kwa jina la
BWAWANI. Kwenye familia moja ambayo ilikuwa
chini ya usimamizi wa bwana Mzee MAMBO SASA,
alikuwa anishi na familia yake mkewe pamoja na
mwanawe wa kike aliyejulikana kwa jina la SIKITU.
Katika maisha ya mzee huyo alijiwekea utaratibu
ambao ulihusiana na kumuweka mwanae katika
utaratiibu na desturi za adabu na heshima, pia
aliweza kumsomesha mwanae japokuwa ndani ya
kijiji cha Bwawani hakikuwa na muamko kabisa na
swala la usomeshaji wa watoto zao. Hivyo ilikuwa
ngumu sana katika maendeleo ya elimu ndani ya
kijiji hiko. Mzee Mambo sasa siku moja aliokaa na
mwanae na kumuambi mambo muhimu sana
ambayo hayakuenda mbali na maswala ya kumjenga
kielimu zaidi.
''Mwanangu mimi baba yako naomba nikueleze
jambo ambalo lina manufaa sana katika maisha
yako ya sasa pamoja na baadae, kwanza naomba
ushike sana masomo mkwani hata wengi wetu
wanasema kuwa elimu ni ufunguo wa maisha sawa
Sikitu''
Mzee Mambo sasa aliweza kumueleza mwanae
swala hilo huku sikitu akiwa makini sana katika
kumsikiliza baba yake. alionekana kumuelewa
vyema sana baba yake kutokana na umakini wake
wa kusikiliza.
''Baba nimekuelewa na nitafanya kama hivyo
unavyoniambia nifanye baba yangu''
baba yake hakuwa na neno zaidii ya kumsisitizia
kwa yale ambayo alishamueleza ayazingatie. lakini
Mzee huyo alionekana kuwa na shauku kubwa ya
kutaka kumueleza mengi sana mwanae juu ya
umuhimu wa hayo mambo kuyashika kwa makini.
''Nakuomba SIKITU uyashike sana haya mambo
usiwe kama wasichana wenzako hapa kijijini sitaki
hata kusikia ukifanya upuuzi kama wanaoufanya hao
wenzako, jitahidi ufikie hatua kama aliyofikia baba
yako mdogo ambae kwa sasa yuko mjini
nilimsomesha vyema mpaka kafikia pale na wewe
napenda ufikie kama alipo yeye, haya mimi
naelekea shambani nitakukuta baadae nikisharudi''
Mzee MAMBO SASA aliinuka na kuelekea ndani na
kuchukua baadhi ya vifaa kama jembe, panga na
dumu la maji. kwa kuwa ilikuwa majira ya asubuhi
yeye alikuwa kachelewa kidogo kutokana na mambo
ya nyumbani ambayo alikuwa akiyafanya hapo
nyumbani kwake. Alifanya haraka kuelekea
shambani huku akiwa anaimba nyimbo za hapa na
pale. Baada ya muda fulani aliweza kufika hadi
shambani na kumkuta Mmama sikitu akiwa
anaendelea kulima. Kumbe mama sikitu alitangulia
na kumuacha mumewe akiwa anaongea na mwanae
sikitu, Mzee huyo alimueleza mkewe kuhusu
mipango yake ya kutaka mwanae akae katika
maisha yenye mwenendo wa kusoma ili atofautiane
na wanawake wengine wa pale Bwawani. Baada ya
muda Mama sikitu aliweza kuondoka kwani alikuwa
tayari keshachoka hivyo akamuaga mumewe na
kumuacha mzee huyo akiendelea kupiga jembe.
Baada ya muda kupita naye aliweza kuchoka na
kuacha kuendelea kulima kisha akakusanya vifaa na
kuanza kuondoka. Akiwa njiani anakutana na Mzee
mwenzake alioyejulikana kwa jina la Mzee SIKUJUA.
Alisalimiana nae kisha wakaongozana pamoja katika
safari nzima ya kwenda majumbani kwao, Mzee
Sikujua alianzisha mazungumzo ambayo hata mzee
Mambo sasa aliweza kuchangia kwa ufasaha, lakini
kila muda ulipozidi mazungumzo hayo yali0onekana
kuwa chachu kwa Mzee Mambo Sasa.
''Bwana Sikujua unafahamu kuwa mwanangu kwa
kipindi hiki alichonacho nataka ajitahidi afike mbali
kupitia elimu yake mana bila kusoma hawezi
kuendelea kabisa kwa sasa'' Aliongea maneno hayo
kumueleza rafiki yake huyo
''Mh! Sawa lakini wewe hukusoma sasa mbona
maisha yako yako mazuri tu bwana Mambo Sasa,
alafu kwa biti wa kike haki ya nani nakuhakikishia
kuwa unamaliza fedha zako tu kumsomesha
mwanao wa kike hivyo cha kufanya acha
kumsomesha kabisa mwanao huyo na hizo fedha ni
boira upeleke kwenye mashamba na upate fedha
nyingi sana''
Maneno hayo yalimchoma kabisa bwana Mambo
sasa hivyo alimuangalia sana bwana Sikujua na
kumtoa umaana kabisa kwa mtu mzima kama huyo.
'' yani wewe nilikuona kama mtu mkubwa wa umri
na utakuwa na mawazo mazuri yenye maendeleo
lakini una ukubwa wa mwili na miaka lakini hakuna
kitu kabisa kichwani mwako unafikiria pumba tu
yani niache kumsomesha ,mwanangu kwa akili zako
finyu kweli '' Mambo sasa alionekana kukasirika
sana
'' kwa hiyo unanitukana mimi, sasa hii taarifa
itawafikia viongozi wa kijiji kuwa umenitusi kama
uanaona kuna ubaya wa haya niliyokuambia basi
tutaona nani mjanja na kama huyo mwanao utafikia
hatua ya kumsomesha mbali na akafika mjinga
wewe, yani wewe ni mdogo kabisa kwangu na
unanitukana mimi tutaona'' Mzee Sikujua nae
hakuwa mbali aliweza kujibu mashambulizi na hapo
pakawa hapaeleweki kabisa na mtafaruku ulitaka
kufika mbali ndipo alitokea bwana mwingine kijana
kwa umri ambae nae alikuwa anatokea shambani na
kuwakuta wakiw wanazozana hapo wazee hao
wawili. Aliamua kuwatawanya kwa busara sana
ambazo ziliweza kueleweka kwa Mzee Mambo sasa
na si kwa Sikujua.
'' Jamani wazee wangu mbona mnataka kufikia
mbali hivyo nyinyi ndio tunawategemea hapa kijijini
na ndio kioo ambacho mnatufunza sisi vijana na
kutukanya pale tunapokosea sasa mkionekana
mnazozana hapa njiani sisi mnatufunza nini ambao
tunawaona cha kufanya nendeni mkae chini na
mtatue msije kufika pabaya jamani''
Kijana huyo alimaliza na kuwaondoa kwani
walikaribiana na kutaka kuonyeshana umwamba.
lakini mzee sikujua hakutaka kuelewa chochote
kabisa zaidi ya kuendelea kuongea maneno
makubwa ambayo hayakuwa na sitara kwa Mee
mwenzake.
'' Yani nakuambia kuwa utanitambua siji kukusaidia
kwa chochote yani unanitukana mimi kuwa ni
mpumbavu nisiyejua kufikili na nina ukubwa wa umri
lakini sina akili sawa mimi naenda lakini
utanitambua''
Mzee Sikujua aliondoka na kumuacha kijana na
Mzee Mambo sasa wakiwa wanaongea. Walirudi na
kuachana pale kisha Mzee Mambo sasa akaenda
nyumbani. Ulipita muda sana mpaka jioni wakiwa
nyumbani hapo walikaa kama familia na Mzee
Mambo sasa akiwa na mawazo juu ya ugomvi ule
ambao ulijitokeza muda mchache uliopita. Hali hiyo
iliweza kuonekana kwa mkewe na sikitu ambae
alikuwa karibu sana na mama yake. kutokana na
hali ya maisha yao yalivyo yalikuwa ni ya duni sana
ndio maana mzee huyo alijikita zaidi kwenye kilimo
cha korosho na kupata fedjha ambazo zinatumika
kumsomeshea mwanae ambae yuko shule ya
msingi Bwawni darasa ;la saba akiwa anakaribia
kumaliza elimu yake.
'' Mume wangu mbona leo hauko sawa kabisa kama
siku zote kuna nini ambacho kinakusibu maana
tangu mchana nimekuacha shambani uko na furaha
yako lakini umerudi aaah umebadilika kabisa'' Mke
wa Mzee huyo alihoji baada ya kumuona mumewe
hayuko kwenye hali ya kawaida kama alivyoizoea.
'' Ni kweli mke wangu lakini si ya kuzungumza sasa
hivi tutaongea baadae au ngoja kwanza sikitu ebu
kaangalie kwanza kuku kama wametimia ndani
humo alafu uje uniambie''
sikitu alinyanyuka na kuelekea kwenye banda la
kuku ambalo aliambiwa na kuwaacha wazazi wake
wakiendelea kuongea
'' Mke wangu nimemtoa mtoto ili nikueleze kuwa
nimegombana na mzee Sikujua'' Aliongea
kimyakimya
'' Heeee kwa yapi tena mume wangu mpaka
ugombane nae jamani''
'' Eh wakati narudi nyumbani, njiani tulikutana na
sikujua sasa akili yake anataka nisimsomeshe sikitu
kwa kuepusha gharama kubwa aliyoifikilia mimi
nikamuambia msimamo wangu juu ya huyu mtoto
ndipo ugomvi ulipoanzia lakini akawa ananitishia
amani jambo ambalo maishani mwangu siliogopi''
wakati wanamalizia maongezi ndipo sikitu alirejea
na kumuambia kuwa wameshatimia. Walilala usiku
huo mpaka asubuhi lakini mzee Mambo sasa
hakutaka kwenda shambani kwani hakuwa sawa
kiakili kutokana na mambo mengi sana
yanayoendelea pale kwake. Wakati huo anagongewa
mlango akiombwa atoke nje alivyotoka anakutana
na mwenyekiti ambae mkononi alikuwa na barua na
akapatiwa aisome baada ya salamu na kukabidhiwa
karatasi hiyo akaaga na kuondoka zake. Mzee huyo
aliduwaa sana kisha akaingia ndani na kutaka
kuanza kuisoma...........