Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
RIWAYA: URITHI WA GAIDI.
NA; BAHATI MWAMBA.
SIMU: 0758573660
Vitabu vilivyopita.
• Kikosi cha pili
• Dakika za mwisho
• Mpango wa Congo
• Mbwa wa geti
• Operesheni jicho la paka
• Sauti ya mtutu
1:HISABATI
Jua lilikuwa linaelekea magharibi na kuelekea kuzamia kabisa ili kutowesha nuru ilioanza kufifia kabisa na kuliacha anga likiwa jeusi na kiza juu yake.
Ilipata saa kumi na mbili kasoro dakika kadhaa!!
Ilikuwa ni furaha kwa watu kadhaa kuukaribisha usiku huku wengi wakiwa njiani kurejea makwao kujumuika na familia zao baada ya kutoka kuhangaika kutwa nzima. Wengine pia walifurahi kwa kuwa muda huu wa usiku kwao ndio ulikuwa muda sahihi kuingia mtaani na kutafuta riziki yao hasa wezi na vibaka lakini pia makahaba.
Furaha ya giza ilikuwa ni njema zaidi kwa watu wenye baa na kumbi za miziki mana kwao giza ndio riziki yao ya halali bila wizi kwa mtu.
Jioni hii haikuwa njema sana kwa mwanadada mrembo aliepata kuwa na miaka thelathini na mbili hadi na nne hivi. Alikuwa ni mdada mwenye familia ya mume na mtoto mmoja aliepata kuwa na miaka kama mitano hadi sita hivi. Lakini pia alikuwa na mume na maisha yao hayakuwa na tabu yoyote. Familia ilijaa upendo na amani lakini pia kipato kwao hakikuwa na utata.
Milo mitatu kamili ilikuwa ni kawaida kwao.
Hakika ilipendeza!!
Lakini hayo yote sasa yalikuwa yametoweka kwa miaka miwili.
Hakuwa na furaha kama ile aliokuwa nayo mwanzo wakati anaingia kwenye mahusiano na mume wake.
Kwanini!
Kwa sababu alikuwa anaishi yeye peke yake na mwanae zaidi ya miaka miwili na miezi kadhaa huku mume wake akiwa ameondoka kwenda kwenye kazi maalumu Nchi za mbali.
Kazi gani, Hakuzijua na hakupaswa kujua.
Ilikuwa ni ahadi ya kurejea kwa miezi sita tu ila sasa ilikuwa ni miaka miwili bila mume wake kurejea na kila aliemuliza hakuwa na jibu la kumpa akaridhika.
Amekufa?
Hata!!
Haiwezi kuwa rahisi hivyo.
Alijakatalia.
Jioni hii ilimkuta mwanadada huyu mwenye urefu na uzuri wa asili akiwa ndani ya gari akitoka Mwenge kurejea nyumbani kwake Kinondoni akitokea ofisini kwake. Ofisi alioianzisha miaka kadhaa nyuma ikiwa inajishugulisha na utafiti wa mambo ya kale.
Yeye alisomea fani hiyo katika chuo kikuu cha Dar es laam.
Alikuwa ni Archeologist.
Mawazo mengi yalikizonga kichwa chake hasa suala la mume wake kutokuwa na mawasiliano nae zaidi ya miaka miwili na ushee.
Je upendo umeisha! Au huko alikoenda kakutana na mabinti wazuri kumliko basi akaamua kulowea kabisa huko?
Haiwezi kuwa!!
Alijikatalia tena.
Mawazo yake yalizidi kumuumiza kichwa chake na kupelekea jasho jepesi limtoke licha ya gari lake kujitahidi kumpa kiyoyozi bila upendeleo.
Foleni nayo ilizidi kumchosha.
Licha ya kuchoka na foleni lakini kwake aliona ni heri zaidi kuliko kurejea nyumbani na kukutana na nyumba tupu isio kuwa na uchangamfu wowote mana ilikuwa ni yake peke yake kwa sababu mume hakuwepo na mwanae wa kiume alikuwa anasoma shule za kulala huko huko hivyo kwake alikuwa ni yeye kama yeye tu.
Karaha ilioje!!.
Alisonya huku fukuto la jaziba na wivu vikimsonga hasa alipofikiria namna mume wake huko aliko anavyowabambia wanawake wa kizungu au kiafrika huku lugha yao ikiwa ni kizungu ama kihindi ama kiarabu ambazo zote mume wake alizimudu vyema kabisa.
Akasonya tena.
***
Ilikuwa ni majira ya saa mbili usiku ndipo alipoingia nyumbani kwake Kinondoni B.O.B ni baada ya kuwa amepita kwa Bonita saloon kuweka Sawa nywele zake ambazo hakuwa amezijali kwa siku kadhaa hivi.
Alipita kuzifunga tu na kuelekea nyumbani kwake.
Alishuka ndani ya gari na kufungua geti kisha akarudi na kuingiza gari ndani ya uzio wa nyumba yake ya kifahali ambayo sasa aliiona kama jehanamu ya nafsi yake.
Ilikuwa ni bora kukaa nje kuliko kurudi nyumbani kwenye nyumba pweke namna ile.
Akachukua makabrasha yake ya kiofisi na kupiga hatua kadhaa kuingia ndani kwake.
Akawasha taa na kujitupa kwenye sofa huku macho yake yakitua ukutani na kujenga kibanda.
Alibaki akiikodolea picha ya mume wake iliokuwa imetundikwa ukutani pale. Mume wake alikuwa ndani ya vazi la kiofisi huku mabegani mwake akiwa amejaa beji tatu zilizotambulisha cheo chake.
Mume wake alikuwa ni ofisa mkubwa wa jeshi la polisi.
Yeye hakuwa anakodolea vyeo vile bali alikuwa anatazama tabasamu adhimu la mume wake pale kwenye picha. Tabasamu ambalo ni nadra kuliona kwenye uso wa mumewe.
Alitazama kidevu cha mumewe kilichokuwa kimejaa ndevu zilizochongwa kwa mtindo wa Timberland.
Hakika alimkumbuka mumewe.
Pembeni ya picha ile pia kulikuwa kuna picha ya mwanae ambae nae kama baba yake alikuwa na tabasamu safi la kitoto huku akiwa ameegemea kwenye mikono imara ya baba yake.
Mwanadada alifumba macho kwa hisia kali. Kisha akanyanyuka na kuelekea maliwatoni, huko alitumia dakika kadhaa kujiswafi na kurejea sebuleni ambapo napo hakukaa sana akaelekea jikoni ambako hakufanya lililompeleka akabaki akiwa amejishika kiuno tu na kulikodolea jiko lake kama mtumishi aliesusiwa upishi.
Uvivu!!
Uvivu wa kupika chakula chake mwenyewe ndio uliomsumbua.
Hakuona umuhimu wa kupika akaamua kufungua jokofu. Humo ndani akakuta chakula cha kopo akakichukua na kukipasha kisha akarudi sebuleni na kukaa kukila huku akishushia na mvinyo mwekundu.
Dakika kadhaa badae uchovu na msongo wa mawazo vikampelekea aelekee chumbani kwake kulala huku akisahau kufunga milango.
Akalala fofofo!.
Ilikuwa yapata usiku wa saa saba kwenda saa nane hivi, mwanamke yule alipata kuhisi kitu ndani ya nyumba yake. Mwanzo alitaka kupuuzia kile alichokihisi akiwa katikati ya usingizi mnene,lakini hisia za kutambua zilizidi kumsumbua.
Akafumbua macho kisha akatulia na kusikilizia kile kilichofanya aamke.
Masikio yake yalinasa mchakacho wa miguu ya kiumbe hai ndani ya nyumba yake.
Haraka nae akaingiza mkono chini ya mto na kuibuka na bastola na kwa kuwa alikuwa amelala na nguo,hivyo hakupata tabu kuinuka na kunyata kuelekea sebuleni.
Hakusikia kitu tena.
Akafumba macho na kutuliza hisia zake.
Bado hakusikia kitu.
Akanyata hadi mlangoni kisha akachungulia sebuleni.
Ajabu!!
Alibutwaika kwa sekunde kadhaa hivi hasa baada ya kugundua aliacha taa zikiwaka kote mle ndani na sasa zinawaka chumbani pekee huku sebuleni kukiwa giza.
Akagwaya!
Mwili ukamsisimka na hofu ikamjaa!.
Mwanamke akatetereka.
Kutoka pale alipokuwa aliendelea kusubiri zaidi ili kumhadaa aliezima taa sebuleni lakini akajishitukia baada ya kukumbuka kuwa pale chumbani kulikuwa kuna mwanga na sebuleni kiza hivyo yeyote ambae angelikuwa amelikaa sebuleni basi alikuwa akimuona yeye ama kivuli chake.
Hata!!
Haraka na kwa wepesi akanesa kwa kutumia ncha za vidole vya miguu na kufikia kiongoza taa na kuzima taa ya chumbani. Wakati akirudi mlangoni, alisikia mlango wa sebuleni ukibamizwa kwa nguvu kumaanisha kuna mtu katoka muda huo.
Kwa wepesi uliokusudiwa, mwanadada yule nae akapiga hatua ndefu na kufika sebuleni kisha kwa kasi ile ile akaufikia mlango wa sebuleni na kuufungua.
Hola!!
Hakuona mtu wala kivuli cha mtu na geti lilikuwa vilevile limefungwa kumanisha hakuna mtu aliepita muda mfupi uliopita.
Mwanadada yule akaona ajaribu kuzunguka nyumba nzima pengine atafanikiwa kuona mtu aliekuwa sebuleni ila alizunguka bila kuona lau dalili ya mtu.
Alibaki akiwa anatazama mlango wa kuingilia ndani na geti kubwa la kuingilia pale ndani.
Akamakinika na kitu na kumbukumbu zilimrejea vyema.
Akasonya kwa gadhabu!!
Hakuwa amemkumbuka askari anaelinda usiku nyumbani kwa kiongozi wake na pia alikumbuka wakati anaingia hakumuona wala kuhisi uwepo wake.
Hatari kabisa!
“Yani najiwaza hadi nasahau mlinzi” alijisemea huku akipiga hatua kwa makini kuelekea kwenye kibanda cha mlinzi.
“Afande! Afande!” aliita mara mbili na aliitikiwa na sauti yake mwenyewe iliokuwa inajirudia kutokana na utulivu wa kifo uliokuwa nyumbani pale. Akazidi kuukaribia mlango wa kibanda cha mlinzi na alipokifikia akatulia na kusikiliza endapo kungekuwa na harakati zozote ndani ya kibanda.
Kimya!!
Hakuna alichokisikia zaidi ya pumzi zake mwenyewe.
Akausukuma taratibu mlango wa kibanda kile kisha akaingia kwa fujo kidogo.
Hakuna alichokikuta!!
Hakukuwa na mlinzi wala dalili za kuwapo mlinzi ndani ya eneo lile na hiyo ilimaaisha kuwa mlinzi hakuwa amefika pale siku hiyo.
Kwanini!!
Hilo hakujua na wala hakutaka kuamini kama limewekwa makusudi ama vipi.
Lakini alibaki na swali moja kichwani ya kuwa inawezekana vipi nyumba ya ofisa mkubwa jeshini tena special operation asahaulike kuletewa mlinzi.
Hata!! Ni ngumu hilo kufanyika. Lakini sasa mlinzi yuko wapi ikiwa haonekani pale ndani?
Mwanadada alipagawa.
Haraka alirudi ndani na moja kwa moja alielekea mezani kulikokuwa na rununu yake ya mkononi na kulitafuta jina la mtu aliemhitaji na kupiga.
“Ndio nakusikiliza!!” iliunguruma sauti ya mtu aliepokea simu upande wa pili ambae alionekana kutoka usingizini.
“Afande leo mlinzi aliandikishwa kufika hapa kwangu?” aliuliza mwanadada.
Ukimya ukapita kidogo.
“Kuna mambo yamebadilika kidogo na mimi sipo ofisini tangu juzi hivyo sijui kama kuna mtu aliekuwa amepangiwa hapo kwenu!!” alijibu mtu yule baada ya kukaa kimya kwa sekunde kadhaa.
Mwanadada akavuta pumzi za kushindwa kuelewa kinachoendelea.
“Kwani kuna tatizo?” alihoji mtu yule baada ya kusikia ukimya ukiwa umetawala kwenye simu.
“Kesho nitakutafuta tuzungumze Afande!” alisema mwanadada.
“Ni ngumu kesho kunipata mana nasafiri kwenda Ufaransa kwenye kikao cha wakuu wa idara za usalama wa jumuia ya madola nikimuwakilisha Mkuu wa jeshi la polisi nchini” alifafanua yule mtu.
“lakini nahisi kuna tatizo, kwanini mlinzi hajafika hapa nyumbani leo!?” aliuliza yule mwanadada .
Mtu wa upande wa pili akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akasema.
“siwezi jua pengine nikupe namba za mtu anaeshugulikia hayo kwa sasa na ambae amekaimu nafasi yangu hadi nikirejea” alisema yule bwana huku akianza kuzitaja namba hizo na alipomaliza alikata simu bila kungoja maelezo zaidi.
Suala lile likamchanganya kidogo mwanadada yule na kumuacha na maswali mengi bila majibu. Ilikuwa ni tabia mpya kuoneshwa na mtu yule tangu amfahamu na pia alikuwa ni rafiki wa karibu wa familia yake licha ya mtu yule kuwa ni kiongozi wa mumewe kikazi.
Akaguna tu na kuendelea kujishugulisha kuipiga namba aliopewa dakika chache zilizopita.
Simu ilianza kuita kwa fujo na punde ikapokelewa.
“Remi Haji; nakusikiliza”
Ebanaee! Maajabu.
Remi alitamani kukata simu dakika hiyo na kutafakari upya alilosikia. Mtu yule aliekaimu alikuwa anamjua jina lake kwa ufasaha kabisa!
Alimjuaje sasa na kwanini amjue ikiwa yeye si mfanyakazi wa idara yoyote ya jeshi la polisi?
Hakika ni maswali yaliomuacha kinywa wazi na alijikuta akikosa la kusema kwa dakika moja nzima.
“Heloo Remi!!” mtu yule aliita kwa madaha jina la Remi baada ya kuona ukimya umetawala.
“aah nimepewa namba na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge.” Aliongea kwa kirefu Remi.
“elekea kwenye suala lililokufanya upige simu tafadhali ninahitaji kupumzika!” mtu yule aliekaimu nafasi ya Zenge wa Zenge alisema kwa utulivu wa majivuno.
“Hapa kwangu hadi sasa sijaona mlinzi akifika wala kuripoti nilitaka kujua nini tatizo tafadhali” aliuliza Remi.
“Kabla ya kunipigia mimi usiku huu ulipaswa kuwapigia maafisa wanaoshugulika na malindo ya wakuu wao, mimi ni mtu mkubwa sana kuulizwa malindo usiku wa manani namna hii” aling’aka bwana yule.
“Nina sababu afande za kukutafuta wewe na…” alikatishwa kusema Remi.
“Hiyo sababu ilikuwa zamani ila sio sasa. Kwa sasa utaratibu unafuatwa kuanzia ngazi za chini binti” alisema yule bwana kwa ujivuni.
Remi alibaki akiwa amezubaa kwa fadhaa na simu sikioni.
Hakupata kuona mambo haya hapo kabla.
“Naomba kesho ufike ofisini kwangu nina ujumbe” alisema bwana yule na kukata simu.
Remi alibaki akiwa hana hamu na majibu ya ujivuni ya kamishina yule wa jeshi la polisi nchini.
Akaitoa simu sikioni na kulitafuta tena jina la Zenge wa Zenge ili apige lakini alikutana na jibu lililozidi kumuacha wazi kichwani.
Hakuwa akipatikana!
Haijawahi kutokea akazima simu tangu wafahamiane miaka kadhaa nyuma wakati akiwa katika misukosuko ya Ukimbizi ndani ya nchi ya Tanzania kisa ambacho kiliandikwa vyema na mwandishi wa riwaya Bwana Bahati Mwamba.
Sasa baada ya muda wote huo eti Kamishina anazima simu.
Kuna namna si bure.
****
Remi Haji Makame; usingizi ulimpaa na hapo akakumbuka kitu baada ya kushindwa kumtafakari vvyema Zenge wa Zenge.
Ujumbe!!
Alikumbuka mchana aliona ujumbe kutoka kwa mwandishi ambae pia aligeuka kuwa rafiki wa familia hasa baada ya kuwa anaandika mikasa mingi inayomhusu mume wake. Aliupokea ujumbe wa Davis Minja ila hakushugulika nao wakati ule.
Aliufungua!
“Siku ya sita sasa kuna gari silielewi nyuma yangu mumeo sikumpata!” ujumbe ulisomeka hivyo.
Sasa hii tena inakuwaje! Alijiuliza Remi na uso wake ulielekea juu ya ukutani na kuitazama saa.
Mishale iliendelea kuwa mashariki kumaanisha ni usiku wa maanani.
Alizima taa na kuacha usiku upite akiwa amekaa sebuleni kuongojea kuona kama mtu aliemtembelea usiku ule atarejea ili amjibu kwa nini alimtembelea kinyamela na alifuata nini.
Lakini kitu kimoja hakujua ni kuwa hesabu zake zilikuwa nyuma ya hesabu za mtu aliemvizia usiku na kumwacha bila kumduhuru.
Mtu yule hakurejea tena hadi mapambazuko.
Na yakawa ni mapambazuko ya Kihisabati; hesabu za akili.
****
Ahsubuhi ilimkuta Remi akiwa amelala kwenye sofa na bastola yake mkononi. Milio ya ndege waliokuwa juu ya miti ndio waliomsitua kutoka kwenye tope la usingizi wa mang’amung’amu.
Alijisonya bila sababu na kuelekea chumbani kwake ambapo moja kwa moja alielekea maliwatoni na kutumia dakika kumi na ushee kujiswafi kisha akarejea chumbani kwake ambapo hakumaliza muda murefu akawa tayari amekwisha kujiweka sawa na kuvaa suruali ya buluu mpauko na T-shirt nyeusi kisha akachukua mkoba wake wenye nyaraka za kiofisi na kuweka bastola yake kisha akaelekea sebuleni ambako alichukua funguo za gari na kutoka nje ambako alichukua gari lake jeusi aina ya Toyota Nadia na kisha akajifungulia geti na kutoka nje na alipokwisha kutoka akarudi tena kwa miguu na kulifunga kisha akaondoka kwa mwendo wa wastani tu.
Hakufika mbali kwa kupitia vioo vya gari ama side mirror akaona jambo.
Kutoka kwenye kona moja ya nyumba yake aliona mtu alievaa kofia akichepuka na kuivuka barabara kwa kasi na kupotelea kwenye nyumba za watu mtaani pale.
Akili yake ilimwambia mtu yule hakupita eneo lile kwa bahati mbaya au labda ni mkazi wa eneo lile.
Hakika akili yake ilikataa kukubaliana na hilo.
Alikuwa pale anafanya nini na kwanini akimbie kwa kujificha namna ile? Au ndie aliemtembelea usiku na…
Alibaki kutikisa kichwa tu bila kujua kama kuna kusudi baya juu yake ama ni akili yake tu.
Kamwe hakujua mana ya matukio yote yale yalioanza kumwandama siku kadhaa nyuma.
Aliendesha gari lake huku kila mara akitizama nyuma kuona kama kuna jambo lolote lisilo la kawaida.
Hakuona!!
Safari yake ilimfikisha hadi makao makuu ya jeshi la polisi na alipokwisha kufika akapaki gari lake eneo maalumu kisha akaomba kuonana Naibu kamishina. Alioneshwa zilipo ofisi zake.
Hatua zake zilimfikisha hadi kwenye korido pana iliokuwa na ofisi nyingi kushoto na kulia. Akasoma namba za ofisi zile na vitengo vyake hadi pale macho yake yaliponasa jina la ofisi alioihitaji. Ilikuwa ni ofisi ya kitengo maalumu yani special operesheni.
Akagonga mlangoni na kukaribishwa kuingia.
Alikaribishwa na uturi ghali ulionyanyasa pua zake kwa harufu kali. Lakini macho yake hayakuhadaika na na harufu za pua bali yalimakinika kumtazama mtu aliekuwa amekaa kwenye kiti nyuma ya meza na kibao kikiwa mbele yake kilichonasibisha jina lake.
Bwana yule aliitwa P. Kagoshima ambae ndie alikuwa Naibu kamishina wa jeshi la polisi kazi maalumu aliekaimu nafasi ya Kamishina Zenge wa Zenge. Bwana yule hakuonekana kuwa na umri wa kutisha ila umri wake aliukadiria kuwa kati ya miaka arobaini na nne hadi hamsini kasoro. Alikuwa ni mrefu wa wastani ila hakufikia urefu wa Mumewe ama Kamishina Zenge wa Zenge. Sura yake ilionesha ni mtu mjivuni sana lakini mbali na hayo Remi aliona kitu ndani ya macho ya yule bwana. Remi aliona tamaa ya kifisi imejaa kwenye mboni za macho ya Kagoshima ila hakujua ni tamaa ya nini, Pesa ama kitu kingine zaidi ila ilitosha tu kujua yule bwana ni mwenye ujivuni na tamaa.
“Naitwa Remi” alijitambulisha Remi.
“Ooh karibu bibie!” alisema Naibu kamishina Kagoshima huku akiachia tabasamu la upande na kuegemea kiti kilichopokea mwili wake wa kikakamavu.
“Nimeitikia wito Afande!!” alisema Remi huku akitizama saa yake ili kuhakikisha yupo ndani ya muda na sikuchelewa pale ofisini.
“OK! Bila shaka mumeo ni ofisa wa jeshi la polisi!” alihoji Kagoshima huku akijishugulisha kupekua makablasha kadhaa yaliokuwa mezani kwake.
Remi hakumjibu.
Kagoshima aliendelea..
“Na ndie Haji Makame!”
“Afande nadhani yote hayo unayajua na unapaswa kujikita kwenye mada tafadhali” alisema Remi kwa kukereka kidogo.
N. Kamishina alitabasamu kivivu huku akichukua kipande cha gazeti na kukitupia karibu na mikono ya Remi ambae alikuwa amekaa na kuweka mikono yake juu ya meza.
Remi alikichukua kipande kile ambacho kilikuwa ni cha ukurasa wa mbele wa gazeti la Daily News la Marekani. Remi alishuhudia picha mbili kubwa na picha moja ndogo. Picha ndogo ilikuwa ni ya mtu mgeni machoni pake na picha moja kubwa nayo hakuifahamu kabisa lakini picha nyingine ilikuwa ni picha ya mumewe Haji Makame licha ya kuwa na mabadiliko makubwa katika uso wake,lakini kamwe hakuwahi kumsahau mwanaume wa maisha yake.
Akasoma kichwa cha habari cha kipande kile cha gazeti ambacho kilikuwa kimeandikwa kingereza.
Mwili ukamwingia ubaridi kwa alichokielewa. Alimtizama Kagoshima; na alikutana na uso makini ukimtizama kisha akarejesha macho yake kwenye kipande kile.
Tafsiri Kiswahili.
“Tanzania yazidi kuzalisha magaidi, Wawili wasakwa na marekani na mmoja atoweka Guantanamo”
Yalikuwa ni maelezo machache lakini yenye kuchoma akili za watu.
“Sijaelewa Afande!” alisema Remi huku dhahiri akionekana kupagawa.
Naibu Kamishina P. Kagoshima alisogeza kiti huku akiguna kusafisha koo lake na mkono wake wa kushoto akikichukua kipande kile cha gazeti kutoka mikononi mwa Remi.
“Huyu anaitwa Ahmed Twalibu” alisema huku akinyooshea picha ndogo ya jamaa mweusi alieonekana kukomaa sura yake licha ya uso wake kuonesha umaridadi wake vyema.
“Na huyu anaitwa Aahmed Boka Ghailani” alionyeshea picha kubwa ya mwanaume ambae nae hakutofautiana sana na yule aliekuwa kwenye picha ndogo licha ya kuwa walionekana kuwa ni wanaume wawili tofauti.
“Na huyu ni Haji Makame” alisema tena huku akielekeza kidole kwenye picha ya mwanaume aliekuwa amenyoa upara na kuchonga ndevu zake kwa mtindo wa Timberland. Licha ya kunyoa ambayo si tabia alioizoea Remi; lakini ndevu zilimhakikishia yule ni mumewe kipenzi Haji Makame.
Gaidi!!
Ameanza lini ugaidi hadi kutafutwa na serikali ya Marekani!? Na kwanini ahusishwe na Ahmed Twalibu ambae siku za nyuma aliaminika ameuwawa kwenye shambulizi lililotekelezwa na Wataleban walishambulia chopa aliokuwamo?
Na vipi alipona na kuhusishwa tena na ugaidi sambamba na mumewe!?
Ebanae!!
Yalikuwa ni maswali bila majibu na hesabu ziligoma kuunganisha kachumbari ile kichwani mwa Remi ambae siku zote alijua mumewe ni mstari wa mbele kupigania masilahi ya taifa kwa kupambana na ugaidi ama uvunjaji wa sheria wa aina yoyote!
Hata haiwezekani.
Remi alijakatalia kata kata.
“eeh! Hapa kuna watu wawili wanafanana majina kwa kutamkwa ila herufi tofauti yani Ahmed na Aahmed .” Alisema tena Kagoshima huku akitoa picha nyingine kubwa kidogo ambayo nayo aliitupia kwenye meza na kuchukuliwa na Remi.
Picha ile ilifanana sawa sawa na picha ndogo ya mtu alieitwa Ahmed Twalibu aliesemekana kutoroka Guantanamo na sasa anatafutwa na serikali ya Marekani.
Remi alimtizama Kagoshima kwa macho ya kuuliza.
“Ok. Huyo bwana anaedaiwa kuitwa Ahmed Reality ambae unaona picha yake hapo,tumefuatilia na kugundua sio Ahmed Reality ila ni amewahi kuwa askari wa jeshi la polisi kitengo maalumu kama mumeo anaitwa Honda Makubi. Swali tunalojiuliza ni kwanini Marekani iseme ilikuwa nae gerezani kwake na ametoroka wakati miaka miwili nyuma alikuwa anahudumu hapa nchini? Lakini pia Ahmed wa kweli anaweza kuwa miongoni mwa hawa watatu yani huyu Aahmed Ghailani; Haji Makame ama Honda Makubi na hapa anaetafutwa sana ni Ahmed Twalibu ambae nasadiki ndie huyu Aahmed” alisema Naibu kamishina Kagoshima.
Remi alibaki akimtizama akiwa hajui ni kwanini anahusishwa katika jambo lile tena kwa kuelezwa kwa marefu na mapana na kiongozi mkubwa wa jeshi la polisi nchini.
“Kwanini unanambia yote haya na mimi nahusikaje na hili sakata!” alivunja ukimya Remi.
Kagoshima aliegemea kiti chake kisha akamtazama Remi kwa tuo huku akiwa amefumbata mikono yake pamoja.
“una hakika huhusiki?” aliuliza Kagoshima.
Jama!!
Remi alibutwaika kwa kauli ile ya ofisa yule wa jeshi la polisi.
“Nahusika vipi na mambo haya ambayo ni kama hadithi za kufikirika?” alihoji Remi.
“Inaonesha mumeo anashirikiana na magaidi muda mrefu kidogo na wewe yaezekana unajua hiko kitu na ndio mana unahusika katika sakata hili mwanamke!” alisema Kagoshima huku akilambalamba midomo yake kama wafanyavyo wasanii njaa wahojiwapo na vituo vya runinga.
“Huko ni kumkosea mume wangu kabisa na kamwe hajawahi kuwa gaidi. Yani mazuri yote alioyafanya leo mnamwita gaidi?” alisema Remi huku akivuruga nywele zake kichwani kwa mikono yake.
Alihisi kichwa kinawasha kwa taarifa zile.
“Kwanza nataka nikwambie mumeo hajawahi kuwa ofisa wa jeshi la polisi na hata katika rekodi zetu hayumo,hivyo inamaanisha hajawahi kuwa ofisa kabisa na hatumtambui Haji Makame na cheo chake na tunamhesabu kama mhujumu nchi tu aliejichomeka jeshini kutimiza matakwa yake ya kigaidi” Jibu la moto kwa Remi Makame.
“Hajawahi!? Inamaana, dah..” alishindwa kuelewa aseme nini katika dakika ile Remi. Alibaki akiwa ameachama mdomo akiwa hajui ama alie ama acheke ama tabasamu, mana hakuona kama kuna utani katika uso wa Kagoshima ambae ni ofisa mkubwa tu wa jeshi la polisi.
Sasa alielewa ni kwanini hakukuta mlinzi usiku wa jana nyumbani kwake.
“Mengine inabidi utuachie kama serikali tuyashugulikie ila kwa sasa taarifa hii inaweza kukuweka pabaya ama pazuri mrembo” alisema Kagoshima huku akikenua meno kama ngiri maji.
Haaa!!
Urembo tena unaingiaje katika sakata hili!
Remi alisimama kisha akauliza.
“kwanini inaweza niweka pabaya ama pazuri?”
“ukimficha mumeo na washirika wake itakuweka pabaya ila ukitoa taarifa utakuwa pazuri” alisema Kagoshima huku akitoa kadi mfukoni mwake na kumpa Remi.
“Ukiwa na shida utanipigia nami nitakusaidia muda wowote” alisema huku akiona Remi anaitazama ile kadi.
“sina hakika kama itafikia hatua ya kukuomba msaada” alisema Remi huku akiisunda kadi ile mkobani mwake.
“unahakika hutauhitaji msaada wangu?” alihoji Naibu Kamishina huku akitabasamu. Remi alimtizama bila kumjibu na kuondoka ofisini mule huku kichwa kikimuwaka moto kwa taarifa zile.
Hakika alichanganyikiwa.
Dakika kadhaa badae alikuwa ndani ya gari lake na lengo lilikuwa ni kuelekea Mwenge zilipo ofisi zake za utafiti wa mambo ya kale.
Tatizo hakujua huko nako ni moto mwingine utakao acha akili yake ikiwaka. Ila hakujua na angejua hakika angejirudia kwake tu akalale.
***
Nb; toa maoni yako kuhusu riwaya hii. Usiache kutupia maoni yako ambayo ni muhimu
NA; BAHATI MWAMBA.
SIMU: 0758573660
Vitabu vilivyopita.
• Kikosi cha pili
• Dakika za mwisho
• Mpango wa Congo
• Mbwa wa geti
• Operesheni jicho la paka
• Sauti ya mtutu
1:HISABATI
Jua lilikuwa linaelekea magharibi na kuelekea kuzamia kabisa ili kutowesha nuru ilioanza kufifia kabisa na kuliacha anga likiwa jeusi na kiza juu yake.
Ilipata saa kumi na mbili kasoro dakika kadhaa!!
Ilikuwa ni furaha kwa watu kadhaa kuukaribisha usiku huku wengi wakiwa njiani kurejea makwao kujumuika na familia zao baada ya kutoka kuhangaika kutwa nzima. Wengine pia walifurahi kwa kuwa muda huu wa usiku kwao ndio ulikuwa muda sahihi kuingia mtaani na kutafuta riziki yao hasa wezi na vibaka lakini pia makahaba.
Furaha ya giza ilikuwa ni njema zaidi kwa watu wenye baa na kumbi za miziki mana kwao giza ndio riziki yao ya halali bila wizi kwa mtu.
Jioni hii haikuwa njema sana kwa mwanadada mrembo aliepata kuwa na miaka thelathini na mbili hadi na nne hivi. Alikuwa ni mdada mwenye familia ya mume na mtoto mmoja aliepata kuwa na miaka kama mitano hadi sita hivi. Lakini pia alikuwa na mume na maisha yao hayakuwa na tabu yoyote. Familia ilijaa upendo na amani lakini pia kipato kwao hakikuwa na utata.
Milo mitatu kamili ilikuwa ni kawaida kwao.
Hakika ilipendeza!!
Lakini hayo yote sasa yalikuwa yametoweka kwa miaka miwili.
Hakuwa na furaha kama ile aliokuwa nayo mwanzo wakati anaingia kwenye mahusiano na mume wake.
Kwanini!
Kwa sababu alikuwa anaishi yeye peke yake na mwanae zaidi ya miaka miwili na miezi kadhaa huku mume wake akiwa ameondoka kwenda kwenye kazi maalumu Nchi za mbali.
Kazi gani, Hakuzijua na hakupaswa kujua.
Ilikuwa ni ahadi ya kurejea kwa miezi sita tu ila sasa ilikuwa ni miaka miwili bila mume wake kurejea na kila aliemuliza hakuwa na jibu la kumpa akaridhika.
Amekufa?
Hata!!
Haiwezi kuwa rahisi hivyo.
Alijakatalia.
Jioni hii ilimkuta mwanadada huyu mwenye urefu na uzuri wa asili akiwa ndani ya gari akitoka Mwenge kurejea nyumbani kwake Kinondoni akitokea ofisini kwake. Ofisi alioianzisha miaka kadhaa nyuma ikiwa inajishugulisha na utafiti wa mambo ya kale.
Yeye alisomea fani hiyo katika chuo kikuu cha Dar es laam.
Alikuwa ni Archeologist.
Mawazo mengi yalikizonga kichwa chake hasa suala la mume wake kutokuwa na mawasiliano nae zaidi ya miaka miwili na ushee.
Je upendo umeisha! Au huko alikoenda kakutana na mabinti wazuri kumliko basi akaamua kulowea kabisa huko?
Haiwezi kuwa!!
Alijikatalia tena.
Mawazo yake yalizidi kumuumiza kichwa chake na kupelekea jasho jepesi limtoke licha ya gari lake kujitahidi kumpa kiyoyozi bila upendeleo.
Foleni nayo ilizidi kumchosha.
Licha ya kuchoka na foleni lakini kwake aliona ni heri zaidi kuliko kurejea nyumbani na kukutana na nyumba tupu isio kuwa na uchangamfu wowote mana ilikuwa ni yake peke yake kwa sababu mume hakuwepo na mwanae wa kiume alikuwa anasoma shule za kulala huko huko hivyo kwake alikuwa ni yeye kama yeye tu.
Karaha ilioje!!.
Alisonya huku fukuto la jaziba na wivu vikimsonga hasa alipofikiria namna mume wake huko aliko anavyowabambia wanawake wa kizungu au kiafrika huku lugha yao ikiwa ni kizungu ama kihindi ama kiarabu ambazo zote mume wake alizimudu vyema kabisa.
Akasonya tena.
***
Ilikuwa ni majira ya saa mbili usiku ndipo alipoingia nyumbani kwake Kinondoni B.O.B ni baada ya kuwa amepita kwa Bonita saloon kuweka Sawa nywele zake ambazo hakuwa amezijali kwa siku kadhaa hivi.
Alipita kuzifunga tu na kuelekea nyumbani kwake.
Alishuka ndani ya gari na kufungua geti kisha akarudi na kuingiza gari ndani ya uzio wa nyumba yake ya kifahali ambayo sasa aliiona kama jehanamu ya nafsi yake.
Ilikuwa ni bora kukaa nje kuliko kurudi nyumbani kwenye nyumba pweke namna ile.
Akachukua makabrasha yake ya kiofisi na kupiga hatua kadhaa kuingia ndani kwake.
Akawasha taa na kujitupa kwenye sofa huku macho yake yakitua ukutani na kujenga kibanda.
Alibaki akiikodolea picha ya mume wake iliokuwa imetundikwa ukutani pale. Mume wake alikuwa ndani ya vazi la kiofisi huku mabegani mwake akiwa amejaa beji tatu zilizotambulisha cheo chake.
Mume wake alikuwa ni ofisa mkubwa wa jeshi la polisi.
Yeye hakuwa anakodolea vyeo vile bali alikuwa anatazama tabasamu adhimu la mume wake pale kwenye picha. Tabasamu ambalo ni nadra kuliona kwenye uso wa mumewe.
Alitazama kidevu cha mumewe kilichokuwa kimejaa ndevu zilizochongwa kwa mtindo wa Timberland.
Hakika alimkumbuka mumewe.
Pembeni ya picha ile pia kulikuwa kuna picha ya mwanae ambae nae kama baba yake alikuwa na tabasamu safi la kitoto huku akiwa ameegemea kwenye mikono imara ya baba yake.
Mwanadada alifumba macho kwa hisia kali. Kisha akanyanyuka na kuelekea maliwatoni, huko alitumia dakika kadhaa kujiswafi na kurejea sebuleni ambapo napo hakukaa sana akaelekea jikoni ambako hakufanya lililompeleka akabaki akiwa amejishika kiuno tu na kulikodolea jiko lake kama mtumishi aliesusiwa upishi.
Uvivu!!
Uvivu wa kupika chakula chake mwenyewe ndio uliomsumbua.
Hakuona umuhimu wa kupika akaamua kufungua jokofu. Humo ndani akakuta chakula cha kopo akakichukua na kukipasha kisha akarudi sebuleni na kukaa kukila huku akishushia na mvinyo mwekundu.
Dakika kadhaa badae uchovu na msongo wa mawazo vikampelekea aelekee chumbani kwake kulala huku akisahau kufunga milango.
Akalala fofofo!.
Ilikuwa yapata usiku wa saa saba kwenda saa nane hivi, mwanamke yule alipata kuhisi kitu ndani ya nyumba yake. Mwanzo alitaka kupuuzia kile alichokihisi akiwa katikati ya usingizi mnene,lakini hisia za kutambua zilizidi kumsumbua.
Akafumbua macho kisha akatulia na kusikilizia kile kilichofanya aamke.
Masikio yake yalinasa mchakacho wa miguu ya kiumbe hai ndani ya nyumba yake.
Haraka nae akaingiza mkono chini ya mto na kuibuka na bastola na kwa kuwa alikuwa amelala na nguo,hivyo hakupata tabu kuinuka na kunyata kuelekea sebuleni.
Hakusikia kitu tena.
Akafumba macho na kutuliza hisia zake.
Bado hakusikia kitu.
Akanyata hadi mlangoni kisha akachungulia sebuleni.
Ajabu!!
Alibutwaika kwa sekunde kadhaa hivi hasa baada ya kugundua aliacha taa zikiwaka kote mle ndani na sasa zinawaka chumbani pekee huku sebuleni kukiwa giza.
Akagwaya!
Mwili ukamsisimka na hofu ikamjaa!.
Mwanamke akatetereka.
Kutoka pale alipokuwa aliendelea kusubiri zaidi ili kumhadaa aliezima taa sebuleni lakini akajishitukia baada ya kukumbuka kuwa pale chumbani kulikuwa kuna mwanga na sebuleni kiza hivyo yeyote ambae angelikuwa amelikaa sebuleni basi alikuwa akimuona yeye ama kivuli chake.
Hata!!
Haraka na kwa wepesi akanesa kwa kutumia ncha za vidole vya miguu na kufikia kiongoza taa na kuzima taa ya chumbani. Wakati akirudi mlangoni, alisikia mlango wa sebuleni ukibamizwa kwa nguvu kumaanisha kuna mtu katoka muda huo.
Kwa wepesi uliokusudiwa, mwanadada yule nae akapiga hatua ndefu na kufika sebuleni kisha kwa kasi ile ile akaufikia mlango wa sebuleni na kuufungua.
Hola!!
Hakuona mtu wala kivuli cha mtu na geti lilikuwa vilevile limefungwa kumanisha hakuna mtu aliepita muda mfupi uliopita.
Mwanadada yule akaona ajaribu kuzunguka nyumba nzima pengine atafanikiwa kuona mtu aliekuwa sebuleni ila alizunguka bila kuona lau dalili ya mtu.
Alibaki akiwa anatazama mlango wa kuingilia ndani na geti kubwa la kuingilia pale ndani.
Akamakinika na kitu na kumbukumbu zilimrejea vyema.
Akasonya kwa gadhabu!!
Hakuwa amemkumbuka askari anaelinda usiku nyumbani kwa kiongozi wake na pia alikumbuka wakati anaingia hakumuona wala kuhisi uwepo wake.
Hatari kabisa!
“Yani najiwaza hadi nasahau mlinzi” alijisemea huku akipiga hatua kwa makini kuelekea kwenye kibanda cha mlinzi.
“Afande! Afande!” aliita mara mbili na aliitikiwa na sauti yake mwenyewe iliokuwa inajirudia kutokana na utulivu wa kifo uliokuwa nyumbani pale. Akazidi kuukaribia mlango wa kibanda cha mlinzi na alipokifikia akatulia na kusikiliza endapo kungekuwa na harakati zozote ndani ya kibanda.
Kimya!!
Hakuna alichokisikia zaidi ya pumzi zake mwenyewe.
Akausukuma taratibu mlango wa kibanda kile kisha akaingia kwa fujo kidogo.
Hakuna alichokikuta!!
Hakukuwa na mlinzi wala dalili za kuwapo mlinzi ndani ya eneo lile na hiyo ilimaaisha kuwa mlinzi hakuwa amefika pale siku hiyo.
Kwanini!!
Hilo hakujua na wala hakutaka kuamini kama limewekwa makusudi ama vipi.
Lakini alibaki na swali moja kichwani ya kuwa inawezekana vipi nyumba ya ofisa mkubwa jeshini tena special operation asahaulike kuletewa mlinzi.
Hata!! Ni ngumu hilo kufanyika. Lakini sasa mlinzi yuko wapi ikiwa haonekani pale ndani?
Mwanadada alipagawa.
Haraka alirudi ndani na moja kwa moja alielekea mezani kulikokuwa na rununu yake ya mkononi na kulitafuta jina la mtu aliemhitaji na kupiga.
“Ndio nakusikiliza!!” iliunguruma sauti ya mtu aliepokea simu upande wa pili ambae alionekana kutoka usingizini.
“Afande leo mlinzi aliandikishwa kufika hapa kwangu?” aliuliza mwanadada.
Ukimya ukapita kidogo.
“Kuna mambo yamebadilika kidogo na mimi sipo ofisini tangu juzi hivyo sijui kama kuna mtu aliekuwa amepangiwa hapo kwenu!!” alijibu mtu yule baada ya kukaa kimya kwa sekunde kadhaa.
Mwanadada akavuta pumzi za kushindwa kuelewa kinachoendelea.
“Kwani kuna tatizo?” alihoji mtu yule baada ya kusikia ukimya ukiwa umetawala kwenye simu.
“Kesho nitakutafuta tuzungumze Afande!” alisema mwanadada.
“Ni ngumu kesho kunipata mana nasafiri kwenda Ufaransa kwenye kikao cha wakuu wa idara za usalama wa jumuia ya madola nikimuwakilisha Mkuu wa jeshi la polisi nchini” alifafanua yule mtu.
“lakini nahisi kuna tatizo, kwanini mlinzi hajafika hapa nyumbani leo!?” aliuliza yule mwanadada .
Mtu wa upande wa pili akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akasema.
“siwezi jua pengine nikupe namba za mtu anaeshugulikia hayo kwa sasa na ambae amekaimu nafasi yangu hadi nikirejea” alisema yule bwana huku akianza kuzitaja namba hizo na alipomaliza alikata simu bila kungoja maelezo zaidi.
Suala lile likamchanganya kidogo mwanadada yule na kumuacha na maswali mengi bila majibu. Ilikuwa ni tabia mpya kuoneshwa na mtu yule tangu amfahamu na pia alikuwa ni rafiki wa karibu wa familia yake licha ya mtu yule kuwa ni kiongozi wa mumewe kikazi.
Akaguna tu na kuendelea kujishugulisha kuipiga namba aliopewa dakika chache zilizopita.
Simu ilianza kuita kwa fujo na punde ikapokelewa.
“Remi Haji; nakusikiliza”
Ebanaee! Maajabu.
Remi alitamani kukata simu dakika hiyo na kutafakari upya alilosikia. Mtu yule aliekaimu alikuwa anamjua jina lake kwa ufasaha kabisa!
Alimjuaje sasa na kwanini amjue ikiwa yeye si mfanyakazi wa idara yoyote ya jeshi la polisi?
Hakika ni maswali yaliomuacha kinywa wazi na alijikuta akikosa la kusema kwa dakika moja nzima.
“Heloo Remi!!” mtu yule aliita kwa madaha jina la Remi baada ya kuona ukimya umetawala.
“aah nimepewa namba na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge.” Aliongea kwa kirefu Remi.
“elekea kwenye suala lililokufanya upige simu tafadhali ninahitaji kupumzika!” mtu yule aliekaimu nafasi ya Zenge wa Zenge alisema kwa utulivu wa majivuno.
“Hapa kwangu hadi sasa sijaona mlinzi akifika wala kuripoti nilitaka kujua nini tatizo tafadhali” aliuliza Remi.
“Kabla ya kunipigia mimi usiku huu ulipaswa kuwapigia maafisa wanaoshugulika na malindo ya wakuu wao, mimi ni mtu mkubwa sana kuulizwa malindo usiku wa manani namna hii” aling’aka bwana yule.
“Nina sababu afande za kukutafuta wewe na…” alikatishwa kusema Remi.
“Hiyo sababu ilikuwa zamani ila sio sasa. Kwa sasa utaratibu unafuatwa kuanzia ngazi za chini binti” alisema yule bwana kwa ujivuni.
Remi alibaki akiwa amezubaa kwa fadhaa na simu sikioni.
Hakupata kuona mambo haya hapo kabla.
“Naomba kesho ufike ofisini kwangu nina ujumbe” alisema bwana yule na kukata simu.
Remi alibaki akiwa hana hamu na majibu ya ujivuni ya kamishina yule wa jeshi la polisi nchini.
Akaitoa simu sikioni na kulitafuta tena jina la Zenge wa Zenge ili apige lakini alikutana na jibu lililozidi kumuacha wazi kichwani.
Hakuwa akipatikana!
Haijawahi kutokea akazima simu tangu wafahamiane miaka kadhaa nyuma wakati akiwa katika misukosuko ya Ukimbizi ndani ya nchi ya Tanzania kisa ambacho kiliandikwa vyema na mwandishi wa riwaya Bwana Bahati Mwamba.
Sasa baada ya muda wote huo eti Kamishina anazima simu.
Kuna namna si bure.
****
Remi Haji Makame; usingizi ulimpaa na hapo akakumbuka kitu baada ya kushindwa kumtafakari vvyema Zenge wa Zenge.
Ujumbe!!
Alikumbuka mchana aliona ujumbe kutoka kwa mwandishi ambae pia aligeuka kuwa rafiki wa familia hasa baada ya kuwa anaandika mikasa mingi inayomhusu mume wake. Aliupokea ujumbe wa Davis Minja ila hakushugulika nao wakati ule.
Aliufungua!
“Siku ya sita sasa kuna gari silielewi nyuma yangu mumeo sikumpata!” ujumbe ulisomeka hivyo.
Sasa hii tena inakuwaje! Alijiuliza Remi na uso wake ulielekea juu ya ukutani na kuitazama saa.
Mishale iliendelea kuwa mashariki kumaanisha ni usiku wa maanani.
Alizima taa na kuacha usiku upite akiwa amekaa sebuleni kuongojea kuona kama mtu aliemtembelea usiku ule atarejea ili amjibu kwa nini alimtembelea kinyamela na alifuata nini.
Lakini kitu kimoja hakujua ni kuwa hesabu zake zilikuwa nyuma ya hesabu za mtu aliemvizia usiku na kumwacha bila kumduhuru.
Mtu yule hakurejea tena hadi mapambazuko.
Na yakawa ni mapambazuko ya Kihisabati; hesabu za akili.
****
Ahsubuhi ilimkuta Remi akiwa amelala kwenye sofa na bastola yake mkononi. Milio ya ndege waliokuwa juu ya miti ndio waliomsitua kutoka kwenye tope la usingizi wa mang’amung’amu.
Alijisonya bila sababu na kuelekea chumbani kwake ambapo moja kwa moja alielekea maliwatoni na kutumia dakika kumi na ushee kujiswafi kisha akarejea chumbani kwake ambapo hakumaliza muda murefu akawa tayari amekwisha kujiweka sawa na kuvaa suruali ya buluu mpauko na T-shirt nyeusi kisha akachukua mkoba wake wenye nyaraka za kiofisi na kuweka bastola yake kisha akaelekea sebuleni ambako alichukua funguo za gari na kutoka nje ambako alichukua gari lake jeusi aina ya Toyota Nadia na kisha akajifungulia geti na kutoka nje na alipokwisha kutoka akarudi tena kwa miguu na kulifunga kisha akaondoka kwa mwendo wa wastani tu.
Hakufika mbali kwa kupitia vioo vya gari ama side mirror akaona jambo.
Kutoka kwenye kona moja ya nyumba yake aliona mtu alievaa kofia akichepuka na kuivuka barabara kwa kasi na kupotelea kwenye nyumba za watu mtaani pale.
Akili yake ilimwambia mtu yule hakupita eneo lile kwa bahati mbaya au labda ni mkazi wa eneo lile.
Hakika akili yake ilikataa kukubaliana na hilo.
Alikuwa pale anafanya nini na kwanini akimbie kwa kujificha namna ile? Au ndie aliemtembelea usiku na…
Alibaki kutikisa kichwa tu bila kujua kama kuna kusudi baya juu yake ama ni akili yake tu.
Kamwe hakujua mana ya matukio yote yale yalioanza kumwandama siku kadhaa nyuma.
Aliendesha gari lake huku kila mara akitizama nyuma kuona kama kuna jambo lolote lisilo la kawaida.
Hakuona!!
Safari yake ilimfikisha hadi makao makuu ya jeshi la polisi na alipokwisha kufika akapaki gari lake eneo maalumu kisha akaomba kuonana Naibu kamishina. Alioneshwa zilipo ofisi zake.
Hatua zake zilimfikisha hadi kwenye korido pana iliokuwa na ofisi nyingi kushoto na kulia. Akasoma namba za ofisi zile na vitengo vyake hadi pale macho yake yaliponasa jina la ofisi alioihitaji. Ilikuwa ni ofisi ya kitengo maalumu yani special operesheni.
Akagonga mlangoni na kukaribishwa kuingia.
Alikaribishwa na uturi ghali ulionyanyasa pua zake kwa harufu kali. Lakini macho yake hayakuhadaika na na harufu za pua bali yalimakinika kumtazama mtu aliekuwa amekaa kwenye kiti nyuma ya meza na kibao kikiwa mbele yake kilichonasibisha jina lake.
Bwana yule aliitwa P. Kagoshima ambae ndie alikuwa Naibu kamishina wa jeshi la polisi kazi maalumu aliekaimu nafasi ya Kamishina Zenge wa Zenge. Bwana yule hakuonekana kuwa na umri wa kutisha ila umri wake aliukadiria kuwa kati ya miaka arobaini na nne hadi hamsini kasoro. Alikuwa ni mrefu wa wastani ila hakufikia urefu wa Mumewe ama Kamishina Zenge wa Zenge. Sura yake ilionesha ni mtu mjivuni sana lakini mbali na hayo Remi aliona kitu ndani ya macho ya yule bwana. Remi aliona tamaa ya kifisi imejaa kwenye mboni za macho ya Kagoshima ila hakujua ni tamaa ya nini, Pesa ama kitu kingine zaidi ila ilitosha tu kujua yule bwana ni mwenye ujivuni na tamaa.
“Naitwa Remi” alijitambulisha Remi.
“Ooh karibu bibie!” alisema Naibu kamishina Kagoshima huku akiachia tabasamu la upande na kuegemea kiti kilichopokea mwili wake wa kikakamavu.
“Nimeitikia wito Afande!!” alisema Remi huku akitizama saa yake ili kuhakikisha yupo ndani ya muda na sikuchelewa pale ofisini.
“OK! Bila shaka mumeo ni ofisa wa jeshi la polisi!” alihoji Kagoshima huku akijishugulisha kupekua makablasha kadhaa yaliokuwa mezani kwake.
Remi hakumjibu.
Kagoshima aliendelea..
“Na ndie Haji Makame!”
“Afande nadhani yote hayo unayajua na unapaswa kujikita kwenye mada tafadhali” alisema Remi kwa kukereka kidogo.
N. Kamishina alitabasamu kivivu huku akichukua kipande cha gazeti na kukitupia karibu na mikono ya Remi ambae alikuwa amekaa na kuweka mikono yake juu ya meza.
Remi alikichukua kipande kile ambacho kilikuwa ni cha ukurasa wa mbele wa gazeti la Daily News la Marekani. Remi alishuhudia picha mbili kubwa na picha moja ndogo. Picha ndogo ilikuwa ni ya mtu mgeni machoni pake na picha moja kubwa nayo hakuifahamu kabisa lakini picha nyingine ilikuwa ni picha ya mumewe Haji Makame licha ya kuwa na mabadiliko makubwa katika uso wake,lakini kamwe hakuwahi kumsahau mwanaume wa maisha yake.
Akasoma kichwa cha habari cha kipande kile cha gazeti ambacho kilikuwa kimeandikwa kingereza.
Mwili ukamwingia ubaridi kwa alichokielewa. Alimtizama Kagoshima; na alikutana na uso makini ukimtizama kisha akarejesha macho yake kwenye kipande kile.
Tafsiri Kiswahili.
“Tanzania yazidi kuzalisha magaidi, Wawili wasakwa na marekani na mmoja atoweka Guantanamo”
Yalikuwa ni maelezo machache lakini yenye kuchoma akili za watu.
“Sijaelewa Afande!” alisema Remi huku dhahiri akionekana kupagawa.
Naibu Kamishina P. Kagoshima alisogeza kiti huku akiguna kusafisha koo lake na mkono wake wa kushoto akikichukua kipande kile cha gazeti kutoka mikononi mwa Remi.
“Huyu anaitwa Ahmed Twalibu” alisema huku akinyooshea picha ndogo ya jamaa mweusi alieonekana kukomaa sura yake licha ya uso wake kuonesha umaridadi wake vyema.
“Na huyu anaitwa Aahmed Boka Ghailani” alionyeshea picha kubwa ya mwanaume ambae nae hakutofautiana sana na yule aliekuwa kwenye picha ndogo licha ya kuwa walionekana kuwa ni wanaume wawili tofauti.
“Na huyu ni Haji Makame” alisema tena huku akielekeza kidole kwenye picha ya mwanaume aliekuwa amenyoa upara na kuchonga ndevu zake kwa mtindo wa Timberland. Licha ya kunyoa ambayo si tabia alioizoea Remi; lakini ndevu zilimhakikishia yule ni mumewe kipenzi Haji Makame.
Gaidi!!
Ameanza lini ugaidi hadi kutafutwa na serikali ya Marekani!? Na kwanini ahusishwe na Ahmed Twalibu ambae siku za nyuma aliaminika ameuwawa kwenye shambulizi lililotekelezwa na Wataleban walishambulia chopa aliokuwamo?
Na vipi alipona na kuhusishwa tena na ugaidi sambamba na mumewe!?
Ebanae!!
Yalikuwa ni maswali bila majibu na hesabu ziligoma kuunganisha kachumbari ile kichwani mwa Remi ambae siku zote alijua mumewe ni mstari wa mbele kupigania masilahi ya taifa kwa kupambana na ugaidi ama uvunjaji wa sheria wa aina yoyote!
Hata haiwezekani.
Remi alijakatalia kata kata.
“eeh! Hapa kuna watu wawili wanafanana majina kwa kutamkwa ila herufi tofauti yani Ahmed na Aahmed .” Alisema tena Kagoshima huku akitoa picha nyingine kubwa kidogo ambayo nayo aliitupia kwenye meza na kuchukuliwa na Remi.
Picha ile ilifanana sawa sawa na picha ndogo ya mtu alieitwa Ahmed Twalibu aliesemekana kutoroka Guantanamo na sasa anatafutwa na serikali ya Marekani.
Remi alimtizama Kagoshima kwa macho ya kuuliza.
“Ok. Huyo bwana anaedaiwa kuitwa Ahmed Reality ambae unaona picha yake hapo,tumefuatilia na kugundua sio Ahmed Reality ila ni amewahi kuwa askari wa jeshi la polisi kitengo maalumu kama mumeo anaitwa Honda Makubi. Swali tunalojiuliza ni kwanini Marekani iseme ilikuwa nae gerezani kwake na ametoroka wakati miaka miwili nyuma alikuwa anahudumu hapa nchini? Lakini pia Ahmed wa kweli anaweza kuwa miongoni mwa hawa watatu yani huyu Aahmed Ghailani; Haji Makame ama Honda Makubi na hapa anaetafutwa sana ni Ahmed Twalibu ambae nasadiki ndie huyu Aahmed” alisema Naibu kamishina Kagoshima.
Remi alibaki akimtizama akiwa hajui ni kwanini anahusishwa katika jambo lile tena kwa kuelezwa kwa marefu na mapana na kiongozi mkubwa wa jeshi la polisi nchini.
“Kwanini unanambia yote haya na mimi nahusikaje na hili sakata!” alivunja ukimya Remi.
Kagoshima aliegemea kiti chake kisha akamtazama Remi kwa tuo huku akiwa amefumbata mikono yake pamoja.
“una hakika huhusiki?” aliuliza Kagoshima.
Jama!!
Remi alibutwaika kwa kauli ile ya ofisa yule wa jeshi la polisi.
“Nahusika vipi na mambo haya ambayo ni kama hadithi za kufikirika?” alihoji Remi.
“Inaonesha mumeo anashirikiana na magaidi muda mrefu kidogo na wewe yaezekana unajua hiko kitu na ndio mana unahusika katika sakata hili mwanamke!” alisema Kagoshima huku akilambalamba midomo yake kama wafanyavyo wasanii njaa wahojiwapo na vituo vya runinga.
“Huko ni kumkosea mume wangu kabisa na kamwe hajawahi kuwa gaidi. Yani mazuri yote alioyafanya leo mnamwita gaidi?” alisema Remi huku akivuruga nywele zake kichwani kwa mikono yake.
Alihisi kichwa kinawasha kwa taarifa zile.
“Kwanza nataka nikwambie mumeo hajawahi kuwa ofisa wa jeshi la polisi na hata katika rekodi zetu hayumo,hivyo inamaanisha hajawahi kuwa ofisa kabisa na hatumtambui Haji Makame na cheo chake na tunamhesabu kama mhujumu nchi tu aliejichomeka jeshini kutimiza matakwa yake ya kigaidi” Jibu la moto kwa Remi Makame.
“Hajawahi!? Inamaana, dah..” alishindwa kuelewa aseme nini katika dakika ile Remi. Alibaki akiwa ameachama mdomo akiwa hajui ama alie ama acheke ama tabasamu, mana hakuona kama kuna utani katika uso wa Kagoshima ambae ni ofisa mkubwa tu wa jeshi la polisi.
Sasa alielewa ni kwanini hakukuta mlinzi usiku wa jana nyumbani kwake.
“Mengine inabidi utuachie kama serikali tuyashugulikie ila kwa sasa taarifa hii inaweza kukuweka pabaya ama pazuri mrembo” alisema Kagoshima huku akikenua meno kama ngiri maji.
Haaa!!
Urembo tena unaingiaje katika sakata hili!
Remi alisimama kisha akauliza.
“kwanini inaweza niweka pabaya ama pazuri?”
“ukimficha mumeo na washirika wake itakuweka pabaya ila ukitoa taarifa utakuwa pazuri” alisema Kagoshima huku akitoa kadi mfukoni mwake na kumpa Remi.
“Ukiwa na shida utanipigia nami nitakusaidia muda wowote” alisema huku akiona Remi anaitazama ile kadi.
“sina hakika kama itafikia hatua ya kukuomba msaada” alisema Remi huku akiisunda kadi ile mkobani mwake.
“unahakika hutauhitaji msaada wangu?” alihoji Naibu Kamishina huku akitabasamu. Remi alimtizama bila kumjibu na kuondoka ofisini mule huku kichwa kikimuwaka moto kwa taarifa zile.
Hakika alichanganyikiwa.
Dakika kadhaa badae alikuwa ndani ya gari lake na lengo lilikuwa ni kuelekea Mwenge zilipo ofisi zake za utafiti wa mambo ya kale.
Tatizo hakujua huko nako ni moto mwingine utakao acha akili yake ikiwaka. Ila hakujua na angejua hakika angejirudia kwake tu akalale.
***
Nb; toa maoni yako kuhusu riwaya hii. Usiache kutupia maoni yako ambayo ni muhimu