mtugani wa wapi huyo
JF-Expert Member
- Dec 5, 2012
- 1,239
- 1,477
BRING BACK OUR GIRLS
SEHEMU YA KWANZA
MTUNZI: PATRICK.CK
Mlango wa ikulu unafunguliwa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania anajitokeza mbele ya waandishi wa habari walioitwa kwa dharura.Vituo vyote vya televisheni vilikatisha matangazo yao kwa muda na kurusha moja kwa moja hotuba ya rais. “ Ndugu wananchi ,siku ya leo ni siku ambayo nchi yetu kwa mara nyingine tena imekuwa muathirika wa mashambulio ya kigaidi. Mwaka huu nchi yetu ilichaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Sullivan ambao niliufungua jana jijini Arusha.Katika mkutano huo wamehudhuria watu wengi akiwamo mke wa raisi wa Marekani Bi Glory Bishop.Mambo mbali mbali yanaendelea katika mkutano huo na kwa mujibu wa ratiba ya leo hii mabinti kumi na mbili kutoka Marekani wakiambatana na wenzao wa hapa Tanzania wakiwamo pia binti yangu mimi na binti wa waziri mkuu walitakiwa kwenda kutembelea shule ya sayansi ya wasichana iliyoko nje kidogo ya jiji la Arusha ikiwa ni mojawapo ya kampeni ya kuhamasisha watoto wa kike kusoma masomo ya sayansi.Baada ya kutembelea shuleni hapo mabinti hawa pamoja na wanafunzi ishirini walielekea katika makumbusho ya viumbe wa kale yaliyoko nje kidogo ya jiji la Arusha.Wakiwa katika makumbusho hayo mabinti hawa pamoja na walinzi wao walivamiwa na kutekwa na kikundi kinachosadikiwa kuwa ni cha kigaidi na kupelekwa mahala kusikojulikana .Katika tukio hilo watu zaidi ya ishirini wanasadikiwa kuuawa baada ya kutokea milipuko miwili kubwa ya mabomu. Baada ya kuwateka watoto wetu magaidi hawa walikwenda pia katika hospitali ya mkoa ya Mount meru na kwa kutumia hewa yenye sumu wameweza kuua watu zaidi ya mia moja na ishirini.Kama hiyo haitoshi hivi ninavyoongea nanyi ndugu zangu ,wajumbe zaidi ya mia tatu waliokuwa ndani ya ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa KICC wameshikiliwa mateka na magaidi hawa.Bado hatujui nini lengo la kufanya mambo kama haya yasiyokuwa ya kibinadamu. Mke wa rais wa marekani pamoja na mke wangu nao pia wamenusurika kuuawa na mlipuko katika soko la bidhaa za utamaduni.Mlipuko huo uliowalenga wao ulitokea ndani ya soko dakika chache kabla hawajaingia humo sokoni.Watu ishirini wanasadikiwa kuuawa katika mlipuko huo. Ndugu zangu haya ni mashambulio makubwa kuwahi kufanywa na magaidi katika nchi yetu.Vyombo vya usalama vinaendelea na juhudi za kuwatafuta na kuwakomboa pamoja na watu wote wanaoshikiliwa mateka katika ukumbi wa mikutano wa KICC wengi wao wakiwa raia wa kigeni.Tumeimarisha usalama katika mipaka yetu yote na katika sehemu zote ambazo tunahisi zinaweza kuwa shabaha ya magaidi hawa.Naomba niwatoe wasi wasi ndugu wananchi kwamba vikosi vyetu viko imara na vimejiweka tayari kukabiliana na shambulio lolote lile ambalo linapangwa kufanywa na magaidi ndani ya ardhi yetu Ninapenda kuwahakikishia ndugu wananchi kwamba tutawasaka wote waliofanya kitendo hiki katika ardhi ya Tanzania ,kokote duniani na kuwatia nguvuni.Hatutamuacha hata mmoja wao.Serikali ya Tanzania haitavumilia kitendo kama hiki na vingine vyote visivyo vya kibinadamu.Tutapambana na yeyote Yule ambaye ana mkono wake katika jambo hili hata kama ana nguvu kiasi gani na mwisho tutahakikisha tunawakomboa mabinti zetu na wote wanaoshikiliwa mateka wakiwa hai. Kwa wazazi ,ndugu na jamaa ambao binti zenu wamepotea,nawasihi muwe watulivu na mviachie vyombo vya usalama vifanya kazi yake.Tukishirikiana na jumuiya ya kimataifa tutahakikisha mabinti wote wanarejeshwa mikononi mwenu wakiwa salama salimini.Tutawatafuta watoto wetu usiku na mchana,tutawatafuta mtaa kwa mtaa,nyumba kwa nyumba,pori kwa pori hadi tuhakikihsie watoto wetu wote wamepatikana.Napenda kuwasihi ndugu watanzania wenzangu tushikamane katika kipindi hiki kigumu na yeyote ambaye anaweza kuwa na taarifa zozote ambazo zinaweza kutusaidia kuwapata mabinti zetu na watu waliofanya kitendo hiki cha kinyama washirikiane na vyombo husika.Vita hii ni yetu sote,makatili hawa wamevamia nchi yetu basi tusimame pamoja na tuwaonyeshe kwamba watanzania siku zote ni wamoja na katu hawavumilii kitendo chochote kisicho cha kibinadamu kwa kusimama pamoja na kupinga vitendo hivi visivyo na hata chembe ya ubinadamu. Narudia tena kutoa pole kwa wale wote walipotelewa na wapendwa wao katika tukio hili.Watanzania na jumuia ya kimataifa tuko pamoja nanyi katika kipindi hiki kigumu.Ninachowaomba ndugu zangu tukio hili lisitugawe na kuvuruga umoja wetu .Tusibaguane kwa misingi ya dini,rangi wala kabila.Sikuzote watanzania ni wamoja na hata pale wanapopatwa na masahibu bado wanaendelea kuwa wamoja.Tushikamane na kwa pamoja tuipigane vita hii ngumu. Mungu ibariki Tanzania Ahsanteni kwa kuniskiliza. Hii ilikuwa ni hotuba fupi ya rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania akiutaarifu umma wa watanzania kuhusiana na kile kilichotokea na kinachoendelea jijini Arusha na hatua ambazo serikali imechukua na inaendelea kuchukua. Maeneo ya kati kati ya Jiji la Arusha kwa siku nzima yalikuwa kimya na tupu.Hii ilitokana na amri iliyotolewa ya kuwataka watu wote wakae ndani na wasizurure hovyo.Magari ya vikosi vya usalama ndiyo yaliyoonekana kuzunguka katika barabara za jiji hili tulivu.Mamia ya askari polisi walitawanyika katika kila kona ya jiji wakifanya doria na kuhakikisha amani inarejea.********************* Baada ya kumaliza kutoa hotuba yake kwa taifa,mheshimiwa rais akaelekea moja kwa moja katika kikao cha dharura na wakuu wa vyombo vya usalama nchini ili kujadili hali ya usalama na namna ya kukabiliana na tukio lililotokea.Wakati wakiwa katika kikao,mmoja wa walinzi wake akaingia na kumnong’oneza kitu.Mheshimiwa raisi akasimamisha kikao kwa muda na kusema “ Nimepewa taarifa kwamba katika laini ya simu kuna mtu anayedai ndiye kiongozi wa kundi linalohusika na mashambulio yote ya leo na anahitaji kuongea nami.” akasema Dr Faustine mkwaza raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Chumba chote kikawa kimya watu wote wakitaka kumsikia kiongozi huyo wa kikundi cha kigaidi.Mheshimiwa rais akabonyeza kitufe cha kupokelea simu katika simu iliyokuwa mbele yake. “ Hallo.Rais wa jamhuri ya muungano anaongea hapa ” akasema Dr Faustine “ Hallo mheshimiwa rais” ilikuwa ni sauti nzito ya kiume toka upande wa pili.Watu wote wakatazamana.Walistuka baada ya kumsikia mtu Yule akiongea Kiswahili safi “ Wewe ni nani na unataka nini? Akauliza mheshimiwa rais “ Huna haja ya kunijua jina langu lakini mimi ndiye kiongozi wa mashambulio yote ya leo.Mimi na vijana wangu tunawashikilia wasichana zaidi ya sabini .Wote wako salama kabisa na hatuna lengo la kuwafanya chochote endapo utakubaliana na matakwa yetu.Tunawashikilia vile vile wajumbe zaidi ya mia tatu katika ukumbi wa mikutano wa KICC .Tumefanya pia shambulio katika hospitali ya mkoa ya Mount meru kwa kuachia gesi ya sumu ya kuua watu wengi.Mheshimiwa rais haya yaliyotokea leo jijini Arusha ni sehemu ndogo tu mashambulio ambayo tumepanga kuyafanya hapa nchini,bado kuna mashambulio makubwa sana yanakuja endapo hautakubaliana nasi.Hivi tunavyoongea kuna watu wetu ambao wako tayari katika sehemu mbali mbali zenye mikusanyiko ya watu hapa nchini wakisubiri amri yangu tu ili waweze kuiachia gesi hiyo inayoua baada ya dakika mbili.Nakuhakikishia mheshimiwa rais kutakuwa na msiba katika kila mtaa endapo nitawapa amri vijana wangu ya kuachia gesi hiyo.” “ Kwa nini mnafanya mambo haya ya kikatili ndani ya ardhi ya tanzania? ?!!..akasema kwa ukali Dr Faustine. “ Relax Mr president.Tumeyafanya haya yote kwa sababu maalum.Tuna ombi moja tu mheshimiwa rais na liko ndani ya uwezo wako” “ Mnataka nini? Akauliza tena Dr Faustine kwa ukali “ Tunataka umuachie huru kiongozi wetu Yasin abdulkadir Husein ndani ya msaa matatu toka sasa.Tutakapompata kiongozi wetu tutawaachia wasichana wote pamoja na wajumbe tunaowashikilia katika ukumbi a mikutano.Chaguo ni lako mheshimiwa rais,utimize matakwa yetu au upeleke msiba katika kila mtaa wa nchi hii” Dr Faustine akavuta pumzi ndefu na kuwatazama wajumbe wake,kisha akasema “ Naomba unisikilize kwa makini sana.” “ Nakusikiliza mheshimiwa rais” “ Tanzania hata siku moja haiwezi kuingia mkataba na magaidi.Futa kabisa wazo kwamba tutafikia makubaliano mimi na ninyi.Kitu cha pili huyo kiongozi wenu Yasin Abdulkadir Husein hataachiwa huru kamwe.Na jambo la tatu na la mwisho ninalotaka ulifahamu ni kwamba serikali ya Tanzania itawakomboa wasichana wote mnaowashikilia ikiwa ni pamoja na kuwatia nguvuni wewe na wenzako wote” akasema kwa ukali dr Faustine “ Mheshimiwa rais tayari nimekwisha kutaarifu tunachohitaji na nimekupa masaa matatu toka sasa.Kila baada ya dakika ishirini katika saa ya kwanza tutaua watoto wawili kwa kuwachinja na katika saa ya pili tutachinja watoto wanne.Saa ya tatu na na ya mwisho tutaua watoto watano kila dakika ishirini.Muda unaanza kuhesabiwa sasa” simu ikakatwa. “ Mheshimiwa rais !!..” akasimama waziri mkuu mara baada ya simu kukatwa “ Tuko katika janga.Nchi yetu imekumbwa na mashambulio makubwa ya ugaidi.Watoto wetu wametekwa na wengine bado wanashikiliwa mateka .Watu hawa hawatanii mheshimiwa rais.Wamekwisha ua watu wetu na wataendelea kuua watu kama walivyoahidi.Tulitakiwa kuongea vizuri na mtu huyu na kujaribu kufanya makubaliano ambayo yanaweza kututoa katika janga hili.Maisha ya wat……..” “ Mheshimiwa waziri mkuu “ Dr Faustine akamkatisha. “ Naomba tuelewane kwamba tuko katika janga zito kwa maana hiyo basi lazima tuwe makini sana katika kila jambo tunalolifanya,na maamuzi tunayoyachukua.Maisha ya watanzania yako hatarini na bado kuna vitisho vingine vya mashambulio zaidi .Tunachotakiwa ni kutafuta namna ya kuhakikisha maisha ya watanzania yanakuwa salama na hakuna tena tishio lolote la mashambulio.Msimamo ninaouweka hapa ni kwamba hatutajadiliana chochote na watu hawa.Wametushambulia ,wameua raia wetu wasiokuwa na hatia,wamewachukua mateka watoto wetu na wanaendelea kuwashikilia wajumbe zaidi ya mia tatu kwa hiyo watu kama hawa si wa kujadiliana nao hata kidogo na ninaomba katika kikao hiki kusiwe na mazungumzo yoyote yanayohusiana na kujadiliana na magaidi hawa.Tutawatafuta katika kila kona ya nchi na tutawapata.Tumechokozwa na lazima tuwaonyeshe kwamba Tanzania si mahala ambapo unaweza ukafanya chochote unachokitaka na ukaachwa.” Akasema Dr Faustine kwa sauti ya amri na hakuna aliyejibu chochote .Kikao kizito kikaendelea.************************** Dakika ishirini baada ya raisi kuzungumza katika simu na kiongozi wa kikundi kilichofanya mashambulio jijini Arusha , kulirushwa video katika mtandao wa intanet iliyomuonyesha mtu mmoja aliyejifunika sura yake akitoa onyo na vitisho kwa serikali .Mtu huyo alikuwa akiongea kwa Kiswahili fasaha kabisa “ Ndugu watanzania, mmetangaziwa na rais wenu kuhusiana na kile kilichotokea jijini Arusha.Ni kweli tumefanya shambulio,tumewachukua mateka wasichana zaidi ya sabini miongoni mwao ni mtoto wa rais wenu na mtoto wa waziri mkuu.Pia tunao wasichana zaidi ya kumi na mbili wa kutoka nchini Marekani.Mateka wote wako salama na wamehifadhiwa katika sehemu salama.Hatuna nia wala lengo la kuwadhuru wasichana hawa na hatutafanya hivyo endapo matakwa yetu yatatimizwa.Tunawashikilia vile vile wajumbe zaidi ya mia tatu katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa KICC.Tuna watu wetu pia katika sehemu mbali mbali nchini zenye mikusanyiko ya watu kama mahospitalini,mashuleni n.k ambao wako na gesi ya sumu na endapo wataiachia gesi hiyo mamia ya watanzania watapoteza maisha yao.Tunachotaka ni kuachiwa kwa kiongozi wetu Yasin Abdulkadir Husein.Tumempa rais wenu masaa matatu awe ametekeleza ombi letu.Tumemwambia katika kila dakika ishirini tutaua wanafunzi wawili.Tunataka kumuonyesha kwamba tukiongea kitu hatutanii,tayari dakika ishirini za kwanza zimepita na tunaua watoto wawili na tutaendelea hivyo kila baada ya dakika ishirini.” Akafanya ishara na wasichana wawili waliokuwa wamefungwa vitambaa machoni wakiwa na sare zao za shule wakaletwa na kupigishwa magoti mbele yake. Akawafungua vitambaa.Macho yao yalikuwa mekundu na yamevimba kwa kulia. “ Binti unaitwa nani? Akamuuliza mmoja wao “ naitwa Lucy Nswami” “ Lucy una miaka mingapi? “ Nina miaka kumi na tano” “ Na wewe unaitwa nani? Akamuuliza na Yule mwenzake “ Naitwa Husna ayoub” “ Husna una miaka mingapi? “ Nina miaka kumi na sita.Tafadhali naomba msituue.Ongeeni na baba yangu ni tajiri anafanya biashara ya madini atawapa kiasi chochote cha pesa mnachohitaji.Tafadhali naomba msituue….” Yule jamaa akamtazama na kusema “ Husna angalia ile kamera na umuombe rais wako awaokoe kwa kutupa kile tulichomwambia atupatie”. Huku uso wake umefunikwa na machozi Husna akaiangalia kamera na kusema “ Mheshimiwa rais baba yetu, tunaomba utuokoe.Tumetekwa na tunahitaji msaada wako.Tumeambiwa kwamba usipowapatia wanachohitaji watatuua wote. Tunakuomba rais tuokoe tusiuawe.Sisi bado ni wasichana wadogo na tuna malengo mengi ya maisha.Tuokoe mheshim……..” akashindwa kuendelea akaangua kilio. “ Ndugu watanzania,wasichana hawa wanakwenda kupoteza uhai wao angali wadogo kwa sababu ya ukaidi wa rais wenu,mtu mliyemuamini mkampa kura na akaahidi kuwalinda.Kila baada ya dakika ishirini uhai wa wanafunzi kadhaa utapotea ikiwemo na mtoto wa rais.” Akasema Yule jamaa na kunyoosha mkono akatokea tena mtu mwingine aliyejifunika sura na mwenye mwili uliojaa akiwa na kisu kikali .Akawafunga vitambaa usoni wale wasichana na bila kupoteza muda kwa kutumia mkono wenye nguvu akamkata kichwa Lucy Nswami na kukitenganisha na kiwili wili.Mwili wa msichana Yule mdogo ukaanguka chini akakiweka kichwa juu yake halafu akamuinamisha Husna Ayoub na kumchinja. Kiongozi wa magaidi wale akaigeukia kamera na kusema “ Hawa ni wa kwanza .Tutaendelea kuua kila baada ya dakika ishirini.Mheshimiwa rais damu ya wasichana hawa ni juu yako.Muda unazidi kuyoyoma” Video ile ya kutisha ikafika mwisho.
ULIMWENGU UNASTUSHWA NA TUKIO LA KIGAIDI LINALOTOKEA JIJINI ARUSHA TANZANIA.ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII HAPA HAPA MASIMULIZI
SEHEMU YA KWANZA
MTUNZI: PATRICK.CK
Mlango wa ikulu unafunguliwa na rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania anajitokeza mbele ya waandishi wa habari walioitwa kwa dharura.Vituo vyote vya televisheni vilikatisha matangazo yao kwa muda na kurusha moja kwa moja hotuba ya rais. “ Ndugu wananchi ,siku ya leo ni siku ambayo nchi yetu kwa mara nyingine tena imekuwa muathirika wa mashambulio ya kigaidi. Mwaka huu nchi yetu ilichaguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Sullivan ambao niliufungua jana jijini Arusha.Katika mkutano huo wamehudhuria watu wengi akiwamo mke wa raisi wa Marekani Bi Glory Bishop.Mambo mbali mbali yanaendelea katika mkutano huo na kwa mujibu wa ratiba ya leo hii mabinti kumi na mbili kutoka Marekani wakiambatana na wenzao wa hapa Tanzania wakiwamo pia binti yangu mimi na binti wa waziri mkuu walitakiwa kwenda kutembelea shule ya sayansi ya wasichana iliyoko nje kidogo ya jiji la Arusha ikiwa ni mojawapo ya kampeni ya kuhamasisha watoto wa kike kusoma masomo ya sayansi.Baada ya kutembelea shuleni hapo mabinti hawa pamoja na wanafunzi ishirini walielekea katika makumbusho ya viumbe wa kale yaliyoko nje kidogo ya jiji la Arusha.Wakiwa katika makumbusho hayo mabinti hawa pamoja na walinzi wao walivamiwa na kutekwa na kikundi kinachosadikiwa kuwa ni cha kigaidi na kupelekwa mahala kusikojulikana .Katika tukio hilo watu zaidi ya ishirini wanasadikiwa kuuawa baada ya kutokea milipuko miwili kubwa ya mabomu. Baada ya kuwateka watoto wetu magaidi hawa walikwenda pia katika hospitali ya mkoa ya Mount meru na kwa kutumia hewa yenye sumu wameweza kuua watu zaidi ya mia moja na ishirini.Kama hiyo haitoshi hivi ninavyoongea nanyi ndugu zangu ,wajumbe zaidi ya mia tatu waliokuwa ndani ya ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa KICC wameshikiliwa mateka na magaidi hawa.Bado hatujui nini lengo la kufanya mambo kama haya yasiyokuwa ya kibinadamu. Mke wa rais wa marekani pamoja na mke wangu nao pia wamenusurika kuuawa na mlipuko katika soko la bidhaa za utamaduni.Mlipuko huo uliowalenga wao ulitokea ndani ya soko dakika chache kabla hawajaingia humo sokoni.Watu ishirini wanasadikiwa kuuawa katika mlipuko huo. Ndugu zangu haya ni mashambulio makubwa kuwahi kufanywa na magaidi katika nchi yetu.Vyombo vya usalama vinaendelea na juhudi za kuwatafuta na kuwakomboa pamoja na watu wote wanaoshikiliwa mateka katika ukumbi wa mikutano wa KICC wengi wao wakiwa raia wa kigeni.Tumeimarisha usalama katika mipaka yetu yote na katika sehemu zote ambazo tunahisi zinaweza kuwa shabaha ya magaidi hawa.Naomba niwatoe wasi wasi ndugu wananchi kwamba vikosi vyetu viko imara na vimejiweka tayari kukabiliana na shambulio lolote lile ambalo linapangwa kufanywa na magaidi ndani ya ardhi yetu Ninapenda kuwahakikishia ndugu wananchi kwamba tutawasaka wote waliofanya kitendo hiki katika ardhi ya Tanzania ,kokote duniani na kuwatia nguvuni.Hatutamuacha hata mmoja wao.Serikali ya Tanzania haitavumilia kitendo kama hiki na vingine vyote visivyo vya kibinadamu.Tutapambana na yeyote Yule ambaye ana mkono wake katika jambo hili hata kama ana nguvu kiasi gani na mwisho tutahakikisha tunawakomboa mabinti zetu na wote wanaoshikiliwa mateka wakiwa hai. Kwa wazazi ,ndugu na jamaa ambao binti zenu wamepotea,nawasihi muwe watulivu na mviachie vyombo vya usalama vifanya kazi yake.Tukishirikiana na jumuiya ya kimataifa tutahakikisha mabinti wote wanarejeshwa mikononi mwenu wakiwa salama salimini.Tutawatafuta watoto wetu usiku na mchana,tutawatafuta mtaa kwa mtaa,nyumba kwa nyumba,pori kwa pori hadi tuhakikihsie watoto wetu wote wamepatikana.Napenda kuwasihi ndugu watanzania wenzangu tushikamane katika kipindi hiki kigumu na yeyote ambaye anaweza kuwa na taarifa zozote ambazo zinaweza kutusaidia kuwapata mabinti zetu na watu waliofanya kitendo hiki cha kinyama washirikiane na vyombo husika.Vita hii ni yetu sote,makatili hawa wamevamia nchi yetu basi tusimame pamoja na tuwaonyeshe kwamba watanzania siku zote ni wamoja na katu hawavumilii kitendo chochote kisicho cha kibinadamu kwa kusimama pamoja na kupinga vitendo hivi visivyo na hata chembe ya ubinadamu. Narudia tena kutoa pole kwa wale wote walipotelewa na wapendwa wao katika tukio hili.Watanzania na jumuia ya kimataifa tuko pamoja nanyi katika kipindi hiki kigumu.Ninachowaomba ndugu zangu tukio hili lisitugawe na kuvuruga umoja wetu .Tusibaguane kwa misingi ya dini,rangi wala kabila.Sikuzote watanzania ni wamoja na hata pale wanapopatwa na masahibu bado wanaendelea kuwa wamoja.Tushikamane na kwa pamoja tuipigane vita hii ngumu. Mungu ibariki Tanzania Ahsanteni kwa kuniskiliza. Hii ilikuwa ni hotuba fupi ya rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania akiutaarifu umma wa watanzania kuhusiana na kile kilichotokea na kinachoendelea jijini Arusha na hatua ambazo serikali imechukua na inaendelea kuchukua. Maeneo ya kati kati ya Jiji la Arusha kwa siku nzima yalikuwa kimya na tupu.Hii ilitokana na amri iliyotolewa ya kuwataka watu wote wakae ndani na wasizurure hovyo.Magari ya vikosi vya usalama ndiyo yaliyoonekana kuzunguka katika barabara za jiji hili tulivu.Mamia ya askari polisi walitawanyika katika kila kona ya jiji wakifanya doria na kuhakikisha amani inarejea.********************* Baada ya kumaliza kutoa hotuba yake kwa taifa,mheshimiwa rais akaelekea moja kwa moja katika kikao cha dharura na wakuu wa vyombo vya usalama nchini ili kujadili hali ya usalama na namna ya kukabiliana na tukio lililotokea.Wakati wakiwa katika kikao,mmoja wa walinzi wake akaingia na kumnong’oneza kitu.Mheshimiwa raisi akasimamisha kikao kwa muda na kusema “ Nimepewa taarifa kwamba katika laini ya simu kuna mtu anayedai ndiye kiongozi wa kundi linalohusika na mashambulio yote ya leo na anahitaji kuongea nami.” akasema Dr Faustine mkwaza raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.Chumba chote kikawa kimya watu wote wakitaka kumsikia kiongozi huyo wa kikundi cha kigaidi.Mheshimiwa rais akabonyeza kitufe cha kupokelea simu katika simu iliyokuwa mbele yake. “ Hallo.Rais wa jamhuri ya muungano anaongea hapa ” akasema Dr Faustine “ Hallo mheshimiwa rais” ilikuwa ni sauti nzito ya kiume toka upande wa pili.Watu wote wakatazamana.Walistuka baada ya kumsikia mtu Yule akiongea Kiswahili safi “ Wewe ni nani na unataka nini? Akauliza mheshimiwa rais “ Huna haja ya kunijua jina langu lakini mimi ndiye kiongozi wa mashambulio yote ya leo.Mimi na vijana wangu tunawashikilia wasichana zaidi ya sabini .Wote wako salama kabisa na hatuna lengo la kuwafanya chochote endapo utakubaliana na matakwa yetu.Tunawashikilia vile vile wajumbe zaidi ya mia tatu katika ukumbi wa mikutano wa KICC .Tumefanya pia shambulio katika hospitali ya mkoa ya Mount meru kwa kuachia gesi ya sumu ya kuua watu wengi.Mheshimiwa rais haya yaliyotokea leo jijini Arusha ni sehemu ndogo tu mashambulio ambayo tumepanga kuyafanya hapa nchini,bado kuna mashambulio makubwa sana yanakuja endapo hautakubaliana nasi.Hivi tunavyoongea kuna watu wetu ambao wako tayari katika sehemu mbali mbali zenye mikusanyiko ya watu hapa nchini wakisubiri amri yangu tu ili waweze kuiachia gesi hiyo inayoua baada ya dakika mbili.Nakuhakikishia mheshimiwa rais kutakuwa na msiba katika kila mtaa endapo nitawapa amri vijana wangu ya kuachia gesi hiyo.” “ Kwa nini mnafanya mambo haya ya kikatili ndani ya ardhi ya tanzania? ?!!..akasema kwa ukali Dr Faustine. “ Relax Mr president.Tumeyafanya haya yote kwa sababu maalum.Tuna ombi moja tu mheshimiwa rais na liko ndani ya uwezo wako” “ Mnataka nini? Akauliza tena Dr Faustine kwa ukali “ Tunataka umuachie huru kiongozi wetu Yasin abdulkadir Husein ndani ya msaa matatu toka sasa.Tutakapompata kiongozi wetu tutawaachia wasichana wote pamoja na wajumbe tunaowashikilia katika ukumbi a mikutano.Chaguo ni lako mheshimiwa rais,utimize matakwa yetu au upeleke msiba katika kila mtaa wa nchi hii” Dr Faustine akavuta pumzi ndefu na kuwatazama wajumbe wake,kisha akasema “ Naomba unisikilize kwa makini sana.” “ Nakusikiliza mheshimiwa rais” “ Tanzania hata siku moja haiwezi kuingia mkataba na magaidi.Futa kabisa wazo kwamba tutafikia makubaliano mimi na ninyi.Kitu cha pili huyo kiongozi wenu Yasin Abdulkadir Husein hataachiwa huru kamwe.Na jambo la tatu na la mwisho ninalotaka ulifahamu ni kwamba serikali ya Tanzania itawakomboa wasichana wote mnaowashikilia ikiwa ni pamoja na kuwatia nguvuni wewe na wenzako wote” akasema kwa ukali dr Faustine “ Mheshimiwa rais tayari nimekwisha kutaarifu tunachohitaji na nimekupa masaa matatu toka sasa.Kila baada ya dakika ishirini katika saa ya kwanza tutaua watoto wawili kwa kuwachinja na katika saa ya pili tutachinja watoto wanne.Saa ya tatu na na ya mwisho tutaua watoto watano kila dakika ishirini.Muda unaanza kuhesabiwa sasa” simu ikakatwa. “ Mheshimiwa rais !!..” akasimama waziri mkuu mara baada ya simu kukatwa “ Tuko katika janga.Nchi yetu imekumbwa na mashambulio makubwa ya ugaidi.Watoto wetu wametekwa na wengine bado wanashikiliwa mateka .Watu hawa hawatanii mheshimiwa rais.Wamekwisha ua watu wetu na wataendelea kuua watu kama walivyoahidi.Tulitakiwa kuongea vizuri na mtu huyu na kujaribu kufanya makubaliano ambayo yanaweza kututoa katika janga hili.Maisha ya wat……..” “ Mheshimiwa waziri mkuu “ Dr Faustine akamkatisha. “ Naomba tuelewane kwamba tuko katika janga zito kwa maana hiyo basi lazima tuwe makini sana katika kila jambo tunalolifanya,na maamuzi tunayoyachukua.Maisha ya watanzania yako hatarini na bado kuna vitisho vingine vya mashambulio zaidi .Tunachotakiwa ni kutafuta namna ya kuhakikisha maisha ya watanzania yanakuwa salama na hakuna tena tishio lolote la mashambulio.Msimamo ninaouweka hapa ni kwamba hatutajadiliana chochote na watu hawa.Wametushambulia ,wameua raia wetu wasiokuwa na hatia,wamewachukua mateka watoto wetu na wanaendelea kuwashikilia wajumbe zaidi ya mia tatu kwa hiyo watu kama hawa si wa kujadiliana nao hata kidogo na ninaomba katika kikao hiki kusiwe na mazungumzo yoyote yanayohusiana na kujadiliana na magaidi hawa.Tutawatafuta katika kila kona ya nchi na tutawapata.Tumechokozwa na lazima tuwaonyeshe kwamba Tanzania si mahala ambapo unaweza ukafanya chochote unachokitaka na ukaachwa.” Akasema Dr Faustine kwa sauti ya amri na hakuna aliyejibu chochote .Kikao kizito kikaendelea.************************** Dakika ishirini baada ya raisi kuzungumza katika simu na kiongozi wa kikundi kilichofanya mashambulio jijini Arusha , kulirushwa video katika mtandao wa intanet iliyomuonyesha mtu mmoja aliyejifunika sura yake akitoa onyo na vitisho kwa serikali .Mtu huyo alikuwa akiongea kwa Kiswahili fasaha kabisa “ Ndugu watanzania, mmetangaziwa na rais wenu kuhusiana na kile kilichotokea jijini Arusha.Ni kweli tumefanya shambulio,tumewachukua mateka wasichana zaidi ya sabini miongoni mwao ni mtoto wa rais wenu na mtoto wa waziri mkuu.Pia tunao wasichana zaidi ya kumi na mbili wa kutoka nchini Marekani.Mateka wote wako salama na wamehifadhiwa katika sehemu salama.Hatuna nia wala lengo la kuwadhuru wasichana hawa na hatutafanya hivyo endapo matakwa yetu yatatimizwa.Tunawashikilia vile vile wajumbe zaidi ya mia tatu katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa wa KICC.Tuna watu wetu pia katika sehemu mbali mbali nchini zenye mikusanyiko ya watu kama mahospitalini,mashuleni n.k ambao wako na gesi ya sumu na endapo wataiachia gesi hiyo mamia ya watanzania watapoteza maisha yao.Tunachotaka ni kuachiwa kwa kiongozi wetu Yasin Abdulkadir Husein.Tumempa rais wenu masaa matatu awe ametekeleza ombi letu.Tumemwambia katika kila dakika ishirini tutaua wanafunzi wawili.Tunataka kumuonyesha kwamba tukiongea kitu hatutanii,tayari dakika ishirini za kwanza zimepita na tunaua watoto wawili na tutaendelea hivyo kila baada ya dakika ishirini.” Akafanya ishara na wasichana wawili waliokuwa wamefungwa vitambaa machoni wakiwa na sare zao za shule wakaletwa na kupigishwa magoti mbele yake. Akawafungua vitambaa.Macho yao yalikuwa mekundu na yamevimba kwa kulia. “ Binti unaitwa nani? Akamuuliza mmoja wao “ naitwa Lucy Nswami” “ Lucy una miaka mingapi? “ Nina miaka kumi na tano” “ Na wewe unaitwa nani? Akamuuliza na Yule mwenzake “ Naitwa Husna ayoub” “ Husna una miaka mingapi? “ Nina miaka kumi na sita.Tafadhali naomba msituue.Ongeeni na baba yangu ni tajiri anafanya biashara ya madini atawapa kiasi chochote cha pesa mnachohitaji.Tafadhali naomba msituue….” Yule jamaa akamtazama na kusema “ Husna angalia ile kamera na umuombe rais wako awaokoe kwa kutupa kile tulichomwambia atupatie”. Huku uso wake umefunikwa na machozi Husna akaiangalia kamera na kusema “ Mheshimiwa rais baba yetu, tunaomba utuokoe.Tumetekwa na tunahitaji msaada wako.Tumeambiwa kwamba usipowapatia wanachohitaji watatuua wote. Tunakuomba rais tuokoe tusiuawe.Sisi bado ni wasichana wadogo na tuna malengo mengi ya maisha.Tuokoe mheshim……..” akashindwa kuendelea akaangua kilio. “ Ndugu watanzania,wasichana hawa wanakwenda kupoteza uhai wao angali wadogo kwa sababu ya ukaidi wa rais wenu,mtu mliyemuamini mkampa kura na akaahidi kuwalinda.Kila baada ya dakika ishirini uhai wa wanafunzi kadhaa utapotea ikiwemo na mtoto wa rais.” Akasema Yule jamaa na kunyoosha mkono akatokea tena mtu mwingine aliyejifunika sura na mwenye mwili uliojaa akiwa na kisu kikali .Akawafunga vitambaa usoni wale wasichana na bila kupoteza muda kwa kutumia mkono wenye nguvu akamkata kichwa Lucy Nswami na kukitenganisha na kiwili wili.Mwili wa msichana Yule mdogo ukaanguka chini akakiweka kichwa juu yake halafu akamuinamisha Husna Ayoub na kumchinja. Kiongozi wa magaidi wale akaigeukia kamera na kusema “ Hawa ni wa kwanza .Tutaendelea kuua kila baada ya dakika ishirini.Mheshimiwa rais damu ya wasichana hawa ni juu yako.Muda unazidi kuyoyoma” Video ile ya kutisha ikafika mwisho.
ULIMWENGU UNASTUSHWA NA TUKIO LA KIGAIDI LINALOTOKEA JIJINI ARUSHA TANZANIA.ENDELEA KUFUATILIA SIMULIZI HII HAPA HAPA MASIMULIZI