SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA SABINI NA MOJA
Sasa askari walijigawa kulinda shule zote za mjini Masoko. Na wazazi wengine waliingiwa na uwoga sana, hawakuruhusu watoto wao waende shule. Kuruhusu mtoto kwenda shule ilikuwa ni sawa na kumpoteza kabisa!
Vilio ndani ya Kilwa vilizidi na kupaa zaidi, vikafika hadi nje ya mipaka ya Tanzania. Umoja wa mataifa kupitia shirika lake la watoto wakatoa kauli, na kuitaka Serikali ya Tanzania kuongeza nguvu katika kuwasaka wauaji hao. Marejani nayo ikatoa kauli, na kulaani pia vitendo hivyo vya kinyama. Hadi sasa watu wa Kilwa wakiwa hawajui chanzo cha mambo hayo kutokea.
Mji ulipoa, watu wakiishi kwa woga kuu. Watu wazima waliogopa, watoto wadogo waliogopa! Uwoga ulioathiri hadi shughuli za kiuchumi za Kilwa. Wakubwa waliogopa kwenda makazini, watoto waliogopa kwenda shuleni.
Wakati ulinzi ukishamiri katika shule zote za Msingi na Sekondari Kilwa. Polisi wakigeuka walinzi wa shule, kundi la Six Killers walibadirisha aina ya pigo sasa. Walevi saba walitoka majumbani kwao jioni lakini hawakurejea kwao usiku wa manane kama ilivyo ada yao. Walipokuwa wanarejea majumbani kwao usiku baada ya kulewa, njiani walidakwa na Six killers na kupelekwa porini ngome. Six Killers walikuwa wanahitaji mioyo, iwe ya watoto, iwe ya wakubwa, iwe ya walevi ama ya wazima.
Kwa bahati mbaya kabisa, miongoni mwa walevi waliokamatwa usiku ule mbaya ni mama Kindumba, rafiki kipenzi wa Mwanasheria mlevi.
Ilikuwa ni wiki kadhaa tangu Mwanasheria mlevi kutoonekana katika kilinge chao cha ulevi. Ilikuwa huzuni kwa walevi wote kutoonekana kwa Mwanasheria mlevi. Huku lawama zote zikiienda kwa jeshi la polisi ambao ndio walimchukua kwa mara ya mwisho. Lakini pamoja na kutoonekana kwa Mwanasheria mlevi, walevi hawakuacha kunywa pombe. Waliendelea kunywa pombe huku wakimlilia Mwanasheria mlevi. Hakuna hata mlevi mmoja aliyewaza kwenda kituo cha polisi kujua hatma ya Mwanasheria mlevi. Wao wenyewe walikuwa wanajihisi wakosefu. Waende kituo cha polisi halafu....
Ikaja usiku huu, usiku ambao walevi saba walipotea katika mazingira ya kutatanisha. Ukiwa ni muendelezo wa kupoteza kwa wanafunzi. Six killers walifanya kazi kwa umakini mkubwa sana, kila Mlevi alikamatwa kwa namna yake. Huku mama Kindumba akiwa mlevi wa mwisho kukamatwa usiku ule.....
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA