mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
-
- #181
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA SABINI NA SABA
Walipoingia tu ndani ya chumba chake, Daniel Mwaseba alimkaribisha Tano kutoka kundi la Six Killers.
"Karibu sana rafiki yangu, haya sasa kwa hiyari yako naomba unambie unaitwa nani?"
"Kunileta hapa haimaanishi kwamba mimi ni mateka yako, eti kwamba nitakwambia chochote unachojisikia kuniuliza" kwa mara ya kwanza Tano alijibu huku mdomo wake akiubetua kijeuri kwenda juu.
"Hahaha kumbe nawe jeuri" Daniel Mwaseba alikuwa anacheka huku akimtazama kwa umakini Tano.
Ilikuwa ni kitendo bila kuchelewa, Daniel Mwaseba alirusha teke la haraka lililotua katika goti la Tano, goti lilelile lililojeruhiwa na daktari makini kabisa, Dokta Yusha. Tano alipiga ukelele mkali sana kutokana na maumivu aliyoyapata katika goti, kutokana na pigo lile la teke toka kwa Daniel Mwaseba.
"Sipendi kukutesa kijana, naomba unambie kila nitakachokuuliza" Daniel Mwaseba aliongea maneno hayo yakienda sambamba na ngumi mbili nzito zilizompata barabara Tano katika shavu lake la kulia. Ngumi hizo zilileta athari kwa Tano, Damu zilikuwa zinamchuruzika mdomoni.
"Utasema husemi?"
"Nitasema" Tano alijibu huku akitema rundo la damu.
"Safi sana kijana"
"Unaitwa nani?"
"Tano"
"Tano nani?"
"Tano wa Six killers"
"Sijakuelewa"
"Naitwa Tano wa Six killers"
"Six killers ndio nini?"
Tano alikaa kimya.
Daniel Mwaseba alipatwa na hasira juu ya ukimya wa Tano, alirusha ngumi ya nguvu iliyotua katikati ya mdomo wa Tano, ngumi iliyorudisha jibu, meno mawili ya Tano yalidondoka sakafuni.
"Six killers ndio nini?" Daniel aliuliza kwa ukali!
Tano aliona hana ujanja, ilimpasa afanye kitu ili aweze kujiokoa katika mdomo wa kifo! Kwa nguvu zake zote Tano alisimama. Ingawa alisikia maumivu makali kwenye goti lakini alisimama. Alirusha teke la nguvu lililomkosa Daniel Mwaseba kidogo sana. Bila wepesi wa Daniel Mwaseba kulikwepa teke lile angepata madhara makubwa sana.
Tano aliyebadirika na kuwa kama mzimu alirusha ngumi ya nguvu iliyompata Daniel Mwaseba katika bega la kushoto. Tano alikuwa amechachamaa, alikuwa anataka kufa na mtu. Daniel nae akajipanga vyema sasa...
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA SABINI NA SABA
Walipoingia tu ndani ya chumba chake, Daniel Mwaseba alimkaribisha Tano kutoka kundi la Six Killers.
"Karibu sana rafiki yangu, haya sasa kwa hiyari yako naomba unambie unaitwa nani?"
"Kunileta hapa haimaanishi kwamba mimi ni mateka yako, eti kwamba nitakwambia chochote unachojisikia kuniuliza" kwa mara ya kwanza Tano alijibu huku mdomo wake akiubetua kijeuri kwenda juu.
"Hahaha kumbe nawe jeuri" Daniel Mwaseba alikuwa anacheka huku akimtazama kwa umakini Tano.
Ilikuwa ni kitendo bila kuchelewa, Daniel Mwaseba alirusha teke la haraka lililotua katika goti la Tano, goti lilelile lililojeruhiwa na daktari makini kabisa, Dokta Yusha. Tano alipiga ukelele mkali sana kutokana na maumivu aliyoyapata katika goti, kutokana na pigo lile la teke toka kwa Daniel Mwaseba.
"Sipendi kukutesa kijana, naomba unambie kila nitakachokuuliza" Daniel Mwaseba aliongea maneno hayo yakienda sambamba na ngumi mbili nzito zilizompata barabara Tano katika shavu lake la kulia. Ngumi hizo zilileta athari kwa Tano, Damu zilikuwa zinamchuruzika mdomoni.
"Utasema husemi?"
"Nitasema" Tano alijibu huku akitema rundo la damu.
"Safi sana kijana"
"Unaitwa nani?"
"Tano"
"Tano nani?"
"Tano wa Six killers"
"Sijakuelewa"
"Naitwa Tano wa Six killers"
"Six killers ndio nini?"
Tano alikaa kimya.
Daniel Mwaseba alipatwa na hasira juu ya ukimya wa Tano, alirusha ngumi ya nguvu iliyotua katikati ya mdomo wa Tano, ngumi iliyorudisha jibu, meno mawili ya Tano yalidondoka sakafuni.
"Six killers ndio nini?" Daniel aliuliza kwa ukali!
Tano aliona hana ujanja, ilimpasa afanye kitu ili aweze kujiokoa katika mdomo wa kifo! Kwa nguvu zake zote Tano alisimama. Ingawa alisikia maumivu makali kwenye goti lakini alisimama. Alirusha teke la nguvu lililomkosa Daniel Mwaseba kidogo sana. Bila wepesi wa Daniel Mwaseba kulikwepa teke lile angepata madhara makubwa sana.
Tano aliyebadirika na kuwa kama mzimu alirusha ngumi ya nguvu iliyompata Daniel Mwaseba katika bega la kushoto. Tano alikuwa amechachamaa, alikuwa anataka kufa na mtu. Daniel nae akajipanga vyema sasa...
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA