Rished Bade: Taarifa ya makusanyo ya kodi

Rished Bade: Taarifa ya makusanyo ya kodi

Hivi lengo la makusanyo lkinapangwa vipi? Maana tusiwe tunasifiana kwa kuvuka malengo kumbe tumeweka malengo ya kuruka sufuria wakati tulikuwa na uwezo wa kuruka pipa au hata simtank lita 10,000!

Mkuu umenena vema! Malengo ya naweza kuwekwa chini ya uhalisia na sisi tukabaki kuchekelea kama mazuzu. ...Kumbe tunapigwa!
 
Hivi lengo la makusanyo lkinapangwa vipi? Maana tusiwe tunasifiana kwa kuvuka malengo kumbe tumeweka malengo ya kuruka sufuria wakati tulikuwa na uwezo wa kuruka pipa au hata simtank lita 10,000!

Uko sawa kabisa mkuu ni kweli kuwa malengo yanaweza pangwa ya chini strategically kuwafanya waTanzania wawe myopic. Kumbe badala ya kuweka malengo kwenye bil 5 ingewezekana kabisa yakawa bil 10
 
Mungu akubariki kama jina lako lilivyo.

Queen Esther

Wewe umenikuna katika post yako mama!hayo maswali yako mengi ndio majibu!Natamani januari kuwe na bunge jipya la bajeti then tuweke malengo ya kukusanya trilioni 5 kwa mwezi!Kama bil 80 zimepigwa kwa siku chini 2 (achana na ambazo hazijastukiwa) vipi kwa mwezi!?
 
Uko sawa kabisa mkuu ni kweli kuwa malengo yanaweza pangwa ya chini strategically kuwafanya waTanzania wawe myopic. Kumbe badala ya kuweka malengo kwenye bil 5 ingewezekana kabisa yakawa bil 10
Kweli kabisa. maana hawa jamaa kila mwaka tunaambiwa wamevuka malengo. Sasa kama kila mwaka tunavuka malengo, kwa nini hatupigi hatua ya kuonekana?
 
Uko sahihi kabisa. Kigezo kikuu cha kukusanya mapato kinapaswa kuwa pato la taifa. Kiwango kilichowekwa kitaalamu kwa kuzingatia mazingira ya hapa kwetu ni kukusanya kodi isiyopungua 25% ya pato la taifa (GDP). Hivyo mwaka huu TRA ingepaswa kukusanya angalau Shs 22tri/- (pato la taifa mwaka huu litakuwa Sh 90tri). Kuweka lengo kiduchu la kukusanya mapato (Sh 12tri au 13% ya GDP) kama ilivyo sasa ni sehemu ya ufisadi wa kitaasisi unaoliangamiza hili taifa. Kwa kuzingatia hii hesabu ni kwamba tabaka la mafisadi (watawala ndani) wamejiwekea lengo la kupora Sh 10tri/- mwaka huu kupitia tax fraud!!

tatizo kubwa linaloikumba serikali yetu sasa hivi ni tafsiri potofu za wajibu wa mashirika ya umma. sasa hivi mashirika ya umma yamejivalisha joho la wawekezaji na kuyabinafsisha mashirika haya kwa manufaa ya wafanyakazi wake na si kwa manufaa ya taifa. angalieni nhc, bandari, atc na mengine. wanajipangia mishahara wenyewe,marupurupu na kuamua nini waipe serikali. ndiyo maana wanaposema wamevuka lengo ni lile walilokuwa wamepanga kuipa serikali. haya ni mawazo yangu .
 
Mkuu Utotole,hii ni moja ya "comment" bora zaidi kwa leo.
Wanaopanga "lengo" ndio hao hao wanaokusanya,je wakisema lengo ni bil.900 kwa mwezi kumbe hali halisi walitakiwa wakusanye bil.1500 kwa mwezi,hizo nyingine zinaingizwa mifukon mwao,nani anajua na nani anahoji na kuchukua hatua?
Hilo ndo tatizo ninaloliona hapa kwetu. Watu wanajiwekea low targets. Wanakusanya ziada wanatafuna halafu wanajisifia, na wanasifiwa na viongozi wakubwa kuwa wamevuka malengo. wanaongezewa na marupurupu kama zawadi kwa "kazi nzuri". mwisho wa siku matunda ya kuvuka malengo hatuyaoni, tunazidi kuchechemea mwaka hadi mwaka.
 
HANA LOLOTE HUYO AMEJIWEKEA VIMALENGO VIDOGO THEN HAJAWAHI KURUKA LENGO ATA SIKU MOJA ETI 99 OO 97 KWA NN ISIWE 200 OR 250 NA ZAID ILI TUJUE KILA KILICHOPATIKANA KILIREKODIWA THEN KILIENDA SERIKALINI WEWE JUST IMAGINE SSB haipo kwenye soko la hisa la DSE ,SSB ni kampuni kubwa inayozalisha bidhaa za aina nyingi, kampuni hii ni import na export wakati huo inamiliki ICD.. katika makampuni 10 yanayoongoza kulipa kodi SSB la Bakhresa halimo ,IPP la Mengi halimo Metl la Dewji hakuna ,Caspian la Rostam halimo, lakini wamiliki wake wanashindana kwa nafasi ya kwanza hadi ya nne kwa utajiri katika ukanda wa Africa Mashariki na kati, wanazidiwa na matajiri wa Nigeria , Misri na South Africa peke yake . Wote hawa hakuna aliyejisajiri kampuni yake kwenye soko la hisa ,wanapata wapi mtaji? ni ukwepaji kodi na ujanja ujanja !
 
Walio chini yake wamemuangusha!

Hiyo ishu ya kusema waliochini yake wamemuangusha ndio sipendi kuisikia kabisa!!!...Hata kwa jk ilikuwa hivyo hivyo, mkuu usipokuwa mfuatiliaji waliochini yako watapiga dili tu, mbona kwa magufuri tunaona hadi wakuu wa wilaya wanaiga mkuu anachokifanya?..
 
Sijui kwa nini ila hisia zangu zaniambia huyu Rished si mbaya. Hebu walio Bongo tuelezeni kweli ana shangingi na hekalu?
Nachukulia kufukuzwa kwake ni kwa sababu ya collective responsibility tu
 
Hivi lengo la makusanyo lkinapangwa vipi? Maana tusiwe tunasifiana kwa kuvuka malengo kumbe tumeweka malengo ya kuruka sufuria wakati tulikuwa na uwezo wa kuruka pipa au hata simtank lita 10,000!

Hilo nalo neno 😁😂
 
Hiyo ishu ya kusema waliochini yake wamemuangusha ndio sipendi kuisikia kabisa!!!...Hata kwa jk ilikuwa hivyo hivyo, mkuu usipokuwa mfuatiliaji waliochini yako watapiga dili tu, mbona kwa magufuri tunaona hadi wakuu wa wilaya wanaiga mkuu anachokifanya?..

Hii ni kauli ya kulindana tu
 
That is also my question....
Kuna kuweka standard za chini ili ku forge mafanikio...
Je hiyo ndio ilikuwa optimum capacity?
Nani anaweza kujiwekea malengo asiyoweza kuyafikia?
Yaani mtu ajisthtaki

Kwa taarifa hiyo na ukwepaji unaoonekana, kuna walakini mkubwa.

Hapa achilia mbali misamaha isiyo na maana n.k.

Nilidhani malengo yangewekwa na chombo kingine kabisa!!
 
Hivi lengo la makusanyo lkinapangwa vipi? Maana tusiwe tunasifiana kwa kuvuka malengo kumbe tumeweka malengo ya kuruka sufuria wakati tulikuwa na uwezo wa kuruka pipa au hata simtank lita 10,000!

mkuu umekula mboga yoooote!!!! Chukua LIKE
 
Uko sahihi kabisa. Kigezo kikuu cha kukusanya mapato kinapaswa kuwa pato la taifa. Kiwango kilichowekwa kitaalamu kwa kuzingatia mazingira ya hapa kwetu ni kukusanya kodi isiyopungua 25% ya pato la taifa (GDP). Hivyo mwaka huu TRA ingepaswa kukusanya angalau Shs 22tri/- (pato la taifa mwaka huu litakuwa Sh 90tri). Kuweka lengo kiduchu la kukusanya mapato (Sh 12tri au 13% ya GDP) kama ilivyo sasa ni sehemu ya ufisadi wa kitaasisi unaoliangamiza hili taifa. Kwa kuzingatia hii hesabu ni kwamba tabaka la mafisadi (watawala ndani) wamejiwekea lengo la kupora Sh 10tri/- mwaka huu kupitia tax fraud!!

Mkuu umewaka hiyob25% kwa assumption ya tax compliance kua ni 100%.
kwa nchi zinazoendela ni vigumu sana kufikia kama ulivoandika. TRA imejaribu kutengeneza mazingira ya compliance kwa kuanzisha EFD machine but still yet tunakua wagumu kuzikubali. lingine watanzania wengi hatudai risiti halali wakati wa manunuzi na kodi inatokana na documents of buying and selling hvo tusilaumu mamlaka as if wao wanapenda kutoweka malengo kama ulivoandika.
Pia tafiti mbalimbali zimefanyka ktk kuweka hayo malengo.
kwa pamoja tukionesha ushirikiano hakika kufikia lengo la 20trilion linawezekana.
 
Wapigaji walikuwa wabajiwekea target ndogo sana.
 
Hiyo taarifa tunaipata baada ya jipu kutumbuliwa? wakome kabisa waliwahi kunitoza kodi ya computa yangu used nilikwenda kumtembelea rafiki yangu ZANZIBAR akanipeleka MWANAKWEREKWE nikanunua ka koputa nilipofika badari ya DAR niligombaniwa kama mpira wa kona wakati ni komputa ya matumizi yangu tuu na zaidi sidhani kama koputa inalipiwa kodi.

Hiyo taarifa ilitolewa kabla Bade hajasimamishwa. Aliyeileta hapa atachanganya wasomaji kwa kutokuweka tarehe taarifa hiyo ilipotolewa. With the benefit of hindsight, naweza kusema kwamba Bade alishanusa kuwa yuko matatani. Hapa alikuwa anajihami kwa kujaribu kujenga taswira kuwa TRA chini ya uongozi wake imeongeza makusanyo ya kodi na kwamba kila kitu kiko sawa. Hapa alikuwa anajaribu ku-preempt Watanzania pengine na Rais Magufuli mwenyewe kwamba hata tuhuma dhidi yake zikitolewa, pengine si za kweli kwa kuwa TRA imefikia malengo yake ya ukusanyaji wa kodi kwa asilimia unaokaribia 100%. Taarifa hiyo ni ya kwanza kuisikia kutoka TRA inayoonesha mwenendo wa ukusanyaji wa mapato (sina hakika kama Bade alipata kutoa taarifa nyingine inayohusu mwenendo/mafanikio ya ukusanyaji mapato kabla ya hii) na ilitolewa siku chache baada ya Magufuli kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa Rais.
 
Hii taarifa kaitoa lini wakati kasimamishwa tayari ukurugenzi mkuu wa TRA? hizi ni akili ndogo sana kwa hiyo ndiyo mmeona njia pekee ya kumsafisha ni kujidai mnaleta hapa taarifa za kipumbavu ili tuone bilioni 80 zetu hazina maana.......naomba mh rais usirudishwe nyuma na huu ujinga ambao wasiofikiri nyuma ya pazia tu ndo utakao wanasa na wewe si mmoja wao......"Hapa kazi Tu"
 
Nasikia faraja sana na michango yenu wakuu ambayo haina uitikadi bali ina utaifa.TRA lilikuwa janga la Taifa ,kazi yao kubwa ilikuwa kuonea wafanyabiashara wadogo na wafanyakazi huku wafanyabiashara wakubwa wakipeta. Dr Magufuli kwa kutumia uzoefu wake mwingi wa kukaa kwenye baraza la Mawaziri atakuwa analijua hilo.Ni muda wa kulitumbua kabisa jipu hilo japokuwa lipo sehemu ya siri.
 
Back
Top Bottom