Serikali inapokusanya Kodi inaweka AKIBA?

Serikali inapokusanya Kodi inaweka AKIBA?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,860
Reaction score
50,644
Pamoja na kukusanya Kodi kwa ajili ya kazi za Serikali, jee Kila mwezi TRA wanapokusanya Kodi, watu wa Hazina huwa wanaweka AKIBA?

Kuna mwaka tuliwahi kuweka akiba angalau ya asilimia kumi ya makusanyo ya Kodi? Au kila tunachokusanya tunakitumia?
 
Kubwa la Mokobaz.
mzee Uchebe.
👇

images (3).jpeg
 
Bajeti ya Tanzania ni tegemezi kwa asilimia kubwa, kwa muktadha huo si rahisi kuweka akiba ya kutosha ya pesa. Labda kama wameanza kuweka akiba ya dhahabu kama malighafi.
 
Bajeti ya Tanzania ni tegemezi kwa asilimia kubwa, kwa muktadha huo si rahisi kuweka akiba ya kutosha ya pesa. Labda kama wameanza kuweka akiba ya dhahabu kama malighafi.
Tuseme unayoyasema ni kweli. Jee Serikali haiwezi kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuweka akiba?
 
Tuseme unayoyasema ni kweli. Jee Serikali haiwezi kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuweka akiba?
Ripoti ya CAG inaonyesha ubadhirifu na matumizi yasiyoeleweka ya zaidi ya shilingi Trillion 1. 5 katika mwaka wa fedha unaoisha Julai. Ambapo zaidi ya shilingi bilioni 600 ni mashirika ya umma, serikali kuu bilioni 300, serikali za mitaa na halmashauri ni bilioni 130. Kama uwajibikaji hakuna katika matumizi ni wazi kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ni jambo lisilowezekana.
 
Adverse Effect ndiyo hoja yangu hiyo. Kwa ivo uwezekano wa kuweka akiba upo, tatizo hakuna utashi wa kufanya hivyo.

Kama Kila mwaka tungekuwa tunaweka akiba angalau ya shilingi trilioni mbili, basi kila baada ya miaka mitano tungekuwa na kiasi kisichopungua trilioni kumi. Jee hizo fedha zisingetosha kuwekeza kwenye sekta muhimu kama Kilimo?
 
Sidhani hata kama kwenye kamusi ya serikali kuna neno AKIBA

Nchi zingine wanaweka sana dhahabu
Sisi tunajua madeni tu na sidhani hata kama yatakuja kwisha

Halafu wengi wanajua deni la Taifa ni kiasi gani, ila hawajui kuwa tunalipa Riba tu deni linaongezeka kila kukicha
 
Sidhani hata kama kwenye kamusi ya serikali kuna neno AKIBA

Nchi zingine wanaweka sana dhahabu
Sisi tunajua madeni tu na sidhani hata kama yatakuja kwisha

Halafu wengi wanajua deni la Taifa ni kiasi gani, ila hawajui kuwa tunalipa Riba tu deni linaongezeka kila kukicha
Na nadhani watawala wetu wamejua watanzania wanadhani maendeleo huletwa na watu binafsi nje ya mipango ya Serikali.

Kwa watanzania wengi Serikali ni dubwasha fulani hivi lisilo na mahusiano nao kwa maisha yao ya kila siku kiuchumi!
 
Na nadhani watawala wetu wamejua watanzania wanadhani maendeleo huletwa na watu binafsi nje ya mipango ya Serikali.

Kwa watanzania wengi Serikali ni dubwasha fulani hivi lisilo na mahusiano nao kwa maisha yao ya kila siku kiuchumi!
Wengi hawajui haki zao kabisa na hata serikali ni nini

Bunge halina nguvu ya kupinga chochote wala kujibu ingawa wao ndio wawakilishi wa wananchi.

Angalia Bunge la UK juzi wamepinga muswada uliotaka kupitishwa na waliopinga ni wabunge 120 wa Chama tawala

Sisi Mbunge mmoja akipinga kitu au kuhoji ni shida wakati mwingine

IMG_0445.jpeg
 
Watu wetu wapo bize na challenge za kuimba na kucheza nyimbo za wasanii!!
 
Serikali ya Kenya kufika mwisho wa mwaka huu watakuwa wameweka akiba ya shilingi za Kenya zaidi ya bilioni mia sita.
 
Back
Top Bottom