Rished Bade: Taarifa ya makusanyo ya kodi

Rished Bade: Taarifa ya makusanyo ya kodi

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya jumla ya shilingi trilion 3.77 kuanzia mwezi Julai hadi Oktoba 2015 ambayo ni sawa na asilimia 97.6. ya lengo la makusanyo ya sh trilioni 3.87 ikiwa ni jitihada za TRA kutekeleza mkakati wa serikali ambao unaitaka kukusanya Ths . Trililioni 12.3 kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Kwa mujibu wa Kamishna Mkuu wa TRA Rished Bade, mwezi Julai TRA ilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 849,582.9 ambacho ni asilimia 99.4 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 854,922.9.

Mwezi Agosti TRA ilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 890,536.7 ambacho ni asilimia 101.5 ya lengo la kukusanya shilingi biilioni 876,974.2 .ambapo mwezi Septemba jumla ya shilingi trilioni 1.07 zilikusanywa ikiwa ni asilima 91.7 ya lengo trilioni 1.16 kwa mwezi mwezi Oktoba TRA iilkusanya shilingi bilioni 970,089.6 ikiwa ni asilima 99.3 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 976,441.5.

Taarifa ya mwenendo wa makusanyo ilipitishwa na Bodi ya Wakurugenzi ya TRA katika kikao cha bodi kilichofanyika jana tarehe 10 Novemba 2015 katika ofisi za makao makuu ya TRA? amesema Bw. Bade.

Mafanikio katika makusanyo haya yametokana na mikakati madhubuti iliyowekwa na mamlaka baada ya kusaini mkataba na Waziri wa Fedha ambapo Kamishna Mkuu alisaini mkataba na kila Mkuu wa Idara na wakuu wa Idara kusaini mikataba na wafanyakazi walioko chini yao ili kila mfanyakazi kuwajibika ipasavyo.

Wito wa TRA ni kwa mfanyabiashara na wadau wote wa kodi kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangia pato la taifa.

Sambamba na hilo TRA imepokea kwa furaha sana wito wa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli wa kuhimiza ukusanyaji wa mapato bila woga na bila kumwonea mtu.

Pamoja Tunajenga Taifa Letu

Rished Bade


KAMISHNA MKUU
http://www.tra.go.tz/index.php/about-tra/465-taarifa-ya-makusanyo-ya-kodi
Hii pesa bado ni ndogo ukilinganisha na wizi unaofanywa bandarini! Haya malengo bado hayashabiani na kiasi halisi kinacho patikana hapo!

Bado kabisa kufikia malengo yaliyo wekwa hakumaanishi hakuna ukwepaji wa kodi!
 
Kama nilisikia vizuri Magufuli alisema serikali inakusanya kodi chini ya kiwango kwa miaka 3 sasa. Sielewi hii taarifa ya TRA kama ni sahihi
 
Kama makusanyo yako almost asilimia 100 na ukwepaji kodi ni mkubwa hivyo kuna shida zifuatazo:-

1. Wakadiriaji malengo hawaitendei haki nchi hii kwa kutoa malengo ya chini sana

2. Wakadiraji kodi wanashirikiana na wakwepa kodi

3. Wanaoweka viwango vya ukusanyaji wanashirikiana na wanaokwepa kodi. Lengo tupige makofi kuwa compliance ni 100% huku tunaibiwa. (Staili ya kuuma na kupuliza)


Kuna mambo hayako SAWASAWA somewhere??? Huwezi kuvuka malengo na kujipongeza wakati tumeibiwa mpaka basi!!!

Queen Esther

Wewe umenikuna katika post yako mama!hayo maswali yako mengi ndio majibu!Natamani januari kuwe na bunge jipya la bajeti then tuweke malengo ya kukusanya trilioni 5 kwa mwezi!Kama bil 80 zimepigwa kwa siku chini 2 (achana na ambazo hazijastukiwa) vipi kwa mwezi!?
 
Pale mwisho angeandika "bila kumuonea mtu huruma." Hakuna mtu anaonewa Mr. Bade. Ni vijisenti tu bilioni 80 vinatafutwa.
 
Pamoja na upigaji wote huo twafika kiwango icho am sure uyu mpya anaweza fika 1.5tril kwa mwezi
 
Hawa wapewe 2tril target na wizi wote huu wanafika 100%
 
Kama hayo malengo ya makusanyo wanajipangia wenyewe, basi ni usanii tu hapo..
 
Hivi lengo la makusanyo lkinapangwa vipi? Maana tusiwe tunasifiana kwa kuvuka malengo kumbe tumeweka malengo ya kuruka sufuria wakati tulikuwa na uwezo wa kuruka pipa au hata simtank lita 10,000!
That is also my question....
Kuna kuweka standard za chini ili ku forge mafanikio...
Je hiyo ndio ilikuwa optimum capacity?
 
naona un bashiri mapungufu
Sio hivyo mkuu. Hii nchi imekubuhu kwa ukwepaji wa kodi na nakumbuka Basil Mramba alifanya kazi kubwa sana kutambua wigo wa kodi na kuingiza walipa kodi zaidi kupitia mfumo wa TIN. Hadi sasa wanasema kama mfumo wa kodi ungelikuwa wa haki na usawa ingeliwezekana kabisa VAT kuwa 12%, PAYE 6% na walipaji kuwa na moyo zaidi wa kulipa kwa hiari.
Cha kushangaza TRA wanasema 'wamefikia malengo', na ndio maana nikasema wangelimuuliza vizuri labda angeliwapa ufafanuzi niliouweka lakini kwa hali ya sasa ilitakiwa aseme wamefikia 40% ya kinachotakiwa ili wananchi wanaoelewa ukubwa wa tatizo waje kumuonyesha ni vipi anaweza kuifikia hiyo 98% ya ukweli!

 
Nina hakika hata hayo malengo waliyojiwekea ni madogo mno.Kwa nchi kubwa na tajiri kama Tanzania kukusanya billioni 850 tu kwa mwezi ni utani.Hawa wamejiwekea malengo madogo ili waibe.Ni lazima kuwe na very independent bodies za kuhakiki malengo yao.Tusiwaamini hao,si mmeona wameshatuingiza mkenge.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya jumla ya shilingi trilion 3.77 kuanzia mwezi Julai hadi Oktoba 2015 ambayo ni sawa na asilimia 97.6. ya lengo la makusanyo ya sh trilioni 3.87 ikiwa ni jitihada za TRA kutekeleza mkakati wa serikali ambao unaitaka kukusanya Ths . Trililioni 12.3 kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Kwa mujibu wa Kamishna Mkuu wa TRA Rished Bade, mwezi Julai TRA ilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 849,582.9 ambacho ni asilimia 99.4 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 854,922.9.

Mwezi Agosti TRA ilikusanya kiasi cha shilingi bilioni 890,536.7 ambacho ni asilimia 101.5 ya lengo la kukusanya shilingi biilioni 876,974.2 .ambapo mwezi Septemba jumla ya shilingi trilioni 1.07 zilikusanywa ikiwa ni asilima 91.7 ya lengo trilioni 1.16 kwa mwezi mwezi Oktoba TRA iilkusanya shilingi bilioni 970,089.6 ikiwa ni asilima 99.3 ya lengo la kukusanya shilingi bilioni 976,441.5.

Taarifa ya mwenendo wa makusanyo ilipitishwa na Bodi ya Wakurugenzi ya TRA katika kikao cha bodi kilichofanyika jana tarehe 10 Novemba 2015 katika ofisi za makao makuu ya TRA? amesema Bw. Bade.

Mafanikio katika makusanyo haya yametokana na mikakati madhubuti iliyowekwa na mamlaka baada ya kusaini mkataba na Waziri wa Fedha ambapo Kamishna Mkuu alisaini mkataba na kila Mkuu wa Idara na wakuu wa Idara kusaini mikataba na wafanyakazi walioko chini yao ili kila mfanyakazi kuwajibika ipasavyo.

Wito wa TRA ni kwa mfanyabiashara na wadau wote wa kodi kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangia pato la taifa.

Sambamba na hilo TRA imepokea kwa furaha sana wito wa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli wa kuhimiza ukusanyaji wa mapato bila woga na bila kumwonea mtu.

Pamoja Tunajenga Taifa Letu

Rished Bade


KAMISHNA MKUU
Tanzania Revenue Authority - Taarifa ya makusanyo ya kodi
 
hawa jamaa wakijiwekea lengo la kukusanya trillion 12 ujue kuna trilion 10 hazijakusanywa zipo mikononi mwa wakwepa kodi.
wao wenyewe wanakuwa wametia hasara ya trilion 5.
 
Uko sahihi kabisa. Kigezo kikuu cha kukusanya mapato kinapaswa kuwa pato la taifa. Kiwango kilichowekwa kitaalamu kwa kuzingatia mazingira ya hapa kwetu ni kukusanya kodi isiyopungua 25% ya pato la taifa (GDP). Hivyo mwaka huu TRA ingepaswa kukusanya angalau Shs 22tri/- (pato la taifa mwaka huu litakuwa Sh 90tri). Kuweka lengo kiduchu la kukusanya mapato (Sh 12tri au 13% ya GDP) kama ilivyo sasa ni sehemu ya ufisadi wa kitaasisi unaoliangamiza hili taifa. Kwa kuzingatia hii hesabu ni kwamba tabaka la mafisadi (watawala ndani) wamejiwekea lengo la kupora Sh 10tri/- mwaka huu kupitia tax fraud!!

Great thinker Nginana uko right kwa 100%, kujisifia ukusanyaji wa 13% ya GDP ni kidogo sana kwa taifa lililodhamiria kukusanya kodi... point of reference Burundi wanakusanya 17.5% ya GDP, Kenya 18.4%, Ghana 21%, South Africa 26%, Swaziland 39%, Lesotho 42%. JPM anayo nafasi ya kutufikishia makusanyo ya 25% ndani ya miaka 10 akiamua. Go JPM, go....!
 
Tusubiri taarifa ya mwaka ujao
tutalinganisha....

Tuanzie kwanza na assessment ya kuweka malengo, malengo yanawekwa based on previous perfomances au capacities? Nimewahi kuchunguza kampuni moja ambayo uwezo wake kuzalisha (Capacity and opportunities) ulikuwa mkubwa sana lakini kutokana na operational inefficiencies nyingi ikawa hawafikii malengo yake, viongozi wakaamua kukaa na kujiwekea malengo madogo kuendana na walichokuwa wanakipata, laiti kama wangeboresha mambo kadhaa tu basi wangefikia malengo yao makubwa at full potential. Tuchunguze, TRA katika ubora wake wanaweza kukusanya kiasi gani ndio iwe target!
 
Wanaweka malengo kidogo ili wafikie na kuiba nyingi,wapuuzi tu ,
 
Back
Top Bottom