PostGE2025 Ripoti ya Jaji Chande: Maswali Mazito Baada ya Uchaguzi

PostGE2025 Ripoti ya Jaji Chande: Maswali Mazito Baada ya Uchaguzi

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Tajiri wa kinyankole

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2019
Posts
1,971
Reaction score
4,890
Kwa taarifa ya tume ya uchinguzi wa mambo yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa raisi wabunge na madiwani october 29.2025 na jaji chande imeonesha kuwa baadaya ya uchunguzi tume imebaini kuwa

1.Polis walikuwa kwenye vituo vya kupiga kura bila siraha.
Sasa maswali mengi watu wanajiuliza je watu waliojeruhiwa kwa vitu vyenye ncha kali je walijeruhiwa na watu gani wakati wa maandamano.

2.kuwepo kwa vifo zaidi 500
Kama vyombo vya dola havikutumia silaha hao waandamanaji waliuawa na nani na wauaji walitumia nini.

3.watu kujiteka kwasababu ya madeni na imani za kishirikina pamoja na usafirishaji wa binadamu nchi za nje
Je ni kweli polepole na watu wengine walijiteka kama anavyosema yeye kwenye uchunguzi kwasababu ya madeni na imani za kishirikina ?

4.kwamba tume haijajikita kutaja watu waliohusika na yaliyotokea october 29 isipokuwa vichocheo vilivyofanya yatokee ya october 29.sawa tumeelewa.

Je hii kauli ya kusema upelelezi ufanyike tena kujuwa watu waliosababisha yatokee ya october 29 na wawajibishwe mnaona yupo sawa huyo mliyemkabidhi makaburasha ya uchunguzi? Unasema unataka kuridhiana ! Unaridhiana na nani na unafanya upelelezi kubsini wahusika wawajibishwe.

Hivi viongozi wa serikali hamuoni mnateketeza fedha za umma kwa hadaa na ulaghai kwa mambo ambayo mnajuwa hamuwezi kuyatekeleza.

Hivi ni lini viongozi wa serikali mtaelewa kuwa kwa sasa tanzania ya sasa haina watu wa miaka 1980 wa kudanganywa kila kitu.

Madaraka yanaisha ipo siku mtajibu kwa matendo yenu ya hatari mliyoyaratibu kabla wakati na baada ya uchaguzi mkuu.

Mtambue kuwa jinai haifi na sheria huwa zinabadilika msishangae kuja kuwa wafungwa wa baadae kwa matendo mliyoyafanya.
 
Swali la msingi kabisa na ambalo linaaibisha serikali na taasisi zake za usalama, Mzee Chande anasema kuna watu wengi walikusanywa kwenye kambi na kupewa mafunzo yaani muda wote usalama hawakujua hadi watu wanafanya fujo na tume kuundwa ndiyo wanajua?

Je kama ni hivyo ingekuwaje kama hao watu wangepewa na silaha?

Je nini ingetokea.

Na hii si kuiweka uchi nchi kwamba haina ulinzi imara?

Yaani anasema kuna kundi kubwa lilikuwa linapatiwa mafunzo karibu na kituo cha polisi na polisi hawakujua lolote.
 
Alisema kuna kijana wa Arusha(16) aliahidiwa atapewa milioni 5 ili afanye vurugu....

Kiukweli ile ripoti ni nyepesi sana.. halafu vitu vya msingi havijaripotiwa na sababu alizotoa hazikuwa na mashiko
 
Alisema kuna kijana wa Arusha(16) aliahidiwa atapewa milioni 5 ili afanye vurugu....

Kiukweli ile ripoti ni nyepesi sana.. halafu vitu vya msingi havijaripotiwa na sababu alizotoa hazikuwa na mashiko
ALiongea upuuzi mtupu mbona huyo kijana hakumtaja jina na walq hakuwataja waliomhaidi hiyo pesa
 
Alisema kuna kijana wa Arusha(16) aliahidiwa atapewa milioni 5 ili afanye vurugu....

Kiukweli ile ripoti ni nyepesi sana.. halafu vitu vya msingi havijaripotiwa na sababu alizotoa hazikuwa na mashiko
Mkuu, kwa akili ya kawaida yaani eti mtu aliyelipwa (na nani?) na kukubali kuandamana ajipeleke mbele ya tume kama shahidi huku akijua kuna uharibifu mkubwa wa mali na vifo vilitokea kwa yeye kukubali kushawishiwa kuandamana??.
Kwangu mie naona haya ni maigizo ya uvccm ili kuhalalisha yale maneno ya samuya wakati ule eti kuna watu walilipwa kuandamana!

Mtu aliyeshawishiwa kwa namna yoyote kushiriki maandamano hawezi kukubali kwenda kutoa ushahidi mbele ya tume,
Ni sawa na mhalifu kujipeleka mwenyewe kituo cha polisi, wabongo tunajuana vzr hakuna wa hivi tume iache utapeli!!!.
 
ALiongea upuuzi mtupu mbona huyo kijana hakumtaja jina na walq hakuwataja waliomhaidi hiyo pesa
Ripoti ina mapungufu mengi kana mwamba mtu alikaa zake ndani akaandika na kuja kuiwasilisha. Jaji ametukosea sana. Halafu anasema kuna watu walioshawishi lakini kashi dwa kuwataja.
Arejeshe pesa zetu asee
Mkuu, kwa akili ya kawaida yaani eti mtu aliyelipwa (na nani?) na kukubali kuandamana ajipeleke mbele ya tume kama shahidi huku akijua kuna uharibifu mkubwa wa mali na vifo vilitokea kwa yeye kukubali kushawishiwa kuandamana??.
Kwangu mie naona haya ni maigizo ya uvccm ili kuhalalisha yale maneno ya samuya wakati ule eti kuna watu walilipwa kuandamana!

Mtu aliyeshawishiwa kwa namna yoyote kushiriki maandamano hawezi kukubali kwenda kutoa ushahidi mbele ya tume,
Ni sawa na mhalifu kujipeleka mwenyewe kituo cha polisi, wabongo tunajuana vzr hakuna wa hivi tume iache utapeli!!!.
Halafu walikaa muda mrefu na ripoti inakuja ile... Yaani mambo mengi yanashangaza kweli.
 
Back
Top Bottom