LordJustice1
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 2,263
- 533
The most stupid way of interpreting things. What do you know about prima facie evidence? Huyu dogo alitoa siku saba kwa waropokaji hawa kuja na ushahidi, ku-retract porojo zao au wafikishwe mahakama. If you are saying the seven days expired yesterday, did you expect him to knock the court doors today? He needs time to prepare court documents that institute proceedings that will sure take a few days. This is not like sighting of the moon, it is a process that starts the moment the accuser fails to take heed to the demand notice.
Lakini ambacho ni cha kushangaza ni taarifa kwamba huyo anayeitwa Dr. na mnayemtukuza sana ame-despatch watu kwenda mikoani kutafuta ushahidi baada ya kupokea demand notice na hii inamaanisha kwamba alitumwa kuropoka na mafisadi wanaomtumia wakati hakuwa na ushahidi wowote ule na kwa sababu amezoea watu kutishia bila kuchukua hatua, sasa ameona kabisa hatari iliyo mbele yake. case ya Mtikila hatuwezi kuisemea kwa sababu case yake ya insanity ni well documented na sasa anachofanya ni kutafuta ajira ya kusogeza siku baada ya kugeuka kuwa irrelevant kwenye political equation ya nchi hii.
Tatizo lako hufuatilii vyombo vya habari! Tarehe 03/05/2011 Dr Slaa na Mch Mtikila walimjibu Fisadi Ridhiwani Kikwete kwamba hakuna haja ya kusubiri mambo ya siku saba, kwa hiyo aende tu mahakamani!
Slaa, Mtikila wamtega mtoto JK
Tuesday, 03 May 2011 21:50
Leon Bahati na Raymond Kaminyoge
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemtega mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, akisema akifanikiwa kukifikisha chama hicho mahakamani atakuwa amefanikiwa kula mfupa ambao uliwashinda vigogo waliowatangazwa hadharani kuwa ni mafisadi nchini.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa msimamo wake kuhusu kauli ya Ridhiwani aliyoitaoa Dar es Salaam juzi, kuwa atamfikisha mahakamani ili kuthibitisha kauli yake kwamba mtoto huyo wa rais ni bilionea aliyepata utajiri wa kutisha kipindi kifupi.
Ridhiwani alimpa siku saba Dk Slaa, kuanzia jana awe amekanusha kauli hiyo ya kumtuhumu kuwa fisadi, vinginevyo atamfikisha mahakamani.
"Sisi tunasema atangulie huko mahakamani sisi tutakuja nyuma," alisema Dk Slaa.
Dk Slaa ambaye katika uchaguzi uliopita aligombea urais na kutoa upinzani mkubwa kwa Rais Kikwete aliyetangazwa kuwa mshindi, alisema kauli za kushtakiwa wanapotangaza taarifa za ufisadi hadharani zimekuwa za kawaida.
Alisema wengi waliwahi kutoa kauli kama hiyo kupitia vyombo vya habari baada ya kuwatuhumu hadharani kuwa ni mafisadi, lakini wakashindwa kwenda mahakamani.
"Chadema tuna uzoefu tulipotaja orodha ya mafisadi walitutishia kuwa watatushtaki mahakamani tukawaambia watangulie sisi tutakuja nyuma, lakini walishindwa kutekeleza ahadi yao," alisema Dk Slaa na kuongeza kuwa, iwapo Ridhiwani atafanya hivyo atakuwa amevunja rekodi ambayo imewashinda watu wazito.
Katibu huyo ambaye umaarufu wake ulikuja kwa kasi kipindi cha miaka 15 aliyokuwa Mbunge wa Karatu, Arusha, alijigamba kuwa hawazungumzi jambo bila vielelezo ndio maana wanajiamini kwa kila wanachokisema hadharani.
Dk Slaa alitupia lawama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwamba amekuwa akisisitiza ifutwe kwa sababu inashindwa kufanya kazi yake, ikiwamo kufanya uchunguzi kwa watu wanaotuhumiwa kupata utajiri katika mazingira yenye utata.
Katika mkutano na waandishi wa habari, Ridhiwani alikanusha kuwa kijana bilionea kama Dk Slaa anavyomtuhumu.Alisema anamiliki shamba mkoani Pwani, lenye ukubwa wa ekari 1.5, gari ndogo na akaunti kwenye benki ya CRDB, NBC na Stanbic, ambazo hakutaja kiasi cha fedha.
Dk Slaa alipinga vikali kauli hiyo na kwamba, alimaliza shule miaka michache iliyopita, lakini sasa ni bilionea na utajiri huo aliupata kwenye mazingira ya utata.
Wakati huohuo, Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema atatoa uthibitisho mahakamani kuhusu mali alizozitaja kuwa zinamilikiwa na Ridhiwani.Siwezi kumuomba radhi mtu, nina uhakika wa kuwa kijana yule anamiliki mali ambazo hajazipata kwa njia halali, itakuwa vizuri ikiwa atanipeleka mahakamani, kwani huko ndiko nitakakoonyesha uthibitisho wangu, alisema Mchungaji Mtikila.
Jumamosi iliyopita, Mtikila alikaririwa na vyombo vya habari akisema, Ridhiwani ni bilionea anayemiliki nyumba za ghorofa, malori, kampuni za ujenzi wa barabara na ardhi.
Source: Mwananchi.