Hakika suala la upumbavu wako lilikuwa hisia mpaka wewe mwenyewe uliapojitolea kulithibitisha kupitia hii thread yako ya kijinga ambayo kwa mara ya kwanza inakiuka misingi ya sheria iliyowekwa na waasisi wa sheria ambao waliidadavua kwa umahiri. Msingi muhimu wa sheria ni ule unaosema "He who alleges must proove". Hawa makanjanja wawili wametoa broadsides ambazo mpaka leo hazina chembe ya uthibitisho. Badala ya kuwataka waonyeshe ukomavu na kuaminika kwao kwa kuja na ushahidi unaothibitisha tuhuma zao basi wewe unaandaa mob justice ambayo nina hakika haitapata uungwaji mkono na yeyote mwenye akili timamu, labda watu wa aina yako.
Unadhani watu watababaishwa na kauli zako ambazo kimsingi zinafanana na hao watoa tuhuma ambao shida yao ni political expedience badala ya kuangalia madhara ya uropokaji wao kwa reputation zao, vyama vyao na kikubwa zaidi, wahanga wa tuhuma zao za kupandikizwa na kutumwa na vinara wa ufisadi wa nchi hii. Tengeneza polisi wako wenye ufinyu wa fikra kama wewe ndipo uwatume wafanya hizo un-ethical behaviours halafu uone kama zitapata uungwaji mkono. Mimi ningekushauri uwe na ujasiri wa kuwashauri hao miungu wako wawili kuja na vielelezo vitakavyotufanya tumtie adabu huyo dogo badala ya kugeuka kunguru ambaye kazi yake ni kunyea watu huku akiendelea kuruka bila kujua madhara ya uchafuzi huo. Kilicho wazi ni kwamba wazee hawa wawili wataburutwa mahakamani na hakika hakuna kipindi muafaka cha kuwavua nguo mbele ya jamii kama hiki. Wakati wewe unashabikia, kwa taarifa yao huyo Dokta wako kachanganyikiwa na sasa ame-deploy watu mikoani kuunga unga kile anachodhani ni ushahidi ambayo maskini haitamsaidia kwani ni afterthought ambayo haina hata chembe ya ukweli.
Brother ni vizuri ukahakikisha kwamba kiungo kilicho katikati ya masikio yako unakishughulisha kabla hujaingia humu jamvini.