Negan The Dead
JF-Expert Member
- Mar 6, 2017
- 340
- 994
hii nchi bila kujipendekeza hakuna cheo.Halafu leo rais analalamika kua watu hawana uzalendo wakati inajulikana cheo kinapatikana kwa kujikomba komba.Naangalia taarifa ya habari startv, namuona Richard Kasesera akitambulishwa kama mwenyekiti wa Bodi ya madini.
Swali lililonijia kichwani mara moja hadi nikaamua kushare nanyi wadau wa JF ni hili; Je huyu kada ana wasifu(sifa) gani hadi kustahili kuwa mwenyekiti wa bodi hiyo?
Kwa kuzingatia changamoto nyingi na kubwa tulizonazo katika sekta ya madini, Je huyu kada anaweza kutoa mchango wowote katika kuiboresha?
Katiba mpya haiepukiki hata magamba wafanye nini!