Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
Miaka ya sabini na themanini Tanzania iliwika katika riadha kwa kutoa wanariadha maarufu kama Filbert Bayi, Suleiman Nyambui, Mwinga Mwanjala, Nzael Kyomo, Mosi Ali, Gidamis Shahanga na wengineo. Baada ya "kizazi" hicho, riadha ikaporomoka na zama za leo hatusikiki tena.
- Kipi kilichotuwezesha kuwika zama hizo na kipi kinatufanya tushindwe zama hizi?
- Ni kupuuza michezo au miaka hiyo ilikuwa ya bahati?
- Tufanye nini kurejesha heshima yetu?