Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika Hodhi la Reli (RAHCO) Bw. Masanja Kadogosa akielezea jambo mbele ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto) wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kimataifa (Standard Gauge) ambapo awamu ya yenye urefu wa Km 205 inajengwa kutoka Dar – Moro.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akikagua ujenzi wa tuta kwa ajili ya njia ya reli alipotembelea eneo la Soga (Kibaha) wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Reli ya kiwango cha kimataifa (Standard Gauge) yenye urefu wa kilomita 205 kutoka Dar – Morogoro leo. Kutoka kulia ni Meneja Mradi wa SGR Mhandisi Maizo Mgedzi, Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Kampuni ya Yapi Merkezi Bw. Abdullah Kilic na Mhandisi Felix Nnalio.
Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Kampuni ya Yapi Merkezi Bw. Abdullah Kilic akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu ujenzi wa tuta la reli ya kisasa ya SGR alipotembele eneo la Soga (kibaha) leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akifafanua jambo mbele ya Meneja wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Kampuni ya Yapi Merkezi Bw. Abdullah Kilic (katikati) alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Reli ya kiwango cha kimataifa (Standard Gauge) ambapo awamu ya kwanza inajengwa kutoka Dar – Moro yenye urefu wa 205km.
Muuonekano wa awali wa tuta la reli linaloendelea kujengwa kwa kuondolewa tabaka la udongo wa kilimo na kuwekewa udongo wa ujenzi katika eneo la Soga (Kibaha) ambapo mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa unaendeleo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitazama kifaa cha kupima mgandamizo wa ardhi mara baada ya ardhi kushindiliwa alipokagua ujenzi wa tuta la reli katika eneo la Soga (Kibaha).
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiendelea na shughuli ya ujenzi wa karakana ya kutengeneza mataluma ya reli alipokagua ujenzi alipofanya ziara katika eneo la Soga (Kibaha).