Regina Mwalekwa atimba Clouds FM

Regina Mwalekwa atimba Clouds FM

Kama ni kweli anaaminika kwa utumishi makini anaweza akachomoza hata kwenye radio za vichaa kwani ukichanganya mafuta na maji uchakachuaji utajidhihiri tu.
 
R.mwalekwa(first from left)
UMAKINI.jpg

Ni kawaida kwenye free market watu ku move. Lakini wakati mwingine binadamu na ajira anafananishwa na ngombe wa kufugwa mmoja anapoona mwenzake kapewa majani anakula anafikiria yale ya mwenzake ni matamu zaidi na akipata mwanya huenda mbio kuonja. Njia pekee inayoweza mwajiri kujali wafanyakazi ni wakianza kuhama. Kama Mengi alikuwa anawabania huenda akabadilika
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Radio Clouds FM ni wabunifu na vipindi vyao ni vizuri tu.
Ukimsema mtu ukiona amekasirika ujue ujumbe umefika, clouds fm kupitia vipindi vyao vya power breakfast, leo tena na jahazi, wamekuwa wakiijulisha jamii mambo mbalimbali.
Binafsi naipenda clouds fm na nadhani regina mwalekwa ataongezea ubunifu zaidi ili kukonga nyoyo za wasikilizaji wa clouds fm. Na leo nimemsikia mwalekwa akila kiapo kuwa atatupasha habari sahihi kutoka mjengoni bungeni,dodoma.

nyaisanga wapi?
 
MILADI AYO naye anafuata soon....ITV & radio One utawala mbovu, majungu na chuki
Kuhama Radio One na kwenda Clouds ni ukosefu wa maarifa tu. unatakiwa uende Radio za juu sio Radio za kubahatisha!
 
there is no a bad company, people leaves bad managers
 
Aliyekuwa mtangazaji wa Radio One na ITV Milad Ayo ajiunga ramsi na Clouds FM na kutambulishwa kwa wafanyakazi wenzake!!
 
Fuata nyayo za Suzan Mungi, hata hivyo huko clauds naona kama umechemka anyway.
 
Jamani tuache majungu. Kuacha kazi ni sehemu ya maisha na si lazima kampuni iwe na matatizo. Hivi Regina aliyepelekwa kusoma na Radio Tumaini then aliporudi tu akaacha kazi na kwenda radio 1, tuseme pia kulikuwa na shida Radio Tumaini?

Kuna watu wanahama kazi kama kwenye bank industry? Kila siku watu wanaacha na kuhamia benki zingine na pia kwenye Cellular companies. Kuna watu wanaogopa kuacha kazi ndo tatizo la kuona kama wanaoacha kazi wanaonewa. Kwa taarifa yenu , watu wanaopata mishahara mikubwa mara nyingi ni wale wanaoacha kazi na kwenda sehemu ingine.

Radio one jamani kuna watu kila siku wanatamani kufanya kazi pale. Kuna watu waliacha kazi alafu wakarudi kuomba msamaha kwa mzee Mengi na sasa wapo wanatangaza ITV.
Kuhusu Clouds, jamani hakuna kampuni kubwa na ndogo. Cha msingi ni kuangalia terms zako wakati wa ajira. Kuna watu wanalipwa zaidi Clouds na kuna wengine wanalipwa posho ; sawa na makampuni mengine.
Fikiria mtu anaacha kazi CRDB na kwenda DCB. nk
 
acha atafute maslahi bora ukubwa au udogo wa kampuni auhu kwa sababu hapendi kuzinunua yeye ni mwajiriwa tu
 
mahija zayumba naye atimkia clouds fm.
Bila shaka kuna maslahi zaidi pale
 
Jinsi sauti yake ilivyo nzuri atakwenda BBC soon,
kuacha kazi kwenye makampuni ni kitu cha kawaida,
pia huenda ni explorer then atarudi Radio one.
 
Back
Top Bottom