Bado itanichukua muda mrefu kukubalina na huu ukweli. Sura inanijia machoni kila nikimkumbuka. Siku tuliyokaa nae alipokuja Arusha hainitoki akilini. Story na ucheshi wake unanirudiarudia kila ninapoziona thread zinazomuhuzu.
Kweli huu msiba umeniumiza sana. Nashindwa hata kupost kwenye baadhi ya thread maana akili haijakubaliana na habari za msiba huu! Napata shida sana ndugu zangu. Ni basi tu!
Raha ya milele umpe ee Bwana, na mwanga wa milele umwangazie, apumzike kwaamani, amina!
Roho ya marehemu ipate rehema kwa Mungu, apumzike kwa aman, amina!
RIP dada yangu Regia Mtema!