Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 56,289
- 92,376
Ndugu zangu nimeshitushwa sana na matangazo ya Redio uhuru siku ya jumatano tarehe 2 mwezi 3 mwaka 2011, muda saa 2 mpaka saa 3 usiku. nikiwa naugulia mgao wa umeme huku nikiwa na kiredio changu cha mchina kinachotumia betri niliona nisikilize redio uhuru, kipindi kinaitwa CCM yajenga nchi mtangazaji wa kipindi ni Angel Akilimali, walianza na hotuba ya JK kujibu hoja za CHADEMA huku waki edit ile hotuba na kuweka vikorombwezo vyao, ilo sikulijali, lakini kilichonistua baadae vikakalibishwa vibibi viwili eti ni waasisi wa TANU, hapo ndipo walipoanza kumshushia matusi yasiosemeka Dr Slaa binafsi Na chadema NA wakadiliki kusema hata mabomu ya gongo la mboto ni Dr Slaa ndio ameyalipuwa. nina hakika kama redio nyingine binafsi ndio ingerusha kipindi kile kuwatuhumu viongizi wa ccm basi ingeshafungiwa, Je viongozi wa Chadema na wapenda haki hamfuatilii vitu hivi na kuripoti tume ya mawasiliana na baraza la habari?