Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Mendy anaweza akakosa game ya marudio dhidi ya City, ni pengo kubwa sana kwetu, maana jana alinisaidia kumzima yule Savio, tukabaki na usumbufu upande mmoja tu wa Doku, baada ya kutoka ndio jamaa wakapata uchochoro., sijui itakuwaje ila acha tusubiri.
 
Noma sana man, sijui alimchungulia aje, wale vijana wa Arbeloa wanajituma hatari, ni kwamba wanataka nafasi ama ni kawaida? Maana kila mahali uwanjani walikuwepo.

Wale watoto washajua mpira ndio maisha yao kwahiyo wakipewa nafasi lazima waitumie vizuri. Lakini safi sana Arbeloa kuwapa nafasi vijana
 
Wale watoto washajua mpira ndio maisha yao kwahiyo wakipewa nafasi lazima waitumie vizuri. Lakini safi sana Arbeloa kuwapa nafasi vijana
Kiukweli wanajitahidi sana, ni muda mrefu sana hatujatumia vijana kutoka Castilla kwa kiwango hiki, kama alikuwa Ancelloti sijui kama angewatumia, ila Arbeloa anawaamini, ndio maana hata Castilla ilifanya vema sana chini yake.
 
Kiukweli wanajitahidi sana, ni muda mrefu sana hatujatumia vijana kutoka Castilla kwa kiwango hiki, kama alikuwa Ancelloti sijui kama angewatumia, ila Arbeloa anawaamini, ndio maana hata Castilla ilifanya vema sana chini yake.

Castilla wamefurahi Arbeloa kuchukua timu, wanajua hata kama sio wote lakini baadhi watapewa debut
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…