Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread


Na hiyo ndio sifa kubwa ya Carlo, anaweza kucheza mifumo tofauti na wachezaji wa style tofauti, Hebu mchukue Pep halafu mkabidhi Valverde, Jude, duarani na nyuma Militao na courtois golini atakula nyingi mpaka atatia aibu. Pep akikosa tu kipa anaeweza kucheza na mpira basi tayari amekwama.
 

Wengi wanashindwa kuelewa hilo, makocha wengi huwa wanakwama pale.
 
Macho yako hua Kwa Bellingham Tu, Wengine wakicheza Chini ya kiwango husemi, Una matatizo wewe

yeye ndio yupo kwa ajili ya kuibeba timu, Star player anatakiwa awazibie mpaka mashimo wengine, ila naona yeye ndio amekuwa Ghost uwanjani kukliko yoyote.

Binafsi mimi sina tatizo nae jamaa, mana namuelewa uwezo wake vizuri, ni everage players at best, anaetemebelea upeopo wa Taifa lake.
Nashindwa kuwaelewa wanaomshabaikia na kusema ni mchezaji bora Dunia, Yani mchezaji bora wa dunia anakaa vile? Dah sijwahi kuona kabisa
 
afu kuna sehemu anakwambia musiala ndio anafaa kuwa mbadala wa Luca modric yani watu wanafatufanya si wengine tunatazama mpira kwa kutumia matumbo

Mkuu, tulimuona Musiala alivyoupiga mwingi, hata humu jamavini wengi wamekuballi kuwa jamaa anaupiga, Lakini Kijana wako Mbona alipotea uwanjani?
 
Nope ni typing error ilikuwa top worst signings ni eden Hazard na kakaView attachment 2978556

Hazard alikuwa destined to fail, Mimi binafsi nililitabiri hilo, NIkawa naitwa hater kama hawa Jude fan boys wanavyonita ssa hivi, Uwezo wake ulikuwa limit kidogo kwa ku perform timu kama Madrid ila sio wengi waliofahamu hilo. Alikuwa ana udhaifu mkubwa ambao niliamini ungelimuangusha pale Real.

Kaka alisumbuliwa sana na majeraha, na alipokuwa tayari ameshapowa vizuri tayari palikuwa na Ozil ambae ameshashika namba akiwa moto, lakini kaka hata hapo alipokuwa real bado alikuwa ana perform vizuri kila alipopata nafasi.
 
Mkuu, tulimuona Musiala alivyoupiga mwingi, hata humu jamavini wengi wamekuballi kuwa jamaa anaupiga, Lakini Kijana wako Mbona alipotea uwanjani?
kwahyo kuupiga mwingi Ndio awe mbadala wa luca modric kirahisi ivo embu acheni utani basi kweny mambo serious apo apo mmenda mbali mnasema don carlo ni kocha wakawaida kuweni serious kidogo
 
ni mawazo yako it's okay yaheshimiwe but hawa waliopo still bado ni wachezaji wetu hata mtu aweje inabidi tumvumilie sisi kama fans tumkumbatie maana huyo ndio wetu sisi

still kwa jude naona bado muda wakutoa conclusion kwa wanaomjua vizur ni one of the best player in the world right now

1 starter for England team CAM hamna wakumuweka benchi

2 price tag of 180m watu walio mvalue sio kwamba hawajui mpira kutuzidi sisi

3 21G/A in laliga ni wapili toka dovbky na amekuwa mchango mkubwa hasa katika mechi za laliga alikuwa on fire

4 he is young with much time to adapt from the best in order for him to be the best

5 ongezea
 
context wise

jude v/s musiala

age... both watoto wa 2003 mmoja june (jude) mwengine feb ( musiala) soo musiala ni kaka

preferred foot and position

jude right foot plays false 9 ... CAM... CM... LCM... LW

musiala right and left foot plays CM... CAM.. LW.. RW

PRICE TAG

JUDE... 180M
MUSIALA... 110M


PLAYING STYLE

JUDE a, mix player of mostly defence at CM ball carrier and good technical passer with solid accuracy plus interceptions

MUSIALA.. an offensive machine an overall better dribbler playmaker lethal wing forward who can cause serious problems to your goal at either RW or LW

JUDE plays somehow in the same composer as Zidane lakini ni mzito flani hivi na hii ndio uzaifu wake mkubwa

MUSIALA.. wachambuzi wanasema huyu ndiye kivuli cha messi kwa mbali maana hakuna best dribbler kwa sasa zaidi ya huyu kijana shida yake hana shot accuracy nzuri inampelekea kuwa na number ndogo za magoli kuzidi jude
 
Ninaangalia marudio hapa, kuna save Neur alifanya dhidi ya Kroos, daah, sijui ule mpira ulionaje, yaani lile lilikuwa goli kabisa.
Mi mwenyewe Nilishangaa Kwa footwork ya toni niliamini lile lilikua bao,

Kati ya magolie ninao waheshimu aliebaki ni huyu wa Buyern, jamaa hua haelewekagi maamuzi take,

Anyway laiti Kama angelimsogeza kidogo Tu kwenye mtambaa panya kule jamaa asinglifika.
 
SUALA LA JUDE BELLIGHAM NA JAMAL MUSIALA SI MJADALA.

Kabla ya Mechi ya Jana sikuwahi kusikia wala kuona mjadala Kama huu ukikua kiasi hiki.

Jude kacheza Bundasliga zaidi ya misimu miwili,
na walikutana Sana Tu kwenye Derby ya Buyern Munich Vs Borussia dortmud,
mashabiki na nyie wachambuzi na vingereza vyenu mlikua kimya kwann?

Kwann huu mjadala umeanza Jana baada ya Mechi na si kabla ya Mechi?

Vipi Kama mechi hiyo Madrid angeshinda je huu mjadala ungekuepo?

Kwann wamesubiri Jude Acheze Chini ya kiwango mechi moja,
then mechi hiyo hiyo mtumie kumlinganisha Kwa kiwango cha jumla na Jamal aliekua kwenye high performance mechi husika?

Kama mkijadili kuhusu mechi ya Jana Tu Jamal Vs Jude,
To be honest Jamal alikua na mechi Bora Sana Jana.

Ila mkitaka tujadili kuhusu kwa ujumla nani zaidi Kati Yao Kwa kuzingatia Performance na Quality ya hawa wawili hapana Kwa kweli,
Jamal kua juu ya Jude nimekataa,

Sijakataa kwamba Dogo ni Talented Footballer,
nachopinga ni kumshindanisha na mtu alie juu yake.

Tazama takwimu zao.

Jamal ana miaka 21 Jude 20,

katika michuano ya UEFA champions League.

Jamal ameanza kushiriki msimu wa 2020-21, Jude hivyo hivyo pia.

Jamal Mpaka sasa amefanikiwa kucheza Mechi 33 Jude 32,

Jamal Kafunga Goal 4 Jude 10.

Jamal katoa Assist 3, Jude 9.

Jamal hajaingia hata mara moja kwenye UEFA Champions League Team of the Week,
Jude kaingia mara 3,

Takwimu hazimbebi Jamal labda anacho-mzidi Jude ni umri na namba ya jezi Tu,
42 Kwa 5.

Japo ni Mjadala huru Sio lazima uamini mwenzako anachokiamini,

Ila Jiulize Kwann JUDE akiwa kwenye ubora wake husikii watu wakimshindanisha na JAMAL?.

Kiungwana kabisa Jamal ni mchezaji mzuri Sana,
Ila kumpandisha mtu sio lazima umshushe mwingine
angalieni na wa kushusha.

Haters Haters Haters

"Ondoeni chuki binafsi Mu-enjoy football".
 
Nope ni typing error ilikuwa top worst signings ni eden Hazard na kakaView attachment 2978556
Hata haukukosea, ni sahihi kabisa, Luka Modric magazeti ya Spain yalim-rate kama worst signing of the season., na haikuwa uongo, Luka alipata wakati mgumu sana kuingia kwenye mfumo, na shida kubwa ilikuwa aina ya wachezaji tuliokuwa nao kwa kipindi kile na aina ya kocha tuliyekuwa nae.
Isingekuwa rahisi kwake kucheza kwenye team iliyokuwa inatumia nguvu kama ile, wewe huwezi kushangaa kuna kipindi Pepe alikuwa anacheza kama kiungo, Essien anacheza kama beki wa kulia, game zetu zilikuwa na matumizi makubwa sana ya nguvu.
 
Sioni haja ya huu mjadala., sana sana kuna watu wanataka kumshusha Jude basi., ila ninachojua ni kuwa kijana bado ana muda wa kubadilika na kuendelea kuimarika, ndio kwanza ana miaka 20 tu.
Kama Vinicius Jr amebadilika na kuimarika sioni kwanini isiwe kwa Jude.
 
Nusu fainali ya Champions leauge 2011 na Barcelona mechi ya pili ile ya Bernabeu jose katikati ya kiwanja alikua na Pepe, Diarra,Alonso afu kweny beki wa kati kaanza na Albiol na Sergio Ramos kulia Arbeloa kushoto Marcelo game mechi nzima kilikua kinatembea kiatu tu had Marcelo alikua anachapa kiatu balaa Pepe aliambulia tu kupata kadi nyekundu Jose ile timu alikua anaipeleka kuwa timu ya WWE sio ya mpira tena
 
yeah wakikaa wakikumbuka vinny alinunliwa kwa almost 40m kutoka flamingo FC mpaka akajakupewa jezi nzito namba 7 basi uvumilivu ni kitu bora sana kwenye mpira

vijana wetu wote wana, quality nzuri na kuhusu hio debate ya jude na musiala ni sawa sawa na mechi ya jana sancho na mbappe nani alikuwa bora

of course sancho made 12 successful dribble most dribble than any other made in English player... last time a person made those amount of dribble was messi v/s Manchester utd final

swali jee sancho ni bora kuzidi mbappe well... its complicated to answer kisa mmoja, jana kafanya poa zaidi ya mwengine wakati bado kuna second leg its the same kwa jude na musiala watu wanasema musiala did wonders than jude sababu musiala alikuwa na, advantage ya home ground fans na ile composer yakufanya anacho kifanya nakupelekea mtu kama jude (mbappe) kuwa kwenye shadow now the next leg ndio itawafunga watu midomo

kila mtu ashinde mechi zake nyumbani kwake
 

Na tatizo kubwa la huyo kijana ndio hilo, one of the best player in the world, sijua huwa mnatoa wapi munakubali kukaririshwa tu, One of the best player in the world ndivyo anavyokua na standard ile? yakupotea uwanjani gam nzima? Jamaa Champion league toka ianze round of 16 hana Goli wala Assist.

1. kuwa stateter England sio hoja yenye mashiko mana hata Magure nae pia ni starter England

2. Aliekwambia nani kuwa watu wakituoa hela ndefu wanajua wanachokifanya? Barca ililipa nearly 160m kwa Coutinho wakaishaia kula hasara nzito, hao Madrid walilipa 100m kwa hazard wakaishia shoti ndefu. chelsea wamtumia nearly 1 B ndani ya misimu miwili na timu ipo kwenye hali mbaya sana, tuache maisha ya kukariri sio kila wanachofanya wazungu ndio lazima kiwe sahihi.

3. nakukosoa mkuu amepitwa pia na lewandowski sio dovbky peke yake, na ni kweli amkua na mchango ila mkuu since January hata goli tano hajafikisha, upeopo umkata mda mrefu sana sasa.

4. Experience yangu inanambia ni ngumu sana kwa wachezaji wa kiengereza kudevolope zaidi ya wanapoanzia, wengi wao best years zao ni wakiwa makinda.
 

Tofauti ya Jude na Vini ni kuwa wakati hicho kipindi vini ana develop hatukusia wala kuwahi kutangazwa kuwa Best Player in the world, wakati huyu kijana wao tumekuwa tukisia hizo nyimbo karibu mwaka sasa kuwa ni best player in the world.
 

Jude yupo juu ya Musiala? Duh! Simchezo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…