Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Hapa naona bado jude hatujampata vizuri yuko chini ya kiwango, akiiva siku si ndio balaaa
Mdogo mdogo team inakaa kwenye mstari, ujio wa Kroos kwenye midfield na Camavinga kama beki wa kushoto umetusaidia sana., uwepo wa hawa watu unatusaidia ku-control dimba vizuri, hii inamsaidia Tchouameni kutimiza majukumu yake vizuri.
Tumebaki na tatizo la kujilinda tu, na huyu Kepa kiukweli simuamini wala nini, nilitamani Lunin aendelee kukaa golini.
 

Yaah toni ndio anamalizia msimu huu tuachane sijui kama camavinga ataiweza iyo nafasi, maana kila akicheza hapo unaona anapwaya sana
 
Ila hii formation kama diamond shape Fulani hv kuanzia kati kwenda mbele kama inaanza kuniingia akilini hivi, timu pinzani lazima uchanganyikiwe hujui anafunga nani, mara paaap Jude anakuja kukufunga daaah naona Jude Kama hachezi deep sana kama alivyokuwa BVB..as Bavaria fan nimeielewa hii system ya Carlo hasa kuanzia kati natamani sana muje kuitekeleza vizuri kwetu Bavarians in UCL though najua tutapigwa.
 

Ni system nzuri ila inatunyima buildup kiasi kikubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…