Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Namshangaa huyu dogo kang'ang'ania Madrid na Barca hazina mashabiki mwanzo mwisho.

Kumbe mashabiki wake tupo na atujaanza kuzishabikia leo wala jana.
For these 2 decades spanish clubs zimedominate major EUROPEAN TITLES hata upande wa international trophies spanish football imedominate sana soka la ulaya na dunia.
Leo city wapo ivo kwa sababu wanacheza mfumo wa spanish football ambayo ni asili ya soka la dutchmen
 
Mkumbushe hvi real madrid ndio club of the century hadi sasa anashikilia iyo tuzo
Hawawezi kuelewa mkuu. Hiyo tuzo nakumbuka ilitolewa Rome siku kadhaa kabla ya kumaliza karne ya 20, December 2000. Madrid ikashinda kwa zaidi ya asilimia 43, Man U akawa wa pili kwa asilimia kama 9 hivi na Bayern wa tatu. Milan tulikua wa 9. Fifa wameitambua Madrid kama klabu bora kwa miaka 100 nyuma kuanzia mwaka 2000, tayari akiwa na European cups za kutosha, na hiyo badge ya Fifa mpaka leo wanayo kwenye jezi yao kifuani pale, afu anatokea mtu anasema mashabiki wa Madrid wamefuata uefa miaka ya karibuni. Sitashangaa wakibeba pia hiyo tuzo kwa karne ya 21. Kubishana nao ni kupoteza muda tu.
 
Mkumbushe hvi real madrid ndio club of the century hadi sasa anashikilia iyo tuzo
Sina tatizo nafahamu Madrid ni team kubwa wana UCL 14. Hoja yetu ni kuwa mashabiki wa Madrid bongo wana timu zao EPL wanashabikia Madrid kama second option.

Na hata mechi za La Liga wengi hawaangalii zaidi zaidi kuona matokeo Livescore na YouTube. Wengi wanaangalia El Classico tu utabisha ila huo ndio ukweli.
 
Hivi huko shuleni mlielewa maana ya karne?, unaposema umefanya vizuri karne 3 au 4 unajua ni miaka mingapi?, kweli mmevurugwa😅😅
 
Hivi unaelewa kweli unachoandika? Kwamba sababu La Liga au Serie A hazionyeshwi vibanda umiza unahisi watu hawafuatilii?
 
Hype fan base popularity massive investment ntakubaliana na ww ila spanish clubs zinawatesa sana english clubs that is black and white when it comes to EUROPEAN CUPS
Sipingi hilo La Liga imekua Ligi bora kwa miaka mingi (Madrid na Barca). Na wameshinda Ballon d or nyingi plus best Fifa XI La Liga wametoa wachezaji wengi.

Point ni kwetu Tanzania watu wengi hawafuatilii La Liga tofauti na El Classico na hao wanaoshabikia Barca na Madrid hao hao wana timu wanashabikia za EPL.
 
Kwa waliozaliwa 2000's ni sahihi unachosema. Sababu ule msimu wa 2010-2011 ambao City alichukua Epl dakika ya mwisho kwa goli la kihistoria la Aguero vs QPR ni mwaka ambao waliozaliwa 2000's ni kama ndo walianza kua na ufahamu wa mpira
Sasa aliezaliwa 2000 si watu wazima hao tupo nao JF na kwenye mabanda umiza. Nimeona madogo wengi sana mashabiki wa city miaka kadhaa mbele wala hatutashangaa kuwaona.
 
Waambie hata PEP ni muispaniola mkatalunya ulipozaliwa mpira.

Aliifanya Barca kuwa timu tishio.Ilicheza mpira ambao wenye akili timamu wote tunakubaliana hakuna timu yoyote duniani itaucheza.

Mwambie pia Mancity imeigeuza EPL kuwa farmers league kwa sababu ya falsasa za Guardiola kuamini katika possesion football kinyume kabisa ma matimu ya uingereza yasiyojua mpira.

Umeona mpira anaoucheza Guardiola?

Anawatesa sana lakini bado wanaona Uingerza kuna mpira kuliko Spain.
 
Hivi huko shuleni mlielewa maana ya karne?, unaposema umefanya vizuri karne 3 au 4 unajua ni miaka mingapi?, kweli mmevurugwa
Ninaweza nikawa nimeongeza chumvi kwa kuweka idadi kubwa ya Karne zakutawala lakini haiondoi ukwel kuwa kwa karne/century hii ya 21,Real Madrid ndio Club Bora kwa sasa.

Ili upunguze nguvu kubwa sana unayotumia kuamini kitu ambacho hakina ukwel,anza kusoma Post ya kwanza kabisa iliyoanzishwa na Salamander na uangalie wachangiaji wake hadi leo itakupunguzia stress zakuamini unachoamini.

Lakini kwa kukusaidia tu soma historia ya hivi vilabu na uelewe misingi yake ya uanzishwaji ulikuwaje,ndio maana utaona hata wanazi wa madrid huku huwa hatuna kelele wala lugha chafu dhidi ya wengine.

Huwa tupo juu and we are the best na ndio maana huwa hatuna haja yakujieleza,mafanikio yanajieleza na pengine ndio maana mnaona kama hata wanazi wa huku wanaringa.

Sent from my SM-A336E using JamiiForums mobile app
 
Hivi unaelewa kweli unachoandika? Kwamba sababu La Liga au Serie A hazionyeshwi vibanda umiza unahisi watu hawafuatilii?
Ngoja nikueleweshe. Nimeongelea kibanda umiza kama sample. Watanzania wengi wa hali ya kawaida hawana uwezo wa kumiliki DSTV hivyo huangalia mechi kibanda umiza au kununua kinywaji bar ili kutazama mechi.

Hivyo basi sijawahi kuona mtu anatoa pesa yake ili akatazame mechi ya Madrid vs Valencia au hata Barcelona vs Espanyol ila ni kawaida kukuta mtu anaenda kuangalia mechi ya Man City vs Brighton, au Liverpool vs Westham, au Man u vs Aston Villa huo mfano unaonesha msingi wa hoja yangu.
 
Mkumbushe tuu anapokuwepo PEP kama cocha wa club hata timu ya taifa alipo hiyo club mfumo wa uchezaji wake hubadilika. Alipo kuwa Buyern soka Dutchland likaanza kucheza tik tak. Leo hii ENGLISH NATIONAL TEAM ni timu shindani ikicheza INTERNATIONAL CUPS huku ikiwa na uchezaji wa pasi nyingi.
 
Kila zama na kitabu chake.
 
Msingi wa hoja yangu haupo kwenye ubora wa La Liga vs EPL. Msingi ni kwamba mashabiki wengi wanashabikia Barca/Madrid kama second option ya kufata glory ya UEFA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…