Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Mwaka 2018
16 bora: vs PSG, bingwa wa France
Robo: vs Juve, bingwa wa Italy
Nusu: vs Bayern, bingwa wa Germany
Final: vs Liverpool, mshindi wa pili EPL
-Psg tumekutana nae 16 bora tena ikiwa na Mbappe ambae ni matured pamoja na Messi.
-Robo tumekutana na Chelsea bingwa wa UEFA kwa wakati huo. Juve haina record nzuri UEFA kufananisha na Chelsea Fc.
-Nusu tumekutana na Mancity bingwa wa England. kwa Bayern ile siwezi kuibeza walikuwa moto pia.
-Finali tumekutana na Liver
ambayo Salah ni mzima, hakuna kisingizio tena.

Bila kusahau kwenye makundi tulikuwa na Inter(bingwa wa Italy)
 
Hii ndio maana halisi ya Ligi ya Mabingwa, huwa ninakuwaga na amani sana pindi tu tunapopangiwa kukipiga na hao wakali, ina maana unapata kipimo sahihi mapema, so ukifanikiwa kupita hapo hata morale ya wachezaji inakuwa juu sana.
Ninakumbuka baada ya kuwatoa PSG Modrić alisema kuwa hii ni mpaka final, kwamba kuvuka pale haikuwa rahisi, so hawakuoana tena team ya kuwasimamisha.
 
Ni kweli, pia vijana waliopata nafasi msimu uliopita hawakutuangusha, hiyo inatupa mwanga hata Modric na Benzema wakiondoka bado tutakuwa na watu wenye uzoefu na haya mashindano.

Niwe muwazi, katika vijana wetu wote Vinicius amenishangaza hasa kuanzia msimu uliopita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…