RC wa Dar es Salaam kutoa usafiri kwa Ombaomba wanaotaka kurudi makwao mwezi wa 6

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,279
1622133021602.png

Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam imesema ipo tayari kutoa usafiri kwa ombaomba wanaotaka kurudi kwao kwa hiari ifikapo mwezi wa sita mwaka huu. Huku akiwataka Wakuu wa wilaya kuratibu zoezi hilo ikiwamo pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria mawakala wanao waleta kutoka mikoani.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makala amewataka ombaomba wote walipo Dar Es Salaam kujiandikisha kwa hiari majina yao pamoja vijiji wanavyo toka ili ofisi yake iweze kuwarudisha nyumbani na kuwaepusha na vitendo vya ukatili wa kijinsia ifikapo mwezi wa sita mwaka huu ofisi yake iweze kuwapa usafiri wa kuwafikisha makwao suala ambalo ameleza limewapa usumbufu wakuu wa mikoa waliopita akiwemo Mzee Yusufu Makamba.

Aidha Mhe. Makala ameongezea kuwa suala la ombaomba limekuwa mradi kwa mawakala ambao uwasaidia ombaomba hao kuwasafirisha kutoka makwao na kuwapagishia vyumba pamoja na kuwapa chakula na kuwataka walelete pesa wanazoomba kila siku.

Katika hatua nyingene Mkuu wamkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye madhimisho ya siku ya kujenga uwelewa juu ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atakuwa mgeni rasmi.


ITV
 
Siyo majambazi, mafisadi na wachezea mifumo ya serikali tu wanaomjaribu rais Samia hata Chadema wanamjaribu.

Leo wametangaza maandamano ya kudai katiba mpya na tume huru yani wanataka rais aache kufocus na kukamilisha SGR ,Bwawa la nyerere ,ajira, viwanda ambavyo ndiyo hitaji la wananchi akaanze kutenga mabilioni ya fedha kwa ajili ya katiba ambayo ni hitaji la wanasiasa tu?

Mbaya zaidi wanataka mchakato wa katiba uanze upyaaaaa na siyo pale ulipoishia zamani
 
Hao jamaa huwa wanapelekwa kwao na kurudi, nauli wanazo, itafutwe njia itakayowafanya watulie wakifika kwao, kama ni kutunga sheria or whatever I don't know.
 
Back
Top Bottom