RC Mtanda atoa maelekezo kwa Mdau aliyedai kuna Kiongozi anamlinda mtuhumiwa wa Ulawiti kwa Mtoto

RC Mtanda atoa maelekezo kwa Mdau aliyedai kuna Kiongozi anamlinda mtuhumiwa wa Ulawiti kwa Mtoto

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mtanda.jpeg
Muda mfupi baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuwasilisha dokezo akihoji Kiongozi gani wa juu ambaye anamlinda mtuhumiwa wa Ulawiti kwa Mtoto kutoka katika Kituo cha Polisi Kirumba, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda ametoa maelekezo kwa Mwananchi huyo kuhusu kipi anachotakiwa kukifanya.

Kusoma hoja ya Mdau bofya hapa ~ Kiongozi gani wa juu Kituo cha Polisi Kirumba anazuia tuhuma hizi za ulawiti kwa mtoto huyu wa Nyakato - Mwanza?

RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui.

Ameongeza “Asiposikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne kila wiki.”

Ikumbukwe Mdau alisema mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sektoure vikaonesha kweli ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Mtu kutoka ‘juu’
RC Mwanza.jpg

WhatsApp Image 2025-08-07 at 15.53.03_f4c7a72d.jpg

Pia soma ~ Sakata la Mtoto aliyelawitiwa Nyakato - Mwanza, RC Mtanda asema suala hilo limefikishwa Mahakamani
 
Kama kila kero ingekua inatatuliwa hv , naamin hakuna angekua above the law
Shukrani kubwa kwenu jamii forum
 
sema huyu mtanda toka ile issue ya kicheche cha nawanda si wa kuaminika sana.
 
Back
Top Bottom