PostGE2025 RC Makalla: Wasiotutakia mema jana wameaibika

PostGE2025 RC Makalla: Wasiotutakia mema jana wameaibika

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
508
Reaction score
898
Ila huyu baba!
===========
"Dunia imeona naWwatanzania wameithibitishia dunia ya kwamba wakiamua kulinda amani wanailinda, wasiotutakia mema jana wameaibika. Watanzania wanapenda amani na hawajazoea mambo ya maandamano na uvunjifu wa amani na wale wote waliokuwa wanataka vurugu leo wamejifungua- wana maumivu kwani hawakufanikiwa." Amesema Makalla.

Makalla amebainisha hayo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za kibiashara kwenye Soko la Kilombero Jijini Arusha, akiahidi kuwa serikali na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Arusha vitaendelea kuhakikisha usalama na amani inakuwepo.

 
Huko serikalini wana tabia ya kujitekenya na kucheka wenyewe.

Yaani wewe unabunduki, uogopi kuitumia na umepiga mkwara karibu mwezi upo tayari kuitumia tena.

Watanzania wa leo sio wa kuwaingiza vita ya ‘maji maji’; hawajashindwa ni kwamba commonsense prevailed; sasa aina maana watanzania wanabariki uongozi uliopata madaraka kwa njia haramu.
 
Ila huyu baba!
===========
"Dunia imeona naWwatanzania wameithibitishia dunia ya kwamba wakiamua kulinda amani wanailinda, wasiotutakia mema jana wameaibika. Watanzania wanapenda amani na hawajazoea mambo ya maandamano na uvunjifu wa amani na wale wote waliokuwa wanataka vurugu leo wamejifungua- wana maumivu kwani hawakufanikiwa." Amesema Makalla.

Makalla amebainisha hayo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za kibiashara kwenye Soko la Kilombero Jijini Arusha, akiahidi kuwa serikali na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Arusha vitaendelea kuhakikisha usalama na amani inakuwepo.


Hawa jamaa washauriwe badala ya kuwadhihaki Wananchi. Walio against ni wengi kuliko CCM na Machawa wao.
 
Dunia imeshuhudia watanganyika wakikosa uhuru siku ya kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika. Hakukuwa na usafiri wa umma, kwa waliotoka kulikuwa na vizuizi vingi kupindukia, helicopter za kijeshi kuzurura hovyo.
Ni aibu raia kutokuwa huru katika siku ya kukumbuka uhuru wa taifa lao.
Dunia imeshuhudia vyombo vya ulinzi vya bongo vikifanya maandamano bila mabango!
Next time wawaombe wananchi watawapa mabango yenye jumbe zilizonyooka.
 
Mh. Makalla tambua wewe Sasa si katibu mwenezi wa CCM bali ni mkuu wa mkoa. Kauli za kubeza au kutamba si wakati wake. Toa kauli za kujenga, kuponya majeraha, kuwaleta watanzania pamoja bila kujali vyama. Usichochee hasira, jifunze kuongea Kwa busara kama Mh. Sbachawene au Kwa hivi karibuni Chalamila.
 
Back
Top Bottom