Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, ameonya na kukemea tabia ya Watumishi na maafisa wa Serikali kuwafokea na kuwatokea kauli mbaya Wananchi pindi wanapohitaji huduma, huku akisema kuwa kufanya hivyo ni utovu wa Nidhamu na kwenda kinyume cha Misingi, taratibu na Kanuni za Utumishi wa Umma.
"Kama hauna majibu ya maswali aliyokuuliza mwananchi, usimfokee.
Tuna maafisa wanafokea Wananchi, Ulimi katika Utumishi ni Kitu muhimu sana, unaweza ukawa Daktari Mzuri, Mwalimu Mzuri, Afisa Mzuri lakini Ulimi mbaya, watu wanahitaji huduma Yako lakini Ulimi wako unawajeruhi kabla ya huduma"
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, wakati akizungumza na Watumishi wa Serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Julai 15, 2025.
"Kama hauna majibu ya maswali aliyokuuliza mwananchi, usimfokee.
Tuna maafisa wanafokea Wananchi, Ulimi katika Utumishi ni Kitu muhimu sana, unaweza ukawa Daktari Mzuri, Mwalimu Mzuri, Afisa Mzuri lakini Ulimi mbaya, watu wanahitaji huduma Yako lakini Ulimi wako unawajeruhi kabla ya huduma"
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, wakati akizungumza na Watumishi wa Serikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo Julai 15, 2025.