RC akerwa na watendaji wanaochelewesha ugawaji wa vitambulisho vya Rais Magufuli

mamayoyo1

JF-Expert Member
Jul 25, 2018
1,011
1,019


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amekuwa mbogo kwa watendaji wanaochelewesha ugawaji na usambazaji vitambulisho vya wajasiriamali katika maeneo yao mkoani humo.

Dk Mahenge alisema hayo baada ya kutembelea halmashauri mbalimbali, kukagua namna vitambulisho hivyo vilivyotolewa kwa wajasiriamali na Rais John Magufuli Disemba 10, mwaka jana vinavyosambazwa kwa wajasiriamali wadogo.

Hali ya usambazaji au ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali katika halmashauri hizo mkoani humo, haujashika kasi kubwa, hivyo aliwataka watendaji hao kuongeza kasi ili kufikia lengo la kukamilisha vitambulisho hivyo.

Mkuu wa Mkoa alifanya ziara katika halmashauri za Chamwino, Kongwa, Kondoa na ziara bado inaendelea katika maeneo mengine ili kuhakikisha usambazaji wa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo unakamilika mapema.

Akiwa katika ziara wilayani Kondoa, Dk Mahenge aliwataka watendaji kuharakisha usambazaji wa vitambulisho hivyo kwa wananchi na viongozi wanatakiwa kuhamasisha wananchi kuvichukua.

Alitawaka watendaji kuongeza kasi kugawa vitambulisho lakini kusimamia na kuhakikisha kwamba wajasiriamali wasio na vitambulisho hivyo hawaruhusiwi kufanya biashara au shughuli zozote. akiwa wilaya ya Chamwino, Dk Mahenge alimtaka Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Athuman Masasi kuharahakisha usambazaji wa vitambulisho hivyo vya wajasiriamali, badala ya kufanya kazi bila kuwa na vitambulisho.

Mkuuu wa Mkoa wa Dodoma alikabidhiwa na Rais Magufuli vitambulisho vya wajasiriamali 25,000, ambavyo alivigawa katika halmashauri zake kwa uwiano wa wingi wa idadi ya watu katika wilaya hiyo.

Katika mgawanyo huo, Jiji lilipata vitambulisho 5,000, Chamwino 4,000, Kongwa 3,750, Mpwapwa 3,500, Bahi na Chemba zote zilipata vitambulisho 2,750 kila moja, Kondoa Mji 2,500 na Kondoa Vijijini 750.
 
Waliambiwa watapimwa kwa kigezo hicho so pressure zinapanda na kushuka na zile nguo za ndani zishabana
 


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge amekuwa mbogo kwa watendaji wanaochelewesha ugawaji na usambazaji vitambulisho vya wajasiriamali katika maeneo yao mkoani humo.

Dk Mahenge alisema hayo baada ya kutembelea halmashauri mbalimbali, kukagua namna vitambulisho hivyo vilivyotolewa kwa wajasiriamali na Rais John Magufuli Disemba 10, mwaka jana vinavyosambazwa kwa wajasiriamali wadogo.

Hali ya usambazaji au ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali katika halmashauri hizo mkoani humo, haujashika kasi kubwa, hivyo aliwataka watendaji hao kuongeza kasi ili kufikia lengo la kukamilisha vitambulisho hivyo.

Mkuu wa Mkoa alifanya ziara katika halmashauri za Chamwino, Kongwa, Kondoa na ziara bado inaendelea katika maeneo mengine ili kuhakikisha usambazaji wa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo unakamilika mapema.

Akiwa katika ziara wilayani Kondoa, Dk Mahenge aliwataka watendaji kuharakisha usambazaji wa vitambulisho hivyo kwa wananchi na viongozi wanatakiwa kuhamasisha wananchi kuvichukua.

Alitawaka watendaji kuongeza kasi kugawa vitambulisho lakini kusimamia na kuhakikisha kwamba wajasiriamali wasio na vitambulisho hivyo hawaruhusiwi kufanya biashara au shughuli zozote. akiwa wilaya ya Chamwino, Dk Mahenge alimtaka Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Athuman Masasi kuharahakisha usambazaji wa vitambulisho hivyo vya wajasiriamali, badala ya kufanya kazi bila kuwa na vitambulisho.

Mkuuu wa Mkoa wa Dodoma alikabidhiwa na Rais Magufuli vitambulisho vya wajasiriamali 25,000, ambavyo alivigawa katika halmashauri zake kwa uwiano wa wingi wa idadi ya watu katika wilaya hiyo.

Katika mgawanyo huo, Jiji lilipata vitambulisho 5,000, Chamwino 4,000, Kongwa 3,750, Mpwapwa 3,500, Bahi na Chemba zote zilipata vitambulisho 2,750 kila moja, Kondoa Mji 2,500 na Kondoa Vijijini 750.
 
Kwani ni lazima vitambulisho viishe? kama wajasieiamali wameisha acheni kutunga wajasiriamali bandia ili tu mpate sehemu ya kukamua pesa. Lengo lilikua wajasiriamali wamachinga lakini zimeamia mpaka kwa house girl na shamba boy acheni matani nyie watu.
 
Kuna nini na haraka gani vitambulisho hivi kuelekea uchaguzi Mkuu 2020? Mbona vinalazimishaa muda mwingine mpaka na polisi? Kuna kitu
 
Vitambulisho waha haina haja ya kutumia nguvu za ziada katika kuvigawa kwa wajasiriamali wadogo ila nadhani busara na hekima inatakiwa kutumia katika ugawaji huo. Sasa kama umepewa vitambulisho nawe unataka uvigawe vyote unahakika kama katika halmashauri zako zote kuna wajasiriamali 25000 ambao ni sawa na idadi ya vitambulisho? ulifanya upembuzi yakinifu wa aina gani katika kujiridhisha na hili la idadi ya wajasiriamali? mambo mengine hayahitaji akili ya Phd wala Master ni akili za kuvukia barabara tu na ukimuelimisha mjasiriamali akakuelewa sidhani kamakutakuwa na mshikemshike mpaka mkuu wa mkoa aamue kutoa matamko ambayo hayajengi zaidi ya kubomoa utu na heshima ya serikali iliyomuweka madarakani. U ndo yale ya ndugu zangu KAMWENE moaka wanarukana wenyewe kwa wenyewe?
 
Hahaha eti ugawaji, kwani vinagawiwa bure?! Icho kitambulisho ni hirizi au dawa ya kuleta wateja?!
Asiigope kufukuzwa Amosi Makalla alifukuzwa kwa sababu hakuwa chaguo la Magufuli, sio vitambulisho vya machinga.
 
Masahihisho - vitambulisho vya wamachinga havigawiwi bure bali vinauzwa kwa bei kali ya tsh 20, 000 kwa kikaratasi kimoja ambacho gharama ya kukiandaa haijazidi mia 5
 
Back
Top Bottom