babumapunda
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 4,644
- 3,314
Na Musa Mateja
MWANADASHOSTI anayejipanga
kurejea kwenye gemu la Bongo
Fleva kwa kishindo, Rehema
Chalamila Ray C amefunguka ya
moyoni akisema kuwa anamshukuru
Mungu kwa kupona madhara ya
madawa ya kulevya bila kupata
matatizo mengine ya kiafya huku
akifafanua suala la kuokoka.
Mwanamuziki huyo alisema kuwa
katika kipindi chote cha kupigana
na madawa ya kulevya zaidi ya
miaka mitatu iliyopita, alipitia
mengi magumu lakini kikubwa ni
kwamba hivi karibuni alipima na
kujikuta yupo salama na hana
Ukimwi.
Kuhusu suala la kuokoka, Ray C
alisema ukweli ni kwamba
mwanzoni alikuwa Mkatoliki lakini
hivi karibuni alibatizwa na maji
mengi katika Kanisa la Sloam
lililopo Mbezi-Beach na kuungana
na mama yake anayesali kwenye
kanisa hilo
Namshukuru Mungu nimepona,
sina tatizo la kiafya kama Ukimwi.
Kuhusu kuokoka, mimi sijaokoka.
Nilibatizwa na maji mengi.
Napenda mahubiri ya Sloam.
Nimeungana na mama yangu
anayesali kanisani hapo ndiyo
maana watu wanatafsiri kuwa
nimeokoka.Watu wakisikia mtu
anasema ameokoka wanatafuta vitu
ili kukujaribu. Kweli mimi sijaokoka
lakini mahubiri yananiweka huru
na nakuwa na amani zaidi,
alisema Ray C.
Source:Global Publishers
MWANADASHOSTI anayejipanga
kurejea kwenye gemu la Bongo
Fleva kwa kishindo, Rehema
Chalamila Ray C amefunguka ya
moyoni akisema kuwa anamshukuru
Mungu kwa kupona madhara ya
madawa ya kulevya bila kupata
matatizo mengine ya kiafya huku
akifafanua suala la kuokoka.
Mwanamuziki huyo alisema kuwa
katika kipindi chote cha kupigana
na madawa ya kulevya zaidi ya
miaka mitatu iliyopita, alipitia
mengi magumu lakini kikubwa ni
kwamba hivi karibuni alipima na
kujikuta yupo salama na hana
Ukimwi.
Kuhusu suala la kuokoka, Ray C
alisema ukweli ni kwamba
mwanzoni alikuwa Mkatoliki lakini
hivi karibuni alibatizwa na maji
mengi katika Kanisa la Sloam
lililopo Mbezi-Beach na kuungana
na mama yake anayesali kwenye
kanisa hilo
Namshukuru Mungu nimepona,
sina tatizo la kiafya kama Ukimwi.
Kuhusu kuokoka, mimi sijaokoka.
Nilibatizwa na maji mengi.
Napenda mahubiri ya Sloam.
Nimeungana na mama yangu
anayesali kanisani hapo ndiyo
maana watu wanatafsiri kuwa
nimeokoka.Watu wakisikia mtu
anasema ameokoka wanatafuta vitu
ili kukujaribu. Kweli mimi sijaokoka
lakini mahubiri yananiweka huru
na nakuwa na amani zaidi,
alisema Ray C.
Source:Global Publishers