Ray aamua...

Dr. Chapa Kiuno

JF-Expert Member
Sep 11, 2009
443
18
Na Mwandishi Wetu

STAA anayemiliki mkwanja mrefu katika tasnia ya filamu za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray', amemvaa ngwiji mwenzake Steven Charles Kanumba na kumchana kwa kitendo cha kumlipua baba yake mzazi, mzee Charles Kusekwa, katika vyombo vya habari, Risasi Jumamosi lina mkanda mzima.

Akizungumza na gazeti hili, Ray ambaye inadaiwa ana bifu baridi na Kanumba, alisema kitendo alichokifanya mshkaji wake si cha kiungwana kwa kuwa aliyekuwa anamzungumzia ni baba yake mzazi.

HABARI KAMILI
Ray alisema, hata kama baba yake angekuwa amefanya kosa kubwa kiasi gani, kumuanika kwenye vyombo vya habari ni kumkosea adabu.

"Kiukweli pale Kanumba alikosea sana, huwezi kumsema mzazi wako. Baba ni Mungu wa duniani. Anatakiwa kuheshimiwa kwa namna yoyote," alisema na kuongeza:

"Kwanza mzazi huwa hakosei...tunatumia uungwana kusema, anasahau! Hata kama alimkosea, tutasema alijisahau...halafu unapomsema mzazi wako kwenye vyombo vya habari unatarajia nini? Adharaulike au? Hakufanya sawa hata kidogo."

NI LAANA

Akiendelea kutambaa na mistari, Ray alisema kitendo alichokifanya Kanumba ni sawa na kutafuta laana.

"Hata kama hatamlaani, lakini moja kwa moja ni laana. Huwezi kumkosesha amani mzazi wako kiasi kile. Nina uhakika Kanumba hakuomba ushauri kabla ya kwenda kwenye runinga.

"Alikurupuka. Kama angezungumza na sisi wasanii wenzake, naamini hakuna ambaye angemkubalia. Tungemshauri vizuri tu. Hili ni kosa kubwa. Ni sawa na kumvua nguo mzazi wako," alisema.

Akaongeza: "Mbaya zaidi, baba yake amejibu tuhuma zake kwenye gazeti, na yeye tena akamjibu. Inaonesha ni kwa namna gani anapenda mashindano na mzazi wake. Si kitu kizuri hata kidogo. Hapo Kanumba alichemka, lazima aelewe huo ukweli.

"Unajua kuna mambo mengine hayapaswi kujulikana na watu. Yeye kama msanii mkubwa, mwenye heshima, leo hii anaanika maisha yake ya utotoni? Eti baba alimtesa? Ili iweje? Amepata nini kwa kusema hayo kama siyo kumdhalilisha tu mzazi wake? Haikuwa sawa.

"Haya mambo wangeyajadili kifamilia ingekuwa na maana zaidi kuliko kuyaanika hadharani."


AMTAKA AOMBE RADHI
Ray alisema, Kanumba akitaka aendelee kupaa katika anga la filamu, anatakiwa kumuomba lazi baba yake.
"Kitu pekee kilichobaki ni kumuomba baba yake msamaha. Amemkosea sana, amuombe amsamehe ili asibaki na kinyongo. Hiyo ndiyo njia pekee ya kumsafisha," alisema na kuongeza:
"Nina imani atamsamehe na watafungua ukurasa mpya. Huu ni ushauri wangu. Ana uhuru wa kuufuata au kuuacha. Mzazi siku zote ana huruma na mwanaye, bila shaka atamsamehe."


NI MWENDELEZO WA BIFU?

Alipoulizwa kuwa sababu ya kusema yote kwa Kanumba ni kwa kuwa ana bifu naye, Ray aliruka kimanga, akaeleza kuwa, amefanya hivyo kama msanii mwenzake na ni kwa nia njema.

"Sizungumzii mambo ya bifu hapa, naongelea usahihi wa alichokifanya. Naamini hata jamii haiwezi kuona eti kumshauri mtu ni bifu. Ni mawazo yangu, kama nilivyosema awali," alisema.

RAY AAMUA... - Global Publishers
 
ray umeonesha una busara kanumba bado umri mdogo atakuwa tu hivi vijisenti vya mpa ngebe .
 
“Kiukweli pale Kanumba alikosea sana, huwezi kumsema mzazi wako. Baba ni Mungu wa duniani. Anatakiwa kuheshimiwa kwa namna yoyote,” alisema na kuongeza:
“Kwanza mzazi huwa hakosei...tunatumia uungwana kusema, anasahau! Hata kama alimkosea, tutasema alijisahau...halafu unapomsema mzazi wako kwenye vyombo vya habari unatarajia nini? Adharaulike au? Hakufanya sawa hata kidogo.”

Hivi mwanaume kumtungisha mimba mwanamke akazaa ndio kunampa sifa ya 'uMungu wa dunia, mHeshimiwa kwa namna yoyote, na hasiyeKosea kamwe'!? Kweli jigy-jigy tu inakupa hiyo heshima yoote?!

To me it takes more than just to impregnate a woman to be a father! uBaba hauishii kwenye kumjaza mwanamke mimba, bali unaanzia hapo kwenye kumjaza mwanamke mimba, sasa kama hukutimiza majukumu yako yaliyotakiwa kufuatia kumtia mwanamke mimba..mtoto akiwa maarufu na mkwanja usirudi eti kujitia wewe ni baba! Nyambaff...

Mimi nalea mtoto wa dada yangu...binti smart (kichwa) kweli kweli kushinda hata mwanangu wa kumzaa, lakini huyu binti alitelekezwa na baba yake tangu akiwa na miaka mi3, na dada akiwa hana uwezo wowote wa kumlea na kumsomesha huyu mtoto. Sasa mtoto now yuko chuo kikuu doing very great baba yake anakuja eti anataka mwanae....nyambaff! Wakati tunambembeleza kumsupport mwanane anatoa matusi alifikiri mtoto atakuwa looser?!

Kama unataka sifa ya baba kuwa mungu wa dunia na kuheshimiwa play your part kama baba!
 
Na Mwandishi Wetu
HABARI KAMILI
Ray alisema, hata kama baba yake angekuwa amefanya kosa kubwa kiasi gani, kumuanika kwenye vyombo vya habari ni kumkosea adabu.
"Kiukweli pale Kanumba alikosea sana, huwezi kumsema mzazi wako. Baba ni Mungu wa duniani. Anatakiwa kuheshimiwa kwa namna yoyote," alisema na kuongeza:


 
well said

Hivi mwanaume kumtungisha mimba mwanamke akazaa ndio kunampa sifa ya 'uMungu wa dunia, mHeshimiwa kwa namna yoyote, na hasiyeKosea kamwe'!? Kweli jigy-jigy tu inakupa hiyo heshima yoote?!

To me it takes more than just to impregnate a woman to be a father! uBaba hauishii kwenye kumjaza mwanamke mimba, bali unaanzia hapo kwenye kumjaza mwanamke mimba, sasa kama hukutimiza majukumu yako yaliyotakiwa kufuatia kumtia mwanamke mimba..mtoto akiwa maarufu na mkwanja usirudi eti kujitia wewe ni baba! Nyambaff...

Mimi nalea mtoto wa dada yangu...binti smart (kichwa) kweli kweli kushinda hata mwanangu wa kumzaa, lakini huyu binti alitelekezwa na baba yake tangu akiwa na miaka mi3, na dada akiwa hana uwezo wowote wa kumlea na kumsomesha huyu mtoto. Sasa mtoto now yuko chuo kikuu doing very great baba yake anakuja eti anataka mwanae....nyambaff! Wakati tunambembeleza kumsupport mwanane anatoa matusi alifikiri mtoto atakuwa looser?!

Kama unataka sifa ya baba kuwa mungu wa dunia na kuheshimiwa play your part kama baba!
 
hawa wote vijisent na kupenda kuonekana kwa watu kunawasumbua..hivi rafiki yako wa kweli huwezi kumshauri mkiwa wawili mpaka wawepo waandishi wa habari?
 
Hivi mwanaume kumtungisha mimba mwanamke akazaa ndio kunampa sifa ya 'uMungu wa dunia, mHeshimiwa kwa namna yoyote, na hasiyeKosea kamwe'!? Kweli jigy-jigy tu inakupa hiyo heshima yoote?!

To me it takes more than just to impregnate a woman to be a father! uBaba hauishii kwenye kumjaza mwanamke mimba, bali unaanzia hapo kwenye kumjaza mwanamke mimba, sasa kama hukutimiza majukumu yako yaliyotakiwa kufuatia kumtia mwanamke mimba..mtoto akiwa maarufu na mkwanja usirudi eti kujitia wewe ni baba! Nyambaff...

Mimi nalea mtoto wa dada yangu...binti smart (kichwa) kweli kweli kushinda hata mwanangu wa kumzaa, lakini huyu binti alitelekezwa na baba yake tangu akiwa na miaka mi3, na dada akiwa hana uwezo wowote wa kumlea na kumsomesha huyu mtoto. Sasa mtoto now yuko chuo kikuu doing very great baba yake anakuja eti anataka mwanae....nyambaff! Wakati tunambembeleza kumsupport mwanane anatoa matusi alifikiri mtoto atakuwa looser?!

Kama unataka sifa ya baba kuwa mungu wa dunia na kuheshimiwa play your part kama baba!

Riwa ubarikiwe mbinguni na duniani,
 
Riwa hapo umesema kweli. Baba au mama aliyenilea kwa upendo nitamthamini zaidi kuliko biological parents ambao hawana habari na mimi
 
Ati Mung wa duniani!!!??? hi kweli kali. Mungu anamjua anamsikia???
baba kama hajatimiza responsibility za ni sawa tu mama anayezaa mtoto na kumtupa chooni
kama hakumtaka akiwa mdogo angekufa kwa kukosa matunzo angeongea nini???
apotelee mbali
 
  • Thanks
Reactions: Sal
Hivi mwanaume kumtungisha mimba mwanamke akazaa ndio kunampa sifa ya 'uMungu wa dunia, mHeshimiwa kwa namna yoyote, na hasiyeKosea kamwe'!? Kweli jigy-jigy tu inakupa hiyo heshima yoote?!

To me it takes more than just to impregnate a woman to be a father! uBaba hauishii kwenye kumjaza mwanamke mimba, bali unaanzia hapo kwenye kumjaza mwanamke mimba, sasa kama hukutimiza majukumu yako yaliyotakiwa kufuatia kumtia mwanamke mimba..mtoto akiwa maarufu na mkwanja usirudi eti kujitia wewe ni baba! Nyambaff...

Mimi nalea mtoto wa dada yangu...binti smart (kichwa) kweli kweli kushinda hata mwanangu wa kumzaa, lakini huyu binti alitelekezwa na baba yake tangu akiwa na miaka mi3, na dada akiwa hana uwezo wowote wa kumlea na kumsomesha huyu mtoto. Sasa mtoto now yuko chuo kikuu doing very great baba yake anakuja eti anataka mwanae....nyambaff! Wakati tunambembeleza kumsupport mwanane anatoa matusi alifikiri mtoto atakuwa looser?!

Kama unataka sifa ya baba kuwa mungu wa dunia na kuheshimiwa play your part kama baba!

Kwa kweli inauma sana aisee. Ngoja nami niutafute umaarufu ili baba yangu ajitokeze!
 
Hivi mwanaume kumtungisha mimba mwanamke akazaa ndio kunampa sifa ya 'uMungu wa dunia, mHeshimiwa kwa namna yoyote, na hasiyeKosea kamwe'!? Kweli jigy-jigy tu inakupa hiyo heshima yoote?!

To me it takes more than just to impregnate a woman to be a father! uBaba hauishii kwenye kumjaza mwanamke mimba, bali unaanzia hapo kwenye kumjaza mwanamke mimba, sasa kama hukutimiza majukumu yako yaliyotakiwa kufuatia kumtia mwanamke mimba..mtoto akiwa maarufu na mkwanja usirudi eti kujitia wewe ni baba! Nyambaff...

Mimi nalea mtoto wa dada yangu...binti smart (kichwa) kweli kweli kushinda hata mwanangu wa kumzaa, lakini huyu binti alitelekezwa na baba yake tangu akiwa na miaka mi3, na dada akiwa hana uwezo wowote wa kumlea na kumsomesha huyu mtoto. Sasa mtoto now yuko chuo kikuu doing very great baba yake anakuja eti anataka mwanae....nyambaff! Wakati tunambembeleza kumsupport mwanane anatoa matusi alifikiri mtoto atakuwa looser?!

Kama unataka sifa ya baba kuwa mungu wa dunia na kuheshimiwa play your part kama baba!

Mzungu alisemaa "Any man can be a father but it needs someone special to be dad", kabla hatujamlaumu Kanumba hebu tujiulize huyu anayeclaim kuwa baba is he a father (biologicaly) or a dad (responsibly)
Kama limtu linakataa mtoto halafu akifanikiwa kimaisha linamsumbua na kumtisha na laana, laana my foot. Laana yako haitapokelewa mbinguni wala duniani.
Nina scenario kama yako mkuu Riwa, nalea huyu mtoto asiye na hatia na yuko bright mno, namsubiri huyo bingwa wa kugawa mbegu aje.
 
hayajawakuta, yakiwakuta wala hamtasema kitu.

Upo sahihi Kongosho, kama baba hakujua umuhimu wa kuwa baba basi hana maana.

Ray alitaka tu kujionyesha yupo sahihi mbele ya jamii wakati jamii ipo fair katika judgement.
 
kweli wanaume tuna tabia ya kudai mtoto baada ya kuona mtoto ana mafanikio ni mbaya sana!
 
Haya MALUMBANO YAMEKWISHA TIME HAVE TOLD US baba anapashwa kuheshimiwa hata afanye kosa lipi! mungu kaweka ktk amri zake kumi WAHESHIMU BABA NA MAMA YAKO UPATE MIAKA MINGI NA HERI DUNIANI! Asiye mheshimu Baba yake hatopata miaka mingi duniani!(atakufa mapema!) MUNGU ndiyo kasema hivyo si mimi!
 
Back
Top Bottom