RAV 4 Yateketea kwa moto Salender Bridge

RAV 4 Yateketea kwa moto Salender Bridge

Ilo litakuwa lingine,lenyewe jeupe.

Duuuh ....basii hilo eneo litakuwaa ndo maalumu la kuunguziiaa..Maana nililolikuta ni Rav 4 new model, hapo hapo ubalozi wa Russia linaungua. Dereva alikuwa amepanic sanaa..
 
Weee,

Yani unawapigia simu faya badala ya kuchukua fire extinguisher yako na kuuzima huo moto? Au hata wewe hukuwa na kizima moto kwa ngari yako? Watu wengine bwana!!!!!!!!!!!!!!!!
 
ndiyo maana kukwawa na booonge la foleni kwa watu tunaokuja mijini nyuma yangu alikuwa dada mmoja akakosa subira akaamua kupita njia tatu ile akate pale unapoishia ubalozi wa ufaransa bahati mbaya kulikuwa na na mwenda kwa miguu anakatiza du aisee baba wa watu aligongwa.. yule dada akashuka na kumuomba ampeleke hosipitali yule mbaba akakataa akaanza kupiga simu polisi du nilikuwa na shauku kujua kilichojiri mara taa zikaruhusu..chanzo ni macho yangu kwani ndiye niliwapigia simu wazee wa ova
 
Hapa nafikiri magari yaliyoungua ni matatu au manne hivi la kwanza ni rav 4 nyeupe la pili ni rav4 ya bluu na ya tatu ni kijivu. hizo ni rav 4 tatu pia inawezekana ni nne kwasababu kuna mmoja ameona gari inaungua ubalozi wa russia na mwengine salendar bridge......duu! au ni tano....??!!
 
ukipita hapo salender bridge kwa mguu mchana wakati jua linawaka nywele zinasisimka!
 
Weee,

Yani unawapigia simu faya badala ya kuchukua fire extinguisher yako na kuuzima huo moto? Au hata wewe hukuwa na kizima moto kwa ngari yako? Watu wengine bwana!!!!!!!!!!!!!!!!

Mkuu sikuwa na gari nilikuwa napitia kwa miguu tu.Kikebiwoka changu kimeisha bima tangu Mwezi wa kwanza
 
kuna ambayo nimeikutaa inaunguaa ya kijvuu leo mida ya saa saba kasoro...ndoo yenyewee???

Mkuu utakuwa umeona imeshaanza kuungua..Nimeiona ikiwa bado barabarani mpaka jamaa akaingiza service road ni nyeupe.Utakuwa umeona impact ya moto na ni muda huo.
 
mfano tu, daaah inaumaaa :A S cry:

toyota_fire.jpg
 
...ni mojawapo ya aina ya magari yanayotakiwa kurudishwa JAPANA!

"HITILAFU MAGARI YA TOYOTA: Magari
milioni 6.6 aina ya Yaris, Urban
Cruiser, RAV4, Hilux kurudishwa
kiwandani kutokana na hitilafu,
kampuni ya Toyota yasema leo."

But sio second hand au mitumba
 
mleta Uzi utakuwa color blindness mie mwenyewe nimeishuhudia ni ya kijivu.sema nashindwa jinsi ya kuweka picha hapa
 
Ila inauma sana,unatoka nyumbani na gari alafu unarudi na majivu...
 
mleta Uzi utakuwa color blindness mie mwenyewe nimeishuhudia ni ya kijivu.sema nashindwa jinsi ya kuweka picha hapa

Duh ngoja nifanye mpango nijiunge na Chawata y ma-blind labda nawezabahatisha ujumbe wa bunge la katiba likirudi mwezi August
 
Back
Top Bottom