Rasmi - Yanga yachomoa kombe la Mapinduzi!!

Hiyo bahati ipo upande mmoja tu siku zote, kwa nini Yanga wasibahatishe walau 3-0?

Siyo ninyi mliotimua makocha wazawa hivi karibuni kwa matokeo mabaya, hivi mna pointi ngapi kwenye ligi? Nyani kumbe haoni kundule eeh? Kumbe, huona la mwenzie!
 
Ukiwa shabiki ni mzigo sana kiasi unasahau kabisa hali halisi...

Mashindano ya Mapinduzi ni mashindano yenye dhima ya kuadhimisha Mapinduzi ya Zanzibar na wala hayapo katika kalenda yoyote ya michezo ya TFF...

Timu zinashiriki kwa kualikwa (mtu yoyote mwenye akili timamu anajua kabisa kuwa mwaliko unaweza kukubaliwa au kukataliwa)...

Kuna timu zinaongozwa na ratiba kutoka benchi la ufundi kwa kuangalia mambo kadhaa ya kiufundi kabla ya kushiriki mashindano au mechi zisizo na ulazima...

Yanga kujitoa mashindano binafsi sioni kama ni nongwa maana mashindano hayo hayana tija kwa timu kwa wakati huu...
 
images (2).jpg
 
Sababu unazotoa watu8 sio sababu za klabu ni za kishabiki tu,
ukiwa shabiki ni mzigo sana kiasi unasahau kabisa hali halisi...

Mashindano ya mapinduzi ni mashindano yenye dhima ya kuadhimisha mapinduzi ya zanzibar na wala hayapo katika kalenda yoyote ya michezo ya tff...

Timu zinashiriki kwa kualikwa (mtu yoyote mwenye akili timamu anajua kabisa kuwa mwaliko unaweza kukubaliwa au kukataliwa)...

Kuna timu zinaongozwa na ratiba kutoka benchi la ufundi kwa kuangalia mambo kadhaa ya kiufundi kabla ya kushiriki mashindano au mechi zisizo na ulazima...

Yanga kujitoa mashindano binafsi sioni kama ni nongwa maana mashindano hayo hayana tija kwa timu kwa wakati huu...
 
Jamani mimi huwa naangalia vitu vingi nyuma ya pazia. Sababu kubwa ya Yanga ni kutokuwa na uhakika wa kuwatumia wachezaji kadhaa ambao inawategemea. Ngasa, Msuva na Canavaro wanaumwa na wangeikosa michuano hiyo. Okwi na Kiiza bado wapo Uganda na wamezima simu zao. Ukiangalia kikosi walau wanachokitegemea kilichocheza na Simba na kufungwa 3-1, wakaona hao waliobaki kambini ndio hawawezi kabisa. Walianza na sababu ya kusema hawajapatiwa mwaliko rasmi, akatokea ofisa wa ZFA na kuthibitisha kwa kuonyesha dispatch waliyosaini Yanga kupokea mwaliko. Yanga wakaja na mpya kwamba wanataka wawekewe wazi kuwa watakula nini na watalala vipi. Kabla hawajajibiwa kuwa watakuwa wanakula nini, ndio wakaja na hiyo mpya nyingine ya kusema hawana benchi la ufundi. Brandts bado yupo ndani ya notisi ya siku 30, Minziro bado yupo, Mkwasa ameshakubali kujiunga nao, hivi kombe la mapinduzi linahitaji Boby Williamson? Ukweli ni kwamba wachezaji wao wa kutegemewa hawapo, waliobaki kambini wana hofu ukizingatia wametoka kufungwa na Simba. Yanga inabidi ianze kuwaamini wachezaji wote waliosajiliwa, kuna kipindi (mwaka jana) kikosi cha kwanza cha Simba kilienda kuweka kambi Uarabuni na huko kwenye kombe la Mapinduzi wakaenda akina Singano na Mkude na wakafika Semi Final, leo hao vijana ndio wanaoitisha Yanga!
 
Ina maana mkuu sababu walizotoa viongozi wa Yanga hujaona kuwa wamegusia suala la ufundi???

Huwezi peleka mashindanoni timu isiyo na kocha, au kwa lugha nyepesi ni kuwa kwa mfumo wa mpira wa kisasa timu isipokuwa na kocha maana yake haina programu ya kiufundi.

Usiponielewa na hapa mkuu nitashangaa...

Sababu unazotoa watu8 sio sababu za klabu ni za kishabiki tu,
 
waambie kabbisa hawa akina Watu8, haiwezekani timu inajitoa masaa 24 kabla ya mechi ilihali mlishavuta hadi nauli
Jamani mimi huwa naangalia vitu vingi nyuma ya pazia. Sababu kubwa ya Yanga ni kutokuwa na uhakika wa kuwatumia wachezaji kadhaa ambao inawategemea. Ngasa, Msuva na Canavaro wanaumwa na wangeikosa michuano hiyo. Okwi na Kiiza bado wapo Uganda na wamezima simu zao. Ukiangalia kikosi walau wanachokitegemea kilichocheza na Simba na kufungwa 3-1, wakaona hao waliobaki kambini ndio hawawezi kabisa. Walianza na sababu ya kusema hawajapatiwa mwaliko rasmi, akatokea ofisa wa ZFA na kuthibitisha kwa kuonyesha dispatch waliyosaini Yanga kupokea mwaliko. Yanga wakaja na mpya kwamba wanataka wawekewe wazi kuwa watakula nini na watalala vipi. Kabla hawajajibiwa kuwa watakuwa wanakula nini, ndio wakaja na hiyo mpya nyingine ya kusema hawana benchi la ufundi. Brandts bado yupo ndani ya notisi ya siku 30, Minziro bado yupo, Mkwasa ameshakubali kujiunga nao, hivi kombe la mapinduzi linahitaji Boby Williamson? Ukweli ni kwamba wachezaji wao wa kutegemewa hawapo, waliobaki kambini wana hofu ukizingatia wametoka kufungwa na Simba. Yanga inabidi ianze kuwaamini wachezaji wote waliosajiliwa, kuna kipindi (mwaka jana) kikosi cha kwanza cha Simba kilienda kuweka kambi Uarabuni na huko kwenye kombe la Mapinduzi wakaenda akina Singano na Mkude na wakafika Semi Final, leo hao vijana ndio wanaoitisha Yanga!
 
Sababu kubwa ya uamuzi huo 'Bado hawajapata benchi la uhakika la ufundi'.
Cha kujiuliza ni nini kisa cha kumtimua Brandts!? Je yawezekana baada ya kuangalia timu pinzani uoga umeingia?kwamba kipigo kingine kutoka kwa mnyama iwapo watakutana kitaleta mtafaruku jangwani? Nini hasa?

Haha, tangu lin YEBOYEBO FiVE MODRN TAARABU wanaweza cheza mpira wa ushindan! Eb nenden mkajumuike na yule mzee wa taarabu leo anaonesho pale Magomen, onyesho la sikukuu ya mwka mpya, mtuache cc tunaocheza mpira na ss ninyi waimba taarabu! Tena inatakiwa ZFA, wawakaribishe kama band wa kusherehesha siku ya kumbukumbu ya znzbr revltn!
Samahan lkn
 
Hivi ni lazima Yanga kushiriki kombe la Mapinduzi?..

Zaidi ya kuyaenzi mapinduzi matukufu mashindano haya yana faida gani hasa kwa timu?...

Nadhani waandaaji wangetoa zaidi fursa kwa timu za vijana badala ya kuangalia fedha zaidi..

Sidhani kama Yanga kushiriki kombe la Mapinduzi kutaisaidia timu katika CAF CL..

Heko uongozi wa Yanga kwa uamuzi huu...
 
Rage hajambo? Upepo wa kumtimua umeishia wapi?

Simba hawana ujanja kwa Rage hata siku moja Nkwingwa..

Ndio maana Rage alikuwa na ujasiri wa kusema kikao kilichomsimamisha ni 'Kikao cha harusi'..Na kudhihirisha hilo bado anadunda madarakani..Simba wameufyata mkia..
 
Ila yanga mmetuaibisha kweli penye miti mingi hapana wajenzi, mpaka kocha analalamika wachezaji wanajiona mastaa halafu nothng wanafanya!! Ustaa unakuja baada ya kuwajibika!! Tubadilike, SIMBA HAWA HAWA WATAENDELEA KUTUPA KICHAPO CHA MBWA MWIZI MPAKA TUKOME!!!
 
Ila yanga mmetuaibisha kweli penye miti mingi hapana wajenzi, mpaka kocha analalamika wachezaji wanajiona mastaa halafu nothng wanafanya!! Ustaa unakuja baada ya kuwajibika!! Tubadilike, SIMBA HAWA HAWA WATAENDELEA KUTUPA KICHAPO CHA MBWA MWIZI MPAKA TUKOME!!!
Anayetakiwa kudhibiti nidhamu ya wachezaji sio uongozi wa timu..Ni Kocha na benchi lake la ufundi na kwa hili Brandts na benchi lake la ufundi wamefail ndio maana kila mtu anamshangaa Brandts kwa kulialia kuhusu nidhamu ya wachezaji ilhali yeye ndio anapaswa kuidhibiti..

Uamuzi wa kuvunja benchi la ufundi la Yanga ni muafaka kabisa..

Heko uongozi wa Yanga kwa maamuzi mazito...
 
Wameogopa kukutana na watoto wa jiji mbeya city hao.
 
Last edited by a moderator:
Ila yanga mmetuaibisha kweli penye miti mingi hapana wajenzi, mpaka kocha analalamika wachezaji wanajiona mastaa halafu nothng wanafanya!! Ustaa unakuja baada ya kuwajibika!! Tubadilike, SIMBA HAWA HAWA WATAENDELEA KUTUPA KICHAPO CHA MBWA MWIZI MPAKA TUKOME!!!

we m.nafiki tu wala sio shabiki wa yanga
 
Siyo ninyi mliotimua makocha wazawa hivi karibuni kwa matokeo mabaya, hivi mna pointi ngapi kwenye ligi? Nyani kumbe haoni kundule eeh? Kumbe, huona la mwenzie!
uzuri wa nyani sisi tunapenda ndizi za njano sana.
 
Back
Top Bottom