Ukiwa shabiki ni mzigo sana kiasi unasahau kabisa hali halisi...
Mashindano ya Mapinduzi ni mashindano yenye dhima ya kuadhimisha Mapinduzi ya Zanzibar na wala hayapo katika kalenda yoyote ya michezo ya TFF...
Timu zinashiriki kwa kualikwa (mtu yoyote mwenye akili timamu anajua kabisa kuwa mwaliko unaweza kukubaliwa au kukataliwa)...
Kuna timu zinaongozwa na ratiba kutoka benchi la ufundi kwa kuangalia mambo kadhaa ya kiufundi kabla ya kushiriki mashindano au mechi zisizo na ulazima...
Yanga kujitoa mashindano binafsi sioni kama ni nongwa maana mashindano hayo hayana tija kwa timu kwa wakati huu...