RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

Kwa kuwa Rasimu iliyozinduliwa jana inazungumizia Serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania tu na siyo nchi washirika,
kwa kuwa Rasimu imependekeza serikali 3 ya Muungano, Zanzibar na Tanganyika, na
kwa kuwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar ina mifumo kamili ikiwepo ofisi, viongozi,sheria mbali mbali zinazoongoza nchi hiyo ikwepo mgawanyo madaraka miongoni mwao, na upande wa Tanganyika hamna kitu, na
Kwa kuwa serikali ya Tanganyika haina sheria yo yote na Tume ya Uchaguzi hasa ktk ngazi za wilaya na kata na mitaa nk,

Hivyo basi, Mimi najiuliza, je Rasimu hii ikipita na kuwa katiba, ndo sisi watanganyika, tutaanzisha upya mchakato wa kutafuta katiba mpya ya Tanganyika yetu kabla ya 2015?

Ikumbukwe kuwa, wazanzibar wana katiba yao tayari inayotoa mwongozo kuhusu uchaguzi na tume ya uchaguzi nk. Tanganyika haina mwongozo wowote. Na Tanganyika inahitaji aina viongozi wanaohitajika na kazi zao, idadi wa wabunge na kazi zao, Tume ya uchaguzi, kama Tunahitaji wakuu wa wilaya/mikoa au la. Tunahitaji mamlaka ya serikali za mitaa iweje nk.

Tunahitaji kujua majukumu na mipaka ya Rais na mawaziri wa Tanganyika. Yote yanatakiwa yawepo ktk katiba mpya ya Tanganyika. Sasa najiuliza, je, rasimu hii ikipita kuwa katiba kamili 2014, ndo sisi watanganyika tutaanzisha upya mchakato upya wa katiba tena? Je, itawahi uchaguzi wa 2015?
Ni swali linalonichanganya.

Au ndo siri ya maombi ya miaka 2 zaidi ya kikwete imejificha hapa?


NB;
Nimetumia Tanganyika Vs Tanzania bara kwa kuwa mujibu wa Mapendekezo ya Tume nchi washrika zinaruhusiwa kuwa na mahusiano ya moja kwa moja na nchi za nje. Kwa hiyo, kuwa na jina Tanzania na Tanzania Bara ktk medani za kimtaifa itawachanganya jumuia za kimataifa.
Nawasilisha
 
usiandike vtu ucvyivjua vzur.rasimu inasema watu wanaohisi wanafaa wataomba kwa tume maalumu thn interview n thn watakao faulu ndo watapitishwa na rais
 
Hapo kwa anna kilango sipo kwani haeleweki kakaa kiushabiki zaidi.

inagawaje kaka kiushabiki lakini atleast anajitutumua kijana sio sawa na wale wengine miaka mitano hajawahi kuchangia hoja hata siku moja aisee.....
 
kwa hili la katiba mpya Jk amethibitisha ujeshi wake kwa kusimama na matakwa ya wananchi kuliko kukumbatia itikadi za vyama vya siasa ambazo zimelitumbukiza taifa katika majanga mengi ya kutisha ikiwa ni pamoja na ufisadi, uporwaji rasilimali, ukumbatiaji wenye nacho, nk. Hapa Jk amewatoka majambazi yote yaliyokuwa yanamtia ujinga na kumfunga mdomo asisimamie taifa ipasavyo na badala yake kufata mkondo wa magenge yaliyojipanga kivyama ili kupata nguvu ya pamoja za uporaji. Hapa JK ameonyesha rangi yake ya kweli ya ujeshi kusimama na nchi yake mda wote badala ya kusombwa na mkondo wa waangamiza nchi. Nyerere ni baba wa uhuru na jk ni baba wa taifa jipya. Aliyebezwa na kudharauliwa na kutukanwa hatimaye ameibuka kuwa shujaa. Mwana jf hebu tiririka hapa chini kuhusu Jk kuruhusu mivyama ya kisiasa kufa na kuwang'oa meno wanasiasa na kubakia mapengo matupu. N sema hili ni la JK kwa maana alikuwa na mabavu ya kutosha kulikwamisha nyuma ya pazia na kwa kuwa kaliacha kama lilivyo ni wazi mafuta yamejitenga na maji.
 
Asalaam aleykhum ndugu zangu wana wa Tanganyika na Zanzibar. Pia amani ya bwana iwe pamoja nanyi ndugu zangu wana wa Tanganyika na Wazanzibari.

Kwanza napenda kutoa pongezi kwa ndugu zangu wana wa Zanzibari kwa kuitetea nchi yao na sasa wameipata na itatambulika katika katiba mpya kama nchi ya Zanzibar. Kweli wameonyesha uzalendo wa hali ya juu sana kwa kuhakikisha historia na hadhi ya nchi yao haipotei hata kidogo. Zanzibar itabaki kuwa Zanzibar hata ndani ya muungano. Hongereni sana wanaharakati wa Zanzibar. Kweli mmeonyesha ujasiri wa hali ya juu sana katika kuipigania Zanzibar yenu.

Pili nataka nichukue nafasi hii kuwapa pole ndugu zangu Watanganyika kwa kupoteza historia na hadhi ya nchi yao tukufu ya Tanganyika. Ni pigp kubwa sana na pia ni dhambi kubwa sana imefanywa na viongozi waliopewa dhamana na Watanganyika kuitetea nchi yao. Hatimaye katika katiba mpya, Tanganyika itakuwa imekufa na kuzikwa rasmi. Kwani itazaliwa nchi mpya kabisa itakayoitwa Tanzania bara. Kweli wanaharakati wa Tanganyika wameonyesha uzembe na uwoga wa hali ya juu sana kwa kukaa kimya na kuacha Tanganyika yao ikiangamia pasipo na mtetezi wa kuifanya iendelee kustawi na kushamiri kama Zanzibar.

Sasa niende katika hoja yangu kuu ambayo inataka kueleza na kuomba ufafanuzi wa ni kwa nini Tanganyika ife na izaliwe Tanzania bara waketi Zanzibar haijafa? Hapa kuna kitu nyuma ya pazia kwa viongozi wetu tuliowapa dhamana ya kuilinda na kuitetea Tanganyika yetu. Kosa kubwa sana tumelifanya na tutahukumiwa na vizazi vijavyo kwa kuruhusu nchi yao tukufu ya Tanganyika ife na kuzaliwa nchi nyingine ya Tanzania bara. Hivi watanganyika wamekuwa na mioyo gani ya kuachia nchi yao tukufu kufa na kuzaliwa nchi nyingine? Binafsi nawachukulia wanaharakati kama ndio wasaliti wakubwa kwa Tanganyika yetu. Nasikia uchungu sana nikiona Tanganyika inaangamia na kutoweka kabisa. Hii dhambi haitosahaulika vizazi na vizazi. Eti leo mtanganyika amekuwa zoba na mbumbu namna hii hadi kudanganywa kuwa nchi yake ya Tanganyika ipo haijafa bali ni jina tu ndio limebadilika na kuitwa Tanzania bara. Kama hoja ni jina tu, kwa nini basi pia na Zanzibar isiitwe Tanzania visiwani? Thubutu kabisa, kwa umakini na uzalendo alokuwa nao Mzanzibari kitu hiko kisingelithubutu kutokea kabisa. Zanzibari itabaki kuwa Zanzibari tu, na hili sio kwa hiyari au hisani ya watawala bali ni kwa ujasiri na uzalendo wa wana wa Zanzibar. Tanganyika itakufa na itazaliwa Tanzania bara sio kwa hiyari ya wana wa Tanganyika, bali ni kwa hujuma na usaliti wa mtanganyika mwenyewe.

Hitimisho langu ni kuwa, kama muungano wa Tanganyika na Zanzibar bado upo na utaendelea kuwepo. Naomba basi pia Tanganyika itambuliwe kama Tanganyika katika hii katiba mpya. Ya nini izaliwe Tanzania bara wakati Tanganyika bado ipo na ina historia yake kama ilivyo Zanzibari?
 
Kuna mambo yaliyomo kwenye rasimu ya katiba mpya ni mazuri lakini mambo mengine tumerudi nyuma kuliko zamani.kuwa na serikali tatu is unbearably too heavy a burden! taifa lenye madeni mengi kama hili halafu tuongeze ukubwa wa serikali? mimi nilifikiri katiba mpya ingeangalia uwezekano wa kuwa na serkali moja na siyo tatu.kimantiki watu watatu kuwa katika maelewano kwa Nchi zetu hizi ni mtihani.uwe na rais wa Zanzibar,Rais wa Tanganyika na Raios wa JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA na wakaelewana!
 
Hii ni kutoka katika rasimu ya katiba mpya!
Kutakua kuna uhuru kweli?
...mkuu tunendeleza mambo yaleyale kwa kuitazama katiba mpya na masuala yanayohusiana zaidi na vyeo, madaraka, na mamlaka, badala ya kutujuza mapungufu ya hiyo rasim ya katiba mpya ktk masuala yenye maslahi ya moja kwa moja kwa kina sisi wa mitaani, mathlani ushirika umepigiwa chapuo ya kutosha? je, rasimu imeweka wazi kwa mfano, zabuni zote za halmashauri na manispaa zipewe kwa makundi ya ushirika ya vijana na kina mama? vp kuhusu haki ya watotot wetu kuelimishwa na taifa kuanzia chekechea mpaka chuo kikuu?...amka kijana wa tanzania!!!
 
Kuna mambo yaliyomo kwenye rasimu ya katiba mpya ni mazuri lakini mambo mengine tumerudi nyuma kuliko zamani.kuwa na serikali tatu is unbearably too heavy a burden! taifa lenye madeni mengi kama hili halafu tuongeze ukubwa wa serikali? mimi nilifikiri katiba mpya ingeangalia uwezekano wa kuwa na serkali moja na siyo tatu.kimantiki watu watatu kuwa katika maelewano kwa Nchi zetu hizi ni mtihani.uwe na rais wa Zanzibar,Rais wa Tanganyika na Raios wa JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA na wakaelewana!

Mkuu kuhusu hilo, na kwa nature ya kibongo bongo, itatuchukua mwaka kujadili kuhusu kuhamisha kiti toka sehemu moja mpaka nyingine,
 
Bwana Zekidon: Tukubaliane kwa consensus ya Watanzania wote kuwa tunahitaji Katiba Mpya.
Wazo lako ni sawa lakini sio 100% valid kwa kuwa unatuambia mambo muhimu zaidi ni ya resources na poverty.

Tukiwa na Katiba ambayo itakuwa na misingi imara ya usimamizi wa rasilimali tunaweza kuhakikisha mabadiliko yanakuja.
 
Wadau leo ndio rasimu ya katiba mpya Inazinduliwa Karimjee .Uzinduzi huo unatarajiwa kurushwa na vituo vya TBC1, TBC Taifa, ITV, Star TV, Channel Ten, ZBC TV na ZBC, kuanzia sasa.Kila anaeweza na afuatilie.Hata hivyo ni vizuri kila mtu angetoa maoni yake ikiwa ni kitu gani ambacho akiona kimewekwa humo angefurahi sana na ni kitu gani ambacho kikiachwa atasikitika sana.

Nawasilisha!
Mbona hakijaeleweka? Huku bara na sisi tutakua na rais wetu? Mbona ndio mwanzo wa kuvunjika muungano. Rais wa shirikisho atakuaje executive kwa kushughulikia mambo 7 tu ya muungano? Hebu waliosoma hiyo rasimu tujuzeni.
 
Calm down everybody! Naona mmekuwa emotional kidogo.

Points kama "hakuna nchi iliyowahi kuitwa Tanzania Bara, kwa hivyo hilo jina lifutwe" zinatoka wapi? Hakuna vile vile nchi iliwahi kuitwa Tanzania!

Tanzania Bara na Tanzania Visiwani ni majina yanayojumuisha jiografia vizuri sana. Tanganyika ni jina lililokuwepo zamani. Limekufa kama yalivyokufa majina Rhodesia, Zaire na Nyasaland.

Serikali tatu is a diversion, but this is a common thread with intellectuals, from Nyalali and now Warioba. This is scarcely new. While I hardly see any utility in the idea, I grant it will remove the awkwardness of our unique union. Sadly, I am not disposed to say the same about our poverty. In fact, you have argued correctly that the added burden of extra bureaucrats will not be negligible.

I do not expect the revival of the use of Tanganyika, a defunct state. That would be confusing and even more awkward than the two government union we have now. To which purgatory did this Tanganyika hybernate for all these years? Did it resurrect like Lazarus?

That said, Tanzania bara is a misnomer if not an outright contradiction, for in Tanzania you have Zanzibar, hence Tan-Zan, which we lived with for sometime while searching for a proper name.

I am not liking either Tanzania Bara or Tanganyika (sentimentalities aside) for this set of Tanzania complement Zanzibar.

I am not sure I like the idea anyway. The bulk of our problems lie with Zanzibaris who want full autonomy (an euphemism for breaking the union), not Tanzanians who want a third government.

In giving Tanzanians a third government, Warioba and team, like a geek programmer sailing high in the tech cloud, provided a technical solution that does not address a nagging pain.

I want to see if they have addressed the nagging pains.
 
ninangojea niipate rasimu na kuisoma niilewe vizuri. Lakini kabla ya hapo, nimefurahishwa na tume kupendekeza katika nchi hizi mbili zilizoungana, kila nchi iwe na serikali yake. Tanganyika (sio tanzania bara) na zanzibar. Kutokana na hilo, je kila nchi itakuwa na raisi wake? Je kiongozi wa kusimamia masuala yale saba yaliyowekwa kuwa ndio masuala pekee ya muungano, naye ataitwa rais? Je katiba ya kushughulikia yale masuala saba ya muungano ndio hiyo inayojadiliwa sasa? Je kama kila nchi itakuwa na katiba yake, mamlaka ya katiba ya muungano yanaishia kwenye yale masuala saba ya muungano na sio vinginevyo? Ninapata kigugumizi sana kwa hili.


kazi kwako. Rasimu hiyo hapo ushindwe mwenyewe
 

Attachments

  • Rasimu _Final_ (1).pdf
    387.8 KB · Views: 31
Its a wastage of resources kuwa na serikali tatu.

If we are seriously into our Union, tuwe na serikali moja.

I see this as a diversion into the facts that need be addressed.

Mambo yote ambayo ni controversial na tyalionekana na wazee wetu hapo mwanzo, (Karume na Nyerere) yamo humu ndani).

I see a clear and crystal intwntion to diversify us from facts such as poverty and natural resources.

Tutaachwa tukijadili haya mambo watu wakifanya yao.

I suggest katika rasimu mpya neno Tanzania Bara be removed and replaced by Tanganyika, Hakuna kitu kama TANZANIA BARA bali kunaTanganyika.


Kuna watu wanadhani zikishaundwa hizo serikali tatu ndiyo Zanzibar itatulia na kusema hewala!! We are very wrong. Baada ya kupata mamlaka kamili ndiyo mwanzo wa Wazanzibar kudai kile walichovuna na Tanganyika huko nyuma, kuna hatari kukaibuka madai ya fidia kwa kile wanachoita 'Ukoloni wa Tanganyika'.

Lakini najiuliza Umajunui wanaoutetea akina Warioba kwenye rasimu ni upi hasa? Kuusambaratisha Muungano kwa kuunda Serikali tatu? Yaani unaunda vinchi ndani ya linchi wakati watu wanapambana kuunda manchi makubwa. Hiki ni kituko kwa karne hii. Sasa tuwe na shirikisho la Tanzania then shirikisho la Afrika Mashariki?

Kitu kingine ambacho kinaniacha hoi, wanatoa sababu ya gharama kubwa za uendeshaji kama sababu ya kukataa sera ya decentralization (Majimbo???) sasa kurundika maserikali matatu si ndio gharama mara dufu?

Another quick look; maana yake tuna kazi tena ya kuandaa katiba ya Tanganyika na Zanzibar tena, maana hii ikipita ni ya Serikali ya Shirikisho (Muungano).In short ile hoja ya JK kuongezewa muda inaweza kuwa na mashiko kwa sasa ili kutoa mwanya wa uandaaji wa katiba za nchi hizi mbili na hatimaye uchaguzi kuja kufanyika. Ni vigumu kwa katiba za Zanzibar na Tanganyika kupatikana sasa sambamba na ile ya Muungano. So kuna vituko vingi zaidi huko mbele.

Shocking enough, wanasema nchi hizi mbili zitafuata mfumo wa vyama vingi, kwa msingi upi? Kwamba vyama vya siasa vya Tanganyika vitakuwepo Zanzibar pia??? Ina maana CCM, CHADEMA nk. vilivyoko Tanganyika vitakuwepo Zanzibar??
 
Kwa siasa za Tanzania, ni jambo gumu sana kuwa na katiba ya Tanganyika kabla ya mwaka 1015. Hata hivyo, maoni ya watanganyika kuhusu katiba ya Tanganyika tume ya katiba wanayo, kwa hiyo ni kiasi tu cha kukaa chini kwa mwezi mmoja na kuyaweka katika maandishi kama hii katiba. Ila, siasa za Tanzania na watu wanavyopenda sitting allowances, inaweza ikachukua mpaka 2020 ndio Tanganyika ipate katiba yake.
Kuhusu Tanganyika vs Tanzania bara. Ni woga wa watawala na kutokuwa objective katika kuwa wazi. Jina halisi la Tanzania bara ni TANGANYIKA, na wanatakiwa wawe BOLD kabisa. Jina Tanzania lilikuja baada ya muungano ulioasisiwa mwaka 1964, which means Tanganyika was there before and it was supposed to be there to stay. Hata hivyo, ulimwengu mzima watu wa visiwani wana inferiority complex, ndio maana Nyerere aliwaachia jina Zanzibar libaki nao. Waingereza wenyewe kwa sababu wako viziwani hata wanataka wajitoe EU.
 
Kwa siasa za Tanzania, ni jambo gumu sana kuwa na katiba ya Tanganyika kabla ya mwaka 1015. Hata hivyo, maoni ya watanganyika kuhusu katiba ya Tanganyika tume ya katiba wanayo, kwa hiyo ni kiasi tu cha kukaa chini kwa mwezi mmoja na kuyaweka katika maandishi kama hii katiba. Ila, siasa za Tanzania na watu wanavyopenda sitting allowances, inaweza ikachukua mpaka 2020 ndio Tanganyika ipate katiba yake.
Kuhusu Tanganyika vs Tanzania bara. Ni woga wa watawala na kutokuwa objective katika kuwa wazi. Jina halisi la Tanzania bara ni TANGANYIKA, na wanatakiwa wawe BOLD kabisa. Jina Tanzania lilikuja baada ya muungano ulioasisiwa mwaka 1964, which means Tanganyika was there before and it was supposed to be there to stay. Hata hivyo, ulimwengu mzima watu wa visiwani wana inferiority complex, ndio maana Nyerere aliwaachia jina Zanzibar libaki nao. Waingereza wenyewe kwa sababu wako viziwani hata wanataka wajitoe EU.

Ikumbukwe, tume ya Warioba ilikuwa na 50% wazanzibar ambao hawana mamlaka ya kujadili mambo ya Tanganyika.
 
Hoja si kuongozwa na wafu au la...kila taifa lina historia yake, na hatuwezi kujitenga na hao watu wawili tukitaka kurudi nyuma katika historia for reference purpose, ni sajabu kuwa na jambo jipya bila ya la zamani, hivyo basi tunahitaji mawazo yaliyoweka msingi wa taifa hili katika kujenga taifa jipya, that is if we want Taifa jipya, We can let Zanzibar go, but faida ya Zanzibar kwenda ni ipi?? iKIBAKI NI IPI?? Ok Zanzibar wanabendera yao, hiyo ina badili nini?? USA the most powerful country in the world bado inaongozwa na misingi ya uhuru waliyoweka kina Abraham Lincon, na Bado wanawaheshimu na kukubali misingi yao bora, sisi taifa changa ambalo bado tunaishi kwa misaada tunajua NINI katika anga za kisiasa na kidemokrasia?? I think we are better of together than being solo, we needa stronger union than this, Warioba and his group daima watakua na laana ya kulibomoa Taifa hili kwa kisingizio cha Katiba mpya.

umeharibu hapo tu RED, mapendekezo ya tume ya warioba sio yao binafsi ni maoni ya wananchi na kama ni yao tunayo fursa ya kukataa wakati wa kura za maoni. Kura ya maoni ikisema sawa yatakuwa ni maoni yetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom