RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

MMh mimi ninavyo kutazama katika ulichokiandika nikwamba wewe rasimu yenyewe hujaielewa na possibly wewe ni slow learner....Anyway hii rasimu inaelezea wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano na sio Tanganyika wala Zanzibar
 
Mabunge ni mangapi jamani? Je bunge la tanganyika lipo?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Watanzania wakati umefika ni lazima tuondokane na mawazo mgando ya serikali mbili, ambazo utekelezaji wake ni mgumu sana kwa nyakati zetu hizi. Lazima tuambatane na fikra mpya na chanya za kuwa na taasisi zilizojengewa misingi ya kikatiba ya uwajibikaji. Demokrasia inayosemwa, sasa inatakiwa iingie kwenye matendo, kuliko kubaki nadharia tuu.

Mfumo huo mpya wa dola utapunguza sana gharama za uendeshaji wa Serikali na Bunge la Muungano kwa kiasi kikubwa, hivyo kuwapunguzia wananchi mzigo. Mfumo huo mpya wa serikali tatu ni cheaper(una gharama nafuu) kuliko mfumo wa sasa, kwasababu:
1.Mfumo mpya una mawaziri wachache(15) kuliko wa sasa(56).
2.Mfumo mpya una wabunge wachache(75) kuliko wa sasa(375).
3.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye wizara husika kuliko wa sasa.
4.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye ofisi za bunge kuliko wa sasa.
5.Mfumo mpya utakuwa na uwajibikaji mkubwa kuliko wa sasa, ambao mamilioni ya pesa za walipa kodi yanapotea.
6.Mfumo mpya hauna ofisi ya wazili Mkuu, hivyo gharama zote zilizopo sasa za kuiendesha ofisi ya PM na makandokando yake hazitakuwepo.

Hivyo basi, mfumo mpya wa dola unapunguza kwa kiasi kikubwa gahrama za uendeshaji wa dola.
Huu mfumo mpya ni mzuri na unaotekelezeka kirahisi, bila kuhitaji gharama kubwa. Mfumo huo upo Ujerumani,Marekani, Afrika kusini, Uingereza, India Nk

Mfumo huu mpya utatoa ajira nyingi kwa vijana wetu wasomi, kwasababu upatikanaji wa fursa za kazi hautakuwa unatawaliwa na mfumo wa kikilitimba, miungu watu, na kupendeleana kama ulivyo sasa. Kwani kwa sasa kupata kazi lazima uwe ulizaliwa ktk familia ya mwanasiasa fulani au unafahimia na mtu fulani maarufu, au utoe rushwa.

Naipongeza tume kwa kufanya kazi kisayansi.

Hili linatekelezeka lakini linahitaji commitment vinginevyo mamabo yaweza kuwa magumu zaidi ya sasa nasema hivyo kwa kuangalia aina ya utawala tulionao sasa.
Tusipokuwa makini huu unaweza kuwa mwanya wa wajanja kupata njia ya kuibia hela kwa sababu kutakuwepo na migawanyo mingi ya mapato kwa serikali zote tatu.
Pia tujiandae kwa mchakato mya wa katiba ya Tanganyika maana hii ni ya Jamhuri ya muungano.
 
Nina wasiwasi na HAKI ZA MAKUNDI MADOGO KATIKA JAMII.makundi gani hayo? .waliberali watakitumia sana hiki kipengele.
 
Nashukura sana kwa comment yako isiyo na utafiti na yenye woga, mawazo mgando yasiyozingatia hitaji la wakati.

Zanzibar toka mwaka 1964 wanayo serikalia yao ambayo inaendesheka mpaka leo.
Tanzania bara(Tanganyika) inatakiwa iunde serikali yake kadiri ya uwezo na hitaji la kweli, siyo kupeana vyeo kwa hoja za kirafiki au kisiasa. Katika ulimwengu wa leo ambapo mambo mengi yanaendeshwa na private sector huhitaji kuwa na serikali kubwa.
Unless unataka kuwapa kazi ndugu na rafiki zako. Kwa Tanzania bara mawaziri 12 watosha kabisa. Idara katika wizara zepewe mamlaka makubwa ya kuamua mambo. This to me is the best solution.

Hivi mkuu jaribu kuchunguza post yako! ulivyoileta kwa mtu wa kawaida inakuwa na hitimisho! ya kuwa serikali itakuwa hivyo. Mimi naona labda hayo uliyonijibu ungeyaunganisha kwenye post yako hapo juu ungelieleweka vizuri.
 
Rasimu ya katiba iliyozinduliwa jana inatupa matumaini bali binafsi naona serikali tatu ni mzigo kwa wananchi. Serikali ya muunganoitakua na wabunge 75 na mawaziri wasiopungua 15. Lakini serikali hii itategemea mapato yake kutoka serikali ya Tanzania Bara na Zanzibar. Watakaoumia zaidi kuibeba ni Tanzania Bara. Sielewi kabisa bunge na mawaziri wa muungano watakua wanafanya nini wakati kila upande wa hizo serikali mbili kuna wabunge na mawaziri wao. Naona pengine tuchague tu rais wa muungano halafu kila upande kuwe na waziri mkuu mtendaji atakaechaguliwa na wabunge wa serikali hiyo. Kwa staili hiyo tutaepuka mzigo mkubwa.
Ni lini wananchi walikuwa na mzigo mwepesi? Zanzibar, bon voyage and God bless you


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Sidhani kama itakua busara hili linipite bila kutia neno...mwanga mpya na matumaini yanataka kuonekana, Nimeikubali hii rasimu...
 
Mkuu acha kuwapotosha watu! tulia soma vizuri rasimu! hao 15 ni wa shirikisho tu, bado wa Tanganyika! upo hapo?

Mimi nina mawazo tofauti. Hivi ni lazima kuungana? Walishindwa wasenegali na wagambia. Kila upande ubaki kuwa ni nchi na mamlaka yake kama ilivyokuwa kabla ya 1964. Hapo tutapunguza gharama za uendeshaji. Tunaweza kuungana kwenye East Afrika.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Demokrasia ina gharama zake. Mfumo huo mpya wa serikali tatu ni cheaper(una gharama nafuu) kuliko wa sasa kwasababu:
1.Mfumo mpya una mawaziri wachache kuliko wa sasa.
2.Mfumo mpya una wabunge wachache kuliko wa sasa(375).
3.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye wizara husika kuliko wa sasa.
4.Mfumo mpya utakuwa na wafanyakazi wachache kwenye ofisi za bunge kuliko wa sasa.
5.Mfumo mpya utakuwa na uwajibikaji mkubwa kuliko wa sasa, ambao mamilioni ya pesa za walipa kodi yanapotea.

Hivyo basi, mfumo mpya wa dola unapunguza kwa kiasi kikubwa gahrama za uendeshaji wa dola.

Naipongeza tume kwa kufanya mambo kisayansi.
Sio kweli Kuwa serikari Tatu ni nafuu ebu toa mfano wa taifa changa lenye serikari tatu lenye maendeleo? ZNZ akiongoza Gavana na Huku Tanganyika akaongoza Gavana mmoja tu huku Rais Akiwa mmoja anayekaa Dodoma Hakuna gharama unakuwa muungano nafuu kuliko Nchi masikini Kuwa na Marais Watatu.
 
Tanzania ni Taifa changa Kuwa na Marais watatu ni mizigo kwa walipa kodi Kama imeshindikana mbinu zote ni bora ifanyike kampeni ya kuwaunganisha watanzania wote Bara na visiwani ikibidi kura ya maoni tuungane tuwe Taifa moja Rais mmoja tu tuepuke hizi Gharama za kuendesha serikari nyingi wakati uwezo wa kituleta pamoja upo
 
Kimsingi Watanzania wanaaminishwa kuwa wakitua mizigo miwili iliyowashinda wataweza kubeba mitatu mikubwa zaidi. Mkiwa na serikali tatu ya Tanganyika itakuwa na nguvu zaidi huku wengine wanaeza kuona Zanzibar itakuwa na nguvu zaidi!
 
Natafuta copy ya rasimu ya katiba mpya. mdau yoyote anayejua nnapoweza kuipata please tujuzane
 
Watu wengi hawajui kwanin muungano ulikuwapo? Hatupendi kujiuliza hilo badala yake tunakimbilia ama kuuvunja au kuuimarisha pasipo kujua chanzo cha uwepo wake. Hata watawala wetu wanapata kigugumiza kusema kam tulilazimishwa na mabepari.hil n tatizo
 
Back
Top Bottom