Rais wetu kupewa jezi ya RONALDO

kipi kina uzito kupewa jezi na Rais kwa club hiyo au kupewa jezi na mchezaji mwenyewe?
Yeye hakwenda kumtembelea Ronaldo - alienda kuongea na uongozi wa Real Madrid na Mmiliki wake juu ya kukuza soka la nchi yetu.

Sasa baada ya mkutano anaulizwa ungependa zawadi gani tukupe toka madrid? hapo yeye akaamua apewe jezi ya Ronaldo, lakini angeweza hata akapewa mipira 10,000 aje aigawe kila wilaya au angeomba madrid isaidie kutujengea soka academy moja as example - hayo yalikuwa maamuzi yake.

Sioni tatizo la Rais kuchagua apewe jezi ya Ronaldo baada ya mkutano - Mlaumuni kwa mengine ila siyo hili mnakwenda mbali.

Angeipokea kimyakimya na familia yake sawa...unapoalika Meya wa JIJI lenye watu 5m na media cover then its for public interest....inakuwa nchi imepewa jezi siyo Jakaya
 
Mimi nashangaa kabisa. Watu wanatumia pesa za walipa kodi kuandaa sherehe ya kukabidhi jezi. Kuna shule zimefungwa kwa sababu ya kukosa madawati, wazazi wanafia wodini kwa kukosa dawa, waalimu wanalia mishahara haitoshi lakini watu wengine wanafuja pesa kwa sherehe zisizo za lazima. Pengine nashindwa kuelewa vipaumbele vya Nchi yetu ni yepi hasa? Kutumia pesa kwa ajili ya mambo yasiyo na ulazima??????
Hao ndio viongozi tulionao ndani ya nchi yetu. Hawajali umasikini uliokithiri wa mtanzania wanaangalia matumbo yao tu.

Tanzania yetu hiyo...
 
- Yaani huyu Rais bwana ninamuonea huruma sana, akibembea makosa, akienda msibani makosa, akisafiri kutafuta misaada makosa, akicheka ooh ni mnyonge, akikasirika ohh muongo, sasa hata kupewa jezi ni breaking news na kuna utata jinsi alivyopewa! Sijui ndio maana ya vyama vingi, loh! huruma kweli hili taifa.

- Ohhh Tanzania, an information starved nation!

FMEs!

Mkuu inbidi tu umuonee huruma jinsi watu wanvyomtumia kama ngazi
Nina hakika 99.99% hiyo jezi Kimbisa kanunua mwenyewe halafu kaenda kumpa ili kujijengea kama imetoka Real Madrid
ANGALIZO: KAMA INGETOKA REAL MADRID INGEKUWA SIGNED NA WACHEZAJI WOTE NA ISINGEKUWA NA JINA
TIMU SIO YA MTU MMOJA ISITOSHE HIZO JEZI NDIO WANAZITOA HATA KATIKA FUND RAISING KWANI INAKUWA EXPENSIVE SANA
HUYO KIMBISA KAMPATA HUYO HUYO RAISI WAKE
 
JK mtu wa WATU bwana. Matamasha yumo, kombe la FIFA yupo, Hashim Thabeet kala naye lunch, kapiga picha na Bi Kidude, Leo kasaini muswada "live" wa pesa za matumizi ya uchaguzi, mawodini kwa wagonjwa utamkuta, misibani, mazishini hakosi,......

Hana lolote mzushi tu..Kwa kipindi cha miaka mitatu sasa jamaa amekwepa kuonana na watu wenye ulemavu..Amekuwa akiwapa appointment kila leo halafu baadaye huwa anaibuka na a very nice excuses ili asikutane nao.Ni sifa tu zinazomsumbua..Sorry kama nimewakwaza baadhi ya watu humu.
 
Suala hapa ni kwamba Rais - Taasisi ya Rais - amedhalilishwa!

Kama kulikuwa na umuhimu wa Rais kupewa TUZO hiyo, isingetolewa na KLABU bali asasi kama FIFA, CAF, CECAFA, etc. Na isingekuwa JEZI! Na kama ingekuwa jezi, basi, isingekuwa ya RONALDO!

Aibu tupu!

Ikulu hakuna wasaidizi, kuna mamluki wa kifisadi!
 
Wakuu,

Juzi nilisoma interview aliyopewa Didier Drogba wakati walipoweka kambi hapa bongolanda alisema " before coming here i didn't know tanzania or anything about tanzania"..jamaa mwafrika mwenzetu doesn't know anything about tanzania....ronaldo ndio atajua? c'mon give me a break...haya mambo ya kupewa jezi ni mkuu wetu kutaka kuwa "omnipresent" which is impossible...i believe our president is a "populist" which is not a bad thing if you want to sell something...lakini presidency is another issue...its not about what you do but how you do it..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom