Dar Es Salaam, Mbona unakwepa kutusaidia kufahamu tatizo la Rais wetu na badala yake unaanza ku-edit messages za watu? hapa kuna koma, pale kuna el hapa pawe hivi na unamaliza kwa mtindo wa jinsia ya aina fulani, kwamba ukizozwa wewe unaishia kuzomea.. Hiloooo! Oooo! yebaaa!
JF tunataka Uandike maoni yako kwa mada iliyoko mbele yetu. Hatujasema haleti maendeleo. Hatujasema hajafanya kitu, nk. Tatizo letu ni hotuba na aina ya maneno anayotumia ktk hotuba. Hata kama atatuletea kocha wa mpira kila mkoa kama kitendo cha maendeleo, bado hiyo siyo sababu ya kufurahia hotuba zilizopinda-pinda kwa uzembe wakati uwezekanao wa kuzionyoosha unaonekana.
Haswa, taswira ya JK ni ukweli na uwazi na anaongea, kwenye hotuba zake ukweli mtupu, chuki binafsi zinawafanya mumchukie, kawakosa nini? Rais aliyewajengea mashule mengi kuliko Rais yeyote aliyepita! Rais aliyewafichua mafisadi wa toka enzi za Nyerere! Rais aliye ahidi na kuanzisha chuo kikuu kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki, katika muda usiofikia miaka miwili toka aahidi, Rais anaemalizia mabarabara yaliyowashinda ma Rais wote waliopita, mpaka sasa unaona raha ukienda Mwanza kutokea Dar, huna haja tena ya kupitia Kenya labda uwe na sababu zako za kupita huko, lakini si kuwa barabara ni mbovu. Rais alieweza kwa mara ya kwanza katika Historia kumuweka na kumfadhili Rais wa Merekani kwa siku nne katika Afrika, Looh, bado tu hajui kutoa hotuba? ooopssss, Rais wa kwanza wa Tanzania kuwa Mkulu wa AU,, Rais wa kwanza katika Tanzania alieweza kushusha bei ya mafuta yanayotumika kwenye magari na viwanda, haijawahi kutokea, bado hajui kutoa hotuba tuu? tafuteni jengine sio hili. Looohhh.
hivi mnataka aeleze nini.msaidieni au mundikieni kwenye web site yake kumueleza mnayopenda kusikiliza.pengine mumezoea porojo
Haswa, taswira ya JK ni ukweli na uwazi na anaongea, kwenye hotuba zake ukweli mtupu, chuki binafsi zinawafanya mumchukie, kawakosa nini? Rais aliyewajengea mashule mengi kuliko Rais yeyote aliyepita! Rais aliyewafichua mafisadi wa toka enzi za Nyerere! Rais aliye ahidi na kuanzisha chuo kikuu kikubwa kuliko vyote Afrika Mashariki, katika muda usiofikia miaka miwili toka aahidi, Rais anaemalizia mabarabara yaliyowashinda ma Rais wote waliopita, mpaka sasa unaona raha ukienda Mwanza kutokea Dar, huna haja tena ya kupitia Kenya labda uwe na sababu zako za kupita huko, lakini si kuwa barabara ni mbovu. Rais alieweza kwa mara ya kwanza katika Historia kumuweka na kumfadhili Rais wa Merekani kwa siku nne katika Afrika, Looh, bado tu hajui kutoa hotuba? ooopssss, Rais wa kwanza wa Tanzania kuwa Mkulu wa AU,, Rais wa kwanza katika Tanzania alieweza kushusha bei ya mafuta yanayotumika kwenye magari na viwanda, haijawahi kutokea, bado hajui kutoa hotuba tuu? tafuteni jengine sio hili. Looohhh.
Dar,
Kama unalipwa kwa kazi hiyo basi unastahili kupata malipo hayo. Hata hivyo Watanzania hawali orodha ya mafanikio!
Dar,
Kama unalipwa kwa kazi hiyo basi unastahili kupata malipo hayo. Hata hivyo Watanzania hawali orodha ya mafanikio!
Dark City, mwenzetu huyu Dar ni die hard fan wa JK, na ni haki yake lakini kama anafanya kazi kubwa hivyo ya kumtetea ni vyema akihakikisha analipwa ipasavyo.
Alafu mi nahisi huyu Dar asije akawa ndo speechwriter wake na issue inamgusa moja kwa moja.... kwikwikwii...
Huyu Rais jamani na hizi hotuba zake! Ni kama Tz hatuna wataalamu wa hotuba kiasi kwamba Rais hajapata mtu wa kumuandikia hotuba za ki-Rais.
Zile za kila mwisho wa mwezi ni kama summary ya matukio. Yeye akaziita hotuba.
Akatoa ile ya half term ikawa imejaa matusi pale alipojidai kutoa michapo. Eti lazima uliwe ndo ule. Tena kwa kurudia-rudia na kucheka. Rais huyo!
Kuna ile nyingine ya siku ya UKIMWI hiyo ndo alitoa mpya. UKIMWI ni wa kujitakia. Mbele ya wananchi wake, wenye ukimwi na wasio na ukimwi. Wakubwa na watoto. Akaendelea na matusi mengine.
Huko Pemba tena ndo kaja na hayo anayodhani ni ushujaa wa kisiasa kwa kutumia maneno kama ya taarabu.
Rais yabidi ashauliwe apate mwandishi wa maana. Aaambiwe asome hotuba na siyo kutoa yake kichwani maana yaonekana uwezo huo hana. Najua ugumu utakuwa ktk kujibu maswali lakini kwa Rais wa Africa ni rahisi kukwepa mahojiano. Tahadhari yaficha aibu.
"Taarifa kamili" iambatane na CV ya mtajwa itakayojumuisha kiwango chake cha elimu.