Rais wangu Kikwete, siwezi kununua hata dagaa sasa!

Rais Kikwete, miezi 2 iliyopita dagaa kilo moja ilikuwa tsh 3000, leo hii dagaa tsh6200.

Nina watoto 3 wanaosoma, siwezi kuwalisha. Nyama siwezi kununua, na hata dagaa siwei kununua kwa mshahara wa laki 250,000.

Nadhani umeshindwa kuongoza nchi kilichobaki ni sisi kuingia mitaani kukuondoa kama hautaki kuondoka mwenyewe. Siwezi kuendelea kuvumilia, kwa maana kama dagaa chakula cha masikini siwezi kukinunua ni nini sasa nitakachoweza kununua kuwalisha wanangu?

Niwalishe wanangu nini? Nilikupigia kura nikiamini kwamba ungeleta mabadiliko uliyoyaahidi...... baba ondoka, kwa maana umekiua chama chetu cha CCM, vinginevyo tunakwenda Chadema wamama wote


Pole sana ndugu, kumbe ulimpigia kura baada ya yote uliyoyaona kwa miaka yake mitano!!! Kweli watz tumefunikwa!!! Pole kaka, vumilia tu hivo hivo mpaka wakati wako uishe, sisi hatuwezi kukujoin wewe uliemfanikisha kufika alipo sasa.
Na aliekuwa akimpa ulinzi usio onekana ndo keshafariki hivyo mtaendelea kuona ya ajabu na hatari kuliko yaliyotokea na yanayotokea sasa.
 
Rais Kikwete, miezi 2 iliyopita dagaa kilo moja ilikuwa tsh 3000, leo hii dagaa tsh6200.

Nina watoto 3 wanaosoma, siwezi kuwalisha. Nyama siwezi kununua, na hata dagaa siwei kununua kwa mshahara wa laki 250,000.

Nadhani umeshindwa kuongoza nchi kilichobaki ni sisi kuingia mitaani kukuondoa kama hautaki kuondoka mwenyewe. Siwezi kuendelea kuvumilia, kwa maana kama dagaa chakula cha masikini siwezi kukinunua ni nini sasa nitakachoweza kununua kuwalisha wanangu?

Niwalishe wanangu nini? Nilikupigia kura nikiamini kwamba ungeleta mabadiliko uliyoyaahidi...... baba ondoka, kwa maana umekiua chama chetu cha CCM, vinginevyo tunakwenda Chadema wamama wote

Ujumbe umefiaka, nukuu hii inatoka kwenye ukurasa wa FB wama mkewe.


372957_149199238444871_46363609_q.jpg Mama Salma Kikwete
Okoa Tanzania. Piga vita ufisadi na utendaji mbovu wa viongozi. Jiandae kutumia kura yako kwa busara mwaka 2015. Usirudie makosa.
 
Mrembo, hakuna haja ya kulia nyie ndo mliompigia huyo JK kura.

waaambie pamoja na kucheza kwenye majukwaa na kina joti na komba ,halafu walaumu au muulize mbunge wako kujiongezea posho ndio kutatua tatizo la maisha magumu,
tafakar........... kama ccm ni chaguo sahihi

 
Wakwere woyeeeeeeee!!!!Msoga woyeeeeeeeeeeeeee!!!!Hiyo ni robo tu JK kawaonjesha je akitoa kilo ni kuchali mazima,Picha ndio limeanza sasa.
 
acha ujinga wewe uza mwili'unamlalamikia kikwete akuletee hela nyumbani''komaa upate elfu22 nyingii hili ununue kilo nyingi za dagaa'hii ndio africa bana nyie vpi'komaaa wewe.'kila cku kikwete kikweteee fanya kazi rais haezi kuwa na roho mbaya kiasi hiki'timu yake ndio inamfanyia hujuma'pumbavu nyie CHADEMA.
Mpumbavu mwenyewe usieona hali ya maisha nchini kwako ilivyo,shame on you!Idiot!
 
Kwa kukujuza tu zaidi, BOT ilichomwa moto kabla ya Nyerere kung'atuka na kila kitu kikaunguzwa, mpaka leo hakuna aliyesema moto ule umesababishawa na nani. Muujiza..
Mi naukumbuka sana huo moto wa BOT, nimezaliwa na kukulia city center. Ila acha porojo wewe mama ule moto haukuwa mkali ku-vaporise gold, unajua hata boiling point ya gold ni kiasi gani?

Mali zilizopo ardhini si zako mpaka pale utapoweza kuzitumia, usijidanganye kuwa una dhahabu iko chini ya ardhi basi ndiyo "reserve" yako, huo ni ukosefu wa utimamu. Dhahabu na maoi nyini zilizopo chini ya Ardhi zingine kuzichimba kwake ni gharama kubwa kuliko thamani yake. Ngoja kwanza uzichimbe uziweke benki ndiyo uhesabu kuwa ni "reserve" yako. Wacha kupiga alinacha.

La haula la kwata! Hivi umesahau ule msemo wetu waswahili, "akiba haiozi"? Naelewa kuwa gharama za extraction zinaweza kuwa kubwa kuliko faida lakini gharama zinaweza kuondolewa baadae kutokana na tekinologia (hata kama ni miaka 50 ijayo). Hii haiondoi ukweli eti hatuna reserve.

We mwenyewe siunajua kuwa Canada wana oil reserve kubwa iliyoganda kwenye barafu, japokuwa siyo proftable kuiyeyusha kwasasa kwasababu bei ya pipa moja la mafuta machafu ni chini ya $160. And last time I checked Canada inajiita ni nchi yenye reserve kubwa ya mafuta.
 
Hana muda na matatizo yako, yuko bize kuchongeshewa suti!
 
Mkuu acha uvivu hakuna maisha rahisi wala ya mkato fanya kazi kwa bidii..

Serikali ya mtu ni kichwa chake mwenyewe hakuna ujanja unjanja kwenye maisha kama saizi upo kwenye Net unatumia pesa umetoa wapi amekupa Kikwete?

Wewe mtoto wa kiume usepende kulalamika pambana
Hizo ni fikra MGANDO,na according to your statement,inaonyesha bado unathamini falsafa ya mwenye nacho ataendelea kua nacho.Unamwambia apambane,HOW?Ashike bunduki na kuibia watu?

Ajira hakuna atapambanaje?Atajiajiri vp wakati mikopo yenyewe inatolewa kwa masharti magumu eg;hati ya nyumba,na mtu huyohuyo ndio amemaliza chuo this year,hiyo nyumba kaijengaje?Wakati mwingine muwe mnaandika vitu ya maana kuliko UPUMBAVU kama huu,Na ukija kutoa kauli kama hizo hadharani utakuja KUUWAWA
 
GDP inazidi kuongezeka. Inflation iliyoto ni temporarly tu. Wengine kwetu dagaa ni superior goods wakati wewe unanziona inferior! Kama ukishindwa kula dagaa...unaweza kushift kwenda kwenye mikate.

mama weeeee wapuuzi kama hawa wapo ccm na ndio wanaongoza nchi
 
Rais Kikwete, miezi 2 iliyopita dagaa kilo moja ilikuwa tsh 3000, leo hii dagaa tsh6200.

Nina watoto 3 wanaosoma, siwezi kuwalisha. Nyama siwezi kununua, na hata dagaa siwei kununua kwa mshahara wa laki 250,000.

Nadhani umeshindwa kuongoza nchi kilichobaki ni sisi kuingia mitaani kukuondoa kama hautaki kuondoka mwenyewe. Siwezi kuendelea kuvumilia, kwa maana kama dagaa chakula cha masikini siwezi kukinunua ni nini sasa nitakachoweza kununua kuwalisha wanangu?

Niwalishe wanangu nini? Nilikupigia kura nikiamini kwamba ungeleta mabadiliko uliyoyaahidi...... baba ondoka, kwa maana umekiua chama chetu cha CCM, vinginevyo tunakwenda Chadema wamama wote

Mkuu laki 250,000 ni sawa na 25,000,000,000. Mbona ni mshahara mkubwa sana?:shock:
 
Na bado mtalia sana ndio gharama ya pilau, kofia, T-shirts, khanga, kwaya, Zeee OK, ubongo wa fuleva, mipasho, upupu, kuanguka majukwaani, vibastola na upuuuzi mwingi tu mlioushangilia October 2010 nchi nzima na october 2011 Igunga. Huu ni mwanzo tu wa kilio cha kusaga meno. Bado dhiki kuu yaja na mtalipa ghali kwelikweli.
 
Pole dadaa,
Umelielezea vizuri tatizo na limeeleweka, ila kwenye solution ndio umeenda kombo kidogo.
Umeshauri kutatua tatizo la kushindwa kununua dagaa kwa kuingia mtaani na kumuondoa Kikwete madarakani.
Je, umetathmini gharama ya kufanya hivyo?
Je, umetathmini kuanzia unaingia mtaani mpaka unafanikiwa kumtoa itachukua muda gani?
Je, umetathmini kuanzia siku unayomtoa madarakani mpaka siku utakayoweza kununua dagaa wapendwa itakuwa siku ngapi?
Je, umetathmini uwezekano wa kumtoa Kikwete na badala yake kupata kiongozi ambaye atakufanya sio tu ukose dagaa ila ushindwe hata kupata access ya internet ya kutujulisha ulichokosa?

Kikwete ameibakiza miaka minne kutuongoza. Baada ya hapo tutakuwa na fursa ya kuchagua kiongozi mwingine kistaarabu na kwa wanaoona wanaliweza jukumu wanaweza kuomba kuchaguliwa.
Kwa sasa endelea kufanya bidii na kuwakumbusha viongozi majukumu yao, wasipotekeleza adhabu ni 2015.
Mambo ya kuingia mtaani usiyape nafasi kwa sababu kwa kufanya hivyo utaharibu hata kidogo kilichopo.
 
hali ni ngumu sana,
umeamua dada twende tuingie barabarani
si uliona yule mama mstaafu wa EA alivyofurama pale posta
ikawa kasheshe inabidi tuanze kinamama ili baba zetu waunge mkono.
 
Hizo ni fikra MGANDO,na according to your statement,inaonyesha bado unathamini falsafa ya mwenye nacho ataendelea kua nacho.Unamwambia apambane,HOW?Ashike bunduki na kuibia watu?

Ajira hakuna atapambanaje?Atajiajiri vp wakati mikopo yenyewe inatolewa kwa masharti magumu eg;hati ya nyumba,na mtu huyohuyo ndio amemaliza chuo this year,hiyo nyumba kaijengaje?Wakati mwingine muwe mnaandika vitu ya maana kuliko UPUMBAVU kama huu,Na ukija kutoa kauli kama hizo hadharani utakuja KUUWAWA

Wewe kijana unaweza kunipiga mkwala mbuzi mimi? Tatizo nyie vijana wa kizazi cha sasa ni wavivu mno.

Hivi unataka ushinde vijiweni na kwenye vilabu vya mbege bila kufanya kazi halafu unalalamikia serikali ikupe pesa!

Hata kodi ya nyumba unataka serikali ukulipie? Hiyo itakuwa serikali au upo peponi? Kama upo tayari njoo nikupe ajira..

Kila mwezi takupa 400,000 kama upo tayari ni-PM
 
GDP inazidi kuongezeka. Inflation iliyoto ni temporarly tu. Wengine kwetu dagaa ni superior goods wakati wewe unanziona inferior! Kama ukishindwa kula dagaa...unaweza kushift kwenda kwenye mikate.

umenikumbusha yule mfalme mjinga aliambiwa watu wako wana njaa...akauliza sasa ni kwani wasile keki?
 
Exchange rate sio kigezo cha mafanikio, leo China wanapigiwa kelele wapandishe thamani ya fedha yao, wanasita.

Hakuna reserve tuliyokuwa nayo benki wakati Nyerere anaondoka, kama huelewi itafute hotuba ya Ali Hassan Mwinyi maarufu "mikuki miwili" alieleza kinaga ubaga alikuta hakuna kitu benki. Kwa kukujuza tu zaidi, BOT ilichomwa moto kabla ya Nyerere kung'atuka na kila kitu kikaunguzwa, mpaka leo hakuna aliyesema moto ule umesababishawa na nani. Muujiza.

Mali zilizopo ardhini si zako mpaka pale utapoweza kuzitumia, usijidanganye kuwa una dhahabu iko chini ya ardhi basi ndiyo "reserve" yako, huo ni ukosefu wa utimamu. Dhahabu na maoi nyini zilizopo chini ya Ardhi zingine kuzichimba kwake ni gharama kubwa kuliko thamani yake. Ngoja kwanza uzichimbe uziweke benki ndiyo uhesabu kuwa ni "reserve" yako. Wacha kupiga alinacha.

Ni ukweli usiopingika kuwa JK ameshindwa kuongoza nchi. Alikuja na kauli mbiu yake eti maisha bora kwa kila mtanzania; kwa kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya. Uchaguzi uliopita akaja na usanii mwingine eti nguvu zaidi, ari zaidi na kasi zaidi... Kilichomsaidia kuendelea kukalia kiti asichokimudu ni ile tume yao(CCM) ya uchaguzi na Polisi-CCM.... Duh! nimesahau plus Usalama wa T.....a......i...f...a.

Hizo Phd wanazompa hazina maana yoyote....... Goooooooooooooooooooooo JK........................Goooooooooooooooooooooooooooo
 
Wewe kijana unaweza kunipiga mkwala mbuzi mimi? Tatizo nyie vijana wa kizazi cha sasa ni wavivu mno.

Hivi unataka ushinde vijiweni na kwenye vilabu vya mbege bila kufanya kazi halafu unalalamikia serikali ikupe pesa!

Hata kodi ya nyumba unataka serikali ukulipie? Hiyo itakuwa serikali au upo peponi? Kama upo tayari njoo nikupe ajira..

Kila mwezi takupa 400,000 kama upo tayari ni-PM

wewe unafanya kazi gani zaidi ya kuiba fedha za wananchi? Halafu unajipigapiga kifua eti unafanya kazi?
 
Njaa tulikuwa nayo wakati wa Nyerere. Tunapanga foleni ya unga wa msaada (wa njano) kwa kaya kwa wiki kilo moja. Dagaa ilikuwa anasa.

Leo mwenye njaa ni ama mvivu kupita kiasi au hana akili timamu. Au ni katika wale wanaongojea kupewa na wanashindwa hata kujituma. Leo tunaona mpaka wageni kutoka Ulaya, Asia na nchi zingine za Kiafrika wakikimbilia hapa kuja kuchuma, fursa wanaziona zimejaa kedekede, halafu mtu analalamika tuna njaa. Mie nasema hamna macho lakini si njaa.
Hiki ni kichekesho cha mwaka huu, rais mwenyewe anazunguka dunia mzima kutembeza bakuri la kuomba misaada halafu mtu mwingine anasema kila kitu kipo. Huo ni uvivu wa kufikiri au kujipendekeza kupita kiasi. Jamaa kaingia madarakani sukari ilikuwa shilling 600 na leo iko 3000, hapo huhitaji uswahiba kuelewa. Watu Kama nyie hamna msaada wowote kwa chama kwa kuwa hamtoi fursa kwa chama chenu kujirekebisha na kuwatumikia vela wananchi. Hakuna kit muhimu kama kusikiliza malalamiko ya mpuga kura kama huyu na kuyafanyia kazi
 
Back
Top Bottom