Tetra
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 1,526
- 771
Kila mmoja katika kuubeba ubinadamu anao uwezo na udhaifu wake.Na sitaki kuamini kuwa kuna binadamu ni mbaya wakati wote wa nafasi yake katika dunia bali yapo mazuri pia.Kwa haya mawili Kikwete nitakukumbuka
::
1
UHURU WA FIKRA
Nakuona kuwa Rais pekee mwenye kifua cha kuvumilia kukosolewa.Umeruhusu maoni,mitazamo,na michango tofauti.Uhuru huu umevuka mipaka lakini unauthamini.Sidhani ingekuwa rahisi kwa wengine nikikulinganisha na watangulizi wako.Ni kweli pia elimu na maarifa yamepanuka sana hivyo jamii inaamini ni vigumu kudhibitiwa Lakini kwa mamlaka uliyonayo ungeweza kutumia ubabe kuzima uhuru.Spika Anna Makinda nadhani anapaswa ajifunze kwa hili ili wabunge wetu awape uhuru wa kujadili hoja.
::
2
KUANIKA UOZO
Nikitazama vizuri hakuna awamu ya Urais iliyoweka hadharani uovu wake na ule wa nyuma kama awamu yako.Umekuwa wazi kuruhusu chunguzi japo matokeo ya chunguzi yanabaki kitendawili Lakini hata kuanikwa tu yakafahamika ni kazi nzuri.Mf. Kuanikwa kwa Uozo wa Richmond,Uozo wa EPA,uozo wa halmashauri nyingi Tanzania kupitia office ya C.A.G (uliyoipa nguvu ya kisheria) n.k Yote ya baraka zako.Ungeweza kuagiza yakafukiwa ila tabia yako ya kuruhusu UNDER CARPET to be ON CARPET inanipa nguvu ya kukusifu.
Rais wangu nitakukumbuka kwa hayo.
=
::
1
UHURU WA FIKRA
Nakuona kuwa Rais pekee mwenye kifua cha kuvumilia kukosolewa.Umeruhusu maoni,mitazamo,na michango tofauti.Uhuru huu umevuka mipaka lakini unauthamini.Sidhani ingekuwa rahisi kwa wengine nikikulinganisha na watangulizi wako.Ni kweli pia elimu na maarifa yamepanuka sana hivyo jamii inaamini ni vigumu kudhibitiwa Lakini kwa mamlaka uliyonayo ungeweza kutumia ubabe kuzima uhuru.Spika Anna Makinda nadhani anapaswa ajifunze kwa hili ili wabunge wetu awape uhuru wa kujadili hoja.
::
2
KUANIKA UOZO
Nikitazama vizuri hakuna awamu ya Urais iliyoweka hadharani uovu wake na ule wa nyuma kama awamu yako.Umekuwa wazi kuruhusu chunguzi japo matokeo ya chunguzi yanabaki kitendawili Lakini hata kuanikwa tu yakafahamika ni kazi nzuri.Mf. Kuanikwa kwa Uozo wa Richmond,Uozo wa EPA,uozo wa halmashauri nyingi Tanzania kupitia office ya C.A.G (uliyoipa nguvu ya kisheria) n.k Yote ya baraka zako.Ungeweza kuagiza yakafukiwa ila tabia yako ya kuruhusu UNDER CARPET to be ON CARPET inanipa nguvu ya kukusifu.
Rais wangu nitakukumbuka kwa hayo.
=