Rais wangu JK: Watanzania wanakufa Ujerumani, tafadhali chukua hatua ya haraka kuwaokoa

Siku nyingine mkipata nafasi za kwenda nje pitieni kwenye vijiwe vya watoto wa mujini mjifunze mbinu nyingine za kuishi nje za nchi.

...kati ya hao wanafunzi kuna ambao wanasoma mwaka wa tatu sasa, miaka mitatu Ujerumani bila ya kuwa na connection ya japo kijikazi cha kuosha vyombo kwenye migahawa ya Kebab si rahisi kumtokea mtoto aliyetokea "kijiweni" hata kukiwa na Wapolish,Wabulgaria,n.k wa kumwaga (Waturuki wapo wengi Ujerumani tokea zamani sana)!

Pia kuna tatizo kwa Watanzania wengi (si wote) ku-intergrate katika nchi wanazoishi.

Vinginevyo natumai kuwa matakwa yenu (waathirika)yaliyo katika mikataba yatatimizwa haraka!

Kua jambo muhimu sana umelisema kwenye thread yako...
Jibu lake ni Kwamba,Katika Wanafunzi ambao wanasoma NCHI za NJE DUNIANi(tofauti na nchi zao),hususani wanaotoka nchi zinazoendelea,WATANZANIA ni Wanafunzi wanaaonekana ni CLASS A citizens kutokana na kwamba wengi wao huwa wanatimiziwa MAHITAJI YAO kadiri iwezekanavyo kutoka kwa serikali zao...

Kama umewahi kusoma Vyuo vya nje,kwa kweli utaweza kuona jinsi Wanafunzi wa kutoka Nchi nyinginezo hususani za Afrika jinsi wanavyopata taabu katika kukidhi mahitaji yao,kwani serikali za Nchi zao either hazina uwezo kabisa wa kuwagharimia chochote,ama hazitimizi kabisa mikataba ya kuwalipia chochote kile,hivyo Waafunzi hao walishajizoesha kwamba serikali zao haziwasikilizi chochote,na mara zote wanajitahidi kufanya kile wawezacho kujikimu.

Hii inaweza kudhihirisha kwamba katika nchi zinazoendelea,Tanzania ni Nchi mojawapo inayojitahidi sana sana katika kutimiza majukumu yake,licha ya kwamba si kwa muda sana,lakini bado serikali ni Tegemeo kubwa sana kwa Wananchi wake.

Ukitaka kujua pia kwamba Tanzania ni Nchi nzuri,linganisha idadi ya Wanafunzi wanaorudi nyumbani mara tu baada ya kumaliza masomo yao katika nchi yeyote huko Ughaibuni.....Watanzania wanaongoza,,,,kwa sababu Nchini kwao kuna "promising future".......Waafrika wengi sana huwa wakimaliza masomo Nchi za nje hubaki huko

Ninakumbuka mwaka mmoja nusu uliopita mliandika pia hapa jamiiforums kuhusu malalamiko yenu kama haya

Ni haki yenu,,,,lakini ninadhani kwamba mnawahi mno kutoa malalamiko,,,,,hivi hamjalipwa hela ya May na June ama ni hela ya June tu?
Kuna Watu wanasoma nje pia,huwa hawalipwi hata kwa miezi 6,lakini huwa wanakuwa wavumilivu kidogo.

Kwa muda huu ninawatakia uvumilivu bora...endeleeni kutumia mishahara yenu(ambayo ninaamini mipango madhubuti ya serikali yenu inawawezesha muendelee kupokea mishahara huku mkiwa masomoni).

Nawatakia kila la kheir.....

Pia mjitahidi kuosha masufuria na kupandisha zege huko maghorofani jamani...Ohoooo
 
Hizo shida wapatazo ni sehemu ya course work, laiti malalamiko haya yangetolewa na undergraduate ningeelewa, lakini PHD, mtu ambaye tunarajia awe na macho yaonayo gizani, opportunity maker, mtu ambaye tunatarajia kila tatizo ali convert to opportunity, leo anatoa kilio cha sauti hivyo! Tena walalamika bila kutoa suluhu, bali mwisho wanaomba kuonewa huruma.
Natambua fika namna wanavyodharirika, na sitetei uzembe wa serikali, mimi najiuliza kwa nini usomi wao ugeuke sumu na silaha dhidi yao wenyewe bada ya kuwa nyenzo ya ukombozi, wa kifikra, na kimazingira?
 
Sijuwi kama Kikwete amekusikia hapa, yaani aache kwenda kupia deki barabara afuatilie hili, sijuwi....yangu macho na masikio.
 
Nyie acheni uoga wa maisha mnashindwa kuosha vyombo kwa restaurant na kutandika vitanda kwenye ma hotel kama wenzenu???

Fungeni mkanda nchi bado changa hii vyuo mliviacha kibao Tanzania mkaenda nje mkizani huko kuna maziwa na asali.
Hii ni fundisho kwa wengine na mjue kabisa ulaya kwa sasa maisha ni magumu kuliko Afrika
 
Poleni sana
Ila mtambue Tanzania kwa sasa ni bahati mbaya sana hatuna Rais sasa sijui itakuwaje
 
Tupo katika karne ya 21 ni jukumu la wanafunzi kuishitaki serikali iwe Ujerumani au Tanzania, mikataba mnayo serikali ambayo siyo sikifu dawa yake ni kuishitaki mahakamani. Jipangeni tena Ujerumani mnaweza mkaweka rehani jengo la ubalozi bila hivyo pesa zote za walipa kodi zitaishia kuwaneemesha wana Msoga na Bagamoyo.
Kuna sheria za immigration
 
Pole sana next time nyie wanafunzi mnaoenda kusoma nje hakikisheni ufadhili unakua 80% kutoka serikali ya nchi husika na 20% ndio iwe kutoka TZ manake si mnafahamu serikali yetu.Sio wewe tu unayeteseka na hii shida hata mimi nina ndugu yangu amepata ufadhili wa kusoma china lakini mpaka anamaliza 4 years ni mara moja tu alipata hela kutoka Serikali wakati mwingine ilikua ni kugangamala tu ndio sasa hivi ameshamaliza anaanza kupambana kupata hela yake hiyo.
 
PhD zote ni ngumu, lakini lazima muwe wabunifu kutokana na hali halisi. Mnao muda wa kutosha kuchacharika na kujipatia kipato. Acheni kulalamika tafuteni solution, ndio maana ya Ph D

Nawasiwasi kama unajua unachokiongea, hivi unafikiri Germany ni kama UK ama US? Kwanza kuna kikwazo cha lugha, pili sababu tunapokea pesa ya DAAD tunatakiwa kulipa kodi kwa kipato tunachokipata ambacho kisizidi 410€ kwa mwezi. Kikizidi 410 € kwa mwezi wanakata kwenye allowance yako. Mwisho ni kama nilivyoandika awali, tunatumia muda mwingi maabara na course work. Hatufanyiwi kazi yoyote na technicians. Sasa tukifreeze masomo kwa semester moja ni lazima tutaongeza muda, sasa kwa scholarship hii usome PhD miaka mitano si tutafia huku. Maana tunapokea kiwango kidogo, na maisha ni ghali sana. Tulifata ELIMU bora ili turudi kulitumikia Taifa, na si kukaa huku kwa miaka mingi.
 
Nawasiwasi kama unajua unachokiongea, hivi unafikiri Germany ni kama UK ama US? Kwanza kuna kikwazo cha lugha, pili sababu tunapokea pesa ya DAAD tunatakiwa kulipa kodi kwa kipato tunachokipata ambacho kisizidi 410€ kwa mwezi. Kikizidi 410 € kwa mwezi wanakata kwenye allowance yako. Mwisho ni kama nilivyoandika awali, tunatumia muda mwingi maabara na course work. Hatufanyiwi kazi yoyote na technicians. Sasa tukifreeze masomo kwa semester moja ni lazima tutaongeza muda, sasa kwa scholarship hii usome PhD miaka mitano si tutafia huku. Maana tunapokea kiwango kidogo, na maisha ni ghali sana. Tulifata ELIMU bora ili turudi kulitumikia Taifa, na si kukaa huku kwa miaka mingi.
Je hampati likizo japo ya week 4 kwa kipindi chote cha miaka 5? Je out of 24 hrs, masaa mangapi upo nje ya masomo? Je hayo masomo yenu ni kwa lugha gani? Maisha ni kuchacharika, hakuna hata siku moja utakuwa na muda mwingi, if you 're looking for excuse, I have a book for you. Kila situation uliyokuwa nayo, kitabu hicho kitakupa excuses
 
labda tu mkuu utujuze huu usumbufu huwa unatokea kila mwaka au ni mwaka huu tu ili tujue labda ni bahati mbaya au ni uzembe wa watendaji katika sehemu husika.
 
labda tu mkuu utujuze huu usumbufu huwa unatokea kila mwaka au ni mwaka huu tu ili tujue labda ni bahati mbaya au ni uzembe wa watendaji katika sehemu husika.

Mkuu,
Hii ya si mara ya kwanza. Hii hali imekuwa ikiwakuta mara kwa mara.
 



Niliweka comment kwenye hii pic lakini Mungiki Brother aligwaya na kuifuta chacha nafahamu anachotaka ni kunifungia. Hivi hawa pimbi kutoka kwa manyang'au tutaachana nao lini? Pambaf kabisa.


BTW Kicheko cha Fisadi papa ni artificial chacha anayebisha alete picha ambayo aliwahi kucheka hivyo maishani mwake. BO very natural .... ..

 
Back
Top Bottom