Tangu ameingia madarakani rais Magufuli amekuwa akijinasibu kuwa yeye ni rais wa wanyonge, kauli hii imekuwa ikinishangaza sana, hivi rais Magufuli ni rais wa wanyonge wapi? Tangu ameingia madarakani hao wanyonge wamenufaika vipi na uongozi wake.
Rais aliingia madarakani wanyonge wakinunua sukari 1800/= leo hii 3000/=, unga 800/= leo hii 1200/=~1,500/= hao wanyonge anaowasaidia ni wa nchi gani?
Kipindi cha nyuma kulikuwa na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa wakulima lakini tangu aingie madarakani ruzuku hiyo haipo, watoto wa wanyonge waliokuwa waingie vyuo vikuu hawana mikopo wapo nyumbani wamekaa, kuna wanyonge wamemaliza vyuo vikuu lakini mpaka sasa hawana ajira na hawajui hatma zao, rais ameua elimu kwenye shule za kata ambazo watoto wa wanyonge wanasoma.
Kwa ufupi ni kwamba ameongeza umaskini kwa jamii, lakini cha ajabu kila akisimama anajinasibu yeye ni rais wa wanyonge, wanyonge wapi hao.
Rais aliingia madarakani wanyonge wakinunua sukari 1800/= leo hii 3000/=, unga 800/= leo hii 1200/=~1,500/= hao wanyonge anaowasaidia ni wa nchi gani?
Kipindi cha nyuma kulikuwa na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa wakulima lakini tangu aingie madarakani ruzuku hiyo haipo, watoto wa wanyonge waliokuwa waingie vyuo vikuu hawana mikopo wapo nyumbani wamekaa, kuna wanyonge wamemaliza vyuo vikuu lakini mpaka sasa hawana ajira na hawajui hatma zao, rais ameua elimu kwenye shule za kata ambazo watoto wa wanyonge wanasoma.
Kwa ufupi ni kwamba ameongeza umaskini kwa jamii, lakini cha ajabu kila akisimama anajinasibu yeye ni rais wa wanyonge, wanyonge wapi hao.