Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,777
Wakuu
Huyu kijana anatakiwa akapewe somo na Vijana wa UDOM, ameshindwa kusemea changamoto zisizokoma za wanafunzi huko vyuoni anatuletea uchawa, na hao vijana wanaomshangilia wakicheleweshewa boom wanatoa milio 24/7.
===
Rais wa Jumuiya ya Taasisi za Wanafunzi Wa Elimu ya Juu, TAHLISO, Geofrey Kiliba ameeleza kuwa Wanafunzi wa Vyuo na vyuo vikuu nchini watashiriki uchaguzi Mkuu kikamilifu Mwezi Oktoba mwaka huu,kama sehemu ya utekelezaji wa haki yao ya Kikatiba pamoja na kudumisha amani kwa kuchagua Viongozi bora.
Kiliba amebainisha hayo wakati wa utoaji wa tuzo za Silent Ocean Uniawards 2025 Jijini Dar Es salaam kwenye chuo cha Mwalimu Nyerere, akisisitiza pia kwamba mitandao ya Instagram na X, sio Tume ya Uchaguzi, hivyo wote wenye ajenda muhimu zenye maslahi na Taifa ni muhimu wakatumia mifumo na njia rasmi zilizopo na zinazokubalika kisheria.
Kiliba kadhalika ameeleza kuwa TAHLISO haitokuwa na hiyana na yeyote ambaye hana nia njema na Tanzania sambamba na wote wanaoenda kinyume na Katiba na sheria za Tanzania, akisisitiza umuhimu wa kutunza amani na ustawi wa Tanzania.
Huyu kijana anatakiwa akapewe somo na Vijana wa UDOM, ameshindwa kusemea changamoto zisizokoma za wanafunzi huko vyuoni anatuletea uchawa, na hao vijana wanaomshangilia wakicheleweshewa boom wanatoa milio 24/7.
===
Rais wa Jumuiya ya Taasisi za Wanafunzi Wa Elimu ya Juu, TAHLISO, Geofrey Kiliba ameeleza kuwa Wanafunzi wa Vyuo na vyuo vikuu nchini watashiriki uchaguzi Mkuu kikamilifu Mwezi Oktoba mwaka huu,kama sehemu ya utekelezaji wa haki yao ya Kikatiba pamoja na kudumisha amani kwa kuchagua Viongozi bora.
Kiliba amebainisha hayo wakati wa utoaji wa tuzo za Silent Ocean Uniawards 2025 Jijini Dar Es salaam kwenye chuo cha Mwalimu Nyerere, akisisitiza pia kwamba mitandao ya Instagram na X, sio Tume ya Uchaguzi, hivyo wote wenye ajenda muhimu zenye maslahi na Taifa ni muhimu wakatumia mifumo na njia rasmi zilizopo na zinazokubalika kisheria.
Kiliba kadhalika ameeleza kuwa TAHLISO haitokuwa na hiyana na yeyote ambaye hana nia njema na Tanzania sambamba na wote wanaoenda kinyume na Katiba na sheria za Tanzania, akisisitiza umuhimu wa kutunza amani na ustawi wa Tanzania.