Jobless graduate
Member
- Apr 1, 2019
- 96
- 135
Ni kawaida kila Rais mpya anapoingia madarakani kuja na kauli mbiu au falsafa yake.
Kauli mbiu hizi au falsafa ndio huonyesha dira au mwelekeo wa serikali inayokuwepo madarakani katika kuleta maendeleo kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Katika awamu ya kwanza chini ya utawala wa hayati Julius nyerere yeye alikuja na kauli mbiu ya ujamaa na kujitegemea. Falsafa hii ilikusudia kutokomeza unyonyaji katika nyanja zote ili kila mtu anufaike na rasrimali tulizonazo na taifa kujitegemea kiuchumi pasipo utegemezi wa misaada toka nje.
Baada ya Nyerere alikuja mzee Ally hassan Mwinyi. Katika kipindi chake alikuja na kauli mbiu ya ''Ruksa'' ambayo ililenga kutoa ruksa kwa kila mtu kufanya chochote akitakacho pasipo kuvunja sheria, kanuni na taratibu za nchi.
Baadaye akaja Hayati Benjamin Mkapa na kauli mbiu ya ukweli na uwazi. Kauli mbiu ambayo ililenga kupambana na vitendo vya ufisadi, rushwa na uzembe serikalini kwa kuimarisha ufanisi, uwazi na uwajibikaji serikalini.
Baada ya mkapa akaja mzee Jakaya. Yeye alikuja na kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania ambayo ililenga kuinua watu kiuchumi na kuwafanya wawe na maisha mazuri(bora).
Ndipo akaja marehemu Magufuli na kauli mbiu ya ''hapa kazi tu''. Ambayo ililenga kuhimiza watu kufanya kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa nchi.
Sasa tunaye mama Samia suluhu ambaye ni Rais wa sita. Je atakuja na falsafa yake au ataendelea kuishi katika falsafa ya magufuli ya hapa kazi tu?
Binafsi nashauri mama Samia aje na kauli mbiu yake ambayo imefanyiwa tafiti mbali mbali kujua matatizo na changamoto tulizopitia watanzania katika miaka mitano iliyopita kwa lengo la kuzitatua au kuzipatia suluhu kama jina lake.
Nachelea kusema hivi kwa sababu kauli mbiu ya "hapa kazi tu" ni kauli mbiu ya hovyo kuwahi kutokea sababu ina hamasisha watu kufanya kazi wakati kazi zenyewe hazionekani huku fursa za kufanya kazi serikalini zikiwa zimepunguzwa au kubanwa kabisa, hivyo kauli mbiu hii imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutengeneza jobless graduates wengi isivyo kawaida.
Kauli mbiu hizi au falsafa ndio huonyesha dira au mwelekeo wa serikali inayokuwepo madarakani katika kuleta maendeleo kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
Katika awamu ya kwanza chini ya utawala wa hayati Julius nyerere yeye alikuja na kauli mbiu ya ujamaa na kujitegemea. Falsafa hii ilikusudia kutokomeza unyonyaji katika nyanja zote ili kila mtu anufaike na rasrimali tulizonazo na taifa kujitegemea kiuchumi pasipo utegemezi wa misaada toka nje.
Baada ya Nyerere alikuja mzee Ally hassan Mwinyi. Katika kipindi chake alikuja na kauli mbiu ya ''Ruksa'' ambayo ililenga kutoa ruksa kwa kila mtu kufanya chochote akitakacho pasipo kuvunja sheria, kanuni na taratibu za nchi.
Baadaye akaja Hayati Benjamin Mkapa na kauli mbiu ya ukweli na uwazi. Kauli mbiu ambayo ililenga kupambana na vitendo vya ufisadi, rushwa na uzembe serikalini kwa kuimarisha ufanisi, uwazi na uwajibikaji serikalini.
Baada ya mkapa akaja mzee Jakaya. Yeye alikuja na kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania ambayo ililenga kuinua watu kiuchumi na kuwafanya wawe na maisha mazuri(bora).
Ndipo akaja marehemu Magufuli na kauli mbiu ya ''hapa kazi tu''. Ambayo ililenga kuhimiza watu kufanya kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa nchi.
Sasa tunaye mama Samia suluhu ambaye ni Rais wa sita. Je atakuja na falsafa yake au ataendelea kuishi katika falsafa ya magufuli ya hapa kazi tu?
Binafsi nashauri mama Samia aje na kauli mbiu yake ambayo imefanyiwa tafiti mbali mbali kujua matatizo na changamoto tulizopitia watanzania katika miaka mitano iliyopita kwa lengo la kuzitatua au kuzipatia suluhu kama jina lake.
Nachelea kusema hivi kwa sababu kauli mbiu ya "hapa kazi tu" ni kauli mbiu ya hovyo kuwahi kutokea sababu ina hamasisha watu kufanya kazi wakati kazi zenyewe hazionekani huku fursa za kufanya kazi serikalini zikiwa zimepunguzwa au kubanwa kabisa, hivyo kauli mbiu hii imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutengeneza jobless graduates wengi isivyo kawaida.