Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Katika kutalii kwangu, nimepata kuitembelea nchi moja iitwayo kusadikika. Katika hiyo nchi, wananchi wanamlaani rais wao. Wanamuombea laana ya milele rais huyu wa ajabu anayetawala nchi kama yuko kwenye mdundiko wa kizaramo.
Nadhani rais huyu anawaza midundko, miduara,kichen pati,sendoff, na safari za kujiuza marekani kuliko hali ngumu ya maisha ya Wanakusadikika. Sasa amezinduka baada ya kuona kinachoendelea Tunisia, Misri na Libya. ila pamoja nakuzinduka wananchi wake wenye hasira naye wanasema kwamba hataweza kufanya lolote kwani kichwani hana jipya zaidi ya midundiko na kutabasamu anapoona nzi wakipita mbele yake
Rais huyu wa nchi ya kusadikika, ni mdini, mchonganishi na mtu mwenye kinyongo na raia wake. Amekuwa akiwajali marafiki zake na mafisadi kuliko raia wa kawaida. Rais huyu aliyetunukiwa shaada nyingi za falsafa amekuwa kama kikatuni fulani kwenye nchi yake. Urais ameugeuza kama mali ya familia yake. Rais analiacha taifa kwenye majonzi makubwa yeye anaelekea kutalii na kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya watu wengine huku nchi yake ikiwaka moto. Raia wamechoka na rais anayeendekeza starehe kuliko maslahi ya taifa. Rais ameiuza nchi. Kucheza ngoma na mduara kwenye ikulu ya kusadikika ina maana kubwa kuliko kutafuta suluhisho ya wanasadikika
Kwa bahati mbaya kuyakumbatia mafisadi ndo chanzo cha kuangamia kwake... Laiti rais wa kusadikika angalijua mapema !
Nadhani rais huyu anawaza midundko, miduara,kichen pati,sendoff, na safari za kujiuza marekani kuliko hali ngumu ya maisha ya Wanakusadikika. Sasa amezinduka baada ya kuona kinachoendelea Tunisia, Misri na Libya. ila pamoja nakuzinduka wananchi wake wenye hasira naye wanasema kwamba hataweza kufanya lolote kwani kichwani hana jipya zaidi ya midundiko na kutabasamu anapoona nzi wakipita mbele yake
Rais huyu wa nchi ya kusadikika, ni mdini, mchonganishi na mtu mwenye kinyongo na raia wake. Amekuwa akiwajali marafiki zake na mafisadi kuliko raia wa kawaida. Rais huyu aliyetunukiwa shaada nyingi za falsafa amekuwa kama kikatuni fulani kwenye nchi yake. Urais ameugeuza kama mali ya familia yake. Rais analiacha taifa kwenye majonzi makubwa yeye anaelekea kutalii na kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya watu wengine huku nchi yake ikiwaka moto. Raia wamechoka na rais anayeendekeza starehe kuliko maslahi ya taifa. Rais ameiuza nchi. Kucheza ngoma na mduara kwenye ikulu ya kusadikika ina maana kubwa kuliko kutafuta suluhisho ya wanasadikika
Kwa bahati mbaya kuyakumbatia mafisadi ndo chanzo cha kuangamia kwake... Laiti rais wa kusadikika angalijua mapema !