"Rais wa misiba"

Usiwe mbinafsi kiasi hiki kijana kuwa na upendo na Jirani zako,ninachokiongea Mimi ni kile ninachokiona na kukisikia,sicho kinachonipata Mimi Bali kina wapata wengine,Mimi na feel maumivu yao kwasababu ni wanadam wenzangu! Mtu mzima aliyebakiza miaka miwili kustaafu amelitumikia taifa hili kwa miaka Yake yote Leo hii anaambiwa ameliibia taifa kwa sababu hana cheti,niambie uchungu anaoupata mzee huyu je atakuwa na upendo kutoka moyoni kwa kiongozi wake?

Wana Kagera walipatwa na majanga,kauli ya kwanza kutoka kwa kiongozi wao ni wafanye kazi wajenge miundo mbinu na nyumba zao kwasababu tetemeko halijaletwa na serikali,michango ya kuwasaidia mkaipeleka kwenye ujenzi wa miundombinu ya serikali wao kama wananchi wakaachwa walalie majani ya migomba.
Upendo wa mwanadam huyu kwa kiongozi wake utatoka wapi? Kijana jitahidi kulichukulia hili jambo liwe kama limekupata wewe.

Tumuogope Mungu,unafiki kitu kibaya sana palipo na ukweli ongea ukweli ila iwe ni kweli kutoka moyoni.

Manung'uniko yao ndio ishara ya kukata tamaa na kiongozi wao.
 
Hawezi kunyamaza labda wewe uende kijijini ndiyo utajua level ya huyo unayemt.t.a. wanavijiji hatujahawahi kuchoka mapema kiasi hiki halafu tunaowategemea wameachishwa kazi ghafla hata bila kufuata kanunu za kazi
 
siyo hilo tu ndugu yangu fikiri kumwachisha mtu kazi Ghafla aliyekuwa kazini kwa miaka 32 bado mmoja astaafu hii siyo haki, kwa sababu alikuwepo hapo kihalali na serikali iliyopita ilimtambua wewe uko tofauti gani na huyo aliye mwajiri na kufurahia matunda ya kazi yake? Jamani twende mbele na kurudi, wakuhukumiwa siyo huyu mlalahoi ni wale waliompokea ili asaidie kuliendesha gurudumu la nchi hii.(
 
we jamaa ni jobless? hauko busy? unatumia muda na rasilimali bundle kuandika upuuzi
 
Asante mkuu kwa kunielewa,Mungu akubariki sana.
 
Alichokifanya mh rais siwezi laumu hata siku moja,wewe mwenyewe nyani ngabu umekiri urais ni mzigo mimi nasema hata sio urais tu tizama tu hata kwa ngazi za kifamilia yaani unaweza fanya jambo ukaishia kupewa lawama tu.

Wewe mwenyewe umekua shahidi hapa wengine wanasema kakosea kutohudhuria, wengine bora hajenda angeleta tafurani, yaani mitanzania tu wanafiki nafikiri tunaongoza, mimi naona aende, asiende poa tu kuongoza watu wa hivi nikujipa stress tu maana hatuishiwi maneno jamani.
Nilikua na mpenda kikwete naninampenda Magufuli kuongoza binadamu si mchezo bwana.
 
 

Attachments

  • 18380766_896346160506681_8488051894655123456_n.jpg
    54 KB · Views: 30
Walau wewe naona umekuwa mkweli.

Yaani hata angefanyaje bado angelaumiwa tu.

He is damned if he does and damned if he doesn't.

It's just the nature of the beast.
 
aibu sana halafu akaingia twita akasema anauchungu sana hahaha kwahiyo msiba aliangalilia kwenye tv????????


my foots there is something wrong pahali iko taabu wala msijitie kusema ni msimamo .......... aliona la maana kwenda kwa masaburi kutangaza wake na watoto lakini hawa malaika aaah!!!!!!!
msimamo................. doooooooooooo,
mnaomshabikia huyu mtu mna walakini naninyi, kikombe cha loliondo kirudi mkimeze tena labda mtapona
 
Wenzetu wanasemaje kuhusu kiongozi wao kuhudhuria "tragedies" ....

'Symbol of the country'


Ahead of Thursday's trip, White House press secretary Josh Earnest said the president sees these condolence trips as a solemn responsibility: "The president understands that he is a symbol of the country, and when he travels to a community and meets with a family that has endured a terrible tragedy, he's offering a message of condolence and comfort on behalf of the American people."

"When these kinds of events occur," Rottinghaus said in an interview, "the public really does look to the president as a true national healer, and somebody who can make sense of the situation, but who can also lend a shoulder to be able to understand what this means in the grand scheme of things."


Source: Obama Is ‘Healer-in-chief,' Comforting Families of Those Slain in Orlando
 

Hiyo ni kweli kabisa.

Magufuli was wrong for not going.
 
Sio lazima aende kwenye misiba wakati wapo makamu wake na anaweza kumuwakilisha... kwenye mambo kama hayo wacheni maneno mengi CHAPENI KAZI.
 
Yule dogo uliyefurahia alipompa peremende yuko wapi?

Ahahahaaa daaaaah....

Umenikumbusha mbali sana aisee.

Hivi hii haikuwa 2008 au 2009 kweli?

Pia naukumbuka vyema kabisa ule mjadala wake.

I pretty much rolled solo in defending him saying there was nothing wrong with him giving candy to that youngster.

Dogo si ajabu atakuwa keshakuwa mtu mzima sasa.....

Umeifukulia wapi hiyo picha lakini?
 
Kwa hiyo unasema Mzee Kikwete alifanya madudu siyo?
 
Kwa hiyo unasema Mzee Kikwete alifanya madudu siyo?
Unaposema Rais Kikwete alifanya madudu una maana gani?

Kumbuka hakuna Rais au Waziri Mkuu duniani anayetoka madarakani bila kufanya madudu.

Hoja ya msingi ni madudu gani na yalikuwa na impact gani kitaifa na kimataifa?

Hukusikia wakati wa kampeni viongozi wa CCM walikuwa wanahubiri mabadiliko ya kweli? Hiyo inakuambia kuwa kuna masuala fulani yalifanywa na serikali ambayo yalitakiwa yafanyiwe mabadiliko ya kweli katika utawala wa serikali ijayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…