Yoyo Zhou
Senior Member
- Jun 16, 2020
- 169
- 287
Katika mkutano huo, Trump alisifu kiwango cha Kiingereza cha Rais Joseph Boakai wa Liberia, ambapo alimuuliza amejifunza wapi Kiingereza vizuri na elimu yake, na kuuliza amesomea wapi, na alipoambiwa kuwa ni Liberia, rais Trump alimsifu kwamba anazungumza vizuri lugha ya kiingereza, tofauti na marais wengine waliokuwa kwenye mkutano huo.
Video ya tukuio hilo la kufedhehesha ilienea mara moja kwenye mitandao ya kijamii, na watumiaji wa mtandao kutoka nchi mbalimbali walimcheka rais Trump kwa kutojua kwamba lugha rasmi ya Liberia ni Kiingereza, na kumkosoa kwa kuwadharau viongozi wa Afrika.
Baadhi ya Waliberia walikasirika sana na matamshi ya rais Trump. Mwakili wa vijana wa Libeŕia Archie Tamer Harris alisema anahisi kutukanwa kwa sababu nchi yake ni nchi inayozungumza Kiingereza, na kusema kuwa alichokifanya rais Trmp si pongezi, bali ni ukweli halisi ambapo watu wa Magharibi bado wanawachukulia Waafrika kama watu wasio na elimu.
Mwanadiplomasia wa Liberia ambaye hakutaka jina lake litajwe pia alisema kauli kama hizo zinaonyesha dharau kwa rais anayetokea nchi inayozungumza Kiingereza barani Afrika.
Video nyingine iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ilionesha kuwa viongozi wa Afrika walizungumza kwa zamu katika mkutano huo, na rais Trump alizidi kukosa subira, na ilipofika zamu ya Rais Mohamed Ould Ghazouani wa Mauritania, Trump alishindwa kujizuia. Kwanza alifanya ishara ya kuhimiza maendeleo, akitikisa kichwa, na kumkazia macho Rais Ghazouani, na mwisho alisema kwamba hataki kutumia muda mwingi kwenye suala hilo na kumtaka kuharakisha kwani kuna mambo mengine yanayofuata.
Vitendo hivyo vya rais Trump pia vimekosolewa kwenye mitandao ya kijamii. Mwanamtandao wa Marekani alilalamika kwa huzuni akisema, Trumo ni rais asiye na uwezo, huku mwanamtandao mwingine akisema, siku si nyingi zijazo, viongozi wa kigeni hawatafanya ziara nchini Marekani ili kukwepa kudharauliwa.
Kabla ya matukio hayo, rais Trump alikosolewa mara kadhaa kutokana na matamshi au vitendo vyake kuhusu nchi za Afrika.
Mwezi Mei mwaka huu, alimlaumu Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini kwamba wakulima wa kizungu nchini Afrika Kusini walikuwa “waathirika wa mauaji ya kimbari,” lawama ambayo haina msingi hata kidogo.
Mwaka 2018, wakati Trump alipokuwa katika muhula wake wa kwanza wa rais wa Marekani, aliwaita wahamiaji Waafrika wametoka “nchi duni.”